Hahahaaa eti katili hivi!
Sikiliza, kama huamini Mungu yupo basi nadhani huamini pia kuwa shetaji yupo. Lakini shetani ndio hupenda kuuliza maswali ya aina hii, kuwa mbona Mungu katili watu wanakufa ametulia tu? Upendo gani sasa? Shetani husema hata upendo inatakiwa kumpa anayestahili tu sio kila mtu, shetani pia husema haiwezekani kumpenda na kumbariki adui yako, au kugeuza shavu la upande wa pili libatuliwe pia baada ya kupigwa la kwanza au kutotaka mdeni wako akurudishie. Haya ni maswali au maneno shatani huwapotezea mbali waaamini walio lege lege. Maana majibu ya maswali yote haya hakika anayo Roho Mtakatifu anayeishi kwa waaminio. Yeye ni mwalimu na mfariji ila kwa wanaoamini tu.
Usiseme Mungu ni katili. Mungu hutimiza alichopanga. Na ana hasira pia, ila usiombe ikikute!! Shukuru umezaliwa kizazi ambacho Mungu haleti tena gharika. Wewe unaongelea ebola wanakufa hao watu sita saba tu, hujui zamani za kale ilikuwa Mungu akichukia anafuta kizazi chote tena kwa kuangamiza? Hujasoma habari ya Sodoma au Nuhu na Safina eeh! Hapana chezea hasira yake! Au hujasoma alivyowayosa askari wote wa misri waliokuwa wanamfuata Musa bahari ya shamu? Hao watu sita saba wa ebola unasema huyu Mungu vipi?
Kumbukq Mungu anatisha! Usichukulie simple tu hii habari aisee