Imetokea loliondo

Imetokea loliondo

Ndugu Zangu,

Hii ni nchi yetu. Tunayaandika haya kwa mapenzi ya nchi yetu. Yanayotokea Loliondo yanaanza kubeba sura ya kashfa. Taratibu, Loliondo inaonekana kuwa ni aibu ya kitaifa kwenye masuala ya kimsingi ya afya ya watu wake.

Si kawaida, na yawezekana ni mara ya kwanza kutokea, kwa blogu ya jamii kutoa msimamo juu ya jambo la kitaifa. Tunauona umuhimu huo, tunafanya hivyo. Ndio, Hali ni mbaya Loliondo. Kuna Watanzania wenzetu wanakufa kila siku. Wanakufa wakiwa kwenye foleni ya kupata kikombe cha Babu au baada ya kunywa kikombe hicho na kuacha kutumia dawa zao walizokuwa wakitumia kabla.

Asubuhi hii nimepokea simu kutoka Dodoma. Kuna mganga aliyenielezea hali mbaya zinazowapata wagonjwa wake wa kisukari mara baada ya kupata tiba ya Babu na kuacha kutumia dawa zao. Anasema ni mbaya zaidi kwa wagonjwa wa kisukari, maana, kisukari kinapanda haraka. Anasema kuna wagonjwa waliokufa baada ya kuacha kutumia dawa zao.

Baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa mstari wa mbele katika kupigia debe tiba ya Babu bila kufanya uchunguzi yakinifu. Ndio, duniani kuna fikra dhanifu na fikra yakinifu. Ya ‘ Babu’ wa Loliondo ni dhania iliyopaswa kuhojiwa kabla ya kupigiwa debe.

Hivi, wanahabari wetu wanashindwaje mpaka hii leo, kuwahoji madaktari bingwa kwenye maradhi kama UKIMWI, kisukari, na mengineyo. Madaktari hawa wako Agha Khan, wako Bugando, Mount Meru na kwengineko. Hivi, Watanzania wenzetu hawa, katika kazi zao, mpaka hii leo hawana cha kusema, cha kitaalam juu ya Tiba ya Babu? Au media imechagua kuficha ukweli?

Tunajua, kuwa habari za ‘ Babu wa Loliondo’ zinauza magazeti kwa sasa. Lakini, ni dhambi na kutoitendea haki nchi yetu kama tutaamua kufanya biashara na afya za watu wetu. Ni laana kubwa.

Ona sasa, Watanzania kwa maelfu wanakwenda gizani bila kuhoji, au kusaidiwa kuhoji. Katika dunia ya sasa ya Sayansi na Teknolojia hatuwezi kwenda mbele kwa kuendekeza ‘ Abrakadabra’ kama hizi za Loliondo.

Huu ni wakati, kwa Wizara na waziri mwenye dhamana, kutoa tamko rasmi juu ya ukweli kuhusu tiba hiyo ya Babu. Na kama ‘ Babu’ ataruhusiwa aendelee na tiba yake kwa wenye imani, basi, Babu huyu asaidiwe kuhamishia shughuli zake Arusha mjini. Lifanyike hilo ili tunusuru maisha ya Watanzania wenzetu walio katika hatari ya kupata maradhi mapya katika mazingira ya sasa ya Loliondo.

Tunayasema haya kwa mapenzi ya nchi yetu, basi.

Maggid,
Iringa,
Ijumaa, Machi, 25,2011

MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo

Chini hapa ni bahadhi ya maoni ya wadau;



Mdau wa kwanza:

Hapa Arusha KILA HOSPITALI IMEPOKEA WATU WA MAGONJWA YA PRESHA, KISUKARI, PUMU, N.K. AMBAO WALIKWENDA LOLIONDO "KUTIBIWA" MARADHI HAYO NA BAADA YA KUPATA "NAFUU" (PSYCHOLOGICAL) KWA KAMA WIKI MBILI TU WAMEANZA KUUMWA SERIOUSLY NA KURUDIA DAWA ZAO ZA HOSPITALI TENA.

Pili, mimi nikiwa mfanyakazi wa maabara ya hospitali ya MT Meru, sijaona hata mgonjwa mmoja wa ukimwi aliyepata "seroconversion" yaani kurudi "seronegative from serpositive status". Kinachosikitisha ni kuwa kuna watu hawataki kabisa kusikia yanayosemwa na madaktari na wafanyakazi wa hospitali mbalimbali hapa Arusha ambao kila siku tuna-deal na watu wanaozidiwa baada ya kwenda Loliondo.

Mbaya zaidi kuna magazeti, tv na redio hayataki kabisa kusikia ukweli wa majanga yaliyowafika watu waliokwenda huko. Ajabu pia ni kuwa kuna watu ambao ukitaka kuwaeleza ukweli wanakuona wewe ni mpagani usiyemwamini Mungu. Naomba waandishi wa habari wawe proactive katika kutafuta ukweli na si kutegemea mass hysteria iliyowakumba maelfu ya watu wanaotafuta miujiza kwa nguvu."



Mdau wa pili:
Kuna madaktari wengi wa hospitali mbalimbali hapa Arusha (k.m. St. Thomas, Mount Meru, n.k.) ambao wametoa onyo kuwatahadharisha wananchi waliokwenda Loliondo wasiwache dawa zao za kisukari na BP. Inaelekea kuwa, kwa sababu zisizojulikana, vyombo vya habari vya Tanzania vimesusia kuchapisha au kurusha tahadhari za madaktari hao. Juzi kituo cha TV NTV ya Kenya imewaonyesha madaktari mbalimbali wa Arusha wakitoa tahadhari hiyo.

Ikiwa madaktari na wafanyakazi wa maabara [medical laboratory technicians] wanaona watu wanakufa kila siku kwa maradhi yaliyowapeleka Loliondo ni wajibu wao waseme ukweli huo. Ni mtu mjinga ndiye anayeweza kusema kutoa tahadhari hizo ni udini. Si udini. Udini ni kutaka watu waamini miujiza ambayo inakwenda kinyume na ushahidi wa kisayansi na hali halisi. Nimeamini kuwa matatizo ya dunia ya tatu ni mengi mno, lakini matatizo kuu ni kutokujua na kutotaka watu waseme ukweli.

Mdau wa tatu:
Mjengwa mimi pia niko Arusha na ni kweli kuwa kila daktari ninayeongea naye anasema kuwa wagonjwa wengi waliokwenda Loliondo imebidi warudie dawa zao na wengine wamefariki dunia. Nina hakika kuwa Wizara ya Afya ina taarifa hizo lakini nadhani Wizara hiyo haiwezi kusema lolote kwa kuwa wanaogopa kuambiwa kuwa wao ni wadini.

Tumefikia hali ambapo madaktari wengi (hasa Wakatoliki, Wasabato, Waislamu, Waanglikana, nk) wanaogopa kujitokeza hadharani na kusema kuwa watu wanakufa BAADA ya kwenda Loliondo simply kwa kuwa wanaogopa kuambiwa kuwa wao ni wadini.

Juzi, daktari mmoja wa hospitali ya AICC hapa Arusha aliniambia kitu kilichonistusha sana. Alisema "Maafa ya tiba ya babu yataanza kuonekana kikamilifu baada ya mwezi moja". Sasa ikiwa watu wameanza kufa tangu Januari (kumbuka watu wa Arusha walianza kwenda Loliondo September 2010) hapa Arusha na Moshi na wengine wanaendelea kufa kila siku porini Loliondo mnataka watu wasiseme na wakisema mnawaita wadini, why? Hiyo ni moral blackmail.
 
YA MUNGU MPE MUNGU, YA KAISARI MWACHIE KAISARI..
Kwa wakristo yesu alisema imani yako imekuponya,
HIVYO ATA KAMA WEWE UKISEMA MTU AKINYWA CHAI ULIOPIKA WEWE KWA IMANI ATAPONA. BASI ATA MWENYEZI MUNGU ATAKUPONYESHA KUTOKANA NA IMANI YAKO..
Hivo ayo mambo yaache kama yalivyo
 
Kwa hili namuunga mkono Maggid 100 %. Ni aibu na ni hatari kwa serikali kusupport hii kitu hadharani bila kutoa tahadhari kwa wananchi. Actually, serikali na viongozi wa CCM wamesaidia sana katika kui-advertise hii dawa ya babu mpaka imefikia Bodi ya utalii kutangaza kuwa itamtangaza Babu nje ya nchi ili asaidie kuleta watalii (Medical tourist). Kilichotusaidia mpaka sasa tusiwe kituko cha mwaka ni kwa kuwa intyerantional media imefocus Libya na middle East. Otherwise, tusije shangaa documentary ikija toka halafu tujifanye kustuka na kukasirika kama tulivyofanya kwenye Darwin nighmare na Albinos!!
 
Wakati Maggid amekuja na hiyo, serikali nayo bado inamipango yake na Babu!!



Serikali yaomba baraka za Mchungaji Loliondo
Send to a friend Thursday, 24 March 2011 21:36 0diggsdigg


abiri.jpg
Abiria wa basi la kukodi kutoka wilayani Nzega, wakisukuma gari lao lililokwama katika mpaka wa mbuga ya wanyama ya Serengeti na Loliondo kutokana na mvua kubwa iliyonyesha jumatano , walipokuwa wakielekea kijiji cha Samunge, mkoani Arusha kwa ajili ya kunjwa dawa kwa Mchungaji Ambilikile Mwasapile.

Na Waandishi Wetu
KIKAO cha kutafuta njia bora ya kuwawezesha wananchi kupata tiba ya magonjwa sugu huko Loliondo kilichoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na viongozi wa mikoa sita wakiwemo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Isdore Shirima na mwenzake wa Mara, Enos Mfuru kimeahirishwa katika kile kinachoaminika kuwa ni hadi pale maazimio yake yatakapopata baraka za Mchungaji Ambilikile Mwasapile.

Lukuvi aliwaambia waandishi wa habari mara baada ya kuahirisha kikao hicho saa 3:35 usiku kuwa bado kuna mambo ya kujadiliwa kabla ya kutoa tamko rasmi."Kikao kimeahirishwa tumepeana majukumu, kesho Mkuu wa Mkoa wa Arusha atakuwa Loliondo kuongea na Mchungaji Ambilikile Mwasapile na kujionea hali ilivyo kwa sasa na wengine wamepewa majukumu mengine, hivyo kesho (leo) tutakuwa na la kuwaambia baada ya RC kurudi," alisema.

Kwa muda wa siku nzima viongozi hao walikuwa katika Ukumbi wa Ofisi namba 40 katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha, wakijadili hali ilivyo huko Loliondo hasa baada ya mvua kuanza kunyesha na kusababisha msongamano mkubwa magari.

Mbali ya viongozi hao, mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi waandamizi wa Serikali kutoka Mikoa ya Singida, Kilimanjaro, Manyara na Shinyanga, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga na vingozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Kati.

Habari zilizopatikana baada ya kikao hizo zinasema Serikali inakusudia kuipatia Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, mahema ya kutosha ambayo yatakodishwa kwa wananchi wanaokwenda huko.

Pia Serikali imerejea ahadi iliyoitoa wiki kadhaa zilizopita ya kuandaa utaratibu wa kuwasaidia wagonjwa waliozidiwa kupata huduma haraka kwa kutumia gari la kubebea wagonjwa (ambulance) ambalo kwa sasa limeshindwa kufanya hivyo kutokana na baadhi ya watu kudai gari hilo linatumika kuwabeba vigogo badala ya wagonjwa wenye hali mbaya.

Taasisi yajitokeza kujenga vyoo, mahema
Taasisi ya kimataifa ya masula ya mazingira ya Solar Oven Society Africa, imetangaza mpango wa kuokoa maisha ya watu na uharibifu wa mazingira katika barabara iendayo Kijiji cha Samunge kwa kutoa vyoo na gari la kubeba wagonjwa.

Akizungumza na Mwananchi jana, Mwakilishi wa Taasisi hiyo hapa nchini, Profesa Solomon Mwenda alisema wamechukua uamuzi huo baada ya kubaini kuwa kuna tatizo la huduma muhimu kwa wagonjwa na uharibifu mkubwa wa mazingira katika eneo hilo ambalo pia ni mapito ya wanyamapori.

"Tumekwenda Samunge na tumeona hali ni mbaya sana na ni hatari kwa afya za watu. Tumekuta bado watu wanajisaidia porini, bado chupa tupu na uchafu mwingi unatupwa barabarani hovyo," alisema Profesa Mwenda.

Alisema kazi ya vyoo itaanza Jumanne ijayo na kwamba kila baada ya kilometa moja kutakuwa na choo cha muda. Pia watatoa gari la kubeba wagonjwa, mifuko ya kutunza taka, mahema na maofisa wa mazingira.

Mpaka sasa hakuna hata choo kimoja kilichokamilika kujengwa wakati Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro imekuwa ikivuna kiasi cha Sh 6.4.milioni kwa siku katika Kijiji cha Samunge.

Tayari halmashauri hiyo imetia kibindoni kiasi cha Sh 140.8 milioni kwa mwezi mmoja lakini hivi sasa kuna taarifa ya mgonjwa mmoja kuhara damu, kwa mujibu wa ripoti kutoka zahanati ya kijiji jicho.

Pato hilo linatokana na tozo la ushuru wa kila siku kwa magari yanayokwenda kwa Mchungaji Mwaisapile kwa ajili ya kupata tiba. Mabasi makubwa na malori yanatozwa Sh10,000 kila moja, mabasi madogo yanatozwa Sh5,000 na madogo Sh2,000 huku pikipiki zikitozwa Sh1,000.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka kijijini, hapo pamoja na pato hilo ambalo awali lilikuwa likikusanywa na kijiji hicho hali bado ni mbaya na uchafu umekidhiri kila mahali vinyesi, mikojo katika chupa za plastiki ni hali ya kawaida eneo hilo .

Hali inazidi kuwa mbaya kiafya kutokana na mvua ziloanza kunyesha huku misururu mirefu inayofikia umbali wa kilomita 28 na watu waoadiriwa kufikia 150,000 wakiwa wanasubiri kupata tiba. Msururu huo unaanzia katika Kijiji cha Mdito.
Wananchi waliokwama katika msururu huo wamekuwa wakihangaika kupata chakula na vinywaji kiasi kwamba kila abiria wanaopita kutoka Kijiji cha Samunge, wamekuwa wakiombwa maji ya kunywa bila kujali kama yametumiwa na wengine au la.

Kijiji cha Mdito chenye kaya zisizozidi 50 hivi sasa kina watu wanaokadiriwa kufikia 200,000 ambao hawana mahitaji muhimu kabisa, huku wengine kama hao wakipata walau huduma kidogo na hao ni wale walio katibu na Kijiji cha Samunge, umbali wa kilometa 10.

Wakati huohuo; mvua zinaendelea kunyesha wilayani Ngorongoro hali ambayo inatishia uharibufu wa barabara.

Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali alisema kuwa kutokana na mvua hizo, ukarabati wa barabara ambao ulikuwa unafanywa na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) umesitishwa kwa muda.

"Ni kweli barabara ni mbaya kutokana na mvua, watu wa Tanroads walikuwa wanatengeneza barabara ila nadhani sasa imekuwa kazi ngumu kwani mvua zimewakuta," alisema Lali.

Tangu kuanza kwa mvua hizo takriban wiki moja sasa, mamia ya watu na magari wamekwama katikati ya Kijiji cha Selela na Ngaresero kutokana na mito kujaa na maeneo mengi kuharibika.

Lipumba aiponda Serikali
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ameishukia Serikali kwa kuruhusu tiba hiyo bila kufanyiwa uchunguzi na mkemia wake mkuu.

Lipumba ambaye hata hivyo, katika maelezo hayo hakuwakatisha tamaa wananchi kwenda kupata tiba hiyo, alisema kiutaratibu, watu hawazuiliwi kufanya tiba, lakini dawa lazima zipite kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili athibitishe ubora wake kabla ya kuruhusu watu waanze kuitumia.

Profesa Lipumba alisema hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika katika Viwanja vya Zakheim, Mbagala Dar es Salaam.

"Katiba yetu haizuii mtu kuendesha shughuli za tiba, lakini taratibu ni kwamba tiba lazima ithibitishwe na maabara za Serikali. Ukiona Serikali inawaruhusu watu kutumia tiba bila kufuata utaratibu huo ujue imekwama," alisema.

Ingawa Lipumba hakutaja moja kwa moja tiba ya Loliondo, tiba iliyoanza kutolewa katika siku za hivi karibuni na kuibua mjadala mkubwa miongoni mwa jamii ni ile inayotolewa na Mchungaji Mwasapile.

Profesa Lipumba aliponda uamuzi wa Waziri Lukuvi kushinikiza tiba hiyo itolewe bila vipimo akisema ni sawa na kuhalalisha mambo yaendee kiholela katika nchi ambayo imejiwekea utaratibu wake kisheria.

"Waziri wa afya alikuwa sahihi sana kutaka dawa hiyo ipimwe kwanza, lakini Lukuvi akapingana naye, hii ni dalili mbaya kwa Serikali," alisema.

Habari hii imeandaliwa na Filbert Rweyemamu, Moses Mashala, Emanuel Herman, Arusha na Kizitto Noya.
 
we ngine si wakasema aaa babu, huwezijua labda wengine tunao lakini hatujijui acha tu tunywe hivyo hivyo..
 
Baada ya Kupata tiba ya mafisadi umeshiba naona unaamia kwa babu lakini 2015 sio mbili utakuwa kinyonga kama kawaida


Kwanini uwe msimamo wa BLOG Yako?? si ungayaacha HUKOHUKO kwenye Blog Yako???
 
Sasa kama 'wenyewe' (viongozi) walienda kwa babu wakanywa kikombe kwa siri na 'wakapona', watapata wapi ujasiri wa kuizuia 'tiba' hiyo?
 
]NEW LAGER IS HERE

Waeva .... i hv one word to describe you click here

Tatizo hata huyu mungu unayemuabudu wewe amejiita (mtu asiyejuwa mambo)
1 Corinthians 1:25 (New King James Version)
25 Because the foolishness of God is wiser than men, and the weakness of God is stronger than men.

kama mungu wako anajiita hayo manenoi katika Red! wewe mfuasi sijui nitarajie nini..?!
 
sijui kama lager inaweza kuwa na alc. 0% labda beer,nadhani neno lager si mahali pake hapo
 
Hivi babu wa Loliondo atoweke ghafla, halafu aache ujumbe mfupi kuwa:
"NDUGU WANANCHI NIMEAMUA KUKIMBIA, NIMEGUNDUA HII DAWA NI SUMU NA HUUA BAADA YA MIEZI 6. WANANGU 3 WAMEKUFA KWA KUWA WAO NDIO WA KWANZA KUWAPA MAJARIBIO, KWELI WALIPONA LAKINI BAADA YA MIEZI 6 WAMEKUFA KWA MKUPUO. BORA NIKALIWE NA SIMBA KULIKO KIPIGO MTAKACHONIPA".
Hebu fikiri nchi itakuwaje kwa mshtuko!!
 
Nimeshangazwa sana na makala aliyoiandika mjengwa humu kwenye jukwaa la siasa kuhusiana na loliondo.

Ameiponda tiba ya loliondo kwa kuangalia yale ambayo watu baadhi wamesema negative kuhusu loliondo. Ila siku zote ata mtu awe mpagan asie na dini uyo atajua jema na baya na dhambi ni ipi. Sio lazima usali sehem fulani.

Ni imani ya mtu ndio itakayo kuponyesha. Na hata usipoenda loliondo kupata kikombe ila ukiwa na IMANI kwamba u tapona, basi ilo lawezekana..

MJENGWA kajisahau kwa siasa zilizomzidi kutokana na kuona serikali yetu ni mbovu. Na kiukweli serikali ni mbovu.
Ila kuingiza tena serikali katika hili ni upuuzi..

Hata hayo unayosema television ya kenya NTV, mjengwa kataja yale yaliyo negative tu.. Mbona umeacha kutaja yale positive waliyosema???

Katika hili wanaJF Tuangalie tusiweke siasa sababu ya chuki na serikali mliyoichagua kwa kuchakachua..

Huo ni mtazamo wangu kuhusiana na ilo..
YA KAISARI MPE KAISARI, NA YA MUNGU MPE MUNGU.G
 
siwezi kuifikiria kwa kuwa babu ana mwaka sasa akitoa huduma hiyo, labda badilisha statement yako
 
TANGAZO..TANGAZO...TANGAZO!! : Babu alisikika

''Wagonjwa wajipange kulingana na matatizo yao tafadhali.
wenye UKIMWI mstari huu kushoto,wenye kisukari katikati na wenye presha kulia ili niweze kugawa dawa kulingana na magonjwa, sasa hivi kila ugonjwa una sufuria tofauti''

Babu: Tafadhali zingatia hili....kila dawa inatibu tu ugonjwa wake na si vinginevyo.

mara wagonjwa wakajigawa mstari wa Kisukari na wa presha ulifurika wagonjwa foleni ikafika hadi kijiji jirani na mstari wa UKIMWI haukua na mtu hata mmoja.
Babu: Kadadaa hebu mwaga hilo sufuria la dawa ya UKIMWI maana hakuna wagonjwa,bakiza hayo mawili ya presha na kisukari!!
Wateja: Aaaaaaaah..... babu sorry hatukusikia tangazo vizuri, tulijichanganya kidogo....usimwageeeeeeeee....weee Kadadaaaaa achaaaaaa tupoo"
 
umecopy bila kusema source ...! huo ni wizi wa kazi za watu...! hii ilikuwa blog ya michuzi..!

plagiarism !!!!!!!!!!!
 
ni forwarded mail, naomba re-post with source maana nimeenda michuzi sijaiona
 
Ndugu PAS, with due respect to IMANI yako, please explain the positive aspects that have come from babu wa Loliondo.
 
Lets make its after 5 years

Nahisi Tanzania itapata pigo hasa kwenye Serikali
 
Hawezi kukimbia kwa sababu mkono wa serikali ni mrefu atakatwa tu, labda ajiue na kuacha ujumbe.
 
..Natambua kwamba wasomaji wengi wamekuwa wakitoa maneno ya kejeli, matusi dhidi ya wale wote wanaojaribu kuonyesha kuwa Babu wa Loliondo hana uwezo wa kutibu maradhi sugu. zimeandikwa thread zikinakili mafunisho ya vitabu vya dini nk lakini bado suala hili limekuwa lenye mabishano makali.

Mimi natakata tujiulize/tutafakari kwanini taarifa kama hizi hatuzisikii sana kwenye vyombo vya habari na mijadala inayoendelea?
  1. Kwamba halmashauri ya wilaya ya ngorongoro imekuwa ikikusanya zaidi ya Sh. Milioni mia moja kila mwezi kama ushuru wa magari, pikipiki zinazoingia kijijini Samunge
  2. Kwamba zinapokelewa maiti kati ya 10 hadi 15 kwa wiki zinapokelewa katika vituo vya afya jirani na kijiji cha Samunge (Wasso, digodigo)
  3. Kwamba hali ya usafi ni ya kusikitisha kukiwa hakuna hata choo kimoja kilichojengwa na halmashauri AU BABU MWENYEWE, licha ya mamilioni yanayokusanywa kila siku
  4. Kwamba hospitali mbalimbali za mkoa wa Arusha zimekuwa zikipokea wgonjwa mahututi amabao waliacha matubabu yao na kueleza kuwa wamekunywa kikombe na wamepona
  5. Kwamba safari moja ya kwenda kijijini humuingizia mmiliki wa gari shs 850,000 hadi 1,000,000 kwa safari ya kwenda na kurudi
.......Kwasasa tujadili na kutafakari hayo machache nitarudi tena.
 
Back
Top Bottom