Iko hivi; no reform,no election ni hitaji la sisi wapiga kura wa vyama vyote kwa muda mrefu,tunashangaa watu wasiotaka usawa,uhuru na haki

Iko hivi; no reform,no election ni hitaji la sisi wapiga kura wa vyama vyote kwa muda mrefu,tunashangaa watu wasiotaka usawa,uhuru na haki

Jamiitrailer

Senior Member
Joined
Oct 20, 2019
Posts
161
Reaction score
382
Habari wakuu
Watu wengi wameandika kuhusu ajenda ya Chadema ya kutaka uwepo wa mabadiliko katika taratibu na sheria zinazosimamia chaguzi zetu kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Wengine wanaunga mkono ajenda ya Chadema,na wengine wanaunga mkono lakini wakisema hakuna muda wa kutosha kati ya sasa na October, na wengine kama Paschal Mayala wanakejeli wakisema ajenda waliyokuja nayo Chadema ni UTOPIA...dhana isiyoweza kutekelezaka...na akaenda mbali zaidi kwa kusema kwamba Chadema imekuwa na fursa nyingi za kushinda chaguzi huko nyuma wakati CCM ikiwa dhaifu lakini hawakushinda kwa vile tu HAWAKUJIPANGA.

Anachomaanisha Mayala ni kwamba CCM ilishinda japo ilikuwa haina mvuto kwa wapiga kura kwa vile tu ilijipanga.

Nnachotaka kumueleza Mayala na wenzie wenye mtazamo huo kwamba SISI WAPIGA KURA tuliliona hilo jambo muda mrefu...na TULIELWEA kwamba kujipanga huko kwa ccm kunatokana sababu moja tu....,WATENDAJI WOTE WANAOSIMAMIA MFUMO WA UCHAGUZI ni wateule wa rais/mwenyekiti wa CCM..na wanawajibika kwake.
Mifano ni mingi sana na inaeleweka....tuchukue mfano..,...uchaguzi wa mkuu 2010 kura za urais jimbo la Karatu aliongoza Dr. Slaa kwa mbali..ndicho kilichopo katika rekodi hata za tume yenyewe, lakini matokeo yaliyotangazwa na tume kwa umma yalionesha Kikwete kumshinda Slaa eneo hilo.
Mfano mwingine, uchaguzi mkuu 2015 matokeo ya urais eneo la Tunduma,Edward Lowassa alimshinda Magufuli kwa mujibu wa matokeo yaliyobabdikwa katika vituo vyote. Lakini matokeo ya tume ya uchaguzi taifa yaliyokuwa yakitangazwa katika TV yalionesha kinyume chake.

Sisi wananchi tuliiona hali hiyo na tukasema ili mgombea tunayemtaka ashinde hapana budi kufanyike mabadiliko makubwa ya mfumo mzima wa uchaguzi, hususan katiba kwa ujumla.
Kilichofanyika uchaguzi wa 2020,bila kutaja kilichofanyika mwaka jana katika serikali chaguzi za serikali za mitaa,..bila shaka mtu yeyote mwenye akili timamu ataungana na wananchi kutaka hayo mabadiliko.

Mabadiliko yanayohitajika ni kwa mapana yake ili kufaidisha wananchi na taifa kwa ujumla na siyo kwa maslahi ya vyama.
Kwa mfano, kwa vile hakuna kipengele kinachoruhusu mgombea binafsi,utakuta wagombea ambao wanapendwa na wananchi lakini hawatakiwi na vyama vyao kwa ubabe wa kichama...wananchi wanakosa mwakilishi makini.
Sisi wananchi tumekuwa tukivishangaa vyama vya siasa vya upinzani vinavyoshiriki chaguzi kila msimu katika mazingira ambayo hata mwendawazimu anajua,yanatoa upendeleo kwa chama tawala.
kwa Chadema kuja na hilo wazo la No reform,No election, kimsingi linagusa kile ambacho sisi wananchi tulikihitaji kwa muda mrefu....na ndo maana umeona muitikio wa wanachi umekuwa mkubwa.

Wenye mamlaka ya kutunza amani ya nchi hii wanatakiwa kujua jambo moja ....unaporuhusu wananchi kudhulumiwa haki zao siku hadi siku,...ile hasira ya kulipuka ikifika ,madhara yake yanakuwa makubwa....,kama Ivory coast ilipomchoka Bagbo, au Burkina Fasso ilipomchoka Campare kwa figisu zao
Sasa tusifike huko kwa vile hakuna watu wapole duniani...binadamu wote ni wanyama wendawazimu...ni suala la muda tu atalipuka kama volcano.

Kuna watu wamesema hoja ya mabadiliko kwa sasa imechelewa.
Sisi wananchi tunauliza imechelewa kwa nani....wakati sisi wenyewe wapiga kura hatuna haraka kihivyo..tuko tayari tuahirishe hata kwa mwaka miaka 2 lakini mabadiliko yafanyike.
Huyo mwenye HARAKA tunataka tujue ana harakia nini.
 
Mabadiliko yanawezekana tena vizuri tu hata kwenye kipindi hiki kilichobaki sema kigugumizi sijui kinatokea wapi !!?

UGUMU ULIPO NDIO UJUE KWELI CCM HUTEGEMEA WIZI WA KULA VINGINEVYO WANGEKUWA WANAJIAMINI WANGERUHUSU MABADILIKO.

WANGEKAA VIKAO USIKU NA MCHANA SEMA NDIO VILE WAOGA KWA SABABU BILA KUIBA NA KUNUNUA WAPINZANI CCM HAWATOBOI.
 
Habari wakuu
Watu wengi wameandika kuhusu ajenda ya Chadema ya kutaka uwepo wa mabadiliko katika taratibu na sheria zinazosimamia chaguzi zetu kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Wengine wanaunga mkono ajenda ya Chadema,na wengine wanaunga mkono lakini wakisema hakuna muda wa kutosha kati ya sasa na October, na wengine kama Paschal Mayala wanakejeli wakisema ajenda waliyokuja nayo Chadema ni UTOPIA...dhana isiyoweza kutekelezaka...na akaenda mbali zaidi kwa kusema kwamba Chadema imekuwa na fursa nyingi za kushinda chaguzi huko nyuma wakati CCM ikiwa dhaifu lakini hawakushinda kwa vile tu HAWAKUJIPANGA.
Anachomaanisha Mayala ni kwamba CCM ilishinda japo ilikuwa haina mvuto kwa wapiga kura kwa vile tu ilijipanga.

Nnachotaka kumueleza Mayala na wenzie wenye mtazamo huo kwamba SISI WAPIGA KURA tuliliona hilo jambo muda mrefu...na TULIELWEA kwamba kujipanga huko kwa ccm kunatokana sababu moja tu....,WATENDAJI WOTE WANAOSIMAMIA MFUMO WA UCHAGUZI ni wateule wa rais/mwenyekiti wa CCM..na wanawajibika kwake.
Mifano ni mingi sana na inaeleweka....tuchukue mfano..,...uchaguzi wa mkuu 2010 kura za urais jimbo la Karatu aliongoza Dr. Slaa kwa mbali..ndicho kilichopo katika rekodi hata za tume yenyewe, lakini matokeo yaliyotangazwa na tume kwa umma yalionesha Kikwete kumshinda Slaa eneo hilo.
Mfano mwingine, uchaguzi mkuu 2015 matokeo ya urais eneo la Tunduma,Edward Lowassa alimshinda Magufuli kwa mujibu wa matokeo yaliyobabdikwa katika vituo vyote. Lakini matokeo ya tume ya uchaguzi taifa yaliyokuwa yakitangazwa katika TV yalionesha kinyume chake.

Sisi wananchi tuliiona hali hiyo na tukasema ili mgombea tunayemtaka ashinde hapana budi kufanyike mabadiliko makubwa ya mfumo mzima wa uchaguzi, hususan katiba kwa ujumla.
Kilichofanyika uchaguzi wa 2020,bila kutaja kilichofanyika mwaka jana katika serikali chaguzi za serikali za mitaa,..bila shaka mtu yeyote mwenye akili timamu ataungana na wananchi kutaka hayo mabadiliko.

Mabadiliko yanayohitajika ni kwa mapana yake ili kufaidisha wananchi na taifa kwa ujumla na siyo kwa maslahi ya vyama.
Kwa mfano, kwa vile hakuna kipengele kinachoruhusu mgombea binafsi,utakuta wagombea ambao wanapendwa na wananchi lakini hawatakiwi na vyama vyao kwa ubabe wa kichama...wananchi wanakosa mwakilishi makini.
Sisi wananchi tumekuwa tukivishangaa vyama vya siasa vya upinzani vinavyoshiriki chaguzi kila msimu katika mazingira ambayo hata mwendawazimu anajua,yanatoa upendeleo kwa chama tawala.
kwa Chadema kuja na hilo wazo la No reform,No election, kimsingi linagusa kile ambacho sisi wananchi tulikihitaji kwa muda mrefu....na ndo maana umeona muitikio wa wanachi umekuwa mkubwa.

Wenye mamlaka ya kutunza amani ya nchi hii wanatakiwa kujua jambo moja ....unaporuhusu wananchi kudhulumiwa haki zao siku hadi siku,...ile hasira ya kulipuka ikifika ,madhara yake yanakuwa makubwa....,kama Ivory coast ilipomchoka Bagbo, au Burkina Fasso ilipomchoka Campare kwa figisu zao
Sasa tusifike huko kwa vile hakuna watu wapole duniani...binadamu wote ni wanyama wendawazimu...ni suala la muda tu atalipuka kama volcano.

Kuna watu wamesema hoja ya mabadiliko kwa sasa imechelewa.
Sisi wananchi tunauliza imechelewa kwa nani....wakati sisi wenyewe wapiga kura hatuna haraka kihivyo..tuko tayari tuahirishe hata kwa mwaka miaka 2 lakini mabadiliko yafanyike.
Huyo mwenye HARAKA tunataka tujue ana harakia nini.
Kwanini mng'ang'aniza kuwa sisi wananchi, sisi wananchi? Kwani wakati mnaleta hiyo No Reform, No Reform mlitushirikisha? Kama imebuma shauri yenu na MKOME kutujumuisha wananchi wote! PUMBAVU!!
 
Habari wakuu
Watu wengi wameandika kuhusu ajenda ya Chadema ya kutaka uwepo wa mabadiliko katika taratibu na sheria zinazosimamia chaguzi zetu kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Wengine wanaunga mkono ajenda ya Chadema,na wengine wanaunga mkono lakini wakisema hakuna muda wa kutosha kati ya sasa na October, na wengine kama Paschal Mayala wanakejeli wakisema ajenda waliyokuja nayo Chadema ni UTOPIA...dhana isiyoweza kutekelezaka...na akaenda mbali zaidi kwa kusema kwamba Chadema imekuwa na fursa nyingi za kushinda chaguzi huko nyuma wakati CCM ikiwa dhaifu lakini hawakushinda kwa vile tu HAWAKUJIPANGA.
Anachomaanisha Mayala ni kwamba CCM ilishinda japo ilikuwa haina mvuto kwa wapiga kura kwa vile tu ilijipanga.

Nnachotaka kumueleza Mayala na wenzie wenye mtazamo huo kwamba SISI WAPIGA KURA tuliliona hilo jambo muda mrefu...na TULIELWEA kwamba kujipanga huko kwa ccm kunatokana sababu moja tu....,WATENDAJI WOTE WANAOSIMAMIA MFUMO WA UCHAGUZI ni wateule wa rais/mwenyekiti wa CCM..na wanawajibika kwake.
Mifano ni mingi sana na inaeleweka....tuchukue mfano..,...uchaguzi wa mkuu 2010 kura za urais jimbo la Karatu aliongoza Dr. Slaa kwa mbali..ndicho kilichopo katika rekodi hata za tume yenyewe, lakini matokeo yaliyotangazwa na tume kwa umma yalionesha Kikwete kumshinda Slaa eneo hilo.
Mfano mwingine, uchaguzi mkuu 2015 matokeo ya urais eneo la Tunduma,Edward Lowassa alimshinda Magufuli kwa mujibu wa matokeo yaliyobabdikwa katika vituo vyote. Lakini matokeo ya tume ya uchaguzi taifa yaliyokuwa yakitangazwa katika TV yalionesha kinyume chake.

Sisi wananchi tuliiona hali hiyo na tukasema ili mgombea tunayemtaka ashinde hapana budi kufanyike mabadiliko makubwa ya mfumo mzima wa uchaguzi, hususan katiba kwa ujumla.
Kilichofanyika uchaguzi wa 2020,bila kutaja kilichofanyika mwaka jana katika serikali chaguzi za serikali za mitaa,..bila shaka mtu yeyote mwenye akili timamu ataungana na wananchi kutaka hayo mabadiliko.

Mabadiliko yanayohitajika ni kwa mapana yake ili kufaidisha wananchi na taifa kwa ujumla na siyo kwa maslahi ya vyama.
Kwa mfano, kwa vile hakuna kipengele kinachoruhusu mgombea binafsi,utakuta wagombea ambao wanapendwa na wananchi lakini hawatakiwi na vyama vyao kwa ubabe wa kichama...wananchi wanakosa mwakilishi makini.
Sisi wananchi tumekuwa tukivishangaa vyama vya siasa vya upinzani vinavyoshiriki chaguzi kila msimu katika mazingira ambayo hata mwendawazimu anajua,yanatoa upendeleo kwa chama tawala.
kwa Chadema kuja na hilo wazo la No reform,No election, kimsingi linagusa kile ambacho sisi wananchi tulikihitaji kwa muda mrefu....na ndo maana umeona muitikio wa wanachi umekuwa mkubwa.

Wenye mamlaka ya kutunza amani ya nchi hii wanatakiwa kujua jambo moja ....unaporuhusu wananchi kudhulumiwa haki zao siku hadi siku,...ile hasira ya kulipuka ikifika ,madhara yake yanakuwa makubwa....,kama Ivory coast ilipomchoka Bagbo, au Burkina Fasso ilipomchoka Campare kwa figisu zao
Sasa tusifike huko kwa vile hakuna watu wapole duniani...binadamu wote ni wanyama wendawazimu...ni suala la muda tu atalipuka kama volcano.

Kuna watu wamesema hoja ya mabadiliko kwa sasa imechelewa.
Sisi wananchi tunauliza imechelewa kwa nani....wakati sisi wenyewe wapiga kura hatuna haraka kihivyo..tuko tayari tuahirishe hata kwa mwaka miaka 2 lakini mabadiliko yafanyike.
Huyo mwenye HARAKA tunataka tujue ana harakia nini.
Ni kweli kwa muda mrefu watanzania walikuwa wanatushangaa tunavyoshiriki uchaguzi ambao Mshindi anajulikana kabla ya kuchaguliwa.
 
Kwanini mng'ang'aniza kuwa sisi wananchi, sisi wananchi? Kwani wakati mnaleta hiyo No Reform, No Reform mlitushirikisha? Kama imebuma shauri yenu na MKOME kutujumuisha wananchi wote! PUMBAVU!!
Kwa muda mrefu wananchi walisubiri Chama kinachoitikia matakwa yao.

Waliokuwepo walikuwa wanakimbilia madaraka tu na ruzuku
 
Kwa muda mrefu wananchi walisubiri Chama kinachoitikia matakwa yao.

Waliokuwepo walikuwa wanakimbilia madaraka tu na ruzuku
Wananchi gani wewe? Yaani mlete ujinga wenu wananchi waukatae eti ni wa wananchi? Huu upumbavu danganyaneni huko huko Chadema!
 
Kwanini mng'ang'aniza kuwa sisi wananchi, sisi wananchi? Kwani wakati mnaleta hiyo No Reform, No Reform mlitushirikisha? Kama imebuma shauri yenu na MKOME kutujumuisha wananchi wote! PUMBAVU!!
Ugumu wako wa kuelewa hilo jambo dogo unatokana na nini?
Mimi ni mwananchi mpiga kura kama wewe. Wapiga kura wenzangu wengi kwa muda mrefu tumelalamikia mfumo wa usimamizi wa uchaguzi ambao hautoi haki ya kutangazwa kwa mgombea tunayemtaka.
Sistoshe, kuna wagombea ambao sisi wananchi tuliwataka lakini wakakatwa na vyama vyao na hivyo kutukosesha haki ya kupata mwakilishi bora...
Sasa Chadema kwa vile wamedandia ombi na kiu yetu ya muda mrefu kwa nini tusiwaunge mkono? Japo wamekuja kwa kuchelewa. Sasa wewe ulitaka uombwe maoni yako katika lipi....,una maanisha unaona sawa hali ikibaki kama ilivyo mshindi wa uchaguzi atangazwe kama watakavyoamua tume na siyo wananchi?

Lakini kuna hili kubwa....,kama unawauliza kwa nini Chadema hawajaomba kwanza ridhaa ya wananchi ili kutaka mabadiliko ya .mfumo wa uchaguzi,..kwa nini hujaiuliza serikali iliyoamua kuzima mchakato wa rasimu ya katiba mpya wakati maoni yaliyochukuliwa na tume ya Warioba yaliweka bayana kile ambacho wananchi wanataka katika mfumo wa uchaguzi?
 
Ugumu wako wa kuelewa hilo jambo dogo unatokana na nini?
Mimi ni mwananchi mpiga kura kama wewe. Wapiga kura wenzangu wengi kwa muda mrefu tumelalamikia mfumo wa usimamizi wa uchaguzi ambao hautoi haki ya kutangazwa kwa mgombea tunayemtaka.
Sistoshe, kuna wagombea ambao sisi wananchi tuliwataka lakini wakakatwa na vyama vyao na hivyo kutukosesha haki ya kupata mwakilishi bora...
Sasa Chadema kwa vile wamedandia ombi na kiu yetu ya muda mrefu kwa nini tusiwaunge mkono? Japo wamekuja kwa kuchelewa. Sasa wewe ulitaka uombwe maoni yako katika lipi....,una maanisha unaona sawa hali ikibaki kama ilivyo mshindi wa uchaguzi atangazwe kama watakavyoamua tume na siyo wananchi?

Lakini kuna hili kubwa....,kama unawauliza kwa nini Chadema hawajaomba kwanza ridhaa ya wananchi ili kutaka mabadiliko ya .mfumo wa uchaguzi,..kwa nini hujaiuliza serikali iliyoamua kuzima mchakato wa rasimu ya katiba mpya wakati maoni yaliyochukuliwa na tume ya Warioba yaliweka bayana kile ambacho wananchi wanataka katika mfumo wa uchaguzi?
Kwahiyo Mimi sio mwananchi mpiga kura? Wewe umesema wananchi,maana yake wote sio? Je, Mimi nimo?
 
Kupiga kura hakuhitqji mtu kuwa lazima awe na chama chochote

Wapiga kura ambaon hawana vyama
Katiba ya nchi inatamka kuwa kila aliyefikisha miaka 18 anaruhusiwa kupiga kura haisemi awe mwanachama wa chama cha siasa

Hivyo hakuna chama cha siasa chenye uwezo wa kumzuia mpiga kura yeyote asipige kura
 
Kwanini mng'ang'aniza kuwa sisi wananchi, sisi wananchi? Kwani wakati mnaleta hiyo No Reform, No Reform mlitushirikisha? Kama imebuma shauri yenu na MKOME kutujumuisha wananchi wote! PUMBAVU!!
Huenda n mnifaika wa No Reform,Yes election. Pole ndugu...ni muda Sasa wa kumjenga Mama Tanzania mpya,atakayemnyonyesha kila mwananchi kwa usawa.
 
Huenda n mnifaika wa No Reform,Yes election. Pole ndugu...ni muda Sasa wa kumjenga Mama Tanzania mpya,atakayemnyonyesha kila mwananchi kwa usawa.
Hayo yanatakiwa kuwa matakwa ya wananchi sio Chadema. Sijui kama utalielewa hili.
 
Hayo yanatakiwa kuwa matakwa ya wananchi sio Chadema. Sijui kama utalielewa hili.
Matakwa ya wananchi ni kutaka katiba mpya ambayo ndani yake kuna tume huru na yenye vipengele vya haki kwa wote.
Matakwa ya wananchi yalishatolewa kupitia maoni yao katika rasimu ya katiba kupitia tume ya Warioba.
Sisi wananchi tunajua yalibakwa na serikali ambayo kimsingi inaongozwa na chama tawala..ambao wananufaika na mfumo uliopo sass..
Chadema hawahitaji kutaka maoni kutoka kwetu wananchi kwa vile wanayajua,na ccm na vyama vyote pia wanajua maoni ya wananchi ni yapi kulingana na kile tulichokisema kupitia rasimu ya katiba.
Yeyote,chama chochote kitakachofufua yale maoni yetu kama wanavyofanya Chadema sasa tutawaunga mkono. Hatuhitaji kuombwa ridhaa wakati wao wanatekeleza jambo letu lilokwamishwa na serikali ya ccm kwa makusudi.
Tunakushangaa wewe mwananchi mwenzetu usiyetaka kuunga mkono ili tupate kile tulichokidai katika rasimu wakati ule.
Au wewe ni mnufaika wa mfumo uliopo? Kama ni mnufaika, una kila sababu ya kupinga .
 
Matakwa ya wananchi ni kutaka katiba mpya ambayo ndani yake kuna tume huru na yenye vipengele vya haki kwa wote.
Matakwa ya wananchi yalishatolewa kupitia maoni yao katika rasimu ya katiba kupitia tume ya Warioba.
Sisi wananchi tunajua yalibakwa na serikali ambayo kimsingi inaongozwa na chama tawala..ambao wananufaika na mfumo uliopo sass..
Chadema hawahitaji kutaka maoni kutoka kwetu wananchi kwa vile wanayajua,na ccm na vyama vyote pia wanajua maoni ya wananchi ni yapi kulingana na kile tulichokisema kupitia rasimu ya katiba.
Yeyote,chama chochote kitakachofufua yale maoni yetu kama wanavyofanya Chadema sasa tutawaunga mkono. Hatuhitaji kuombwa ridhaa wakati wao wanatekeleza jambo letu lilokwamishwa na serikali ya ccm kwa makusudi.
Tunakushangaa wewe mwananchi mwenzetu usiyetaka kuunga mkono ili tupate kile tulichokidai katika rasimu wakati ule.
Au wewe ni mnufaika wa mfumo uliopo? Kama ni mnufaika, una kila sababu ya kupinga .
Kwahiyo unahisi wewe ndiye mwananchi zaidi ya wengine sio?
 
Back
Top Bottom