Inawezekana Magufuli sio tatizo?

Inawezekana Magufuli sio tatizo?

Tunapenda kujenga MLIMA mahali ambapo panatakiwa kuwa KICHUGUU.Wakati wote ule alikuwa anatengeneza PR tu hakuna cha maana alichofanya.Vitanda havikuwa vya wadi za kawaida bali jengo lwa wagonjwa maalum la MOI.

Waandishi wetu nao wanatakiwa kuchapwa viboko tu.Tena gazeti la UHURU ndiyo kabisa.Kama Muhariri wa Gazeti la uhuru anagekuwa na nafasi nzuri ya kuandika matatizo ya serikali ili kuweza kuboresha utendaji serikalini.LAkini wako kama maboya ya maji machafu
 
Tatizo hapa nchini kwetu tumekua waoga kiasi cha kupitiliza mpaka vyombo vya habari uandika propaganda kwa wingi kumbe laghasha
 
Leo ukifuatilia taarifa ya habari Magufuli katembelea tena Muhimbili kwa kustukiza
kakuta matatizo tele hasa amewakuta wamama waki share vitanda hadi watu watano
na wengine wakilala chini.....

Utakumbuka few months ago tulitangaziwa kuwa baada ya Magufuli kwenda Muhimbili
vitanda vilipelekwa hadi vikakosa wagonjwa
kuna picha zilisambazwa paka kalalia kitanda kipya Muhimbili
na kwamba sasa mambo ni tofauti kabisa...vitanda tele na kila kitu saafi

Sasa binafsi siamini kabisa Muhimbili imewahi kuwa safi na matatizo yakaisha
ambacho najiuliza why 'maigizo yale ya kuwa mambo ni saafi' yaliruhusiwa
kuendelea ?

why sisi wananchi na waandishi wa habari hatukupinga kabisa habari za kuwa
mambo ni saafi muhimbili?
why habari ya leo iwe kama habari mpya
while in reality watu wameendelea kulala chini tu kama zamani?

Inawezekana kabisa tatizo haliko kwa wanasiasa?

tatizo liko kwetu wananchi na hasa media?
tumeletewa 'sanaa tukaishangilia huku ukweli tunaujua'?
sababu muhimbili hali yake sio siri
lakini tulipoambiwa mambo sasa ni saafi tuliruka ruka na kushangilia...
huku kiukweli hali ni ile ile tu.....

Na leo tena wananchi wamemlilia tena Magufuli bila kujiuliza
ni kweli Magufuli hali iliyopo haijui?si alikwenda juzi tu hapo hapo Muhimbili?
au haya matatizo ni mapya kabisa?
ME.naisi labda msimu wa wagonjwa umeaanza.sasa ikiwa wamejaa dah.hivi me sijui lakini hakuna maeneo pale tukaongeza wold.maana zile naisi toka jk.wa kwanza
 
The Boss, samahani sana naomba ruhusa nitoe summary ya michango iliyotolewa na watetezi wa hapa kazi tu kuhusu hali ya Hospitali Kuu ya Muhimbili. Kwa sasa hawa ndio wanawakilisha think tank ya status quo ambayo ilimwezesha Magufuli kuingia madarakani na hivi sasa naambiwa kuna mpango wa kuwapa tuzo. Haya tuendelee...

  1. Nkasumuni: Muhimbili ilijengwa na mkoloni. population sasa ni kubwa kwa secta ya afya na miundombinu yake hata ukifanya nini idadi ya watu haitapungua.
  2. Eli79: Naamini tatizo sio muhimbili kama taasisi, tatizo kubwa ni population ya wakazi wa Dar ukilinganisha na idadi ya hospitali zilizopo. Kama jiji lilikuwa designed kwa wakazi 2m na leo lina zaidi ya mara mbili ya watu, usitegemee kuwa kuna miundombinu itakayostahamili, sio barabara, maji wala afya.
  3. Barbarosa: Tatizo la Wagonjwa kushirikiana vitanda halisababishwi na uhaba wa vitanda, bali linasababishwa na uwingi wa wagonjwa na nafasi ni ndogo hivyo hakuna kitu Muhimbili wanaweza kufanya kwa maana hakuna nafasi sasa vitanda wataviweka wapi? Vitanda siyo tatizo tena hilo lilishatatuliwa na viko vya kutosha tu ila tatizo ni nafasi utaviweka wapi?
  4. Ruttashobolwa: Vitanda vilinunuliwa kwa ajili ya ward ya kawaida haikuwa ya wazazi...kwa hiyo swala la ward ya wazazi ni case mpya ambayo inahitaji ufumbuzi!
  5. Queen Esther: ili kuweka kumbukumbu vizuri. Vile vitanda vilitolewa general ward. Hapo mtu Wa kwanza kuwajibika ni Head Wa idara husika, mgt ya Muhimbili na wizara husika. Pia hivi kujifungua tuu mtu hana shida kwanini anaenda referees hosp Muhimbili?? Hawa madaktari husika nao napata shida kidogo.
  6. Barbarosa: Hilo siyo suluhisho la matatizo ya TanZania hata kama Serikali ikihamia Dom bado idadi ya watu itaendela kuongezeka Dar kwa maana Dar ndiyo mji tajiri TZ na utabakia kuwa hivyo, suluhisho hapa ni population control basi, hakuna lingine ni lazima Serikali ije na mpango wa kudhibiti uzaaji hovyo wa bila mpango!
  7. Judy wa Kishua: Kuna vingi vimefanyika hapo Muhimbili ila wenye nongwa wamesubiri kuona mapungufu ndio waje kuporomosha lawama kama kawaida yao ila likifanyika zuri hautakaa uwaone wakipongeza na pia awapendi kuona tunaappreciate chochote kizuri toka kwa Magufuli.
  8. donbeny: Muhimbili ni kubwa sana,ni ukweli kuwa vitanda vilipelekwa kwa amri ya raisi ila ile ilikuwa wodi ya Wagonjwa wa Moi, na Moi ina wodi mpya ndiyo iliyopelekewa vitanda vipya na wagonjwa waliolala chini wakahamishwa kwenye vitanda vipya. Wodi ya wazazi ya jana nayo ni jengo la zamani kidogo ila wagonjwa wamekuwa wengi kadiri miaka inavyoenda na kuna upungufu wa vitanda.
  9. Barbarosa (akikana picha iliyopigwa jana): Wewe hauna akili kwanza hiyo picha ni ya lini? Hiyo picha ni kabla ya Utawala wa Raisi Magufuli, sasa nakupa changamoto kapige picha kama hiyo kwenye Hospitali hapa Dar halafu ulete tena!
  10. Barbarosa: lazima Uchumi wetu ukuwe kuzidi ongezeko la watu ili ilete maana na hili kwa hali ya kawaida na ngumu hakuna nchi waliowahi kufanikiwa na ndiyo njia pekee ni kupunguza ongezeko la watu kwa mfano iwekwe utaratibu mwisho watoto wawili ambao Serikali inawalipia kila kitu na kila mtoto wa tatu au nne unamlipia mwenyewe na kodi unayokatwa inaongezeka hii itasaidia vinginevyo hakuna kitu tutafanya!
  11. Phillipo Bukililo: Tatizo letu Watanzania ni kufikiri kwamba kuna mtu fulani sehemu fulani mwenye wajibu wa kuyashughulikia matatizo yetu kwa mapana yake!. Serikali ni mimi na wewe, ni wewe na yule, ni kila mtu. Anatazamwa Magufuli na wasaidizi wake kama vile ni watu wametoka sayari nyingine kuja kutuondolea maelfu ya matatizo yetu. Kila mtu atambue kuwa yeye ni serikali.
  12. twahil: Mkuu hao vijana wasikuumize kichwa...luwasa ameishatangaza kuwania urais 2020 sasa wameishaanza kampeni hao...ila wasichojua ni kuwa wanapambana na kivuli chao...Magufuli ni namba nyingine. Ni aibu kuona kampeni ndio zimeisha ila watu wanaendeleza siasa badala ya kazi...ukiona hivyo jua watu hao hawako sawa yaani ni punguani....
  13. Barbarosa: nchi zilizoendelea wote wanafanya population control sema mbinu tu ndiyo tofauti kwa mfano nchi tajiri zote watoto wa kike hupewa birth control pills au vidonge vya kuzuia ujazito sasa maana yake nini? Ukiangalia hiyo picha hapo chini utaona ninachoongelea, wapo wengi kama wangekuwa na vidonge vya kuzuia kupata mimba wengi wao wasingeamua kupata mimba!
  14. ...
The Boss, sidhani kama kuna haja ya kuendelea zaidi, huu ni mfano halisi wa jamvi letu pendwa lilivyoshuka hadhi na taswira ya tunakoelekea. Fikiria jibu unaloweza kuwapa hao watu wa aina hii hapo juu likatosheleza, hakuna. Hawa si wa kukimbizana nao, unaweza kuta watu wanashindwa kuona tofauti kati yako na wao. Hawa ndio wamemwagwa mtandaoni eti kuitetea serikali ya Magufuli na kwa majibu wanayoyatoa unaweza kuona taifa linakoelekea.
 
The Boss, samahani sana naomba ruhusa nitoe summary ya michango iliyotolewa na watetezi wa hapa kazi tu kuhusu hali ya Hospitali Kuu ya Muhimbili. Kwa sasa hawa ndio wanawakilisha think tank ya status quo ambayo ilimwezesha Magufuli kuingia madarakani na hivi sasa naambiwa kuna mpango wa kuwapa tuzo. Haya tuendelee...

  1. Nkasumuni: Muhimbili ilijengwa na mkoloni. population sasa ni kubwa kwa secta ya afya na miundombinu yake hata ukifanya nini idadi ya watu haitapungua.
  2. Eli79: Naamini tatizo sio muhimbili kama taasisi, tatizo kubwa ni population ya wakazi wa Dar ukilinganisha na idadi ya hospitali zilizopo. Kama jiji lilikuwa designed kwa wakazi 2m na leo lina zaidi ya mara mbili ya watu, usitegemee kuwa kuna miundombinu itakayostahamili, sio barabara, maji wala afya.
  3. Barbarosa: Tatizo la Wagonjwa kushirikiana vitanda halisababishwi na uhaba wa vitanda, bali linasababishwa na uwingi wa wagonjwa na nafasi ni ndogo hivyo hakuna kitu Muhimbili wanaweza kufanya kwa maana hakuna nafasi sasa vitanda wataviweka wapi? Vitanda siyo tatizo tena hilo lilishatatuliwa na viko vya kutosha tu ila tatizo ni nafasi utaviweka wapi?
  4. Ruttashobolwa: Vitanda vilinunuliwa kwa ajili ya ward ya kawaida haikuwa ya wazazi...kwa hiyo swala la ward ya wazazi ni case mpya ambayo inahitaji ufumbuzi!
  5. Queen Esther: ili kuweka kumbukumbu vizuri. Vile vitanda vilitolewa general ward. Hapo mtu Wa kwanza kuwajibika ni Head Wa idara husika, mgt ya Muhimbili na wizara husika. Pia hivi kujifungua tuu mtu hana shida kwanini anaenda referees hosp Muhimbili?? Hawa madaktari husika nao napata shida kidogo.
  6. Barbarosa: Hilo siyo suluhisho la matatizo ya TanZania hata kama Serikali ikihamia Dom bado idadi ya watu itaendela kuongezeka Dar kwa maana Dar ndiyo mji tajiri TZ na utabakia kuwa hivyo, suluhisho hapa ni population control basi, hakuna lingine ni lazima Serikali ije na mpango wa kudhibiti uzaaji hovyo wa bila mpango!
  7. Judy wa Kishua: Kuna vingi vimefanyika hapo Muhimbili ila wenye nongwa wamesubiri kuona mapungufu ndio waje kuporomosha lawama kama kawaida yao ila likifanyika zuri hautakaa uwaone wakipongeza na pia awapendi kuona tunaappreciate chochote kizuri toka kwa Magufuli.
  8. donbeny: Muhimbili ni kubwa sana,ni ukweli kuwa vitanda vilipelekwa kwa amri ya raisi ila ile ilikuwa wodi ya Wagonjwa wa Moi, na Moi ina wodi mpya ndiyo iliyopelekewa vitanda vipya na wagonjwa waliolala chini wakahamishwa kwenye vitanda vipya. Wodi ya wazazi ya jana nayo ni jengo la zamani kidogo ila wagonjwa wamekuwa wengi kadiri miaka inavyoenda na kuna upungufu wa vitanda.
  9. Barbarosa (akikana picha iliyopigwa jana): Wewe hauna akili kwanza hiyo picha ni ya lini? Hiyo picha ni kabla ya Utawala wa Raisi Magufuli, sasa nakupa changamoto kapige picha kama hiyo kwenye Hospitali hapa Dar halafu ulete tena!
  10. Barbarosa: lazima Uchumi wetu ukuwe kuzidi ongezeko la watu ili ilete maana na hili kwa hali ya kawaida na ngumu hakuna nchi waliowahi kufanikiwa na ndiyo njia pekee ni kupunguza ongezeko la watu kwa mfano iwekwe utaratibu mwisho watoto wawili ambao Serikali inawalipia kila kitu na kila mtoto wa tatu au nne unamlipia mwenyewe na kodi unayokatwa inaongezeka hii itasaidia vinginevyo hakuna kitu tutafanya!
  11. Phillipo Bukililo: Tatizo letu Watanzania ni kufikiri kwamba kuna mtu fulani sehemu fulani mwenye wajibu wa kuyashughulikia matatizo yetu kwa mapana yake!. Serikali ni mimi na wewe, ni wewe na yule, ni kila mtu. Anatazamwa Magufuli na wasaidizi wake kama vile ni watu wametoka sayari nyingine kuja kutuondolea maelfu ya matatizo yetu. Kila mtu atambue kuwa yeye ni serikali.
  12. twahil: Mkuu hao vijana wasikuumize kichwa...luwasa ameishatangaza kuwania urais 2020 sasa wameishaanza kampeni hao...ila wasichojua ni kuwa wanapambana na kivuli chao...Magufuli ni namba nyingine. Ni aibu kuona kampeni ndio zimeisha ila watu wanaendeleza siasa badala ya kazi...ukiona hivyo jua watu hao hawako sawa yaani ni punguani....
  13. Barbarosa: nchi zilizoendelea wote wanafanya population control sema mbinu tu ndiyo tofauti kwa mfano nchi tajiri zote watoto wa kike hupewa birth control pills au vidonge vya kuzuia ujazito sasa maana yake nini? Ukiangalia hiyo picha hapo chini utaona ninachoongelea, wapo wengi kama wangekuwa na vidonge vya kuzuia kupata mimba wengi wao wasingeamua kupata mimba!
  14. ...
The Boss, sidhani kama kuna haja ya kuendelea zaidi, huu ni mfano halisi wa jamvi letu pendwa lilivyoshuka hadhi na taswira ya tunakoelekea. Fikiria jibu unaloweza kuwapa hao watu wa aina hii hapo juu likatosheleza, hakuna. Hawa si wa kukimbizana nao, unaweza kuta watu wanashindwa kuona tofauti kati yako na wao. Hawa ndio wamemwagwa mtandaoni eti kuitetea serikali ya Magufuli na kwa majibu wanayoyatoa unaweza kuona taifa linakoelekea.


Kwa mwendo huu very soon utawala wa JK utaanza kuonekana ulikuwa na ma genius watupu..
tunazidi kushuka na kushuka hata kwenye 'viwango vya porojo' tu achilia mbali serious issues...
 
kinachotuumiza tanzania ni kuendekeza usiasa watu bado wapo kwenye kampeni ila wamesahau muda unasonga watakapo jitambua watakosa la kuwaambia watanzania haiwezekani muhimbili muhimbili rais akikaa ikulu ataenda muhimbili na waandishi wa habari kibao kwenda kushitukiza sasa me binafsi sielewi anaenda ku record au kushitukiza na mambo yalivyo kuigizana utasikia naibu waziri amepiga suti mpya anaenda kushitukiza na na waandishi wa habari fuso mbili

Acha mbwembwe Raisi alienda kusalimia na kumjulia Hali Yule shehe na sio swala kwamba alienda kustukiza. Kina mama ndio waliomzoazoa njiani na kumpeleka wodini ashuhudie aliyoyaona. Acheni ushabili.
 


Tatizo la Wagonjwa kushirikiana vitanda halisababishwi na uhaba wa vitanda, bali linasababishwa na uwingi wa wagonjwa na nafasi ni ndogo hivyo hakuna kitu Muhimbili wanaweza kufanya kwa maana hakuna nafasi sasa vitanda wataviweka wapi?

Changamoto kwenye sekta ya Afya kama kulivyo sehemu nyingine bado ni kubwa sana, ni lazima kwanza Hospitali zetu za Wilaya kama Amana, Temeke, Mwananyamala zote ziboreshwe na pia kujengwa nyingine zitakazoendana na idadi ya wakazi wa Dar, kumbuka Hospitali zote Dar zimejengwa wakati Dar ikiwa na wakazi chini ya milioni Moja leo hii tuko zaidi ya milioni 4.5 na kila mama anapata wastani wa watoto 2.6 Tanzania ambayo ni kasi kubwa sana!
Rejea taarifa tulizopewa kuwa vitanda vilipelekwa muhimbili hadi vikazidi wagonjwa! Inakuwaje leo ndani ya miezi2 watu wanalala chini!,jibu ni kwamba zile hazikuwa taarifa za kweli na nchi haiwezi kuendeshwa kwa propaganda na vigeregere hakuna zaidi
 
Kwa mwendo huu very soon utawala wa JK utaanza kuonekana ulikuwa na ma genius watupu..
tunazidi kushuka na kushuka hata kwenye 'viwango vya porojo' tu achilia mbali serious issues...
Eti kwa miaka 20 aliyokuwa serikalini akiwa Waziri, Magufuli alijua hadi idadi ya samaki Tanzania lakini hakuwa na habari kuwa huko Muhimbili wagonjwa wanalala sakafuni...Believe this and you'll believe anything (thanks to James Hadley Chase)
 
Rejea taarifa tulizopewa kuwa vitanda vilipelekwa muhimbili hadi vikazidi wagonjwa! Inakuwaje leo ndani ya miezi2 watu wanalala chini!,jibu ni kwamba zile hazikuwa taarifa za kweli na nchi haiwezi kuendeshwa kwa propaganda na vigeregere hakuna zaidi


Wewe ninani mpaka usema taarifa hazikuwa za kweli? Unafikiri wanaweza kumdanganya Raisi kijinga namna hiyo? Miezi 2 kwa Muhimbili ni mingi sana, kwa maana unaweza kusema ndiyo Hospitali pekee inayotegemewa na watu zaidi ya milioni 40, kila anayeugua TZ hii anakwenda Muhimbili!

Raisi alivyokwenda Muhimbili mara ya kwanza wagonjwa walikuwa wanalala chini kwa sababu hawakuwa na vitanda aidha vilikuwa vimeharibika au hakuna kabisa na baadaye vikanunuliwa wakapewa lkn idadi ya wagonjwa inaendelea kuongeza siku hadi siku hivyo vitanda vipo vingi tu lkn hakuna pa kuviweka kwa maana nafasi hakuna, na ndiyo maana wagonjwa wanalala wawili!

Hivyo tumieni akili kidogo wkt mwingine kwenye kukosoa, Dar Hosp. za Wilaya zote kama Amana, M'la, Temeke ziko hoi, hivyo mama mja mzito wa Mbagala badala ya kwenda Temeke anakwenda Muhimbili kila anayevunjika mfupa anakwenda Muhimbili na hiyo ni kwa TanZania nzima, sasa hawo wagonjwa wote watawekwa wapi?

Jikite kwenye mambo positive zaidi na hata kama unakosoa jaribu kuwa mkweli na kutumia akili hili litasaidia nchi kwa ujumla badala ya kukaa kama mchawi na kusubiri serikali imekosea wapi na ili uanze kukosoa huko ni kukosa akili na dhambi pia!
 
Leo ukifuatilia taarifa ya habari Magufuli katembelea tena Muhimbili kwa kustukiza
kakuta matatizo tele hasa amewakuta wamama waki share vitanda hadi watu watano
na wengine wakilala chini.....

Utakumbuka few months ago tulitangaziwa kuwa baada ya Magufuli kwenda Muhimbili
vitanda vilipelekwa hadi vikakosa wagonjwa
kuna picha zilisambazwa paka kalalia kitanda kipya Muhimbili
na kwamba sasa mambo ni tofauti kabisa...vitanda tele na kila kitu saafi

Sasa binafsi siamini kabisa Muhimbili imewahi kuwa safi na matatizo yakaisha
ambacho najiuliza why 'maigizo yale ya kuwa mambo ni saafi' yaliruhusiwa
kuendelea ?

why sisi wananchi na waandishi wa habari hatukupinga kabisa habari za kuwa
mambo ni saafi muhimbili?
why habari ya leo iwe kama habari mpya
while in reality watu wameendelea kulala chini tu kama zamani?

Inawezekana kabisa tatizo haliko kwa wanasiasa?

tatizo liko kwetu wananchi na hasa media?
tumeletewa 'sanaa tukaishangilia huku ukweli tunaujua'?
sababu muhimbili hali yake sio siri
lakini tulipoambiwa mambo sasa ni saafi tuliruka ruka na kushangilia...
huku kiukweli hali ni ile ile tu.....

Na leo tena wananchi wamemlilia tena Magufuli bila kujiuliza
ni kweli Magufuli hali iliyopo haijui?si alikwenda juzi tu hapo hapo Muhimbili?
au haya matatizo ni mapya kabisa?

We mwenyewe hapa kwa makusudi unatupiga kamba na inaonekana hujajua tatizo nini, andiko linajichanganya mara wana changia kitanda wamama 5 mara wanalala chini kwanini tatizo liko kwako kwamba hisia zako Zaidi zinakuendesha bila kutazama ukweli halisi. JPM sio Mungu na hata Mungu yote haya anayajua na ameyaacha kwa makusudi, ukumbuke demand imeongezeka sana baada ya taarifa zile za mwanzo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom