Idris Sultan atimiza siku 7 Rumande

Mchekeshaji na mwanamitindo maarufu nchini Idris Sultan ameendelea kusota rumande kwa siku saba kutokana na makosa ya kimtandao. Idris aliitwa kuhojiwa na jeshi la Polisi toka may 19, 2020 ambapo anashikiliwa hadi leo.

Sheria zinasemaje kwa mtuhimiwa? Ana haki zake nae pamoja na kutuhumiwa.
#KatibaNiYetu

View attachment 1459884


Huyu Mwarab Koko Beach aachwe tu asote huko, amezidi sana ujinga wa kulazimisha ili apate kicki. Dada zake uchwara kina Maria Sarungi na Ankal wake Zitto ndiyo wanamtumia vibaya biya yeye kujitambua. Ujinga wa kutojitambua ni mbaya sana.
 
Tauche kuangalia suala hili kwa kuangalia watu, taungalie dhana.

Moja ya matatizo makubwa ya siasa za Afrika ni kuangalia watu badala ya kuangalia dhana.

Kimsingi hapa, huna hoja ya kidhana ya kumtosa Idris na kumtetea Kipanya.

Kwa sababu, ukishaweka upenyo wa Idris kunyanyaswa kwa minajili ya kumdhalilisha rais, umeshaweka upenyo kwa Kipanya kunyanyaswa kwa minajili ile ile.

Kuna haki za msingi za kikatiba za uhuru wa watu kujieleza zinavunjwa hapa, hili si suala la Idris tu.

Ni suala la haki za kikatiba kuvunjwa.
Generally bongo hakuna freedom of speech kama Marekani ila tujifunze kuishi na hali. Tusijitoe ufahamu maana itatugharimu big time.

Ukibisha ama kukaza kichwa hutakuwa huna tofauti na mtu ambaye analala na pipa la petroli lililo wazi pembeni ya jiko la kuni ilihali akijua kuwa cheche moja toka jikoni inaweza kubadilisha maisha yake jumla jumla ati sababu kuna fire extinguisher.
 
Mchekeshaji na mwanamitindo maarufu nchini Idris Sultan ameendelea kusota rumande kwa siku saba kutokana na makosa ya kimtandao. Idris aliitwa kuhojiwa na jeshi la Polisi toka may 19, 2020 ambapo anashikiliwa hadi leo.

Sheria zinasemaje kwa mtuhimiwa? Ana haki zake nae pamoja na kutuhumiwa.
#KatibaNiYetu

View attachment 1459884



Hili dogo jinga sana, sijuwi nani anamdanganyaga kuwa staa bongo ni lazima uwe mjinga?
 
Actually kuishi maisha ya kukalili huwa siyo poa si kila mtu unaye muona kwa mbele yako anapenda masiala kama ulio waacha nyuma yako
 
Generally bongo hakuna freedom of speech kama Marekani ila tujifunze kuishi na hali. Tusijitoe ufahamu maana itatugharimu big time.

Ukibisha ama kukaza kichwa hutakuwa huna tofauti na mtu ambaye analala na pipa la petroli lililo wazi pembeni ya jiko la kuni ilihali akijua kuwa cheche moja toka jikoni inaweza kubadilisha maisha yake jumla jumla ati sababu kuna fire extinguisher.
Nyerere na wazee wa TANU wangekuwa na mawazo kama haya, pengine mpaka leo tungekuwa tunatawaliwa na Muingereza.

George Washington na wenzake wangekuwa na mawazo kama haya, pengine mpaka leo Marekani ingekuwa chini ya himaya ya Muingereza.

Kuna msemo kwamba revolutions look impossible before they happen, but they look inevitable after they happen.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Kuna trick hua Jpm anaitumia kukwepa baadhi ya maswali kuyatolea majibu ya moja kwa moja.

Hamna kitu amejibu kutokea swali la msingi hadi swali dogo!
Anawapumbaza wengine tu.

Tunaojua kufuatikia logic point by point tumezidi kumdharau tu.

Hata kifungu alichotaja hakijibu lolote kuhusu maswali aliyoulizwa.

Ameziea hoja ya nguvu badala ya nguvu ya hoja.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Umemsikiliza jpm kwa makini hapo?
Serikali inayoshikilia dola ni ile yenye mamlaka juu ya pesa.
Hio miamala mingine ni dummy tu.
Hakuna kitu kama hicho kwenye katiba.

Hayo ni maneno ya aibu kabisa katika nchi ambayo Nyerere alitufundisha "Utu wa mtu ni kazi, pesa ni matokeo".

Sasa huyu kwa msingi huu, anaweza kusema serikali yake ndiyo inayogharimia uchaguzi, hivyo apitushwe tu.

Kwani hizo fedha ni za Magufuli na serikali yake au ni za wananchi?

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Huyo jamaa akae tu huko hata mwaka mzima, anaonekana ana mambo ya kitoto pamoja na umaarufu wake.... Kubwa jinga hilo.
Ukae ukijua wakimalizana na huyo wanakuja kukushukia wewe.

Mpaka upige magoti na kukiri Magufuli ni Bwana!

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Ukae ukijua wakimalizana na huyo wanakuja kukushukia wewe.

Mpaka upige magoti na kukiri Magufuli ni Bwana!

Sent from my typewriter using Tapatalk

Mkuu Kiranga, unaeleweka sana hoja yako.

Na pia umetoa mifano mbalimbali kutanabaisha hoja yako.

Lakini Idris amechukua picha ya mheshimiwa halafu akaifanyia editing (maana original yamwonyesha akiwa na watu wengine wawili).

Lengo ni kuonyesha jinsi mheshimiwa alivyokuwa hafahamu namna ya kushona au kuchagua aina ya suti za kuvaa.

Na hiyo kwenye nedia itasambaa kwa kasi kubwa na imefanya hivyo.

Sasa hiyo ni dhihaka na kejeli kwa raisi na kama binadamu akaiona hiyo picha na kuambiwa imesambaa nchi nzima na nje ya mipaka, wewe wadhani angefanyaje aipuuze tu kwa kuzingatia alikwishapuuzia mzaha mwingine ulofanywa na Idriss?

Raisi Magufuli ameachia media ifanye kila inachotaka na ndo maana hata wewe waweza kusomwa maoni yako Tanzania.

Ila kwa mazingira ya sasa ya nchi hayaruhusu aina hiyo ya dihaka kwa kiongozi wa nchi, maana shida zilizopo halafu ukachanganya na mizaha isiyotarajiwa, matokeo yake ni hayo tunayoyaona.

Hao ulowaona huko Ikulu ya White House wakidine pamoja na Donald Trump wengine ni rafiki zake, jamaa na watu ambao ni Circle ya utawala wa Marekani hivyo wanaweza kutaniana na kusemeana kejeli watakavyo.

Mwisho, hao wote uwasemao wameshiba na wana kipato wana kila kitu, hivyo kwa Tanzania tungoje watu washibe na kisha wawe na uwezo wa kufanya shows kwenye runinga na watu wacheke.

Hata simba akishiba si waweza kumpita tu uende zako?

Kinachotakiwa ni hao watu kwa Tanzania kuanza kumzoesha raisi na viongozi juu ya maazimio yao ya kuweka vipndi vya namna hivyo au hata kutoa angalizo in advance kwa Mr Msigwa ili kuona kwamba hakutakuwa na problem endapo picha itakuwa edited halafu kuwekwa ili ifanyiwe dhihaka.
 
Huyu mjinga kwanza alitakiwa awe ameisha chezewa ndogo mda mrefu,sema nae hakujitambua kama mdude.
 
Muacheni kwanza apumzike mbona kule yupo sehemu salama.
Kuna wenzie wameuliwa kabisa .
Awamu ya 5 ni awamu ya ANACONDA
 
Mkuu Kiranga, unaeleweka sana hoja yako.

Na pia umetoa mifano mbalimbali kutanabaisha hoja yako.

Lakini Idris amechukua picha ya mheshimiwa halafu akaifanyia editing (maana original yamwonyesha akiwa na watu wengine wawili).

Lengo ni kuonyesha jinsi mheshimiwa alivyokuwa hafahamu namna ya kushona au kuchagua aina ya suti za kuvaa.

Na hiyo kwenye nedia itasambaa kwa kasi kubwa na imefanya hivyo.

Sasa hiyo ni dhihaka na kejeli kwa raisi na kama binadamu akaiona hiyo picha na kuambiwa imesambaa nchi nzima na nje ya mipaka, wewe wadhani angefanyaje aipuuze tu kwa kuzingatia alikwishapuuzia mzaha mwingine ulofanywa na Idriss?

Raisi Magufuli ameachia media ifanye kila inachotaka na ndo maana hata wewe waweza kusomwa maoni yako Tanzania.

Ila kwa mazingira ya sasa ya nchi hayaruhusu aina hiyo ya dihaka kwa kiongozi wa nchi, maana shida zilizopo halafu ukachanganya na mizaha isiyotarajiwa, matokeo yake ni hayo tunayoyaona.

Hao ulowaona huko Ikulu ya White House wakidine pamoja na Donald Trump wengine ni rafiki zake, jamaa na watu ambao ni Circle ya utawala wa Marekani hivyo wanaweza kutaniana na kusemeana kejeli watakavyo.

Mwisho, hao wote uwasemao wameshiba na wana kipato wana kila kitu, hivyo kwa Tanzania tungoje watu washibe na kisha wawe na uwezo wa kufanya shows kwenye runinga na watu wacheke.

Hata simba akishiba si waweza kumpita tu uende zako?

Kinachotakiwa ni hao watu kwa Tanzania kuanza kumzoesha raisi na viongozi juu ya maazimio yao ya kuweka vipndi vya namna hivyo au hata kutoa angalizo in advance kwa Mr Msigwa ili kuona kwamba hakutakuwa na problem endapo picha itakuwa edited halafu kuwekwa ili ifanyiwe dhihaka.
Hujatoa hoja ya msingi ya kuondoa uhuru wa kikatiba wa Watanzania kutoa maoni yao.

Yani hata mtu akitaka kuwa msanii akiichukua picha ya Magufuli na kui edit iwe kikaragosi, hilo limo katika haki za kikatiba za uhuru wa kujieleza.

Mbona Kipanya anamchora Magufuli mara kibao na bichwa lenye mabonde yaliyo exaggerated?

Mtasema Kipanya naye afungwe kwa kumdhalilisha rais?

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Mkuu Kiranga, unaeleweka sana hoja yako.

Na pia umetoa mifano mbalimbali kutanabaisha hoja yako.

Lakini Idris amechukua picha ya mheshimiwa halafu akaifanyia editing (maana original yamwonyesha akiwa na watu wengine wawili).

Lengo ni kuonyesha jinsi mheshimiwa alivyokuwa hafahamu namna ya kushona au kuchagua aina ya suti za kuvaa.

Na hiyo kwenye nedia itasambaa kwa kasi kubwa na imefanya hivyo.

Hiyo picha Idris kaitoa wapi? Kwenye photo album ya Magufuli au kaitoa kwenye mtandao, ambao ni public domain?

Sasa hiyo ni dhihaka na kejeli kwa raisi na kama binadamu akaiona hiyo picha na kuambiwa imesambaa nchi nzima na nje ya mipaka, wewe wadhani angefanyaje aipuuze tu kwa kuzingatia alikwishapuuzia mzaha mwingine ulofanywa na Idriss?

Rais wa Tanzania hakejeliwi? Hadhihakiwi? Hachekwi?

Sikubaliani kabisa na wewe. Rais ameutaka mwenyewe urais. Kazi ambayo inahitaji uvumilivu usio wa kawaida.

Magufuli siyo mungu.

Raisi Magufuli ameachia media ifanye kila inachotaka na ndo maana hata wewe waweza kusomwa maoni yako Tanzania.

Ameachia media ifanye inachotaka? You can’t be serious!

As if everything in this country is at the pleasure of Magufuli.

Nope. It ain’t like that.

Ila kwa mazingira ya sasa ya nchi hayaruhusu aina hiyo ya dihaka kwa kiongozi wa nchi, maana shida zilizopo halafu ukachanganya na mizaha isiyotarajiwa, matokeo yake ni hayo tunayoyaona.

Hao ulowaona huko Ikulu ya White House wakidine pamoja na Donald Trump wengine ni rafiki zake, jamaa na watu ambao ni Circle ya utawala wa Marekani hivyo wanaweza kutaniana na kusemeana kejeli watakavyo.

Mwisho, hao wote uwasemao wameshiba na wana kipato wana kila kitu, hivyo kwa Tanzania tungoje watu washibe na kisha wawe na uwezo wa kufanya shows kwenye runinga na watu wacheke.

Hata simba akishiba si waweza kumpita tu uende zako?

Kinachotakiwa ni hao watu kwa Tanzania kuanza kumzoesha raisi na viongozi juu ya maazimio yao ya kuweka vipndi vya namna hivyo au hata kutoa angalizo in advance kwa Mr Msigwa ili kuona kwamba hakutakuwa na problem endapo picha itakuwa edited halafu kuwekwa ili ifanyiwe dhihaka.

Hoja za kitoto sana hadi nimejisikia uvivu kukujibu mstari kwa mstari!!!
 
Kwa ufupi Idris si mchekeshaji! Hicho kipaji hana! Mr. Khan ameliweka wazi hili aangalie wapi pa kufanya mzaha.

Unapoishi ndani ya jamii inakubidi utambue silika za watu wanaokuzunguka. Kuna baadhi ya watu hawapendi mizaha kabisa. Ni watu hao katika jamii, inabidi uheshimu msimamo wao na uutambue. Kuna wengine wanapenda mizaha! Ni sehemu nao katika jamii! Inabidi uheshimu msimamo wao na uutambue.

Siafiki anachofanyiwa ila awe na utambuzi huo! Na hiyo fursa ya kulielewa hili walimpatia mara ya kwanza! Karudia tena kwa Bw. Yule asiyependa mizaha. Kajitakia!
Ni kweli mkuu halafu siku hizi wa fawanya mizaa wako wengi sana wanajifanya wanachekesha wengine ni watangazaji nguli kabisa.
 
Nyerere na wazee wa TANU wangekuwa na mawazo kama haya, pengine mpaka leo tungekuwa tunatawaliwa na Muingereza.

George Washington na wenzake wangekuwa na mawazo kama haya, pengine mpaka leo Marekani ingekuwa chini ya himaya ya Muingereza.

Kuna msemo kwamba revolutions look impossible before they happen, but they look inevitable after they happen.

Sent from my typewriter using Tapatalk
Hamna tatizo mkuu, njia nyeupe unaweza ukawa pioneer wa revolution! Anza wewe...
We have a life to lead and families to feed!
 
Mwache aendelee kukaa rumande mpaka akili itakapomkaa sawa. Mtu kipaji hana ana kazi ya kujifanya Mockingbird tu.

Yeye kila tukio analigeuza mzaha ili afurahishe vi slay queen vinavyo mfollow huko insta.
wivu tu
 
Back
Top Bottom