Imani yangu ni kuwa Tanzania moja, Serikali moja itatutoa

Kakati

Senior Member
Apr 11, 2009
167
47
Naiangalia Tanzania ya mwaka 2073 miaka 50 kutoka leo. Najitenga na ubinafsi nifikiri bila kuzugwazugwa. Nauangalia mfumo wa Muungano wa Tanzania. Najikumbusha mazingira ya kuanzishwa kwake wakati sultani amefurushwa na hatihati za kutinga kwake tena.

Nafikiria wapendavyo wapemba na waunguja kutopoteza utaifa wao wa Zanzibar. Nayajua mapungufu ya mfumo wa unioni yetu unaokinzana na nadharia ya hisabati ya seti, ungano na muungano.

Nawaona wajukuu wetu wakitushangaa kwa nini tumetengeneza dude lisilowezekana. Nawaona wakipiga viboko makaburi yetu.

Natamani tufanye maamuzi magumu lakini ya maana. Tuunganishe kabisa Tanganyika na Zanzibar. Iwe nchi moja, serikali moja.

Mmakonde aweze kumiliki ardhi pemba au unguja kama mpemba anavyomiliki ardhi kigogo au ujiji. Kusiwe na kusigana.

Hoja yangu haijakamilika. Naikamilisha kwa kusema wakati mzuri wa kutimiza hili ni awamu ya sita. Kwa nini?

Kwanza, katika awamu ya hii ya sita hata tukijitahidi vipi, tutaweza tu kukamilisha miradi ya ujenzi ya awamu ya tano, kwa hiyo majengo, mabarabara, reli nk vyote vipya havitatupa sifa mpya. Pili tunaweza tukajenga nchi kuwa moja ikawa ni legacy bora sawa na hiyo miundo mbinu.

Na muhimu zaidi imani yangu ni kuwa jemedari wetu japo kuwa jambo hili laweza kuwa gumu kwake binafsi, kwa baadhi ya wazanzibari au hata watanganyika kutopenda muungano kamili lakini ndiye mwenye nafasi nzuri ya kulifanya kwa kuwa anatoka Zanzibar na ni mwanamke.

Hata kama ni mfupa mgumu, tafuna mama.
 
Matukio yatapita, hata sisi tutapita, tuache hadithi nzuri kwa wajao.
 
Wanyonyaji wa Zanzibar watakataa! Sujui ni kwa nini tuliungana na watu wabinafsi, wajuaji, wavivu, wazembe, wategemezi, wabaguzi, wadini, na walalamishi kama Wazanzibari!!
 
Tanganyika tumejitoa kwa hali na mali kuiwezesha Zanzibar isimame ila hawana shukrani. Wangeacha ubinafsi TANZANIA MOJA INAWEZEKANA
 
Wanyonyaji wa Zanzibar watakataa! Sujui ni kwa nini tuliungana na watu wabinafsi, wajuaji, wavivu, wazembe, wategemezi, wabaguzi, wadini, na walalamishi kama Wazanzibari!!
Jibu lake ni kuwa tuliungana nao kwa kuwa walikuwa na ni majirani. Na walikuwa na soo tukawa tunawakingia kifua kiaina. Muhimu turudi mezani kwa uwazi. Tujadiliane, tuungane kabisa. Ina faida kubwa. Na dunia itatuheshimu. Faida kwa wote zitakuwa zaidi kuliko hivi tunavyoendelea sio baridi sio moto.
Tanganyika tumejitoa kwa hali na mali kuiwezesha Zanzibar isimame ila hawana shukrani. Wangeacha ubinafsi TANZANIA MOJA INAWEZEKANA
Nikwambie, muhimu tujadili mustakabali wa muungano wetu kwa ukweli na uwazi. Kwa kweli kuna wakati wazanzibari wanahisi wanabanwa na muungano kuliko kama wangekuwa nchi kamili. Wakati huohuo wanavitu wanafaidi na hivyo watanzania bara au watanganyika wanahisi kuwatumikikia wazanzibari. Vyovyote ukweli ulivyo, jabo hili sio jema. Tuliweke sawa. Inawezekana na wakati ni sasa.
 
ccm imetulea
Ni kweli CCM imetulea na tuko vizuri. Hata hivyo kwa kweli ni muhimu tukipata wasaa tujadili mambo ya msingi kwa uhalisia.

Muungano lazima udumu daima. Tunachozungumza ni kuweka mfumo mzuri udumu hata milele.
 
Back
Top Bottom