Inawezekana Magufuli sio tatizo?

Inawezekana Magufuli sio tatizo?

viongozi wamefikia mwisho wa kufikiri. wao wanaamini kila kitu ni Dar. Hamoshia serekali dodoma utaona jinsi gani jiji litaacha nafasi. ukiuliza kisa cha kitokuhamoa dodoma kwa serekali hakuna bali ni porojo tu


Hilo siyo suluhisho la matatizo ya TanZania hata kama Serikali ikihamia Dom bado idadi ya watu itaendela kuongezeka Dar kwa maana Dar ndiyo mji tajiri TZ na utabakia kuwa hivyo, suluhisho hapa ni population control basi, hakuna lingine ni lazima Serikali ije mpango wa kudhibiti uzaaji hovyo wa bila mpango!
 
Tatizo kubwa ni Media ambayo ilichukua hili swala kwa utashi wa kutaka kuuza (kasi ya awamu mpya) wakati wakitoa matumaini hewa kwa wananchi."Muhimbili ile ileee "..sababu hata CT scan iliyoletwa kumbe ilikuwa ni ya Morogoro wamefanya kuhamisha tu.


masahihisho kidogo mkuu. Ile CT Scan ilikuwa ni ya kutoka dodoma UDOM!
 
Leo alikuwa mpole
kasema amejifunza atayabeba ayafanyie kazi
utasema leo ndo mara ya kwanza anakwenda Muhimbili....
Hahahaha aisee.... siasa bhana. Tangu awe rais hii nadhani ni mara ya nne anaenda Muhimbili. Ngoja aendelee kujifunza.... labda atafanya kazi ya waziri wa afya.
 
Leo alikuwa mpole
kasema amejifunza atayabeba ayafanyie kazi
utasema leo ndo mara ya kwanza anakwenda Muhimbili....

Siku ile hakujifunza?

Halafu, hivi kweli alikuwa hajui matatizo ya sekta yetu ya afya?

Ina maana yeye huko nyuma hakuwahi kabisa kuona wagonjwa wakilala chini, iwe kwenye picha au kwa macho yake mwenyewe?

Mbona mimi tokea nikiwa mdogo nimekuwa nikiona?

Hata watoto kukaa chini nimeshaona mara nyingi tu na wala sihitaji kuona picha kwenye mtandao ndo nijui kuwa kuna hilo tatizo.

Hawa viongozi wetu wao wanaishi nchi gani kwani?
 
Kama wewe ni mzalendo utakubaliana nami Muhimbili kuna shida ya ki uongozi zaidi ya tunavyofikiri. Pia baada ya Mhe. Rais kumaliza awamu ya kwanza ilibaki waziri na timu yake kujipanga!!!!

Nimemkumbuka Ag. CEO Dr. Kidantu na issue ya ST SCAN mashine na mbwembwe za mstaafu Prof Museru!!!

Pia nikusaidie uweke kumbukumbu vizuri. Vile vitanda vilitolewa general ward. Hapo mtu Wa kwanza kuwajibika ni Head Wa idara husika, mgt ya Muhimbili na waizara husika.

Pia hivi kujifungua tuu mtu hana shida kwanini anaenda referees hosp Muhimbili?? Hawa madaktari husika nao napata shida kidogo.

Queen Esther
Taire ! taire! QE. Ahsante, maana tulipoonyesha hayo unayosema ulisimama kidete ukitukejeli , kuturushia madongo. Leo tunakukaribisha upande wetu.

Tunataka kuona kesho asubuhi #Hapakazi wahusika wanafutika kama alivyoondoka na mkurugenzi
Tumeeleza sana hili kuhusu mkurugenzi aliyeondolewa na ukubwa tatizo! Nkumbuka tukaambi vijeba na vijiba vya roho

Ukweli kitu kizuri sana, utakuweka huru popote pale . The Boss Nyani Ngabu

Mpe salam mpwa wangu Judi wa Kishua , mwambi aje jamvini tutete ya nchi.
 
Siku ile hakujifunza?

Halafu, hivi kweli alikuwa hajui matatizo ya sekta yetu ya afya?

Ina maana yeye huko nyuma hakuwahi kabisa kuona wagonjwa wakilala chini, iwe kwenye picha au kwa macho yake mwenyewe?

Mbona mimi tokea nikiwa mdogo nimekuwa nikiona?

Hata watoto kukaa chini nimeshaona mara nyingi tu na wala sihitaji kuona picha kwenye mtandao ndo nijui kuwa kuna hilo tatizo.

Hawa viongozi wetu wao wanaishi nchi gani kwani?


Naona wananchi pia washaanza kuchoka na sinema hizi
watu hawajadili sana tena ziara hizi....
manake hii ya leo inachosha hata kujadili
 
Hilo siyo suluhisho la matatizo ya TanZania hata kama Serikali ikihamia Dom bado idadi ya watu itaendela kuongezeka Dar kwa maana Dar ndiyo mji tajiri TZ na utabakia kuwa hivyo, suluhisho hapa ni population control basi, hakuna lingine ni lazima Serikali ije mpango wa kudhibiti uzaaji hovyo wa bila mpango!

Hili jambo halihusiani na population control kabisa
kuna thread niliwahi weka hapa nikiuliza idadi ya madaktari Muhimbili
kulinganisha na nchi nzima
wagonjwa wa muhimbili asilimia 70 wanatoka mikoani
serikali ilipaswa kuweka hospitali kubwa kama muhimbili
mikoa kama Dodoma na Mbeya...na na idadi ya madaktari na vipimo vya kutosha
watapunguza wagonjwa muhimbili kwa asilimia 70...

Na mikoa ya Moro na Pwani nayo wawe na hospitali yao ya rufaa
Muhimbili iwe kwa wakazi wa Dar tu....hawakuwa na wagonjwa wa kulala chini..
muhimbili ni sawa na bandari na ni sawa na Airport
nchi nzima inahudumiwa pale
 
Wengine tulishasema hakuna jipya...ni more of the same.

Hivi hujawahi kuona baadhi ya hao viongozi wetu wakienda sehemu ati kuona na kujifunza kuhusu shida na matatizo yanayowakabili Watanzania?

Hivi kweli mtu anaweza kuamini kwamba huyo Magufuli alikuwa hajui matatizo yanayoikabili hiyo hospitali ya taifa na sekta ya afya kwa ujumla?

Hii hali ya wagonjwa kulala chini mbona sioni kilicho kipya.

Kuna picha nyingi tu miaka iliyopita ambazo zimekuwa zikizunguka kwenye mitandao zikionyesha hali halisi ya hospitali zetu.

Na kusema ukweli wala mtu huhitaji kuona picha ndo ushtuke kwamba kumbe kuna watu huwa wanalala chini mahospitalini.

Nenda tu mwenyewe hospitali na utajionea hilo.

Mimi mara kibao nimeshaona wagonjwa wakilala chini kwenye hospitali ya Somanda, Bariadi na hospitali ya mkoa wa Shinyanga.

Nakumbuka marehemu mzee wangu mwaka 1996 alipatwa na dharura ndogo akaenda Muhimbili na wakamlaza chini.

So what is new here?
Nothing new,ila kesho tena atarudi ataahidi yale yale na atashangiliwa na akitoka hapo myb atekeleze robo ama asitekeleze kabisa, kusubiri muda mwingine wa kampeni atumie mwanya huo.
 
K
Taire ! taire! QE. Ahsante, maana tulipoonyesha hayo unayosema ulisimama kidete ukitukejeli , kuturushia madongo. Leo tunakukaribisha upande wetu.

Tunataka kuona kesho asubuhi #Hapakazi wahusika wanafutika kama alivyoondoka na mkurugenzi
Tumeeleza sana hili kuhusu mkurugenzi aliyeondolewa na ukubwa tatizo! Nkumbuka tukaambi vijeba na vijiba vya roho

Ukweli kitu kizuri sana, utakuweka huru popote pale . The Boss Nyani Ngabu

Mpe salam mpwa wangu Judi wa Kishua , mwambi aje jamvini tutete ya nchi.


Kikwete anataka kina Ester na wenzie walipwe
sasa nguvu kubwa na focus ya CCM na serikali yake
ni kuwa na watu wa kuitetea mitandaoni kuliko
kutazama namna ya ku fix matatizo for good....
 
Wewe unatujua Wabongo kwa Munyu!!!???? Tutumie Logic tu wala haitakiwi Uwe rocket scientist pale kwenye kitanda cha Hospitali wakinamama watano wenye ujauzito wanatoshaje mkuu!!!???? I mean seriously!!

Hivi hukuona
Taire ! taire! QE. Ahsante, maana tulipoonyesha hayo unayosema ulisimama kidete ukitukejeli , kuturushia madongo. Leo tunakukaribisha upande wetu.

Tunataka kuona kesho asubuhi #Hapakazi wahusika wanafutika kama alivyoondoka na mkurugenzi
Tumeeleza sana hili kuhusu mkurugenzi aliyeondolewa na ukubwa tatizo! Nkumbuka tukaambi vijeba na vijiba vya roho

Ukweli kitu kizuri sana, utakuweka huru popote pale . The Boss Nyani Ngabu

Mpe salam mpwa wangu Judi wa Kishua , mwambi aje jamvini tutete ya nchi.


hivi kweli kumbe hawa wanahitaji maombi!
 
Nothing new,ila kesho tena atarudi ataahidi yale yale na atashangiliwa na akitoka hapo myb atekeleze robo ama asitekeleze kabisa, kusubiri muda mwingine wa kampeni atumie mwanya huo.

Sasa ngoja tusubiri tuone Ummy na Hamisi [Kigwangalla] watafanya nini kesho.
 
Sasa ngoja tusubiri tuone Ummy na Hamisi [Kigwangalla] watafanya nini kesho.

Si ajabu wakamfukuza mtu kesho
mimi nimegundua kuwa yawezekana kabisa
watu ambao wanaweza kuwa msaada na nchii hii wako mitaani tu
wanahangaika..with plenty to offer...
ila wale ambao wako so empty ndo wako incharge...
 
Mimi nafikiri kwa kuwa Serikali ss inakusanya kodi ya nguvu bas watenge bajeti kujenga hosp zingine kama Muhimbili kila Wilaya zikiwemo Wilaya mpya za mkoa wa Dar na pia maeneo hayo yawe nje ya mji lkn karibu na wananchi mfano Kigamboni,Mbezi juu,Ukonga,Bunju na Mbagala problem solved,na itapunguza hata foleni barabarani.
 
Kigwangala kesho atawahi asubuhi kufungia wachelewaji nje pale muhimbili badala ya kutafuta vitanda.
 
Hili jambo halihusiani na population control kabisa
kuna thread niliwahi weka hapa nikiuliza idadi ya madaktari Muhimbili
kulinganisha na nchi nzima
wagonjwa wa muhimbili asilimia 70 wanatoka mikoani
serikali ilipaswa kuweka hospitali kubwa kama muhimbili
mikoa kama Dodoma na Mbeya...na na idadi ya madaktari na vipimo vya kutosha
watapunguza wagonjwa muhimbili kwa asilimia 70...

Na mikoa ya Moro na Pwani nayo wawe na hospitali yao ya rufaa
Muhimbili iwe kwa wakazi wa Dar tu....hawakuwa na wagonjwa wa kulala chini..
muhimbili ni sawa na bandari na ni sawa na Airport
nchi nzima inahudumiwa pale


Ninaposema population control namaanishwa kwamba ongezeko la watu nchini mwetu ni kubwa sana na haliendani na ukuwaji wa uchumi wetu hivyo hakuna kitu tunafanya ni kama uwe na watoto 2 una mshara wa laki tano halafu unaongeza watoto wawili tena na mshahra unaongezeka mpaka laki tano na nusu tu ni dhahiri kwamba utakuwa na mapungufu ya karibia kila kitu kwenye familia yako ukilinganisha na ulivyokuwa na watoto 2 tu!

Na ndicho kinachotokea TZ, hizo Hospitali za Rufaa za Mikoani unazoziongelea utazijenga na nini? Unahitaji kwanza ukuaji wa uchumi ili uweze kuwa na fedha ya kuzijenga, sasa maadamu kila mwanamke Tanzania anapata wastani wa 2.6 na uchumi wetu unakuwa kwa asilimia 6 - 7 tu hatuwezi kufanya hayo yote ni lazima Uchumi wetu ukuwe kuzidi ongezeko la watu ili ilete maana na hili kwa hali ya kawaida na ngumu hakuna nchi waliowahi kufanikiwa na ndiyo njia pekee ni kupunguza ongezeko la watu kwa mfano iwekwe utaratibu mwisho watoto wawili ambao Serikali inawalipia kila kitu na kila mtoto wa tatu au nne unamlipia mwenyewe na kodi unayokatwa inaongezeka hii itasaidia vinginevyo hakuna kitu tutafanya!
 
Au...sitashangaa kabisa kama yeye huyo Kigwangala akienda hapo Muhimbili na kulala chini usiku mzima ili kujifunza tabu wazipatazo wananchi walio wagonjwa.

Hahaa haki ya Mungu nimecheka kwa sauti....
 
Hakuna kitu Muhimbili watafanya, hakuna nafasi wamezidiwa na wagonjwa sasa hivyo vitanda wataviweka wapi? Hilo ndiyo swali!
Imefika wakati sasa tuanze kuliangalia swala la ongezeko la watu , tunazaliana sana matokeo yake ndiyo hayo kila huduma hazitoshi!
Hebu rudia tena kusoma ulichoandika, kama hutajionea aibu, basi akili zako haziko sawa!
 
Back
Top Bottom