Unajua walijibuje..aaaha babu usimwage tumejichanganya tu!!!
Wewe mtani wa jadi Futa Kauli yako mara moja !
Kwa nini si unamuona hapo mzee anapiga kikombe!!!
View attachment 25621Malkia wa muziki wa Injili nchini, Rose Muhando, amedai kupanga safari ya kwenda kijiji cha Samunge, wilayani Loliondo kukutana na Mchungaji, Ambilikile Mwasapile kwa lengo la kunywa dawa ili siku ya Tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika mwezi ujao limkute akiwa fiti.
Rose alitoa kauli hiyo hivi karibuni ndani ya Studio za Zoom Production, zilizopo Magomeni Usalama jijini Dar es Salaam anakorekodia nyimbo zake kumi kwaajili ya albamu yake ya tatu.
taarifa ya tiba za Babu huyo alikuwa na mashaka nazo lakini kadiri siku zinavyokatika ameanza kuziamini kutokana na ushuhuda za watu mbalimbali wanaohudumiwa.Endapo Rose atatekeleza adhima yake hiyo, atakuwa mwimbaji wa kwanza wa muziki huo kujitangaza kwenda kupata tiba kwa Babu wa Loliondo ambayo imekuwa ikiwagawa watumishi mbalimbali wa Mungu ambao kila mmoja amekuw akisema lake.
IMANI YAKO IKAKUPONYE DADA YETU ROSE UWE USHUHUDA.