Salaam,
Kama mtakumbuka eneo la stand ya Mwenge ambapo ni maarufu wakati ule kwa wamachinga palivunjwa kwa lengo la kufanyia maboresho.
Sasa kilichotokea, inasemekana Mnada kwa wale yale mabanda mapya umefanyika Usiku wa kuamkia Jana na GSM amepata zaidi ya nusu ya mabanda ya Stand.
Kama ni kweli, hii sio haki kabisa kwa watu wa pale na walikuwa na uwezo wa kushinda mnada.
NB: kama ni kweli, sidhani kama Rais ataenda kuzindua kwa kuwa ilitegemewa iwe hivyo.
=====
Ufafanuzi kutoka Manispaa ya Kinondoni kuhusu upangishaji wa fremu Mwenge kutoka kwa Akwilinus Shiduki Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Manispaa ya kinondoni na Shedrack Mbonika Afisa uwekezaji Manispaa
Akwilinus Shiduki amesema;
Upangishaji umekwenda hatua kwa hatua kwa kutangaza kwa wafanyabiashara au wananchi wenye nia ya kupanga katika eneo la Mwenge wajisajiri katika mfumo wa Tausi TAMISEMI na muda utakapofika (tar 18 Oktoba) mchakato wa kuanza kuomba kupitia mfumo wa mnada wa mtandao utaendelea. Akiongeza pia, tangazo lilitoka kuanzia mwezi wa 6 kusambaza taarifa hizi.
Akiongeza juu suala hilo Bwana Shedrack Mbonika amesema kuwa mchakato umeanza na hatua inayoendelea sasa ni kujisajiri pekee huku wakisubiri hatua nyingine kufuata, ambapo tar. 18 Oktoba ndio hatua nyingine inaanza kwa watu kuanza kuingia kwenye mnada na kushinda kwa kupata fremu husika, na kwamba si kweli kuwa kuna watu wameshagawiwa fremu hizo kabla ya mnada kuanza.
Ameendelea kuwa, kuna jumla ya vyumba 148 vikiwa kwenye sakafu 3 vilivyogawanywa kwenye minada ya aina mbili. Mnada wa kwanza ni mnada wa wazi (open auction) ambao utakuwa na vyumba 39 kwaajili ya biashara mchanganyiko na vyumba vilivyosalia vitatolewa kwenye mnada fungwa (closed auction) uliofungwa kwaajili ya watu wanaotoa huduma mahususi mfano huduma za kibenki, dawa nk.
Akieleza kuhusu wafanyabiashara waliopisha ujenzi huo kuahidiwa kupewa kipaumbele, Bwana Shedrack amesema; waliopisha ujenzi ni wafanyabiashara 1500 ambao hawaendani na uwiano wa soko, namna pekee ya mtu kupata fremu ni kwa njia ya ushindani, na kwa atakayekosa fame hizo bado Halmashauri imewazingatia kwa kutengeneza mradi pembezoni na mradi wa stendi Mwenge, kwa kutengeneza soko la wamachinga upande wa Coca Cola kwa kuweka ruti ya daladala, vyoo vya kisasa na vibanda vinavyoweza kuhimili wafanyakazi 1,000 kwa wakati mmoja.
Na kwa ambaye haelewi mfumo huu unavyofanya kazi wanakaribishwa kwenda kupatiwa elimu juu ya mfumo huu katika katika vituo vyao 6 vilivyopo Bunju, Kibo-Tegeta, Mwenge, Mikocheni pamoja na Namanga.
Kama mtakumbuka eneo la stand ya Mwenge ambapo ni maarufu wakati ule kwa wamachinga palivunjwa kwa lengo la kufanyia maboresho.
Sasa kilichotokea, inasemekana Mnada kwa wale yale mabanda mapya umefanyika Usiku wa kuamkia Jana na GSM amepata zaidi ya nusu ya mabanda ya Stand.
Kama ni kweli, hii sio haki kabisa kwa watu wa pale na walikuwa na uwezo wa kushinda mnada.
NB: kama ni kweli, sidhani kama Rais ataenda kuzindua kwa kuwa ilitegemewa iwe hivyo.
=====
Ufafanuzi kutoka Manispaa ya Kinondoni kuhusu upangishaji wa fremu Mwenge kutoka kwa Akwilinus Shiduki Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Manispaa ya kinondoni na Shedrack Mbonika Afisa uwekezaji Manispaa
Akwilinus Shiduki amesema;
Upangishaji umekwenda hatua kwa hatua kwa kutangaza kwa wafanyabiashara au wananchi wenye nia ya kupanga katika eneo la Mwenge wajisajiri katika mfumo wa Tausi TAMISEMI na muda utakapofika (tar 18 Oktoba) mchakato wa kuanza kuomba kupitia mfumo wa mnada wa mtandao utaendelea. Akiongeza pia, tangazo lilitoka kuanzia mwezi wa 6 kusambaza taarifa hizi.
Akiongeza juu suala hilo Bwana Shedrack Mbonika amesema kuwa mchakato umeanza na hatua inayoendelea sasa ni kujisajiri pekee huku wakisubiri hatua nyingine kufuata, ambapo tar. 18 Oktoba ndio hatua nyingine inaanza kwa watu kuanza kuingia kwenye mnada na kushinda kwa kupata fremu husika, na kwamba si kweli kuwa kuna watu wameshagawiwa fremu hizo kabla ya mnada kuanza.
Ameendelea kuwa, kuna jumla ya vyumba 148 vikiwa kwenye sakafu 3 vilivyogawanywa kwenye minada ya aina mbili. Mnada wa kwanza ni mnada wa wazi (open auction) ambao utakuwa na vyumba 39 kwaajili ya biashara mchanganyiko na vyumba vilivyosalia vitatolewa kwenye mnada fungwa (closed auction) uliofungwa kwaajili ya watu wanaotoa huduma mahususi mfano huduma za kibenki, dawa nk.
Akieleza kuhusu wafanyabiashara waliopisha ujenzi huo kuahidiwa kupewa kipaumbele, Bwana Shedrack amesema; waliopisha ujenzi ni wafanyabiashara 1500 ambao hawaendani na uwiano wa soko, namna pekee ya mtu kupata fremu ni kwa njia ya ushindani, na kwa atakayekosa fame hizo bado Halmashauri imewazingatia kwa kutengeneza mradi pembezoni na mradi wa stendi Mwenge, kwa kutengeneza soko la wamachinga upande wa Coca Cola kwa kuweka ruti ya daladala, vyoo vya kisasa na vibanda vinavyoweza kuhimili wafanyakazi 1,000 kwa wakati mmoja.
Na kwa ambaye haelewi mfumo huu unavyofanya kazi wanakaribishwa kwenda kupatiwa elimu juu ya mfumo huu katika katika vituo vyao 6 vilivyopo Bunju, Kibo-Tegeta, Mwenge, Mikocheni pamoja na Namanga.