Ilikuwa nife jioni hii ya leo!!!

Ilikuwa nife jioni hii ya leo!!!

Ni faini ya kuwakimbia tu....na baada ya kuhakiki tulikuwa wema kwa kuichangua gari kila mahali ilibidi waripoti katika radio call kuwa hatuna 'mzigo' (maana habari zilishaenea kwa simu ya upepo ili waongezewe vikosi na nguvu zaidi) wakuu wakasema waachieni iwapo wapo sawa.
Usiniogope mkuu mimi sio Takukuru najua laki ilikutoka mimi ni mkuu wao wa kazi walisema umetoa 50 hebu niweke wazi mkuu walinizunguka
 
Mkuu pole sana,ila hongera kwa kupost maana pamoja na kipigo lakini ukaona ututahadharishe wenzako.
Na haswa hilo ndiyo lengo langu watu wajihadhari.....nimekuwa tofauti na wale wanaopost mambo mazuri tu yanayo wakuta na mabaya kuyaficha.

Hakika kama jamii ingesimama katika ukweli tungejenga taifa imara, changudoa angejitokeza na kueleza majuto yake, mwizi angejitokeza na kueleza majuto yake, aliathirika angejitokeza na kueleza hali ilivyokuwa na watu wangejifunza hakika......ila kwa bahati mbaya wanaogopa kukashifiwa na kuvunjwa moyo na uzao huu wa sasa na mwisho wake jamii haijifunzi na makosa waliyotenda wao au mapito yanarudiwa kila leo na kupoteza nguvu kazi ya Taifa.
 
Huyu ametoa si chini ya laki mbili... Nimepita hapo saa tatu nikitokea mkinga kwa stori ilivyo, watakuwa wamemkamua vilivyo....
Tii sheria bila shuruti na polisi ni wema wapo kwa ajili yetu, hili ndiyo funzo ninalotaka tujifunze.
 
Wewe ni mjinga yani ubahilii wa kulipa elf 30 ya fine ukataka kuua familia yako yote???
Je wangeamua kukumiminia risasi ingekuaje???? We umekua mwili tu lakini kichwani huna tofauti na le mutuz
 
Wewe ni mjinga yani ubahilii wa kulipa elf 30 ya fine ukataka kuua familia yako yote???
Je wangeamua kukumiminia risasi ingekuaje???? We umekua mwili tu lakini kichwani huna tofauti na le mutuz
Bora hata ingekuwa 30! Wale hawahusiki na hayo zaidi ya doria tu.....hili ni somo nililo lipata kwa wana usalama wetu na tangu sasa nitajifunza zaidi sheria za Nchi yangu niipendayo.
 
Huyu ametoa si chini ya laki mbili... Nimepita hapo saa tatu nikitokea mkinga kwa stori ilivyo, watakuwa wamemkamua vilivyo....
Duuuu halafu eti anasema alilipa faini tu polisi walivyo na njaa hivi.tena nasikia aliwahamishia kwa tigo pesa
 
Yaani bado unajiona wa kiume kwa kuhatarisha maisha ya mwanao kisa leseni?? Mtu wa masafa yupi anaekimbia polisi?? Masafa na karina??? Masafa kutoka dar mpaka tanga?? Masafa leseni inaishaga??? Acha kujisifu ujinga wewe. Masafa hujui Hali ya kiusalama ya tanga??? Hujui ulivyomwathiri kisaikolojia mwanao... Ni mpaka utakapomgombeza akikosea halaf akuambie baba nitakuitia polisi sasa hivi... Ndo utajua ulifanya upumbavu. Eti masafa halaf unasikiliza mafundi wanakwambia kula kona....fundi mwenyewe hata sehewa hana. Yaani bwashe umezingua pumbavu kabisa.
Mimi ni dereva wa Lori na miaka mingi nipo barabarani ila hili sina wa kumbebesha zaidi ni kama changamoto.
 
Yaani kati ya watu fair ni Polisi, hasa unapokubali kuzungumza nao. Ulichofanya ulikuwa unawajaribu, na wao hawajaribiwi. Umeaibika mbele ya mwanao
 
Yaani bado unajiona wa kiume kwa kuhatarisha maisha ya mwanao kisa leseni?? Mtu wa masafa yupi anaekimbia polisi?? Masafa na karina??? Masafa kutoka dar mpaka tanga?? Masafa leseni inaishaga??? Acha kujisifu ujinga wewe. Masafa hujui Hali ya kiusalama ya tanga??? Hujui ulivyomwathiri kisaikolojia mwanao... Ni mpaka utakapomgombeza akikosea halaf akuambie baba nitakuitia polisi sasa hivi... Ndo utajua ulifanya upumbavu. Eti masafa halaf unasikiliza mafundi wanakwambia kula kona....fundi mwenyewe hata sehewa hana. Yaani bwashe umezingua pumbavu kabisa.
Yaaani umeua kabisa. Mna utani na wagosi?
 
Duh kama movie vile ni bora ungesimama ukatoa elf 30 ya lesen yakaisha mkuu ila pole wakunyumba
 
Mkuu wangu mi yote hayo 9; mi bado akili yangu ipo kwa mtoto tu matokeo yangu akili imegoma kusikia la mnadi sala msikitini wala la mpiga kengele kanisanii!! Yaani kama isingekuwa mtoto... hii kwangu ingekuwa ni one of the best road adventure! Ingawaje mimi mwenyewe sifahamu uchungu wa mtoto kv sinae lakini nikiona mtu anacheza na maisha ya mtoto; nakuaga mkali sana... dada zangu wenyewe wananijua! Si unajua wanawake wanavyopenda kupiga watoto?! Hawawezi kufanya ushenzi kama huo mbele yangu hata siku moja.
Upo sahihi mkuu hao walikuwa na subira kwa vile waliona na mtoto yupo ndani.
Nina uhakika wakat wanamsimamisha walimuona na mtoto ndani na ndio maana hawakuwachakaza kwa risasi.
Kimsingi mleta mada popote utakapokuwa tambua mtoto kaokoa maisha yako na yenu wote,kama anavyosema mleta mada kuna askari wengine walokuja na private cars na walikuwa zaid ya 30 tafsir yake ni kuwa walijua ni magaidi au majambazi ila mtoto ndio aliwafanya wasichukue maamuzi mengine.
 
Back
Top Bottom