Ijue Historia ya Kabila la Wapare

Chakula kikuu kwa wapare kilikuwa ni makande(mchanganyiko wa mahindi na maharage).Aghalabu chakula hiki kiliandaliwa siku ya Ijumaa jioni hadi Jumapili jioni ili watu waweze kupumzika vizuri mwisho wa wiki bilaa kuwaza masuala ya upishi.Samaki pia ni kipenzi cha wapare wengi na ndio maana utawasikia watani wao wakuu yaani wachaga wakiwatainia kuwa wapare wanakula ugali kwa picha ya samaki wakimaanisha kuwa ni wabahili.Wakati mwingine utawasikia wapare wenyewe wakisema "ipere ethi kindu,kindu ni mshombe"kuwa samaki si kitu kitu ni mchuzi kuonesha ubahili wao kuwa samaki anayebaki atumike tena wakati mwingine bqaada ya mchuzi kuisha.
umejitahidi kuiandika historia ya wapare ila hapo kwenye Red umetudanganya, wanaopika chakula hicho siku ya ijumaa ni wasabato wapare na sio wapare, usichanganye dhehebu la kisabato na kabila la wapare....
 
The hammer, Dingiswayo, Sendoro Mbazi, Queen Esther, Nguruvi3,
nimeangalia matokeo ya shule za Same na Mwanga kwa kweli utatamani kulia. wilaya zetu hazikubahatika kuwa na maliasili kama wilaya nyingine za tanzania. elimu ndiyo iliyotuwezesha wenyeji wa same na mwanga kuwa na mchango katika nchi hii. katika mkoa wa KILIMANJARO wilaya ya Same ndiyo inashika mkia kwa kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa. miaka ya zamani, enzi wa wilaya ya Pare, tulikuwa tunaongoza katika masuala ya elimu. Kwa kweli katika mazingira haya itachukua miongo mingi sana kuwapata wakina Elangwa Shaidi, Abdulrahman Msangi, Akili Danieli,Nassoro Mnzava, Mishael Muze, Mahamoud Mwindadi, Keto Mshigheni,na wasomi wengine wa kupigiwa mfano. ninasema hivi kwasababu wasomi wote hao walitokea vijijini ambako miaka hii kumekuwa na hali mbaya mno. kwa kifupi wilaya zetu zinarudi nyuma badala ya kusonga mbele.
 
Last edited by a moderator:
The hammer, Dingiswayo, Sendoro Mbazi, Queen Esther, Nguruvi3,
nimeangalia matokeo ya shule za Same na Mwanga kwa kweli utatamani kulia. wilaya zetu hazikubahatika kuwa na maliasili kama wilaya nyingine za tanzania. .

Hapo inaumiza na sijajua tatizo linazozikumba wilaya hizo mbili nni nini,na hapo hatuwezi sema kuna mazingira magum sana ya kusoma tofauti na zamani....
Hapo inabidi wahusika ktk ngazi ya wilaya wanaohusika na elimu pamoja na wasimamizi wote wafanye utafiti na kuchukua hatua stahiki
 
miaka ya zamani, enzi wa wilaya ya Pare, tulikuwa tunaongoza katika masuala ya elimu.

Sijawahi sikia hiyo Wilaya kabla! Sijawahi sikia Wapare wameongoza kimasomo nchini labda Wachaga

Nick yako kidogo ifanane ya neno Bangusilo alilotumia aliyekuwa Waziri Ibrahim Msabaha...
 
Duduwasha,
wakati wa ukoloni na miaka ya mwanzoni ya uhuru mwanga na same zilikuwa wilaya moja iliyokuwa ikijulikana kama wilaya ya pare. wilaya ya pare ilikuwa inaongoza kwa kufikia malengo ya kuandikisha watoto shule ya msingi. kitendo hicho kiliwezesha wilaya kupeleka watoto wengi pia sekondari na matokeo yake ndiyo hii hali ya leo kuwa wilaya yetu ni masikini ila tumeweza kutoka kidogo na kufika mjini. wazee wetu wasingewekeza katika elimu leo hii wengi tungekuwa na hali mbaya sana nchi hii, yaani msingesikia kabisa kwamba tuna exist.
 
Last edited by a moderator:
Duduwasha,
wakati wa ukoloni na miaka ya mwanzoni ya uhuru mwanga na same zilikuwa wilaya moja iliyokuwa ikijulikana kama wilaya ya pare. wilaya ya pare ilikuwa inaongoza kwa kufikia malengo ya kuandikisha watoto shule ya msingi. kitendo hicho kiliwezesha wilaya kupeleka watoto wengi pia sekondari na matokeo yake ndiyo hii hali ya leo kuwa wilaya yetu ni masikini ila tumeweza kutoka kidogo na kufika mjini. wazee wetu wasingewekeza katika elimu leo hii wengi tungekuwa na hali mbaya sana nchi hii, yaani msingesikia kabisa kwamba tuna exist.
Evava Sikuwahi isikia Wilaya ya Pare ol ila me naijua zaidi Same kuliko Mwanga
 
Duduwasha,
Evava!!ukisema hujawahi kuisikia wilaya ya Pare unawafanya wasomaji waweze kutambua umri wako, na hata wetu sisi tunaojaribu kukupa habari zake. Kama nilivyokueleza wilaya ya Pare ndiyo iliyozaa wilaya za Same na Mwanga. Mbunge wa wilaya ya Pare mpaka ilipogawanywa alikuwa ni Chediel Yohane Mgonja. Huyu naye ana historia yake itafute hapa Jamii Forums, au kwenye kitabu chake alichoandika kinaitwa "Johari ya Maisha Yangu--C.Y.Mgonja"

ngoja basi nikupe kipande kidogo kuhusu harakati za maendeleo[uchimbaji wa barabara] enzi za wilaya ya Pare kama alivyosimulia Mzee wetu Chediel Mgonja katika kitabu chake. wananchi walichimba BARABARA ya kwenda VUDEE kwa MIAKA NANE bila msaada wa serikali.

"mbinu zilizotumika kuzichimba barabara zote za milimani zilikuwa ni karibu sawa. kila mahali walitumia mila ile ya kuweka siku maalum kwa wananchi wote kufanya kazi kwa pamoja, kwa manufaa yao wote. kazi za ina hiyo ziliitwa za "MISARAGAMBO." mila hiyo ilikuwa na nguvu sana. karibu wananchi wote walishiriki kwa moyo mkuu na kwa furaha. wachache walioacha kuhudhuria kutokana na utegaji au uzembe, walipigwa faini ambazo zilikuwa zinajulikana sana kama vile kuchukuliwa kwa kuku, mbuzi au hata mali nyingine iuzwe na mapato yatumike kuendeleza "MSARAGAMBO." barabara ya kwenda milimani vudee na ndolwa ilitumia nguvu nyingi za wananchi ambao waliiichimba kuanzia 1961 mpaka gari la kwanza lilipoweza kuingia milimani vudee mnamo mwaka wa 1969. gari hilo lilikuwa la serikali na liliendeshwa na dereva ayubu wa Same Bomani. "

"barabara ilikuwa imefika mahali pagumu kuliko kote, wakati Mwalimu alipafanya ziara yake hiyo ya pili. ilikuwa imefika ktk jabali kubwa liitwalo mhewe. jabali lenyewe lilikuwa limesimama wima sana na lilienea umbali upatao robo kilometa. ilikuwa imeleta picha kuwa bara ulifika hapo, ikaingia kwenye jabali na kukwama kabisa isiweze kuendelea tena. hata mimi mwenyewe, ambaye nilishirikiana na wananchi kuichimba barabara hiyo ktk vipindi mbalimbali kwa miaka mingi, moyoni nilikuwa na mashaka kuwa huenda tusiweze kupita mhewe. lakini sikuthubutu kumweleza mtu yeyote mashaka yangu hayo.

wananchi walikuwa na ari na moyo mkubwa sana ingekuwa ni kuwaumiza sana kujaribu kuleta wazo la kushindwa. risala ya wananchi kwa raisi mwalimu Nyerere ilisomwa kwa moyo mkuu na kwa ukakamavu sana, na mwanamke mwalimu napendaeli mgonja, mwalimu wa shule ya msingi vudee, hembua. akisoma risala alimwonyesha Raisi lile jabali la kutisha na akamweleza kwa imani kuwa juhudi za wananchi zilikuwa zimewafikisha pale, na kutokana na uamuzi wa dhati wa wananchi, jabali lilikuwa na wasiwasi mkubwa, kwa vile hi hakika watalipasua na kupitisha barabara hiyo."

"MWALIMU NYERERE aliagiza serikali itoe msaada ikiwa ni pamoja na baruti za kupasulia mawe ktk kukamilisha barabara ile. alifanya hivyo wakati akijibu risala ya wananchi. ni siku hiyo pia ndipo aliwaita wananchi wa Wilaya ya Pare kuwa ni "Wachina wa Tanzania, " na akaongeza kusema, kama ingeliwezekana, angewaleta Watanzania wengine waione kazi hiyo ya ajabu iliyokuwa inafanywa na wananchi waliojizatiti kujipatia maendeleo
"
 
Last edited by a moderator:
Bangusule, nimepitia hayo matokeo Ni kweli Ni mabaya na yanasikitisha. Naungana na waliosema kuchanganya siasa na elimu Ni janga la kitaifa.
Hawa wabunge wa maeneo haya wote wanaishi Dar na watoto wao wanasoma nje ya nchi. Sasa unategemea nini hapo?
Wekeni mdahalo wa wakazi wa haya maeneo let say Same as an example Mahali Kama Diamond Jubilee, bila kuanfalia chama tukadili mustakabali wa watoto wetu hata Kama hatuishi huko. Ukumbuke udongo wa same, mwanga nk ndio uliokufinyanga hivyo ziko baraka zako huko. Wale wakristo wanakumbuka Yakobo alivyorudi kufufua visima vya baba zake.

Naamini mdahalo huo itazungumzia mgongano wa kimaslahi pale machimbo ya mlima shengena.
Queen Esther

The hammer, Dingiswayo, Sendoro Mbazi, Queen Esther, Nguruvi3,
nimeangalia matokeo ya shule za Same na Mwanga kwa kweli utatamani kulia. wilaya zetu hazikubahatika kuwa na maliasili kama wilaya nyingine za tanzania. elimu ndiyo iliyotuwezesha wenyeji wa same na mwanga kuwa na mchango katika nchi hii. katika mkoa wa KILIMANJARO wilaya ya Same ndiyo inashika mkia kwa kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa. miaka ya zamani, enzi wa wilaya ya Pare, tulikuwa tunaongoza katika masuala ya elimu. Kwa kweli katika mazingira haya itachukua miongo mingi sana kuwapata wakina Elangwa Shaidi, Abdulrahman Msangi, Akili Danieli,Nassoro Mnzava, Mishael Muze, Mahamoud Mwindadi, Keto Mshigheni,na wasomi wengine wa kupigiwa mfano. ninasema hivi kwasababu wasomi wote hao walitokea vijijini ambako miaka hii kumekuwa na hali mbaya mno. kwa kifupi wilaya zetu zinarudi nyuma badala ya kusonga mbele.
 
Last edited by a moderator:
Hii kama ilivyokuwa ktk historia fupi hapo juu,ni kuwa wachaga na wapare wote ni wahamiaji kutoka sehemu za Kenya ila wote walihamia ktk vipindi tofauti.Wachaga walitangulia na kuchukua sehemu zote zilizokuwa na hali nzuri ya hewa na zenye rutuba hii ikiwa sehemu zote zinazunguka mlima kilimanjaro nk.Hivyo Wapare walivyofika walikuta sehemu zenye hali ya hewa na rutuba nzuri zilishachukuliwa na Wachaga wakajaribu kuchukua kwa mabavu wakashindwa hivyo wakakimbilia milimani na sehemu kame.

Aikambe ndumii. Wapare puu, wapare puu, hahahahaha.
 
Duduwasha, The hammer,

nitapenda kuwakumbuka Machifu 9 wa iliyokuwa Pare Native Authority. pamoja na kwamba napinga Uchifu, lakini nitaeleza kwanini ninawaenzi Machifu hawa pamoja na mapungufu waliyokuwa nayo.

baada ya vita kuu ya pili Muingereza aliweka lengo kwa koloni la Tanganyika kuandikisha 36% ya watoto shule ya msingi. Tanga Province ambako wilaya ya Pare waliweka lengo kwamba mpaka kufikia mwaka 1956 wawe wamefikia 50%. Machifu wa Pare Native Authority waliweza kuhamasisha wananchi wao na ilipofika 1952 waliweza kuandikisha 90% ya watoto shule ya msingi.

pia vilikuwepo VIKUNDI VYA ELIMU YA WATU WAZIMA katika maeneo mbalimbali kama Usangi, Mbaga, Same, Ugweno. wakinamama hawakuwa nyuma katika kuanzisha vikundi vya kujifunza kusoma. mwamko huo wa kinamama kujifunza kusoma ktk utu uzima ndiyo uliochochea elimu ya mtoto wa kike katika maeneo hayo. historia inapaswa kuwakumbuka kinamama hao.

kampeni ya elimu ya watu wazima ilipelekea kuanzishwa kwa GAZETI lilloitwa HABARI ZA UPARE. gazeti lilianzishwa 1951 na kuna kipindi lilikuwa likitoa makala 2000 kwa mwezi. nitatafuta makala ya gazeti hilo na kuwawekea mlisome.

shule nyingi za msingi haswa zile za WALUTHERI, SDA, na WAISLAMU, na hata SERIKALI, zilijengwa kwa mwamko wa kujitolea wa wananchi wenyewe. wananchi wa maeneo kama Usangi na Ugweno kwa miaka karibu 14 bila msaada wa fedha au utaalamu walishiriki ujenzi wa barabara za milimani kuwaunganisha na mji wa Mwanga. wananchi wa Chome, Mamba,Vudee, nao hawakuachwa nyuma katika ujenzi wa barabara kwa njia ya kujitegemea.

Machifu au Wafumwa 9 ninaowakumbuka ni Chifu/Mfumwa Sabuni wa Usangi, Mfumwa Kibacha Singo wa Same, Mfumwa Manento Sekimanga wa Mamba, Joseph Mamphombe wa Mbaga, Kigono Chuma wa Gonja, Folong'o Makange wa Chome, Minja Kukome wa Ugweno, Yoeli Mtindi wa Hedaru.
 
Last edited by a moderator:
Sifa zoote mmezieleza, lakini sifa kuu na ya muhimu mmeisahau....yaani,.... wapare wanapenda chini.....:A S 112:...sio mchezo!

....Huwa wanawatania wachagga kuwa, Mungu amekothea katika amri zake kuu, ilitakiwa itangulie (usiibe) ndio ije (usizini)..wakiamini dhambi zimepangwa kutokana na uzito wake.....!lol


Chunguza, utaona kuwa sio wapare wakiume wala wakike, kale kamchezo ketu....wanakipenda balaa!
 
nilijua tu Mentor asilike wakati ni wa huko ipere ethi kindu ningeshangaa tena sana kwani namjua mume wangu huyu ila yeye mbona hana hizo tabia za kipare jamani wala jinalake sio la kipare au alinidanganya kuwa anatokea same?
 
Last edited by a moderator:
mkuu sijaona ukisema kilevi chao... mnapendaga mirungii???

Kuna kitu inaitwa Puya Hiyo Puya Iatengenezwa na Miwa Na Huo Mtambo wa kukamua miwa unatoa Sauti kama Ndege ya Fokker Utasikia Sauti yake hadi zaidi ya km hadi Mbili ulipo mtambo japo ni wa Mbao tu hautumii Umeme Unazungushwa kwa kuuzunguka mzungushaji akipata kizungu zungu anampisha mwingine
 
Kuna kitu inaitwa Puya Hiyo Puya Iatengenezwa na Miwa Na Huo Mtambo wa kukamua miwa unatoa Sauti kama Ndege ya Fokker Utasikia Sauti yake hadi zaidi ya km hadi Mbili ulipo mtambo japo ni wa Mbao tu hautumii Umeme Unazungushwa kwa kuuzunguka mzungushaji akipata kizungu zungu anampisha mwingine

iyo pombe ya miwa weka pembeni (i gs inaitwa dengurii) kuna majani flani ivi yana kilevi yanatafunwa na big G... (mirungi, gomba etc)??? wapare wa huku mjini wanayapenda sana... na pia huwa yanapatikana ata hedaru...
 
Sifa zoote mmezieleza, lakini sifa kuu na ya muhimu mmeisahau....yaani,.... wapare wanapenda chini.....:A S 112:...sio mchezo!

....Huwa wanawatania wachagga kuwa, Mungu amekothea katika amri zake kuu, ilitakiwa itangulie (usiibe) ndio ije (usizini)..wakiamini dhambi zimepangwa kutokana na uzito wake.....!lol


Chunguza, utaona kuwa sio wapare wakiume wala wakike, kale kamchezo ketu....wanakipenda balaa!

Msese, wetetie mongo kweri, nethikimanje una mongo tha uvo!!!!
Hivi walioongoza na wanaoongoza kufa kwa HIV/AIDS ni WAPARE????????
Je kupenda ngono kuna kabila au tabia ya mtu??????
Ushindwe kwa Jina la Yesu Kristo wa Nazareth.
Queen Esther
 
Mrungu akughenje we mwandishi,harika kave vaasu vyena historia yedi huvu.HAVOME!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom