Amnesty International yaitaka Tanzania ifute mashtaka dhidi ya Idris Sultan

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Shirika la kutetea haki za binadamu Amnesty International limeitaka Tanzania kuachana na mashtaka dhidi ya mchekeshaji maarufu nchini humo Idris Sultan

Idris anatarajiwa kufika mahakamani kesho tarehe 9 mwezi Julai, kujibu mashtaka ya ''kushindwa kusajili kadi ya simu ambayo awali ilikuwa ikilimilikiwa na mtu mwingine'' na kushindwa kuripoti umiliki wa kadi ya simu''.

Idris alikamatwa mwezi Mei baada ya video iliomuonesha akicheka huku akiitazama picha ya zamani ya rais wa Tanzania John Magufuli, kusambaa mitandaoni.

Baada ya kushikiliwa na polisi kwa zaidi ya wiki moja Sultan alifikishwa katika mahakama ya Kisutu na kusomewa shitaka la kutosajili nambari ya simu aliyokuwa anaitumia ambayo imesajiliwa kwa jina la mtu mwingine.

Anayetajwa kusajili laini hiyo, Innocent Maiga pia alishtakiwa pamoja na Bw Sultan kwa kosa la kutoarifu mabadiliko ya umiliki wa laini ya simu iliyosajiliwa kwa jina lake.

Msanii huyo aliachiwa kwa dhamana baada ya watu wawili kusaini bondi ya Shilingi za Tanzania milioni 15 kila mmoja, wakili wake Bennedict Ishabakaki aliieleza BBC.

Wawili hao wanatuhumiwa kufanya makossa hayo kinyume cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektoniki na Posta, na endapo watakutwa na hatia watakabiliana na adhabu ya faini isiyopungua Shilingi milioni tano, ama kifungo kisichopungua miezi 12 ama vyote faini na kifungo.

Mkurugenzi wa Amnesty International wa kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Deprose Muchena alisema:
''Ni ushahidi kwamba mamlaka nchini Tanzania hazina kesi dhidi ya Idris Sultan na wako tu wanamnyanyasa kwasababu uchekeshaji wake umewakwaza. Mahakama lazima ifute mashtaka yaliyobuniwa kupata sababu dhidi yake''.

Kabla ya kufikishwa mahakamani, polisi na wakili wa msanii huyo waliiambia BBC kuwa alikuwa pia akihojiwa kwa tuhuma za kutenda makosa ya kimtandao.

Wakili Ishabakaki pia aliiambia BBC kuwa mteja wake alikamatwa na kuhojiwa na polisi juu ya mkanda wa video uliosambaa mitandaoni hivi karibuni akionekana akiicheka picha ya zamani ya rais Magufuli.

Hata hivyo, hakufunguliwa mashtaka yoyote kuhusiana na suala hilo.
 
Hawa vibaraka wa Magufuli huwa vichwa ngumu sana. Idris is no body in Tz ila wanamkuza wao kuzembe ivyo kama walivyowakuza wakina abdul nondo leo hii et nao wanagombea ubunge.
Nakubaliana nawe.Au ulikuta na yeye alifanya huku akijua fika baadaye watamganda hivyo na hiyo itampaisha zaidi.
Sijui wanamshikilia wa nini wamwache aende na njaa zake.
 
Amnesty International proclamations are never heeded by Dictators! Stop proclamations particularly in African dictators, devise other means to enforce your policies on human rights!
 
Shirika la kutetea haki za binadamu Amnesty International limeitaka Tanzania kuachana na mashtaka dhidi ya mchekeshaji maarufu nchini humo Idris Sultan

Idris anatarajiwa kufika mahakamani kesho tarehe 9 mwezi Julai, kujibu mashtaka ya ''kushindwa kusajili kadi ya simu ambayo awali ilikuwa ikilimilikiwa na mtu mwingine'' na kushindwa kuripoti umiliki wa kadi ya simu''.

Idris alikamatwa mwezi Mei baada ya video iliomuonesha akicheka huku akiitazama picha ya zamani ya rais wa Tanzania John Magufuli, kusambaa mitandaoni.

Baada ya kushikiliwa na polisi kwa zaidi ya wiki moja Sultan alifikishwa katika mahakama ya Kisutu na kusomewa shitaka la kutosajili nambari ya simu aliyokuwa anaitumia ambayo imesajiliwa kwa jina la mtu mwingine.

Anayetajwa kusajili laini hiyo, Innocent Maiga pia alishtakiwa pamoja na Bw Sultan kwa kosa la kutoarifu mabadiliko ya umiliki wa laini ya simu iliyosajiliwa kwa jina lake.

Msanii huyo aliachiwa kwa dhamana baada ya watu wawili kusaini bondi ya Shilingi za Tanzania milioni 15 kila mmoja, wakili wake Bennedict Ishabakaki aliieleza BBC.

Wawili hao wanatuhumiwa kufanya makossa hayo kinyume cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektoniki na Posta, na endapo watakutwa na hatia watakabiliana na adhabu ya faini isiyopungua Shilingi milioni tano, ama kifungo kisichopungua miezi 12 ama vyote faini na kifungo.

Mkurugenzi wa Amnesty International wa kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Deprose Muchena alisema:
''Ni ushahidi kwamba mamlaka nchini Tanzania hazina kesi dhidi ya Idris Sultan na wako tu wanamnyanyasa kwasababu uchekeshaji wake umewakwaza. Mahakama lazima ifute mashtaka yaliyobuniwa kupata sababu dhidi yake''.

Kabla ya kufikishwa mahakamani, polisi na wakili wa msanii huyo waliiambia BBC kuwa alikuwa pia akihojiwa kwa tuhuma za kutenda makosa ya kimtandao.

Wakili Ishabakaki pia aliiambia BBC kuwa mteja wake alikamatwa na kuhojiwa na polisi juu ya mkanda wa video uliosambaa mitandaoni hivi karibuni akionekana akiicheka picha ya zamani ya rais Magufuli.

Hata hivyo, hakufunguliwa mashtaka yoyote kuhusiana na suala hilo.
Hapo ndio wameharibu kabisa ,jamaa atateseka sana ,wamemchongea

Sent from my Infinix X627 using JamiiForums mobile app
 
Kutumia kadi ya simu yenye usajili wa mtu mwingine ni kosa kisheria, hilo lipo wazi.

Yajayo hayafurahishi kabisa.
 
Wanafanya makosa makubwa ya kizembe
Hawa vibaraka wa Magufuli huwa vichwa ngumu sana. Idris is no body in Tz ila wanamkuza wao kuzembe ivyo kama walivyowakuza wakina abdul nondo leo hii et nao wanagombea ubunge.
 
Ukitaka kuruka sharti agana na nyonga, ukiikebehi serikali hakikisha huna makando kando, la sivyo you will suffer the consequences.
 
Hawa ndo watakaomfanya afungwe au kulipa fine kubwa maana mahakama itataka ijioneshe kuwa haindeshwi na mashirika ya kimataifu...wamemuharibia
 
Nikiwa sina salio, nikaomba simu yako nipige simu ni kosa?

Hilo sio kosa.

Kosa ni kuimiliki hiyo simu ambayo haina usajili wako. Jikite kwenye ishu ya Idris ambe mada ndio ina muhusu. Ni kosa kisheria hivyo kwa busara tu wangeacha hizi kelele maana hazitasaidia kitu.
 
Sijaelewa, kwani bado wanamshikilia?? Au ni nani alomshikilia??
Nakubaliana nawe.Au ulikuta na yeye alifanya huku akijua fika baadaye watamganda hivyo na hiyo itampaisha zaidi.
Sijui wanamshikilia wa nini wamwache aende na njaa zake.
 
Back
Top Bottom