Ijue afya yako kupitia aina ya kinyesi unachokitoa

Dr. Zaganza

JF-Expert Member
Jul 15, 2014
1,195
1,661
1690777583948.png

Chati ya kinyesi ya Bristol ilitengenezwa mnamo 1997 kama zana ya tathmini ya kliniki. Kuna aina saba za kinyesi kulingana na Chati ya hiyo.

Chati ya kinyesi ya Bristol ni msaada wa matibabu ulioundwa na kuainisha kinyesi katika vikundi saba.

Baada ya kujisaidia, kile unachokiona chooni kimsingi ni matokeo ya lishe yako, maji unayokunywa, dawa unazotumia na mtindo wa maisha.

Unaweza kutumia Chati ya Kinyesi ya Bristol kuangalia kile kinyesi chako kinamaanisha nini kulingana na muonekano wake.

Aina ya kwanza na ya pili ya kinyesi ni vidonge vigumu vilivyotengana kama karanga ambavyo inakuwa ngumu kutoka wakati wa kujisaidia.

Hii inamaanisha kuwa mhusika amevimbiwa kutokana na kutokula matunda au mboga mboga.

Aina ya tatu na nne ni kama sausage au nyoka au ndizi, kwa kawaida hii huwa rahisi kutoka wakati wa kujisaidia. Hii huchukuliwa kama aina bora ya kinyesi ambayo humaanisha mhusika ana afya nzuri.

Aina ya tano mpaka ya saba kwa ujumla hizi huonesha kuhara. Aina hizi tatu zinaonesha kinyesi ambacho kina maji maji ambayo husababishwa na kukosa aina fulani ya vyakula kama vile matunda.

Ni muhimu kutambua aina ya kinyesi chako na kama kinaishara isiyo nzuri ni vyema kubadilisha mtindo wa maisha.
 
Kuna watu hawapendi kuona walichokunya. Wapo watu wanakunya mavi magumu kiasi cha kutoka na damudamu na wakati mwingine divi hukwama katikati inakuwa shughuli kulimomonyo kwa vidole mpaka litoke lote lilikokwama unyeoni. Huu ni ugonjwa gani? Yale mavi malaini kama uji ni uharo tumbo bovu, je mavi magumu nini tatizo?
 
Back
Top Bottom