Inawezekana Magufuli sio tatizo?

Inawezekana Magufuli sio tatizo?

Hilo siyo suluhisho la matatizo ya TanZania hata kama Serikali ikihamia Dom bado idadi ya watu itaendela kuongezeka Dar kwa maana Dar ndiyo mji tajiri TZ na utabakia kuwa hivyo, suluhisho hapa ni population control basi, hakuna lingine ni lazima Serikali ije mpango wa kudhibiti uzaaji hovyo wa bila mpango!
Sijawahi kushuhudia mtu mjinga kama wewe hapa jf.sasa ndio umeandika utumbo gani huu?
 
The Boss, labda kuna jambo kubwa hilijui! Unadhani hata yale mapato ya serikali ya trilioni 1. 4 Tshs kwa mwezi ni ya kweli? Usidanganywe mkuu! Hii serikali ya Magufuli imejua kuwa watanzania wanahitaji nini! Matangazo mazuri! Hawahoji, hawaulizi, wao wanaitika "Hapa kazi tu" Mpango ameenda nao sambamba! Magufuli anamalizia! Sisi tunaohoji na kuchambua tunaonekana wachawi wa Magufuli!

Usione watu wanalipwa ili kumsifia mzee, lipo jambo! Ila mimi ninachojipa moyo ni kuwa "wengi watang'amua mapema"
 
Ninaposema population control namaanishwa kwamba ongezeko la watu nchini mwetu ni kubwa sana na haliendani na ukuwaji wa uchumi wetu hivyo hakuna kitu tunafanya ni kama uwe na watoto 2 una mshara wa laki tano halafu unaongeza watoto wawili tena na mshahra unaongezeka mpaka laki tano na nusu tu ni dhahiri kwamba utakuwa na mapungufu ya karibia kila kitu kwenye familia yako ukilinganisha na ulivyokuwa na watoto 2 tu!

Na ndicho kinachotokea TZ, hizo Hospitali za Rufaa za Mikoani unazoziongelea utazijenga na nini? Unahitaji kwanza ukuaji wa uchumi ili uweze kuwa na fedha ya kuzijenga, sasa maadamu kila mwanamke Tanzania anapata wastani wa 2.6 na uchumi wetu unakuwa kwa asilimia 6 - 7 tu hatuwezi kufanya hayo yote ni lazima Uchumi wetu ukuwe kuzidi ongezeko la watu ili ilete maana na hili kwa hali ya kawaida na ngumu hakuna nchi waliowahi kufanikiwa na ndiyo njia pekee ni kupunguza ongezeko la watu kwa mfano iwekwe utaratibu mwisho watoto wawili ambao Serikali inawalipia kila kitu na kila mtoto wa tatu au nne unamlipia mwenyewe na kodi unayokatwa inaongezeka hii itasaidia vinginevyo hakuna kitu tutafanya!


Sijui kama umewahi kukutana na maelezo kwamba idadi ya watu hupungua sana uchumi ukiwa mzuri


kuna mahala nilisoma inaonesha nchi zote zilizotoka kwenye umasikini idadi ya watu ilipungua sana
na the best way ya ku control watu ni kupambana na umasikini..
watu masikini wanazaliana zaidi......
 
Tatizo letu Watanzania ni kufikiri kwamba kuna mtu fulani sehemu fulani mwenye wajibu wa kuyashughulikia matatizo yetu kwa mapana yake!. Serikali ni mimi na wewe, ni wewe na yule, ni kila mtu. Ni dhana potofu kudhani kwamba kuna watu fulani ambao wao humaanisha uwepo wa serikali. Hizi akiliza lawama lazima zitutoke vichwani mwetu kwanza, halafu baada ya hapo ndipo tutakuwa tayari kuelewa maana ya uwajibikaji. Anatazamwa Magufuli na wasaidizi wake kama vile ni watu wametoka sayari nyingine kuja kutuondolea maelfu ya matatizo yetu.

Hakuna kitu kama hicho. Tatizo ni sisi wote kwa ujumla wetu. Kila mtu atambue kuwa yeye ni serikali. Kule Marekani anaposhinda urais mgombea mmoja, haapishwi na kupewa ofisi siku inayofuata, hupewa muda wa miezi zaidi ya miwili ili aweze kuelezwa mambo yote yanayohusiana na urais wake. Haijalishi yeye ni republican au democrats, lazima aelezwe ni mambo gani anayotakiwa kuyatanguliza kwa maslahi ya taifa la Marekani.

Siasa za vyama vingi zimekuja kwetu pasipo ujio wa miiko ya usimamiaji wake. Uvivu wetu binafsi tunataka kuutafutia sababu za kuuhalalisha. Tujitathmini kwa kina ili tuweze kuikoa nchi hii.
 
The Boss, labda kuna jambo kubwa hilijui! Unadhani hata yale mapato ya serikali ya trilioni 1. 4 Tshs kwa mwezi ni ya kweli? Usidanganywe mkuu! Hii serikali ya Magufuli imejua kuwa watanzania wanahitaji nini! Matangazo mazuri! Hawahoji, hawaulizi, wao wanaitika "Hapa kazi tu" Mpango ameenda nao sambamba! Magufuli anamalizia! Sisi tunaohoji na kuchambua tunaonekana wachawi wa Magufuli!

Usione watu wanalipwa ili kumsifia mzee, lipo jambo! Ila mimi ninachojipa moyo ni kuwa "wengi watang'amua mapema"


Lile la kuchukua t scan Dodoma naona limewaumbua hadi basi....
 
Correction: Pombe alikwenda Muhimbili kumjulia hali sheikh wa Bakwata aliyelazwa hapo, akiwa aneo la hospital kinamama wakamsonga na kumuomba akajionee mateso wanayopata wodi ya wazazi na akakuta hayo aliyoyakuta.

Je kungekuwa hakuna mgonjwa mashuhuri wa kwenda kumjulia hali hapo hospital pangeendelea kubaki hivyohivyo bila kumulikwa?

Yule waziri dr kilaza anayewahi asubuhi wizara ya afya na kufungia mageti wachelewaji yuko wapi?

Kinamama wanaolala chini hospital za huko Tandahimba watatuliwa tatizo lao baada ya nani kwenda hapo hospital au Pombe ni spiderman atakuwa anapaa hewani kukagua wodi zote tanzania?
Eti yule Waziri Dr. Kilaza jamani....wivu huu haufai

Haya...chagadema mapovu yanawatoka hapa kwani Magufuli ameishaanza kutekeleza bajet yake?. Subirini bajeti ipite ndio tuanze kuhororoja...

Serikal inachofanya kwasasa ni kujenga misingi ya uwajibikaji serikalini...na pale inapopata fursa inatatua changamoto zilizopo kama alivyofanya Magufuli alipopeleka vitanda hapo Muhimbili...

Serikali ya awamu ya tano imeahidi kujenga hospitali za rufaa na wilaya ili kuboresha huduma za afya na kusogeza huduma hizo karibu na wananchi ili waache kurundikana Muhimbili...

Sasa ndio siku 100 hizo za Magufuli hata nusu mwaka bado hata bajeti yake ya kwanza bado...yani kama ni mechi bado sana ndio dakika 5 sasa...
 
Hahaa haki ya Mungu nimecheka kwa sauti....

But seriously though, can you put such a stunt past him?

Uakumbuka kipindi flani alipigwa picha kapanda bodaboda bila helmet?

Huyo jamaa ana mapepe sana.

Hivi tokea awafungie geti wale wafanyakazi siku ile hajaenda kwingine na kufanya hivyo?
 
Juzi tuliambiwa eti changamoto ya kufeli kwa program ya kwanza ya elimu bure ni wanafunzi wengi kuandikishwa darasa la kwanza! Tukaambiwa kuwa kuna shule wameandikishwa la kwanza watoto 900! Tukaitika "Hapa kazi tu" Hatukuhoji wala kuchambua!

Hatukujiuliza inakuwaje hivi? Hatukujiuliza ni kwa vipi mtoto wa darasa la kwanza ambaye Tshs 1500 huko vijijini (wengi wao) kwa mwezi anashiba na kusaza! Tukaishia kuitika "Hapa kazi tu"
 
Tuliopinga propaganda zile kuwa hazina ukweli tuliitwa majina yote mabaya. Tulikua na mijadala mirefu sana tukielezea kwa details namna hata kauli za Mkurugenzi wa MSD msanii Bwanakunu zilivykuwa zikijifunga matandabui watu hawakutuelewa. Tukawaeleza kuwa picha wanazoonyeshwa ni za MOI wakabisha wengine wakakataa na wengine wakadai hata MOI ni Muhimbili kwa kushindwa kutofautisha kati ya MOI na MNHC.
 
Tuliopinga propaganda zile kuwa hazina ukweli tuliitwa majina yote mabaya. Tulikua na mijadala mirefu sana tukielezea kwa details namna hata kauli za Mkurugenzi wa MSD msanii Bwanakunu zilivykuwa zikijifunga matandabui watu hawakutuelewa. Tukawaeleza kuwa picha wanazoonyeshwa ni za MOI wakabisha wengine wakakataa na wengine wakashindwa kutofautisha kati ya MOI na MNHC.


Mie nashindwa kuelewa why so much efforts na so much energy kwenye uongo na usanii?
why wasiamue kutatua matatizo for real?
 
Hata afike muhimbili kila siku tatizo halitaisha waboreshe hospitali zingine au wajenge mpya watu ni wengi sana dar kuliko huduma zilizopo.
 
hapa issue sio idadi ya wagonjwa ktk kitanda kimoja.Hapa tujadili hali halisi ya hospitality zetu.Wizara ya Afya imekosa watendaji yaani Waziri na Naibu wake na Katibu mkuu wote ZERO.Wanapotezà muda mwingi kwenye vyombo vya habari ili waonekane na JPM kuwa wapo...wanafanya mini HAIWÀHUSU...Kina J ma Mwaka ndio issue kwa UMMY MWALIMU NA HAMIS KINGWANGALA..RAIS; ONDOA HIZI TAKATAKA HAPO WIZARANI.Hawajui wanapaswa kufanya nini...kulipiza kisasi(?)kuuza sura?kunyanyasa wafanyakazi wenzao wa wizara hiyo?WAJIPIME!
 
Mie nashindwa kuelewa why so much efforts na so much energy kwenye uongo na usanii?
why wasiamue kutatua matatizo for real?
Na sasa hivi ili kufanikiwa kukemea kukosoa serikali tuombe Mods wa JF wasiwe kati ya wale 46. Ingawa hilo ni gumu sana.
 
Tatizo letu Watanzania ni kufikiri kwamba kuna mtu fulani sehemu fulani mwenye wajibu wa kuyashughulikia matatizo yetu kwa mapana yake!. Serikali ni mimi na wewe, ni wewe na yule, ni kila mtu. Ni dhana potofu kudhani kwamba kuna watu fulani ambao wao humaanisha uwepo wa serikali. Hizi akiliza lawama lazima zitutoke vichwani mwetu kwanza, halafu baada ya hapo ndipo tutakuwa tayari kuelewa maana ya uwajibikaji. Anatazamwa Magufuli na wasaidizi wake kama vile ni watu wametoka sayari nyingine kuja kutuondolea maelfu ya matatizo yetu.

Hakuna kitu kama hicho. Tatizo ni sisi wote kwa ujumla wetu. Kila mtu atambue kuwa yeye ni serikali. Kule Marekani anaposhinda urais mgombea mmoja, haapishwi na kupewa ofisi siku inayofuata, hupewa muda wa miezi zaidi ya miwili ili aweze kuelezwa mambo yote yanayohusiana na urais wake. Haijalishi yeye ni republican au democrats, lazima aelezwe ni mambo gani anayotakiwa kuyatanguliza kwa maslahi ya taifa la Marekani.

Siasa za vyama vingi zimekuja kwetu pasipo ujio wa miiko ya usimamiaji wake. Uvivu wetu binafsi tunataka kuutafutia sababu za kuuhalalisha. Tujitathmini kwa kina ili tuweze kuikoa nchi hii.
Mkuu hao vijana wasikuumize kichwa...luwasa ameishatangaza kuwania urais 2020 sasa wameishaanza kampeni hao...

Usitarajie kuisema vizuri serikali ya Magufuli...ila wasichojua ni kuwa wanapambana na kivuli chao...Magufuli ni namba nyingine.

Magufuli ameishaeleweka dhamira yake na watanzania tuko nyuma yake tunamuunga mkono kwa kufanya kazi na sio kumvizia kakosea wapi ili tuanzishe thread...

Ni aibu kuona kampeni ndio zimeisha ila watu wanaendeleza siasa badala ya kazi...ukiona hivyo jua watu hao hawako sawa yaani ni punguani....
 
Leo ukifuatilia taarifa ya habari Magufuli katembelea tena Muhimbili kwa kustukiza
kakuta matatizo tele hasa amewakuta wamama waki share vitanda hadi watu watano
na wengine wakilala chini.....

Utakumbuka few months ago tulitangaziwa kuwa baada ya Magufuli kwenda Muhimbili
vitanda vilipelekwa hadi vikakosa wagonjwa
kuna picha zilisambazwa paka kalalia kitanda kipya Muhimbili
na kwamba sasa mambo ni tofauti kabisa...vitanda tele na kila kitu saafi

Sasa binafsi siamini kabisa Muhimbili imewahi kuwa safi na matatizo yakaisha
ambacho najiuliza why 'maigizo yale ya kuwa mambo ni saafi' yaliruhusiwa
kuendelea ?

why sisi wananchi na waandishi wa habari hatukupinga kabisa habari za kuwa
mambo ni saafi muhimbili?
why habari ya leo iwe kama habari mpya
while in reality watu wameendelea kulala chini tu kama zamani?

Inawezekana kabisa tatizo haliko kwa wanasiasa?

tatizo liko kwetu wananchi na hasa media?
tumeletewa 'sanaa tukaishangilia huku ukweli tunaujua'?
sababu muhimbili hali yake sio siri
lakini tulipoambiwa mambo sasa ni saafi tuliruka ruka na kushangilia...
huku kiukweli hali ni ile ile tu.....

Na leo tena wananchi wamemlilia tena Magufuli bila kujiuliza
ni kweli Magufuli hali iliyopo haijui?si alikwenda juzi tu hapo hapo Muhimbili?
au haya matatizo ni mapya kabisa?
Nakubaliana na wewe 100%
 
Sijui kama umewahi kukutana na maelezo kwamba idadi ya watu hupungua sana uchumi ukiwa mzuri


kuna mahala nilisoma inaonesha nchi zote zilizotoka kwenye umasikini idadi ya watu ilipungua sana
na the best way ya ku control watu ni kupambana na umasikini..
watu masikini wanazaliana zaidi......

Kuna ngazi ya maendeleo ambayo nchi hufikia ambapo sasa wananchi wenyewe wanaweza kujicontrol kama zilipofikia nchi zilizoendelea lkn hii ni hatua ya mbele kabisa!

Lkn asikudanganye mtu nchi zilizoendelea wote wanafanya population control sema mbinu tu ndiyo tofauti kwa mfano nchi tajiri zote watoto wa kike hupewa birth control pills au vidonge vya kuzuia ujazito sasa maana yake nini?
Ni kwamba mtoto wa kike wa Ulaya, Marekani, Japani au nchi tajiri yoyote hawezi kupata mimba ya bila kutarajia yaani kama atapata mimba ni kwamba ameamua kupata mimba na siyo bahati mbaya sisi kwetu hakuna hilo ina maana msichana yoyote yule anayelala na mwanaume ana hatari ya kupata mimba wakati wowote ule na ukiangalia takwimu za serikali wasichana wanaopata mimba bila ya kupanga yaani kuwa tayari kuwa na mtoto ni wengi sana jaribu kuangalia tu mtaani na hesabu wasichana waliozaa kabla ya wao kuwa tayari kuwa na familia au kijijni ukienda, sasa hii maana yake nini?
Ina maana huyu msichana kwanza hana elimu ya kumuwezesha kupata ajira yaani yeye mwenyewe bado hajaweza kujisimamia halafu tayari tena ana kiumbe ambacho anapaswa akihudumie sasa Umaskini utawezaje kuisha au kupungua hapo?!

Hivyo basi kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kuwapa wasichana wetu vidonge vya kuzuia mimba hatuna budi kutafuta njia mbadala, ili mtoto azaliwe tu na yule mwenye uwezo wa kumuhudumia na si vinginevyo!

Ukiangalia hiyo picha hapo chini utaona ninachoongelea, wapo wengi kama wangekuwa na vidonge vya kuzuia kupata mimba wengi wao wasingeamua kupata mimba!

images
 
Hapa issue ni Kwamba wagonjwa wakiwa zaidi ya mmoja kitandani haifai.Sasa mtu Akisema watano hata kumi haiondoi tatizo .Mjamzito kwanza kitanda hakimtoshi Sasa wakiwa wawili??
 
Mkuu hao vijana wasikuumize kichwa...luwasa ameishatangaza kuwania urais 2020 sasa wameishaanza kampeni hao...

Usitarajie kuisema vizuri serikali ya Magufuli...ila wasichojua ni kuwa wanapambana na kivuli chao...Magufuli ni namba nyingine.

Magufuli ameishaeleweka dhamira yake na watanzania tuko nyuma yake tunamuunga mkono kwa kufanya kazi na sio kumvizia kakosea wapi ili tuanzishe thread...

Ni aibu kuona kampeni ndio zimeisha ila watu wanaendeleza siasa badala ya kazi...ukiona hivyo jua watu hao hawako sawa yaani ni punguani....
Hawaniumizi kichwa, wanabadilisha lengo zima la ziara ya rais pale Muhimbili, alikwenda kumtazama Mufti, sasa wanajaribu kuwadanganya walio wengi kwamba rais alifanya ziara maalum, kumbe kutembelea zile wodi ilikuwa ni by the way
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom