Kuna tofauti kati ya kutotaka kufanya kazi za ndani na kukosa muda wa kufanya hizo kazi ndani. Wewe sio kwamba umekosa mda wa kufanya kazi ndani, bali hutaki kwa sababu hupendi kufanya hivyo.
Nataka nikwambie kitu kimoja; upendo sio ngono peke yake. Na kama unadhani upendo ni ngono peje yake basi wewe bado hujajua maana ya upendo.
Hivyo vishughuli vidogo vidogo ambavyo wewe unavidharau na hutaki/huna mda wa kuvifanya ndio ambavyo vinasaidia kuongeza upendo katika ndoa. Na kwa taarifa yako, kufanya hizo shughuli kwa mke sio ombi bali ni lazima kwa sababu ni wajibu wako, hata kwenye mafundisho ya ndoa inafundishwa hivyo.
Hakuna mtu katika ulimwengu huu anayependa kuishi na mtu mvivu. Kama nyinyi wanawake msivyopenda kuwa na mwanaume asiyekuwa na kazi ya kufanya hali kadhalika wanaume pia hawapendi mwanamke ambaye hataki kujishughulisha na kitu chochote. Hakuna mwanaume anayependa mwanamke ambaye amekaa nyumbani kama pambo tu; kazi yake yeye ni kula, kwenda chooni, kuoga, dudu na kulala.
Uvivu wako wa kipumbavu utasababisha kutoa mwanya wa ndoa yako kuja kuvunjika kwa sababu ipo siku atatokea mwanamke ambaye atagundua mapungufu hayo katika ndoa yako na atayatumia mapungufu hayo kama silaha ya kumteka mumeo.
USHAURI WA BURE
Usiruhusu uvivu wako na mawazo yako ya kipumbavu yakawa ndio chanzo cha kuharibu ndoa yako. And yes, ninasema ni uvivu na mawazo ya kipumbavu kwa sababu unajua jambo sahihi unalopaswa kufanya, lakini kwa sababu ya uvivu na mawazo yako ya kipumbavu unaamua ku-justify wrong as right.