IGP Said Mwema aongezewa mkataba

IGP Said Mwema aongezewa mkataba

Mkuu kwa hatua iliyofikia, ni wakati muafaka kabisa kwa wananchi sasa kusema tunataka serikali adilifu ambayo haitatumia vyombo vya usalama kuhujumu nchi bali wataviacha vyombo vya usalama visimamie maslahi ya Taifa, raia, na ustawi tena kwa kufanya kazi kwa uhuru na kuzingatia weledi.Zaidi ya hapo; nashindwa kupata picha halisi ya hatima ya nchi hii kwa jinsi mambo yanavyoenda.
Serikali ya aina hiyo haipatikani chini ya mbingu mimi nawashangaa sisiem kutumia rungu kuuwa inzi hakuna upinzani hapa wa kuleta serikali yenye uwezo nusu ya hii ya sasa pamoja na ubaya wk wote
 
Kwa mujibu wa kipindi cha magazeti cha channel 10 cha saa 2 asubuhi hii,kuna gazeti limeripoti kuwa IGP Mwema ameongezewa mkataba.Sijui ni kwa muda gani maana mtangazaji hakusema na wala sikumbuki ni gazeti ila hiyo ndio taarifa kwa ufupi kama ilivyosomwa.

MY TAKE:Hivi hakuna watu wengine?Haya si matumizi mabaya ya madaraka ya Raisi?


Shemeji mwema nisubir tutastafu wote 2015


Sent from my BlackBerry 9700 using Jamii Forums
 
Jamani, kumbukeni pia kuna kaundugu hapo na Vasco daGAMA tena ka mambo ya naniiiii!
Chezea naniiii?
 
Tanzania inanukia Syria sasa
Ili kuwa hivi hivi kwa general mwamunyange
 
Chezea Arusha ww?hata wapewe miaka kumi zaidi tena,lakini Chuga inawanyima usingizi,bado Tarime kwetu ndo balaa.endeleeni tu kuitikia "zidumu fikra sahihi za mwenyekigoda",Kwa MUNGU si kwa mzungu.:yell:
 
wachochezi na waongo ndio wamejaa humu jf! official hakuna hicho kitu,nimesoma leo kwenye gazeti la mtanzania hizo ni rumors ndani ya jeshi la polisi,sasa wao wametoa kama habari hawajasikiliza upande wa pili wa jeshi wanasemaje,ndio maana mm huwa nawadharau waandishi wa habari wa tanzania
 
Sifa kubwa ya kuongezewa mkataba ni kwamba anaujasiri wa kuuwa.
kingine anafanya kazi kwa vimemo toka Lumumba.
pia ni kada mwaminifu wa CCM.!!

hapana hana ujasiri huo, anaujasili wa kuunganisha jamii na jeshi la polisi mfano yeye ndiye mwanzilishi wa POLISI JAMII NA ULINZI SHIRIKISHI, kutokana na programu hiyo kuwa na mafanikio hata TANAPA wameiga wana ulinzi shirikishi kwa kaya zinazopakana na hifadhi, Idara ya Uhamiaji nao hali kadharika. He is a good Man Mzee wala usihofu manenomaneno na lawama za watu, hakuna kiongozi ambaye hajawahi kupata lawama, waswahili wanasema ukiwa mkubwa Jalala.
 
hongera rais kwa kuwaongezea muda igp na kova! igp amelibadilisha jeshi la polisi. nidhamu na uadilifu vimeongezeka tofauti na miaka ya nyuma. kipindi cha mahita ujambazi ulikua juu sana kupindukia. kova amejitahidi kuliongoza vizuri jiji gumu la dar. yuko karibu na watu na anaendelea kuimarisha amani. hongera muh rais!
 
Me Nawachukia sana Baadhi ya Watanzania,kama wapumbavu wapumbavu,

Kila siku kulalamika lalamika tuuh??

Sasa sijui wanadhan mabadiliko ya nchi hii yataletwa na malaika au na watu kutoka nje??

Upuuzi kabisa,ikifika 2015 utaona mijitu na suruali zao kimbele mbele kuipigia kura CCM..!

SHENZY KABISA,KAMA WANA LAANA VILE,
 
Lazima aongezewe mkataba kauwa wananchi Mwanza,Arusha,Mbeya,Iringa,Mtwara,Songea,Shinyanga,Geita Igunga,Arumeru lazima apewe zawadi bwana ukiwa IGP unayebariki mauaji bila kukamata wauaji unaongezewa madaraka ataachishwa kazi mwezi mmoja kabla ya kikwete kuondoka na kupewa ubalozi ,halafu watanzania tupo tu tunakenue mtu mmoja anaendesha nchi kama yuko mfukoni mwake
 
Hii nchi aliyeilaani amekufa!

hakuna alitulaani, ni ujinga, upumbavu na uoga ndio umetujaa. Watanzania wote ni wanafiki. hatuwezi kusimama na kuwa kitu kimoja cha kuwatoa hawa wapumbavu wanaojiona wajanja.

Kama hatuta simama pamoja basi wataendelea kula pesa zetu na kuepeana vyeo na kujiongezea mikataba ya kijinga mpaka tutakampo amka.

watanzania tuacheni woga na unafiki katika masuala yanayotugusa kimaisha
 
Wanatubania ajira hao waende zao. JK acha kutuchulia,kwa kuwa nawe huwezi kazi nenda nao hao jamaa zako.
 
IGP Mwema ni mtu mzuri sana kuliko angechaguliwa mwingine "The devil you know is better than one you don't know"
 
Tunashukuru kwa hatua hiyo. ICC the Hague haitakuwa na wakati mgumu wakati wa kumfikisha mahakamani jk. Players wote watakuwa bado wabichi katika kumbukumbu zao.
 
...nchi ya utawala wa ajabu hii....watumishi viongozi wajuu wanafuja na kuiba mali za umma wanaachwa wanastaafu.....viongozi wa juu wanamaliza muda wao (tena wegine kwa kashfa)wa utumishi lakini wanaongezewa muda ili kuilinda status quo....haya yote yanafanyika kama vile nchi hii inamilikiwa na watu binafsi...au raia wake wamelala usingizi wa pono.....Yote haya yana mwisho....even natural causes can end this nonsense....seems watawala wanasahau hili.....
 
Lazima aongezewe mkataba kauwa wananchi Mwanza,Arusha,Mbeya,Iringa,Mtwara,Songea,Shinyanga,Geita Igunga,Arumeru lazima apewe zawadi bwana ukiwa IGP unayebariki mauaji bila kukamata wauaji unaongezewa madaraka ataachishwa kazi mwezi mmoja kabla ya kikwete kuondoka na kupewa ubalozi ,halafu watanzania tupo tu tunakenue mtu mmoja anaendesha nchi kama yuko mfukoni mwake

Baada ya hapo anapewa ubalozi ili ajipumzishe vyema.
 
Back
Top Bottom