Imetokea loliondo

The reporting is professional. It puts to shame the coverage I have seen so far on our own TV's.
 



Na Maggid Mjengwa,

TUNAWAPITISHA watu wetu kwenye njia yenye giza. Kwenye njia yenye matope. Kwanini?

Socrates, mwanafalsafa wa Uyunani ya kale alipata kuonekana akimulika kurunzi mchana wa jua kali. Inaandikwa, kuwa Socrates yule alizunguka sokoni na kurunzi (tochi) yenye kumulika. Watu walimwuliza, kulikoni? Socrates akawajibu; ”Kwenye nuru hii , kuna walio gizani.”
Kwa Socrates lilikuwa ni tendo la kifalsafa lenye kuelezea hali halisi. Hata katika dunia hii ya kisasa, bado tuna miongoni mwetu, walio gizani mchana wa jua kali. Angalia ya kwa ’ Babu’ wa Loliondo. Ndio, kuna wanaohitaji kumulikiwa mwanga.

Na kuna tofauti ya ujinga na upumbavu. Marehemu Mzee Jongo alipata kutamka; ” Kusoma sio kuufuta ujinga, bali ni kuupunguza”. Kila mwanadamu ana ujinga wa jambo moja au mia moja. Kuwa na ujinga wa jambo si kosa, hata Profesa anaweza asijue namna ya kuchochea kuni za kuchomea hindi bichi likachomeka. Kijana wa darasa la saba anaweza kuwa hodari wa jambo hilo kumshinda Profesa.

Lakini upumbavu ni ile hali ya mwanadamu kufanya jambo isivyotakiwa huku akiwa na uelewa wa namna ya kufanya inavyotakiwa. Huo ndio upumbavu. Na ndio maana binadamu kuitwa mpumbavu ni tusi. Kuitwa mjinga si tusi, kila mmoja ana ujinga wake. Kuwa na ujinga wa jambo fulani ni kutoelewa jambo hilo. Ni nani anayeelewa kila jambo?

Na mwanadamu unafanyaje unapoamka na kukuta dunia unayoishi ardhi yake imeanza kumegeka na kuchotwa na bahari? Kuna niliyemwuliza swali hilo. Naye akanijibu; ” Huo ndio utakuwa mwisho wa dunia!” Aliyenijibu alikuwa amechoka kufikiri. Nilidhani amgetamka, kuwa angeanza kujifunza kuogelea. Maana, kwa kuogelea majini angeweza kukutana na kisiwa, au nchi kavu.

Wanadamu tumejaliwa akili ili tuweze kufikiri. Na kufikiri ndio njia mojawapo ya kuiteka kweli. Kufikiri kunahamisha milima na hata kuiweka kando kuruhusu mwanga upite. Inakuwaje basi mwanadamu anapoacha kufikiri? Haya ya kwa ’ Babu’ wa Loliondo ni kielelezo cha Watanzania kuamua kuacha kufikiri. Kuna umma uliojifunika vilemba vya ujinga. Umma uko gizani, unahitaji mwanga.

Yumkini wakatokea Watanzania wenzetu, wakaoteshwa na Mungu juu ya dawa za tiba kwa mwanadamu. Na hapo wakaingiza suala la imani. Lakini, jambo hilo halituzuii wanadamu kuhoji na kudadisi. Ndio, kuuliza maswali. Na kwa Serikali, jambo hilo haliizuii kufuata taratibu zake za kawaida ikiwamo kufanyia utafiti jambo hilo na kutoa msimamo wa Kiserikali. Hata kama Watanzania watakuwa na uhuru wa kwenda kwenye tiba za imani, lakini msimamo wa Serikali uwepo. Na kwa wengi utabaki kuwa ndio mwongozo, maana, watakuwa wameufanyia utafiti.

Si tumemsikia yule Nabii mwingine wa Tarakea, naye n i kijana wa miaka 28. Ikasemwa, kuwa naye kaoteshwa na Mungu dawa ya kutibu wagonjwa. Mpaka Serikali ilimpomzuia ili ifanye uchunguzi, tayari alikuwa na wagonjwa mia moja. Ndio, Watanzania tu wagonjwa tunaogombewa. Na viongozi wetu pia ni wagonjwa. Si tumewaona wakipanga foleni ya kikombe kwa ’ Babu’ wa Loliondo.

Katika dunia hii Serikali hupendwa na watu, lakini, si vema na busara, kwa Serikali za dunia kutaka kujipendekeza kwa watu. Kuna mambo yenye kupendwa na watu, na watu wakawa na haraka ya kutaka kuyafanya. Lakini, kama Serikali itahitaji kufuata taratibu ili kinachopendwa na watu kifanyike, basi, Serikali haina namna nyingine, bali kufuata taratibu. Si tuliona yale ya DECI. Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisimamia taratibu, akasimamisha wimbi lile la DECI. Kuna wengi walishutumu, lakini , hao hao, leo wanaishukuru Serikali. Maana, DECI nayo ilikuwa ni Abrakadabra.


Na si juzi hapa tumemsikia Paroko wa Kigango cha Mt. Yohane wa Msalaba Parokoia ya Mbezi Luis.Padri Vivian. Niweke wazi, Paroko yule amesema kile ambacho kuna wengi hawataki kukisikia. Ameusema ukweli wake. Ameifanya kwa dhati, kazi ya utumishi wa Mungu wake.

Paroko yule wa Mbezi Luis alitamka; "Sina chuki wala tatizo lolote na tiba ya Loliondo, lakini kama unataka kwenda lazima ujiulize maswali manne yafuatayo;


Kwanza, tiba inayotokana na miujiza ya Mungu lazima iwe endelevu isiwepo kwa kipindi kifupi tu.


Pili, watu wajiulize kama miujiza kutoka kwa Mungu huwa na masharti?

Tatu, wajiulize kama tiba hiyo inafanya kazi ndani ya Loliondo, kwanini isifanye kazi Dar es Salaam na kwingineko?


Nne, wajiulize kuhusu tiba hiyo ya magonjwa sugu ukiwemo UKIMWI ni je, Mungu aliwaumba wanadamu na kisha kuamua kuwaangamiza? Au wanadamu wanaangamia kutokana na vitendo vyao vya ujanja ujanja?


Mwisho Paroko yule akasema; "Ukiishajiuliza maswali hayo na kujiridhisha kwa majibu utakayopata, basi, unaweza kufanya maamuzi ya kwenda Loliondo.


Ndio, tujiulize; katika mataizo yetu haya, tumechoka kufikiri? Tumechoka kuuliza maswali? Hapana. Tusichoke kuutafuta ukweli, hata kama umegubikwa na ukungu. Hivi ni Watanzania wangapi wamesikia au kusoma maelezo ya Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru Dr. Toure?

Nahofia si wengi, maana, maelezo yake yaliyopaswa kuwa habari kubwa ya ukurasa wa mbele yalipewa nafasi ndogo sana kwenye moja ya magazeti ya kila siku. Tena yaliwekwa katika ukurasa wa pili ndani ya habari nyingine. Si tunafahamu, kuwa baadhi ya wanahabari nao wanachagiza ’ Abrakadabra’ za ’ Babu’ wa Loliondo. Zinauza magazeti, na msimu ndio huu!

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Hospitali ya Mount Meru alisema, kuwa tangu tiba ya ’ Babu’ ianze, hajapata hata mgonjwa mmoja wa UKIMWI aliyepata kikombe cha ’ Babu’ na kurudi hospitalini hapo kupimwa tena. Hivyo, mpaka hii leo hatuna ushuhuda wa kimaabara kwa maana ya hospitalini. Ushuhuda tunaousikia ni wa mitaani. Ndio maana tiba ya ’ Babu’ itabaki kuwa ’ Abrakadabra’ mpaka hapo itakapothibitishwa vinginevyo kimaabara hospitalini na na si kwenye vijiwe vya barabarani.

Halafu tunaambiwa, kuwa tiba ya ’ Babu’ inatibu kansa pia. Hivi Kliniki ya Kansa ya pale Ocean Road mpaka hii leo imeshindwa kuwapeleka kwa ’ Babu’ wagonjwa watano tu walio kwenye matibabu ya kansa. Waende huko wakapate kikombe halafu wachukuliwe vipimo tena tuone nguvu ya tiba ya ’ Babu’ katika kuwasaidia wagonjwa wa kansa.


Ndugu zangu, Mfalme Suleiman alimwambia Mola wake; ” Watu wangu wanaangamia kwa kukosa hekima”. Ndio, Mfalme Suleiman alipoambiwa na Mola kitu cha kuchagua, basi, aliichakua hekima ili aweze kuwaongoza watu wake.

Angalia leo, walio wagonjwa na kwenye hali ngumu za kiuchumi wanazidi kuwa wagonjwa na hali zao za kiuchumi zinazidi kuwa duni. Ndio, kuna wanaofunga safari zenye gharama kubwa kwenda Loliondo. Wanakwangua akiba zao. Kuna hata wanaokopa fedha za kwendea Loliondo.

Ndio, wanakwenda kupata tiba isiyo na hakika katika wakati huu tunaozungumza. Kuna wagonjwa walioacha kutumia dawa zao. Wamerudi na kuanza upya. Kuna waliopoteza maisha. Inasikitisha sana. Ni nani wa kuwasaidia kuwamulikia mwanga?

Naam. Kwenye nuru hii kuna walio gizani. Tuwasaidie.


http://mjengwa.blogspot.com

 
The reporting is professional. It puts to shame the coverage I have seen so far on our own TV's.
Huyo ni John Alan Namu, bonge ya reporter. Alishinda CNN African Journalist of the year mwaka jana. Yani angalia Kazi alizofanya zamani za rogue tracker na kazi nyingine utaona kwamba jamaa ni fearless. Waandishi wetu ni kuogopa ogopa tu. Huyu Namu alitoa report ya Drug Lords wa Mombasa ilibidi akimbie nchini miezi mitatu baada ya story kutolewa. We need help Tanzania
 
Govt in crisis meeting over Loliondo saga Send to a friend Wednesday, 23 March 2011 23:29

lukuviw.jpg
Minister of State in the Prime Minister’s Office,Mr William Lukuvi

By Zephania Ubwani
The Citizen Bureau ChiefArusha: A senior Cabinet minister was last night still chairing an emergency closed-door meeting with administrators and security chiefs from seven regions on how to deal with safety fears over the continuing influx of the Loliondo “miracle cure” seekers.

Mr William Lukuvi, the Minister of State in the Prime Minister’s Office, in charge of Policy, Co-ordination and the National Assembly, arrived in the northern city, apparently in response to mounting concern over the large numbers of people headed for Samunge Village and the hundreds of motor vehicles still stuck there following torrential rains.

The minister, who chaired the meeting at the Arusha District Commissioner's office from early yesterday morning, could not be reached for comment on the measures the government intends to take to address the crisis.
Sources said Mr Lukuvi had summoned top officials from Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Shinyanga, Mwanza, Mara and Singida regions to the meeting, as the government grappled with the problem.

Of particular concern to the authorities is the rising number of patients reportedly dying in the queues of vehicles stretching back over 20km from the pastor’s home. The Citizen team saw at least five bodies on Tuesday and yesterday. The problems cited are lack of food, water and toilets – the perfect recipe for epidemics.
The victims are among the thousands who have sought remedies for their critical illnesses from retired Lutheran Church pastor Ambikile Mwasapile, 76, who dispenses herbal medicine.

The government officials were reportedly deliberating on the means and ways to forestall a looming humanitarian crisis in the tiny remote village, with the sick and their relatives having ignored repeated appeals to delay their trips, until proper amenities are provided and those still in Loliondo are able to get out.

Arusha regional commissioner Isidore Shirima said: "Our main concern is how to address the deteriorating situation in Samunge Village either by blocking the vehicles taking people there or using any other means."
He told The Citizen before the meeting resumed at around 7pm that the situation in Loliondo was pathetic and getting worse day after day.

He said hundreds of vehicles continued to ferry the sick to the village, over 400km from Arusha.
On Tuesday, Mr Shirima had announced that the government would restrict traffic to Samunge in a bid to avert a health catastrophe.

Yesterday, he reiterated that the key concern was the possibility of an outbreak of communicable diseases due to the poor sanitation, worsened by the rains that have been pounding the area since last week.

"We are looking at the possibility of reducing the congestion at Samunge. That is our only agenda,” he said, of the meeting being attended by regional police chiefs and their assistants, security and other officials involved in disaster management from the various regions.

Mr Shirima could not say how many people have died since the rush to Loliondo peaked nearly a month ago.

On March 8, Ngorongoro District Commissioner Elias Wawa Lali reported that six people had died in the queue before being attended to by the Rev Mwasapile, who claims to use divine powers to treat people suffering from chronic diseases.

More deaths have been reported since then, as more and more people take their sick relatives there to drink a cupful of the herbal concoction offered by the healer.

Last weekend, there were alarming reports that up to 10 people had died after being rushed to the healer from their hospital beds, while in critical condition or a result of the fatigue from the tortuous journey and the many days they spent waiting in the long queues.

The increased traffic to Loliondo, through the dirt road that passes near Lake Natron and Oldonyo Lengai Mountain, has also seen its share road accidents, which until last week had claimed eight lives, according to the police.

Yesterday, the Arusha RC said the crisis meeting would probably continue until this morning. "Whatever we decide will be made public. The media will be briefed on measures to be taken to address the crisis,” he pledged.

Despite reports of many vehicles stuck on the way to or from the traditional healer's village, more vehicles continued to leave Arusha for Loliondo.

A survey by The Citizen last night revealed that scores of people, mainly from outside Arusha, were queuing near the central bus station to buy tickets to Loliondo."People are still going to Loliondo despite reports of many who have been stuck there for days," a taxi driver said. Some people were using the longer route to Loliondo through the Serengeti Plains.



Comments




0 #6 Sune 2011-03-24 09:13 Watch Part 1 of this Kenyan report on Loliondo. At the very end listen to what the doctor has to say about people getting healed...I'm sure Part 2 will be even more interesting.

YouTube - The Loliondo Wonder Pt. 1
Quote









+1 #5 Emma 2011-03-24 07:30
sleeping.gif
You realize how crazy the human race can be. Just have a little bit of Psychology, philosophy, anthropology knowledge, you will understand what is going on in Loliondo, Arusha, TZ
Quote









+2 #4 jiga 2011-03-24 06:51 lets buld roads and monuments around Loliondo. we can make it the Mecca of Africa. More dollars from healing tourism how about that. we need to market it well. people will come from all around the world just like they go to vetican city to see the pop and mecca for hajj and israel. this is our chance to take to the bank. come on Government channgamkia kidogo. lol
Quote









-1 #3 Doctor No 2011-03-24 05:51 With the population of patients keep grown like mushroom, mordern bathrooms,tents , water and ligh utilities need to be priorities as much as the gvt does to priorities fun for small election. Open police station and maintain security to be as tighy as drum! Control foods vending to make sure they meet health standars. Some people will take advantage to sell dog and snake that could put people in more health hazard.Short of doing that, the gvt will find itself putting lipstic in pig's mouth!
Quote









0 #2 Dzemba Dzemba 2011-03-24 05:40 This is a very uplifting move and hopeful the gvt will come up with a good solution. Good job bill Lukuvi!Stomach has no window, we never know how much would people with lifelong illness are going to benefit from Mchungaji's miracle's maximum cure. So let us constract a good livable envinroments upon which people would feel confortable to dwell. Under chama chashika hatamu the cadres would open tawi la chama at mchungaji's house but at this age of democracy the government is working hard to see patients meet basic need. That is the most humorous action!
Quote









-1 #1 Shammah 2011-03-24 00:52 I think that's a right move, not a bad one. I plead with the government and other organisations to device means to facilitate the healing given by our mzee.

I believe in the healing provided by the retired pastor. Its not a matter to be judged by political or religious/denominations factors. Let everybody who believes go there, and the rest keep quiet, just like how we do concerning the other witchdoctors.

We,Tanzanians, are the ones to build our country. Let's unite!

Peace be upon Tanzania.
 
PHP:
Last  weekend, there were alarming reports that up to 10 people had died  after  being rushed to the healer from their hospital beds, while in  critical  condition or a result of the fatigue from the tortuous journey  and the  many days they spent waiting in the long queues.
 
The increased  traffic to Loliondo, through the dirt road that passes  near Lake Natron  and Oldonyo Lengai Mountain, has also seen its share  road accidents,  which until last week had claimed eight lives,  according to the police.


cure versus faith.....................
 
kwa kweli Inavutia na imetengenezwa kiutaalamu,
Hivi mpaka sasa vyombo vya habari vimetoa documentary kama hii?
 
Kwa mtazamo wangu kitendo cha VIONGOZI WA SERIKARI KWENDA LOLIONDO KWA KISINGIZIO KWAMBA WANAENDA KUKAGUA HALI YA HUKO NA KUANZA KUONGEA NA BABU WAKATI WANGONJWA WANA SUBIRI NAONA SIO SAWA WANAMUHOJI BABU WEEEEEEEEEEEEE HALAFU MWISHO WANAOMBA KIKOMBE NI HERI WAUNGE FOLENI WAACHE KUWACHEREWESHA WAGONJWA KUPATA DAWA.
 
road road and temporary toilet that solution,as i know there are mfuko wa maafa just take money from there
 



"If it was a white bastard doing this thing it will be believed by many,this to me might be a 100% right depending that this old guy is charging peanuts for the medicine i.e he is there to help sick people and not mint money.God is great and he is nowadays revealing it to poor people because the rich-men and white especially don't even believe in God. God help us...."
 
Last edited by a moderator:
The drink works . Its similar to Kabwere/ Kajiwe/kamuti/ Ngata thing that most Wakamba drink. I drank it years back so that i can get a visa to USA and it worked 100%.
 
Back
Top Bottom