siioni kabisa, ile chadema iliyoenda kupiga kambi kanda ya pwani zaidi ya wiki moja.
Ile chadema iliyosambaa kanda zote kuelemisha wananchi kuhusu ufisadi na maovu ya ccm kwa ujumla.
Ile ya lema, mnyika, mdee, kwa upande mmoja sugu,silinde,msigwa kwa upande mwingine. Lissu, wenje na wengineo.
Ile ya viongozi wenye upeo toka makao makuu,pr.safari, pr.baregu na wengineo.
Ile ya vijana makamanda tofauti toka idara tofauti makao makuu.
Kweli leo chadema ni ya kupelekwa ikulu na akina sumaye, masha, msindayi na mahanga?
Wako wapi makamanda wa ukweli tuliowazoea wananchi, waliokipaginia chama kwenye jua na mvua usiku na mchana.?
Najua mtasema wengi wapo bize na kampeni kwenye majimbo yao.
Lakini binafsi naamini lema, lissu alieashinda asilimia tisini ya serikali za mitaa, silinde ambae wananchi wake wanaimba chadema hadi usingizini, sugu ambaye ni rahisi wa mbeya, mdee mwanamke shujaa wa siasa za upinzani tanzania na wengineo.
Hawawezi kushindwa kupoteza siku mbili kwenye majimbo yao na kumnadi lowassa kwenye mbio za urais.
Poleni makamanda najua wengi wenu mnamadukuduku mioyoni mwenu ila ni ngumu kusema kwa kuogopa kuitwa wasaliti.
Kwa hatua ilipofikia chadema, kilikuwa sio chama cha kutegemea sumaye awapeleke ikulu wala masha wala msindayi hata lowassa mwenyewe.!
Bado naililia chadema yangu ya ukweli na mtetezi halisi wa watanzania sio hawa wasaka madaraka tu.!
Tukutane october 25
Yaani pumba tupu ...hao uliowataja wote ni wagombea ubunge na wana kazi maalumu ya kuzunguka na chopa kwenye msjimbo kadhaa kumnadi mgombea urais hata ratiba ya chama hamuijui then mnaajiita chadema......hamjalazimishwa c muondokee
Hata hivyo kwa sasa iliyokuwa CHADEMA ni ccm na iliyokuwa CCM ndio chademaKwanini tunaamini Lowasa atasimamia kile tulichopigania kwa miaka mingi ...... Akiwageuka mtalia na nani ..... Hivi kama swala ni Uchadema .....Chadema ni nini .....tukiamua Leo CCM kuiita Chadema na Chadema kuwa CCM bado utaichagua Chadema ..... nini kimetuingia hadi tunamsaliti jemedari wetu aliyesimama na sisi wakati wa jua na mvua ...
Mkuu bandiko lako linaacha hisia kali za kizalendo ndani ya chama, lakini hakuna namna.Hivi Chadema wanategemea dakika hii ku handle issue ya Dr Slaa na kushinda uchaguzi .....issue ya Zitto ilichukua muda mrefu na bado ikaacha majeraha ....sijui tumekumbwa na nini .....tumeacha vijanà wa M4U na watu wetu kueneza uongo dhidi ya mtu anayejua alijenga wapi na abomoe wapi tena dakika hizi ....huu ni upuuzi kufikiri mnaweza kumfanyia propaganda Dr Slaa .... Muda haupo na atawaumiza vibaya ....
Kweli mkuu, its very painful to see the 'real' and strong chadema dying that easily.Very painful ... Watu hawajitambui tena .... Kama wengi wape kwa mtindo huu Muumba wangu anisamehe .....
Siioni kabisa, ile Chadema iliyoenda kupiga kambi Kanda ya pwani zaidi ya wiki moja.
Ile Chadema iliyosambaa Kanda zote kuelemisha Wananchi kuhusu Ufisadi na maovu ya ccm kwa ujumla.
Ile ya Lema, Mnyika, Mdee, kwa upande mmoja Sugu,Silinde,Msigwa kwa upande mwingine. Lissu, wenje na wengineo.
Ile ya viongozi wenye upeo toka makao makuu,Pr.Safari, Pr.Baregu na wengineo.
Ile ya vijana makamanda tofauti toka idara tofauti makao makuu.
Kweli leo Chadema ni ya kupelekwa ikulu na akina Sumaye, Masha, Msindayi na Mahanga?
Wako wapi makamanda wa ukweli tuliowazoea wananchi, waliokipaginia chama kwenye jua na mvua usiku na mchana.?
Najua mtasema wengi wapo bize na kampeni kwenye majimbo yao.
Lakini binafsi naamini Lema, Lissu alieashinda asilimia tisini ya serikali Za mitaa, Silinde ambae wananchi wake wanaimba Chadema hadi usingizini, Sugu ambaye ni Rahisi wa Mbeya, Mdee mwanamke shujaa wa siasa za upinzani Tanzania na wengineo.
Hawawezi kushindwa kupoteza siku mbili kwenye majimbo yao na kumnadi Lowassa kwenye mbio za urais.
Poleni makamanda najua wengi wenu mnamadukuduku mioyoni mwenu ila ni ngumu kusema kwa kuogopa kuitwa wasaliti.
Kwa hatua ilipofikia Chadema, kilikuwa sio chama cha kutegemea Sumaye awapeleke ikulu wala Masha wala Msindayi hata Lowassa Mwenyewe.!
Bado naililia Chadema yangu ya ukweli na mtetezi halisi wa watanzania sio hawa wasaka madaraka tu.!
Tukutane October 25
naona siku hizi kulitaja jina la mbowe kumekuwa chungu! au sijaangalia vizuri kwenye hiyo list yako nini?Nakumbuka chadema yetu Dr slaa mnyika mdee lissu
Nakwambia tutamkumbuka dr Slaa daima.mtazungumka weeeee lakkni mwisho wa siku mtarudi kwa Dr Slaa. Na nasema Mbowe atakuwa wa kwanza kupiga magoti kwa Slaa pale Chadema itakapokuwa imepasuka na kusambaratika, na wafuasi sasa kuanza kudai haki zao
Kwanini tunaamini Lowasa atasimamia kile tulichopigania kwa miaka mingi ...... Akiwageuka mtalia na nani ..... Hivi kama swala ni Uchadema .....Chadema ni nini .....tukiamua Leo CCM kuiita Chadema na Chadema kuwa CCM bado utaichagua Chadema ..... nini kimetuingia hadi tunamsaliti jemedari wetu aliyesimama na sisi wakati wa jua na mvua ...
Hakuna gamba hapa watu tunapenda mabadiliko ya ukweli siyo ya maigizo na yanayodhaminiwa na akina Rostam.!Wacheni mchezo wa kitoto, nyie magamba mnajifanya makamanda kujadili mambo ya CDM. ukilia kuliko mwenye mtoto ujue wewe ni ...