Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,502
- 9,282
ASKARI Polisi saba wamefariki dunia huku 50 wakijeruhiwa nchini India, katika mashambuliano ya risasi ya wenyewe kwa wenyewe , yaliyoibuka Jumatatu, tarehe 26 Julai 2021, kwenye Mji wa Vairengte nchini humo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Tukio hilo lisilo la kawaida limetokea baada ya Polisi katika majimbo ya Assam na Mizoram, yaliyoko Kaskazini Mashariki mwa India, kurushiana risasi, hatua iliyotokana na mgogoro wa muda mrefu wa mipaka ya majimbo hayo.
Mgogoro huo ulishika kasi mwezi mmoja uliopita, baada ya Polisi wa Jimbo la Mizoram, kudai kwamba Polisi wa Jimbo la Assam, wamejiongezea eneo la mpaka.
Waziri Mkuu wa Jimbo la Assam, Himanta Biswa Sarma, ameshutumu mapigano hayo akisema Polisi wa Mizoram hawakupaswa kutumia nguvu, katika kukabiliana na mgogoro huo.
MwanahalisiOnline
Tukio hilo lisilo la kawaida limetokea baada ya Polisi katika majimbo ya Assam na Mizoram, yaliyoko Kaskazini Mashariki mwa India, kurushiana risasi, hatua iliyotokana na mgogoro wa muda mrefu wa mipaka ya majimbo hayo.
Mgogoro huo ulishika kasi mwezi mmoja uliopita, baada ya Polisi wa Jimbo la Mizoram, kudai kwamba Polisi wa Jimbo la Assam, wamejiongezea eneo la mpaka.
Waziri Mkuu wa Jimbo la Assam, Himanta Biswa Sarma, ameshutumu mapigano hayo akisema Polisi wa Mizoram hawakupaswa kutumia nguvu, katika kukabiliana na mgogoro huo.
MwanahalisiOnline