Image of virgin Mary grows on tree

Image of virgin Mary grows on tree

Umenena vizuri. Lakini hajajibu swali la msingi, naomba unijibu:

Bikira Maria yuko hai kama alivyo Musa na Eliya huko mbiguni?

Kama ndiyo, unaweza ku-justify kwa angalia mstari mmoja wa Biblia?

Kama hayuko hai, point iko wapi kuwasiliana na mfu?

Pia naomba jibu, kuna shida gani mkiomba kwa Yesu moja kwa moja?

Mkuu nimevutiwa sans na busara zako...

Ukichunguza sala zote za Wakatoliki mwisho wa Sala huwa tunamaluzia
"TUNAOMBA HAYO KWA NJIA YA KRISTO BWANA WETU...AMINA)
Kwamba Kristo ndio Mshenga wetu wa Mwisho
 
... Pia naomba jibu, kuna shida gani mkiomba kwa Yesu moja kwa moja?
Nitaanza na hili. Kuwepo kwa sala za Mama Maria pamoja na Watakatifu wengine hakumaanishi HAKUNA sala za kumuomba Yesu Kristu. Kuna sala nyingi sana za RC zinazomalizia na kifungu hiki: "Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu" (jaribu kuGoogle hayo maneno, utapata sala nyingi tu). Naomba uwaambie na watoto wengine wa KiProtestant, kwamba RC tunapoomba maombezi ya Maria kamwe haimaanishi kuwa tumeyaweka kando maombezi yetu kwa Yesu Kristu. Ili kuthibitisha hilo, uwe unahudhuria mafundisho na misa za Kanisa Katoliki, vinginevyo utakuwa ukiendelea kudanganywa na wachungaji wako kuwa RC hawamuombi Yesu Kristu, lakini wao waProtestant wakubwa (wachungaji) wanaujua ukweli, ila lazima wakuambie hivyo ili ubaki kuwa nao!
 
Mkuu nimevutiwa sans na busara zako...

Ukichunguza sala zote za Wakatoliki mwisho wa Sala huwa tunamaluzia
"TUNAOMBA HAYO KWA NJIA YA KRISTO BWANA WETU...AMINA)
Kwamba Kristo ndio Mshenga wetu wa Mwisho
Imetokea kama coincidence, na mimi nimemwambia vivyo hivyo!
 
Umenena vizuri. Lakini hajajibu swali la msingi, naomba unijibu:

Bikira Maria yuko hai kama alivyo Musa na Eliya huko mbiguni?

Kama ndiyo, unaweza ku-justify kwa angalia mstari mmoja wa Biblia?
Nakuja kwenye hili. Sina uhakika kama hili linafanyika pia kwa Waprotestant pia, au kama ni baadhi au wote, ila kwa kuwa mimi ni RC, nitajibu kwa faith ya Kanisa Katoliki. RC huwa wanatumia reference za aina tatu katika mafundisho ya imani ya Kanisa, ambayo ni Maandiko Matakatifu (Biblia), Mapokeo Matakatifu, na Ualimu wa Kanisa. Katika Mapokeo Matakatifu, tunafundishwa kwamba watakatifu wa Mungu wapo mbinguni, na kwa msingi huo, Mama Maria yupo mbinguni.
Utaweza kuuliza, kwa nini mnaenda zaidi (sio kinyume) ya yaliyoandikwa katika Biblia? Jibu lake lipo humo humo katika Biblia! Ni kwamba si kila kitu alichotenda na kuagiza Kristu kimeandikwa na kalamu, yaani kwa njia ya maandishi. Yohana 21:25 "Kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa yote, moja baada ya lingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa."
Kwa mantiki hiyo, mapadre wa RC wanakuwa wamesoma mambo mengi sana ndio maana hata upeo wao wa mambo huwa ni mkubwa ukilinganisha na wachungaji wengi (sio wote), kwani wanakuwa wamelazimika kusoma vya kutosha kuhusu Maandiko Matakatifu (Biblia), Mapokeo Matakatifu, na Ualimu wa Kanisa.


 
Nakuja kwenye hili. Sina uhakika kama hili linafanyika pia kwa Waprotestant pia, au kama ni baadhi au wote, ila kwa kuwa mimi ni RC, nitajibu kwa faith ya Kanisa Katoliki. RC huwa wanatumia reference za aina tatu katika mafundisho ya imani ya Kanisa, ambayo ni Maandiko Matakatifu (Biblia), Mapokeo Matakatifu, na Ualimu wa Kanisa. Katika Mapokeo Matakatifu, tunafundishwa kwamba watakatifu wa Mungu wapo mbinguni, na kwa msingi huo, Mama Maria yupo mbinguni.
Utaweza kuuliza, kwa nini mnaenda zaidi (sio kinyume) ya yaliyoandikwa katika Biblia? Jibu lake lipo humo humo katika Biblia! Ni kwamba si kila kitu alichotenda na kuagiza Kristu kimeandikwa na kalamu, yaani kwa njia ya maandishi. Yohana 21:25 "Kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa yote, moja baada ya lingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa."
Kwa mantiki hiyo, mapadre wa RC wanakuwa wamesoma mambo mengi sana ndio maana hata upeo wao wa mambo huwa ni mkubwa ukilinganisha na wachungaji wengi (sio wote), kwani wanakuwa wamelazimika kusoma vya kutosha kuhusu Maandiko Matakatifu (Biblia), Mapokeo Matakatifu, na Ualimu wa Kanisa.



Sasa kama hayakuandikwa yote, hayo mengine wanayosoma wao yalitoka wapi, maana hayakuandikwa!!
 
Sasa kama hayakuandikwa yote, hayo mengine wanayosoma wao yalitoka wapi, maana hayakuandikwa!!
Nimekwishakujibu hilo, hayakuandikwa katika Biblia (Yohana 21:25), ila yametolewa katika Mapokeo Matakatifu (ambayo yanaweza kuwa ni historia ya Kanisa iliyoandikwa sehemu nyingine). Ni kama vile ambavyo Martin Luther haandikwa wala kutajwa katika Biblia, ila mapokeo ya kihistoria yanaonyesha jinsi gani alivyoamua kujiondoa RC na kuanzisha Lutheran Church
 
Kinachonishangaza huyu mwanamke mpaka leo anaitwa virgin eti
Hata mimi sielewi inakuwaje mwanamke kazaa hafu bado awe bikira na wakati huo huo alikuwa na mume. Labda kama ni Ubikira wa heshima kama zilizo digrii za heshima kama udakitari na uprofesa ambao hupewa watu wasiosomea kufikia hadhi hizo.
 
Hata mimi sielewi inakuwaje mwanamke kazaa hafu bado awe bikira na wakati huo huo alikuwa na mume. Labda kama ni Ubikira wa heshima kama zilizo digrii za heshima kama udakitari na uprofesa ambao hupewa watu wasiosomea kufikia hadhi hizo.

Kwa Mungu hakuna linaloshindikana..
 
Hata mimi sielewi inakuwaje mwanamke kazaa hafu bado awe bikira na wakati huo huo alikuwa na mume. Labda kama ni Ubikira wa heshima kama zilizo digrii za heshima kama udakitari na uprofesa ambao hupewa watu wasiosomea kufikia hadhi hizo.
Inaelekea wewe bado sana kudiscuss na watu JF, subiri subiri upate maarifa kwanza
 
Sasa kama hayakuandikwa yote, hayo mengine wanayosoma wao yalitoka wapi, maana hayakuandikwa!!

Mkuu dotnet Biblia kwa uhakika kabisa imekamilika kama unavyoiona miaka ya 300AD...Je! Unafikiri kabla ya mwaka huo Wakristo wa kwanza wwalikuwa wanasali kwa kutumia kitu gani...?

Hapo ndo tunapata kitu kinaitwa Mapokeo ya KAnisa.....

Biblia pia ni mapokeo ya Kanisa ila yamekusanywa kwa style yake ...
 
Hata mimi sielewi inakuwaje mwanamke kazaa hafu bado awe bikira na wakati huo huo alikuwa na mume. Labda kama ni Ubikira wa heshima kama zilizo digrii za heshima kama udakitari na uprofesa ambao hupewa watu wasiosomea kufikia hadhi hizo.

Hii ya kuitwa Bikira sioni kama ina shida. Ni "jina" lake mbalo kimsingi lilitokama na yeye kubeba mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu (not biologically, but spiritually). Ni heshima kwake pia. Not a problem.
 
Mkuu dotnet Biblia kwa uhakika kabisa imekamilika kama unavyoiona miaka ya 300AD...Je! Unafikiri kabla ya mwaka huo Wakristo wa kwanza wwalikuwa wanasali kwa kutumia kitu gani...?

Hapo ndo tunapata kitu kinaitwa Mapokeo ya KAnisa.....

Biblia pia ni mapokeo ya Kanisa ila yamekusanywa kwa style yake ...

Neno zuri😊
 
Nafahamu mmekuwa mkifudishwa huo uongo hivyo na wachungaji wenu, na ni mengi tu huwa wanawaongopea kuhusu Roman Catholic. Nafahamu huwa wanawaambia kuwa kule RC muda wote ni Salamu Maria (kama ulivyoandika). Nafahamu pia kuwa huwa wanawadanganya kuwa kule RC hawawasiliani na Yesu (hii ni ajabu sana!). Kwa ufupi, watoto waliozaliwa katika familia za Kiprotestant, hawajawahi kupata fursa ya kuujua Ukatoliki, kwa hiyo ni rahisi kukaririshwa maneno kuwa RC huwa wanafanya hiki na kile. Lazima hao (wachungaji wenu) wawaambie hivyo ili kuhalalisha their protest (refer neno 'Protestants') against the Church of Our Lord Jesus Christ. Si kazi rahisi kuwafamisha ukweli wa mambo watoto waliozaliwa na wazazi ambao ni Waprotestant, lakini mtu akitaka kujua bila kushinikizwa, ataijua kweli.
Jabulani, Laudetur Jesus Christus...... Tumsifu Yesu Kristu........:israel:
 
Kama Bikira Maria anaweza kuwaombea Dhambi mkasamehewa sasa kwanini Yesu alikuja. Mungu angeweza kumtumia huyo bikira maria yakaisha.
pili ni wapi kwenye bibble Yesu alisema ombeni kupitia Mama yangu nami nitawasamehe??? Sana Sana alisema MTU hawezi kufika kwa baba ila kupitia kwangu but sio kwa mama take
Tatu kwanini mnachoga sanamu na kuzipigia magoti ilihali hao mnaowapigia magoti wako hai???
kwa mawazo yangu Mimi ni kuwa kilichokufa ndio kinachochongewa sanamu....why mnachonga sanamu kwa MTU aliye hai???
 
Mkuu dotnet Biblia kwa uhakika kabisa imekamilika kama unavyoiona miaka ya 300AD...Je! Unafikiri kabla ya mwaka huo Wakristo wa kwanza wwalikuwa wanasali kwa kutumia kitu gani...?

Hapo ndo tunapata kitu kinaitwa Mapokeo ya KAnisa.....

Biblia pia ni mapokeo ya Kanisa ila yamekusanywa kwa style yake ...

Huwezi kukuta mchungaji wa kiprotestant akifundisha hili .....ili ule msingi wao wa SOLA SCRIPTURA ambao mwasisi wake ni Martin Luther usipate changamoto ............
 
Twende Taratibu.

Yesu ni mwana wa Mungu na ni Mungu.

Jesus aliexist mda mrefu sana before hata Mary kuwepo. Amejidhihirisha kwetu kupitia Mary. But haimanishi wanauhusian Mary na Jesus wapo kama mimi na Mama yangu.

Sema indivyo ilivyofundishwa ila ukweli utabaki palepale, she is full of grace and blessed. labda kama huelewi maandiko matakatifu
 
Back
Top Bottom