Hammaz
JF-Expert Member
- May 16, 2018
- 5,182
- 10,493
Hili swali kama linalenga kibonzo cha chini huo siyo mzaha! Hicho kibonzo kinamaanisha Magu ni show ya mtu mmoja...[/QUOTE]Huo sio mzaha?
Unataka nikirudie kilekile nilichokiandika? Fahamu ya kwamba ewe muanzisha Uzi; Kicheko kinagawanyika sehemu mbili. Kuna kicheko cha furaha kinaashiria jambo jema.
Kuna kicheko cha dhihaka! Aina zote hizo za vicheko vinatokana na mazingira baada ya, haya ndiyo yanatafsiri ni kicheko cha aina gani.
Idris aliambatisha picha ubavuni mwake, na ni picha ya mtu mmoja. Mazingira yapo wazi yanaonyesha kilichokuwa kinafanyika. Akacheka!
Kilichomchekesha ni muonekano wa picha. Mazingira ya picha ndiyo yatakayo fafanua ni kicheko cha namna gani! Kama ni kicheko cha kuonyesha furaha/jambo jema! Au ni kicheko cha dhihaka!
Mzaha ni utani. Utani ni mojawapo ya kipengele cha sanaa na maigizo ndani ya jamii. Lakini si kila aliye ndani ya jamii ni mwenye kufanyiwa mzaha.
Siafiki anachofanyiwa Idris, siafiki alichokifanya Idris.