Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,103
- 128,718
Wanabodi,
Naomba kuanza na angalizo!
Simple Mind Discuss People
Ordinary Mind Discuss Events
Great Minds Discuss Ideas。
Hili ni moja ya mabandiko yangu ya great minds ku discuss ideas, hakuna kutaja majina,simple minds nawaombeni kaeni pembeni!, hapa hatu discuss watu!。
Naomba wachangiaji tujadili hoja tuu ya msingi iliyopo mezani bila kutaja jina la mtu yoyote!,na ikitokea ukajisikia kuwashwa washwa kutaja majina,wewe ujijue bado ni simple mind,bandiko hili sii saizi yako!,nakuomba jipitie zako kimya kimya,nenda kwenye mabandiko ya saizi yako!,na nimuombe mode,tuirudishe ile nidhamu ya jf ya zamani,ya watu kujadili hoja iliyopo mezani, hoja kujibiwa kwa hoja na sio hoja kujibiwa kwa viroja vya kutaja taja watu!, ukiona mtu yoyote kataja jina lolote kwenye bandiko hili,mode nakuomba futilia mbali hiyo post,tuanze kurudisha ile jf ya enzi zile,watu wanakata issues hivyo kutenganisha hawa wana jf wa kisasa ambao kutwa wanajadili watu, na sisi wana jf wa zamani ambao tunajadili issues, mambo ya watoto humu yamekuwa mengi, machawa wametamalaki na uchawa hivyo kupelekea wote kuonekana ni watu wa hovyo!.
Hili ni bandiko la swali,huu ni mwaka wa uchaguzi,kuna vitu Watanzania tumekuwa tunaviomba vifanyike kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa 2025,miongoni mwa vitu hivyo, ni kufanyika kwa mabadiliko madogo ya katiba, kurejesha haki kuu za msingi za kidekrasia zilizoporwa, tukaomba kufanyike mabadiliko ya sheria ya uchaguzi, na kuundwa kwa tume huru na shirikishi ya uchaguzi.
Lakini mpaka sasa tumeingia mwaka wa uchaguzi,lile kubwa kuliko yote, mabadiliko madogo ya katiba, halijafanyika!.
Naomba kukiri kuna baadhi ya vitu vimefanyika right,ikiwemo kuruhusu mikutano ya vyama vya siasa, kubadili baadhi ya sheria, ikiwemo。sheria ya uchaguzi, kuna vingi vimefanyika but not the right way,mfano tumeunda Tume Huru, tume ya uchaguzi ni issue ya kikatiba, Bunge halina mamlaka yoyote kubadili jambo lolote kwenye katiba, hata kuongeza herufi moja tuu toka NEC kuwa INEC, bila mabadiliko madogo ya katiba!. Serikali yetu imepata wapi mamlaka ya kuifuta NEC na kuunda INEC kwa mabadiliko ya kawaida ya sheria wakati NEC ni zao la katiba?!
Kwenye hili la kutofanyika a minimum reforms ya katiba, limepelekea mimi kujiuliza,hivi hawa watu wetu wanaijua kweli katiba ya JMT ya mwaka 1977??!, inawezekana ni kiburi tuu na jeuri jeuri tuu ya serikali yetu, katiba tunaijua ila tumeamua kuwa hatufanyi mabadiliko yoyote ya katiba ili kuwakomoa kina fulani na kuwakomesha kina fulani bila kujua hao inaowakomoa ni Watanzania na hao inao wakomesha ni Watanzania!, na matokeo yake,tunakwenda kufanya uchaguzi kwa tume batili ya uchaguzi na sheria batili ya uchaguzi!
Inawezekana ni kiburi na jeuri ya wasaidizi wake sheria,hawajamwambia ukweli wa the legal status ya katiba yetu na sheria yetu ya uchaguzi,au ameambiwa na anajua ila kwa vile ubatili huo, hajaufanya yeye, yeye kaingia kaukuta, hivyo ameamua atafanya mabadiliko kwa muda wake, ila mkilazimisha ndio sifanyi kabisaa,kwani nisipo fanya, mtanifanya nini?!。
Japo katiba yetu ya JMT,inamruhusu kufanya jambo lolote,au kutofanya jambo lolote na asiwe amefanya kosa lolote kwasababu,katiba yetu imemruhusu,anaruhusiwa kushauriwa tuu na yeyote,lakini kwenye kufikia maamuzi,atafikia maamuzi yeye mwenyewe kama yeye,halazimiki kufuata ushauri wa yeyote,na maamuzi yake hayahojiwi na mamlaka yoyote!。
Na hata ikitokea akafanya maamuzi yoyote kwa makosa ya kisheria,kikanuni na kiutaratibu,tumempa kinga ya kutokushitakiwa popote,unless kama makosa hayo ni makosa ya ukiukwaji na uvunjaji wa katiba ya JMT,then anashitakiwa kwa mujibu wa Ibara ya 56A ya katiba
Lakini Bunge letu halina mamlaka ya kutunga sheria yoyote inayokwenda kinyume na katiba!, kitendo cha serikali kupeleka bungeni muswada wowote kinyume na katiba, ni ukiukwaji wa katiba!. Kitendo cha bunge kutunga sheria yoyote inayokwenda kinyume na katiba ya JMT, ni ukiukwaji wa katiba!, na kitendo cha rais wa JMT kusaini sheria batili kuanza kutumika ni ukiukwaji wa katiba!.
Je ni mara ngapi viongozi wetu wamekiuka katiba,wamekanyaga katiba,wamevuja katiba bila kufanywa chochote?!。
Tena imefikia mpaka kiwango cha Mahakama Kuu ya Tanzania,imetoa uamuzi na imetamka wazi jambo fulani ni kinyume na katiba,lakini bado viongozi wetu wanalitenda?!,wanakanyaga katiba,wanavunja katiba,wanakiuka katiba na hawafanywi lolote!itakuwa haya ya kusema tuu humu, kuandika magazetini na kwenye mitandao, itasaidia?.
Au inawezekana ni kweli kabisa yuko real very busy sana,na hapati kabisa muda wa kutusoma?,kututazama na kutusikiliza,awategemea zaidi wasaidizi wake tuu!,wamsomee,wamtazamie na kumsikilizishia,na hao wasaidizi wake nao ikatokea na wao pia wako too busy sana,hawajapata kabisa
nafasi ya kumwambia ukweli wa ubatili wa katiba yetu na ubatili wa hii sheria yetu mpya ya uchaguzi aliyoisaini mwaka jana ambayo ndio tunakwenda kuifanyia uchaguzi wa mwaka huu, kuwa ni sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba ya JMT?.
Kuna vitu vya ajabu ajabu vya kisheria vinavyofanyika nchini mwetu, ukiwa ni mwanasheria, ni vigumu sana kuvielewa, kama hili la ubatili wa katiba na ubatili wa sheria yetu ya uchaguzi!.
Mahakama Kuu ya Tanzania, imetoa uamuzi kuhusu ubatili wa sheria ya uchaguzi, tukaamua kutunga sheria mpya ya uchaguzi, wanasheria nguli, wabobezi na wabebovu wakatungaje muswada wenye ubatili ule ule?!.
Tuliposhirikishwa kwenye hatua zote tatu, kwenye kukusanya maoni ya wadau, kuna watu tulisema,
View: https://youtu.be/PBpjDhH2XiA?si=8EEhNkNVlONuph1b
Kabla ya muswada kusomwa kwa mara ya kwanza, tukaitwa kutoa maoni, tukasema
View: https://youtu.be/3a4SjkV46JY?si=ky_DyqMycv_SBH7I
Na baada ya muswada kusomwa kwa mara ya kwanza, tukaitwa kutoa maoni Bungeni Dodoma, tukasema
View: https://youtu.be/lBC3xKODSvY?si=fbeeEcbqtBYjuyrJ
Sheria ilipokuja kutoka, ina ubatili ule ule tulioupigia kelele!mtu unajiuliza Bunge chini ya mwalimu wangu nguli mbobezi na mbobevu wa
sheria, wa kitivo cha sheria, chuo kikuu cha DSM, UDSM, linatungaje sheria batili kinyume na katiba?!. Halafu bila aibu, anapelekewa rais wa JMT kusaini sheria batili!.
Kwenye hili la ubatili wa katiba na ubatili wa sheria, nimesisitiza mtu asiye
mwanasheria hawezi kuujua
ubatili wa katiba au ubatili wa sheria, bila kuelezwa na wanasheria!, hivyo inawezekana mpaka ninapoandika hapa, mwenyewe wala hajui tuna katiba batilifu, wala hajui ametungiwa sheria batili, na yeye kuisaini bila kujua ni batili!.
Hivyo kumlaumu mtu kama huyu ni kumuonea bure tuu,kumbe masikini wa watu yeye wala hajui?!。
Kwa vile huu ndio mwaka wa uchaguzi,something must be done kuhusu hii sheria mpya ya uchaguzi,ni sheria batili kwasababu ina vifungu fulani batili,viko kinyume cha katiba ya JMT,ya mwaka 1977
Mahakama Kuu iliisha utangaza ubatili huo ni kinyume na katiba!。
Serikali ikauchukua ubatili huo,ukauchomekea kiubatili ndani ya katiba yetu,ili sasa ule ubatili wa sheria ya uchaguzi,uliotangazwa na Mahakama Kuu,kuwa ni batili,sasa umehalalishwa kwasababu ubatili huo sasa umechomekewa ndani ya katiba yetu!.
Mahakama Kuu ikakomaa kuwa sheria hiyo ni batili,na uchomekeaji wa vifungu hivyo batili ndani ya katiba yetu, nao umefanyika kiubatili!.
Mahakama ya Rufani,ikakiri ubatili huo,ila kwa vile sasa ubatili huo,umechomekewa ndani ya katiba yetu,upo ndani ya katiba, hata kama uchomekeaji huo umefanywa kiubatili, lakini upo!, na aliyechomekea ubatili huo ni Bunge letu tukufu!,kwa kuliheshimu Bunge, Mahakama ya Rufaa, ikaamua,Mahakama haiwezi kuliingilia Bunge katika jukumu lake la kutunga sheria,hivyo mpira huo wa ubatili wa katiba na ubatili wa sheria, ukarudishwa mezani kwa Bunge,liuondoe!。 Bunge likatia mpira kwapani na kula kobisi mpaka leo hii ninapoandika hapa!,ubatili huo bado upo ndani ya katiba yetu!,tumetunga sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule sasa tunajiandaa kufanya uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwa katiba batilifu na sheria batili!。Je tufanye nini?.
A Way Forward
Ikitokea this time akaliona bandiko hili na kuvisikia vilio hivi, naendelea kusisitiza kuna kufanya, jambo zuri, doing the right thing, amefanya makubwa mazuri mengi!, na tumemoongeza sana!.
Ila.kwenye dunia ya sasa ya utandawazi na usasa, doing the right thing, is not enough, one has to do the right thing, at the right time and do it right!. Kuna vitu amevifanya ni right thing lakini havijafanyika the right way!
Nashauri
Paskali
Rejea
Naomba kuanza na angalizo!
Simple Mind Discuss People
Ordinary Mind Discuss Events
Great Minds Discuss Ideas。
Hili ni moja ya mabandiko yangu ya great minds ku discuss ideas, hakuna kutaja majina,simple minds nawaombeni kaeni pembeni!, hapa hatu discuss watu!。
Naomba wachangiaji tujadili hoja tuu ya msingi iliyopo mezani bila kutaja jina la mtu yoyote!,na ikitokea ukajisikia kuwashwa washwa kutaja majina,wewe ujijue bado ni simple mind,bandiko hili sii saizi yako!,nakuomba jipitie zako kimya kimya,nenda kwenye mabandiko ya saizi yako!,na nimuombe mode,tuirudishe ile nidhamu ya jf ya zamani,ya watu kujadili hoja iliyopo mezani, hoja kujibiwa kwa hoja na sio hoja kujibiwa kwa viroja vya kutaja taja watu!, ukiona mtu yoyote kataja jina lolote kwenye bandiko hili,mode nakuomba futilia mbali hiyo post,tuanze kurudisha ile jf ya enzi zile,watu wanakata issues hivyo kutenganisha hawa wana jf wa kisasa ambao kutwa wanajadili watu, na sisi wana jf wa zamani ambao tunajadili issues, mambo ya watoto humu yamekuwa mengi, machawa wametamalaki na uchawa hivyo kupelekea wote kuonekana ni watu wa hovyo!.
Hili ni bandiko la swali,huu ni mwaka wa uchaguzi,kuna vitu Watanzania tumekuwa tunaviomba vifanyike kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa 2025,miongoni mwa vitu hivyo, ni kufanyika kwa mabadiliko madogo ya katiba, kurejesha haki kuu za msingi za kidekrasia zilizoporwa, tukaomba kufanyike mabadiliko ya sheria ya uchaguzi, na kuundwa kwa tume huru na shirikishi ya uchaguzi.
Lakini mpaka sasa tumeingia mwaka wa uchaguzi,lile kubwa kuliko yote, mabadiliko madogo ya katiba, halijafanyika!.
Naomba kukiri kuna baadhi ya vitu vimefanyika right,ikiwemo kuruhusu mikutano ya vyama vya siasa, kubadili baadhi ya sheria, ikiwemo。sheria ya uchaguzi, kuna vingi vimefanyika but not the right way,mfano tumeunda Tume Huru, tume ya uchaguzi ni issue ya kikatiba, Bunge halina mamlaka yoyote kubadili jambo lolote kwenye katiba, hata kuongeza herufi moja tuu toka NEC kuwa INEC, bila mabadiliko madogo ya katiba!. Serikali yetu imepata wapi mamlaka ya kuifuta NEC na kuunda INEC kwa mabadiliko ya kawaida ya sheria wakati NEC ni zao la katiba?!
Kwenye hili la kutofanyika a minimum reforms ya katiba, limepelekea mimi kujiuliza,hivi hawa watu wetu wanaijua kweli katiba ya JMT ya mwaka 1977??!, inawezekana ni kiburi tuu na jeuri jeuri tuu ya serikali yetu, katiba tunaijua ila tumeamua kuwa hatufanyi mabadiliko yoyote ya katiba ili kuwakomoa kina fulani na kuwakomesha kina fulani bila kujua hao inaowakomoa ni Watanzania na hao inao wakomesha ni Watanzania!, na matokeo yake,tunakwenda kufanya uchaguzi kwa tume batili ya uchaguzi na sheria batili ya uchaguzi!
Inawezekana ni kiburi na jeuri ya wasaidizi wake sheria,hawajamwambia ukweli wa the legal status ya katiba yetu na sheria yetu ya uchaguzi,au ameambiwa na anajua ila kwa vile ubatili huo, hajaufanya yeye, yeye kaingia kaukuta, hivyo ameamua atafanya mabadiliko kwa muda wake, ila mkilazimisha ndio sifanyi kabisaa,kwani nisipo fanya, mtanifanya nini?!。
Japo katiba yetu ya JMT,inamruhusu kufanya jambo lolote,au kutofanya jambo lolote na asiwe amefanya kosa lolote kwasababu,katiba yetu imemruhusu,anaruhusiwa kushauriwa tuu na yeyote,lakini kwenye kufikia maamuzi,atafikia maamuzi yeye mwenyewe kama yeye,halazimiki kufuata ushauri wa yeyote,na maamuzi yake hayahojiwi na mamlaka yoyote!。
Na hata ikitokea akafanya maamuzi yoyote kwa makosa ya kisheria,kikanuni na kiutaratibu,tumempa kinga ya kutokushitakiwa popote,unless kama makosa hayo ni makosa ya ukiukwaji na uvunjaji wa katiba ya JMT,then anashitakiwa kwa mujibu wa Ibara ya 56A ya katiba
Lakini Bunge letu halina mamlaka ya kutunga sheria yoyote inayokwenda kinyume na katiba!, kitendo cha serikali kupeleka bungeni muswada wowote kinyume na katiba, ni ukiukwaji wa katiba!. Kitendo cha bunge kutunga sheria yoyote inayokwenda kinyume na katiba ya JMT, ni ukiukwaji wa katiba!, na kitendo cha rais wa JMT kusaini sheria batili kuanza kutumika ni ukiukwaji wa katiba!.
Je ni mara ngapi viongozi wetu wamekiuka katiba,wamekanyaga katiba,wamevuja katiba bila kufanywa chochote?!。
Tena imefikia mpaka kiwango cha Mahakama Kuu ya Tanzania,imetoa uamuzi na imetamka wazi jambo fulani ni kinyume na katiba,lakini bado viongozi wetu wanalitenda?!,wanakanyaga katiba,wanavunja katiba,wanakiuka katiba na hawafanywi lolote!itakuwa haya ya kusema tuu humu, kuandika magazetini na kwenye mitandao, itasaidia?.
Au inawezekana ni kweli kabisa yuko real very busy sana,na hapati kabisa muda wa kutusoma?,kututazama na kutusikiliza,awategemea zaidi wasaidizi wake tuu!,wamsomee,wamtazamie na kumsikilizishia,na hao wasaidizi wake nao ikatokea na wao pia wako too busy sana,hawajapata kabisa
nafasi ya kumwambia ukweli wa ubatili wa katiba yetu na ubatili wa hii sheria yetu mpya ya uchaguzi aliyoisaini mwaka jana ambayo ndio tunakwenda kuifanyia uchaguzi wa mwaka huu, kuwa ni sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba ya JMT?.
Kuna vitu vya ajabu ajabu vya kisheria vinavyofanyika nchini mwetu, ukiwa ni mwanasheria, ni vigumu sana kuvielewa, kama hili la ubatili wa katiba na ubatili wa sheria yetu ya uchaguzi!.
Mahakama Kuu ya Tanzania, imetoa uamuzi kuhusu ubatili wa sheria ya uchaguzi, tukaamua kutunga sheria mpya ya uchaguzi, wanasheria nguli, wabobezi na wabebovu wakatungaje muswada wenye ubatili ule ule?!.
Tuliposhirikishwa kwenye hatua zote tatu, kwenye kukusanya maoni ya wadau, kuna watu tulisema,
View: https://youtu.be/PBpjDhH2XiA?si=8EEhNkNVlONuph1b
Kabla ya muswada kusomwa kwa mara ya kwanza, tukaitwa kutoa maoni, tukasema
View: https://youtu.be/3a4SjkV46JY?si=ky_DyqMycv_SBH7I
Na baada ya muswada kusomwa kwa mara ya kwanza, tukaitwa kutoa maoni Bungeni Dodoma, tukasema
View: https://youtu.be/lBC3xKODSvY?si=fbeeEcbqtBYjuyrJ
Sheria ilipokuja kutoka, ina ubatili ule ule tulioupigia kelele!mtu unajiuliza Bunge chini ya mwalimu wangu nguli mbobezi na mbobevu wa
sheria, wa kitivo cha sheria, chuo kikuu cha DSM, UDSM, linatungaje sheria batili kinyume na katiba?!. Halafu bila aibu, anapelekewa rais wa JMT kusaini sheria batili!.
Kwenye hili la ubatili wa katiba na ubatili wa sheria, nimesisitiza mtu asiye
mwanasheria hawezi kuujua
ubatili wa katiba au ubatili wa sheria, bila kuelezwa na wanasheria!, hivyo inawezekana mpaka ninapoandika hapa, mwenyewe wala hajui tuna katiba batilifu, wala hajui ametungiwa sheria batili, na yeye kuisaini bila kujua ni batili!.
Hivyo kumlaumu mtu kama huyu ni kumuonea bure tuu,kumbe masikini wa watu yeye wala hajui?!。
Kwa vile huu ndio mwaka wa uchaguzi,something must be done kuhusu hii sheria mpya ya uchaguzi,ni sheria batili kwasababu ina vifungu fulani batili,viko kinyume cha katiba ya JMT,ya mwaka 1977
Mahakama Kuu iliisha utangaza ubatili huo ni kinyume na katiba!。
Serikali ikauchukua ubatili huo,ukauchomekea kiubatili ndani ya katiba yetu,ili sasa ule ubatili wa sheria ya uchaguzi,uliotangazwa na Mahakama Kuu,kuwa ni batili,sasa umehalalishwa kwasababu ubatili huo sasa umechomekewa ndani ya katiba yetu!.
Mahakama Kuu ikakomaa kuwa sheria hiyo ni batili,na uchomekeaji wa vifungu hivyo batili ndani ya katiba yetu, nao umefanyika kiubatili!.
Mahakama ya Rufani,ikakiri ubatili huo,ila kwa vile sasa ubatili huo,umechomekewa ndani ya katiba yetu,upo ndani ya katiba, hata kama uchomekeaji huo umefanywa kiubatili, lakini upo!, na aliyechomekea ubatili huo ni Bunge letu tukufu!,kwa kuliheshimu Bunge, Mahakama ya Rufaa, ikaamua,Mahakama haiwezi kuliingilia Bunge katika jukumu lake la kutunga sheria,hivyo mpira huo wa ubatili wa katiba na ubatili wa sheria, ukarudishwa mezani kwa Bunge,liuondoe!。 Bunge likatia mpira kwapani na kula kobisi mpaka leo hii ninapoandika hapa!,ubatili huo bado upo ndani ya katiba yetu!,tumetunga sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule sasa tunajiandaa kufanya uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwa katiba batilifu na sheria batili!。Je tufanye nini?.
A Way Forward
Ikitokea this time akaliona bandiko hili na kuvisikia vilio hivi, naendelea kusisitiza kuna kufanya, jambo zuri, doing the right thing, amefanya makubwa mazuri mengi!, na tumemoongeza sana!.
Ila.kwenye dunia ya sasa ya utandawazi na usasa, doing the right thing, is not enough, one has to do the right thing, at the right time and do it right!. Kuna vitu amevifanya ni right thing lakini havijafanyika the right way!
Nashauri
- Muda uliopo unatosha,kufanya minimum reforms za katiba kwa hati ya dharura,kuucholopoa huo ubatili uliochomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu na kuifanya iwe ni katiba safi na halali。
- Sheria mpya ya Uchaguzi,is the right thing done on a wrong way!, sheria hii ifumuliwe,vile vifungu batili viondolewe,kila Mtanzania awe huru kupiga kura kumchagua kiongozi anayemtaka kwa mujibu wa ibara ya 5。Kwa sasa Mtanzania hayuko huru kumchagua kiongozi anayemtaka,analazimishwa lazima amchague kiongozi aliyeletewa na chama cha siasa!.
- Ibara ya 21 yakatiba irekebishwe kila mtu aruhusiwe kugombea uongozi,kwa sasa Mtanzania haruhuhusiwi kugombea uongozi,analazimishwa kwanza ni lazima ajiunge na chama cha siasa,hicho chama ndio kimdhamini,ndipo aruhusiwe kugombea uongozi wa umma, matokeo yake tunawakosa watu wazuri, watu makini kutuwakilisha huku tukijaza mazagazaga na matutusa kule kwenye vyombo vyetu vya uwakilishi,matutusa na mazagazaga mengine kazi yao ni kugonga tuu meza kupiga makofi na kusema ndiooo!,nawengine haswa wale wa vitu maalum,wako pale kwa kazi maalum!,tungekuwa na watu makini mule wa kutosha,yale madudu ya ajabu ajabu yaliyopitishwa mule yasinge pita kwa mserereko kivile!。
- Watanzania walitaka Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi,na sio kuibadili tuu jina kutoka Tume ya Uchaguzi NEC,kuwa Tume Huru ya Uchaguzi INEC,lakini tume ni ile ile,watu ni wale wale!. Tume Huru ya Uchaguzi is the right thing,tuirekebishe,isukwe upya na iwe shirikishi!。
- Creation of level playing field kwenye the game of politics。The political game playing field is not level, we need to create a level playing field ili kupata ushindani wa haki. Hili nalo ni tatizo la kikanuni, mfano, kuna mgombea mmoja anaingia kwenye kinyanganyiro cha uchaguzi, anatoka chama dola, anatembea na dola, misafara mirefu na vingora, media, 2025 sio media tuu, media, Bongo movie, Bongo Fleva, Social media influences, mpaka ma chawa, na wasaidizi huku budget yake is fully footed by state, kwasababu ni head of state ashindane na wagombea kutoka chama makapuku!, ni kama kugombea kisu cha makali kuwili, huku mmoja ameshika kwenye mpini! unategemea nini?.
Paskali
Rejea
Similar Discussions
- Asking Aloud: Rais Samia anajua Katiba yetu ni batilifu, na Sheria mpya ya uchaguzi aliyosaini ni sheria batili kinyume cha katiba?
- Asante Rais Samia Kutuletea Prof. Kabudi Pale Sheria, Ni Best Brain, High IQ. na Bingwa wa Katiba. Je, Atakuwa Mkweli Ubatili wa Katiba na Sheria au?
Jukwaa la Siasa - Wajua Kuna Sheria Halali, Batili na Batilifu, Ndoa Halali, Batili na Batilifu, Je Wajua Katiba ya JMT ni Batilifu?. Why Ubatili Huu wa Katiba Yetu?!
Jukwaa la Siasa - Je, Bunge Litimize Wajibu Wake KikamiliIfu Ikiwemo Kutunga Sheria, Au Liendelee Kuwa "Rubber Stamp" ya Kupitishia Miswada ya Serikali Bila Kuhoji?
Jukwaa la Siasa - Bunge Letu Kibri na Jeuri ni Bunge Kweli la Kutunga Sheria au ni Bunge Ruber Stemp ya Serikali? Kwanini Linaogopwa Hivi na Mhimili wa Mahakama?
Jukwaa la Siasa