Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,183
..Natambua kwamba wasomaji wengi wamekuwa wakitoa maneno ya kejeli, matusi dhidi ya wale wote wanaojaribu kuonyesha kuwa Babu wa Loliondo hana uwezo wa kutibu maradhi sugu. zimeandikwa thread zikinakili mafunisho ya vitabu vya dini nk lakini bado suala hili limekuwa lenye mabishano makali.
Mimi natakata tujiulize/tutafakari kwanini taarifa kama hizi hatuzisikii sana kwenye vyombo vya habari na mijadala inayoendelea?.......Kwasasa tujadili na kutafakari hayo machache nitarudi tena.
- Kwamba halmashauri ya wilaya ya ngorongoro imekuwa ikikusanya zaidi ya Sh. Milioni mia moja kila mwezi kama ushuru wa magari, pikipiki zinazoingia kijijini Samunge
- Kwamba zinapokelewa maiti kati ya 10 hadi 15 kwa wiki zinapokelewa katika vituo vya afya jirani na kijiji cha Samunge (Wasso, digodigo)
- Kwamba hali ya usafi ni ya kusikitisha kukiwa hakuna hata choo kimoja kilichojengwa na halmashauri AU BABU MWENYEWE, licha ya mamilioni yanayokusanywa kila siku
- Kwamba hospitali mbalimbali za mkoa wa Arusha zimekuwa zikipokea wgonjwa mahututi amabao waliacha matubabu yao na kueleza kuwa wamekunywa kikombe na wamepona
- Kwamba safari moja ya kwenda kijijini humuingizia mmiliki wa gari shs 850,000 hadi 1,000,000 kwa safari ya kwenda na kurudi
Loliondo ni mradi wa watu wewe. Utasababisha JF ifungwe.