Idd Simba atetea posho za Wabunge

Cha Moto

JF-Expert Member
Jul 2, 2011
945
153
"Ninachosema ni hivi, kwa mbunge wa kweli ambaye anasimamia maslahi ya wananchi wake, hizo fedha si nyingi. Kwa sababu mbunge makini anahitaji kutoa misaada, kuona malengo ya wapiga kura wake yametimia na mambo mengi angependa kufanya,
Nilipokuwa mbunge niliandamwa sana na wananchi na nilikuwa nawasaidia kila wanapohitaji msaada kutoka kwangu,”

Hii ni kauli ya Idd Simba.

Source: Mwananchi 20/12/2011

Hivi ni kweli hizi ndio kazi za Mbunge Jimboni kwake?
 
"Ninachosema ni hivi, kwa mbunge wa kweli ambaye anasimamia maslahi ya wananchi wake, hizo fedha si nyingi. Kwa sababu mbunge makini anahitaji kutoa misaada, kuona malengo ya wapiga kura wake yametimia na mambo mengi angependa kufanya,
Nilipokuwa mbunge niliandamwa sana na wananchi na nilikuwa nawasaidia kila wanapohitaji msaada kutoka kwangu,"

Hii ni kauli ya Idd Simba.

Source: Mwananchi 20/12/2011

Hivi ni kweli hizi ndio kazi za Mbunge Jimboni kwake?

Is this guy still alive?
 
No no no!
I dont buy that!
Kwanini mbunge atoe fedha kama huruma yake na si kutumia mfuko wa Ofisi yake?
 
"Ninachosema ni hivi, kwa mbunge wa kweli ambaye anasimamia maslahi ya wananchi wake, hizo fedha si nyingi. Kwa sababu mbunge makini anahitaji kutoa misaada, kuona malengo ya wapiga kura wake yametimia na mambo mengi angependa kufanya,
Nilipokuwa mbunge niliandamwa sana na wananchi na nilikuwa nawasaidia kila wanapohitaji msaada kutoka kwangu,"

Mimi huwa ninajiuliza hivi ukiwa mwana CCM, hata uwezo wa kawaida tu wa kujenga hoja unapunguwa? Kama ni hivyo basi CCM is a mental disease. Hivi kazi za mbunge ni kugawa hela kwa wapiga kura wake? Huyu Idd Simba kweli hakupewa job description ya mbunge wakati alipokuwa mbunge.

Afterall wabunge siku hizi wana mfuko wa jimbo. Kwanini basi wasitumie mfuko huo jimbo kufanya maendelea katika majimbo yao? Idd Simba, FYI mbunge makini ni yule ayeisimamia serikali barabara ktk kutekeleza majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo. Mbunge makini si yule anayelilia kuongezewa posho ili apate pesa nyingi za kuwagawia wapiga kura wake, get real dude.

Kama wabunge wetu ndiyo hivi wanavyojenga hoja, basi huko kwenye mabunge ya EA, AU, Madola we are a laughing stock!
 
"Ninachosema ni hivi, kwa mbunge wa kweli ambaye anasimamia maslahi ya wananchi wake, hizo fedha si nyingi. Kwa sababu mbunge makini anahitaji kutoa misaada, kuona malengo ya wapiga kura wake yametimia na mambo mengi angependa kufanya,
Nilipokuwa mbunge niliandamwa sana na wananchi na nilikuwa nawasaidia kila wanapohitaji msaada kutoka kwangu,"

Hii ni kauli ya Idd Simba.

Source: Mwananchi 20/12/2011

Hivi ni kweli hizi ndio kazi za Mbunge Jimboni kwake?

Shughuli za kijamii katika Jimbo zina fungu lake - Mfuko wa Jimbo. Kumpa mtu kipato kikibwa kwa mategemeo kuwa atatumia sehemu ya hicho kipata kuna uhakiki gani unafanyika? Badala ya kuwapa ili waje tuwaombe Serikali ilipie dawa zote za magonjwa yanayowasumbua Watanzania wengi kama Malaria na Neumonia.

IDD Simba mwenyekiti wa kudumu wa PRIDE akaongeze Posho huko PRIDE ili azidi kuwalipisha riba wakopaji wake
 
Yaani, hawa watu hawajui wanachosema au ni sababu wanatuona sisi wananchi wapiga kura wao ni majuha?
 
What the @#$###$$%!!!! Hivi ndio vichwa ambavyo vilikuwa vinaweza kufikiri? This kind of reasoning? So kwanini wanaomba hela za serikali kwenda kwenye majimbo yao kama wanazopewa nikwa ajili ya misaada ya wananchi? Hivi ni Mtanzania gani ambaye haombwi misaada na familia, ndugu au hata rafiki zake? So serikali ianze kutenga kwenye bajeti posho ya misaada ya familia? $%$## him!
 
Tanzania anaeandamwa kuombwa misaada si mbunge peke yake. Yoyote yule anaejuulikana kuwa na kipato chochote mwisho wa mwezi huombwa msaada asubuhi, mchana na jioni

Asitake kuwafanya wabunge demi-god, kuwa wao wanastihili zaidi kwa sababu wanaombwa zaidi.
 
Idd simba ndio maana pride inakushinda hivihivi unaongea vitu visivyo na msingi eti posho ni sahihi kuongezwa! Badala ya kutetea fedha ya mfuko wa jimbo iwe inatolewa ripoti ya matumizi yake kwa wananchi we unatetea posho iongezwe, ama kweli hatuna viongozi wa wananchi Tz.
 
Iddi Simba anajaribu kupata huruma ya Wabunge ili wamnusuru pale kesi yake itakapotinga bungeni... Anajua kwa kuwatetea wao hasa kwenye issue ya posho, basi wabunge Magamba hawatamsulubu.

This is too low, too cheap for a person like him... Zamani tulikuwa tunaamini kuwa ukiwa mtu mzima au mzee basi busara zinakuwa zimekomaa na za kutosha kumbe busara nazo zinazeeka kama mtu mwenyewe.

Nyambaf.........



What the @#$###$$%!!!! Hivi ndio vichwa ambavyo vilikuwa vinaweza kufikiri? This kind of reasoning? So kwanini wanaomba hela za serikali kwenda kwenye majimbo yao kama wanazopewa nikwa ajili ya misaada ya wananchi? Hivi ni Mtanzania gani ambaye haombwi misaada na familia, ndugu au hata rafiki zake? So serikali ianze kutenga kwenye bajeti posho ya misaada ya familia? $%$## him!
 
Posho hizo zinatetewa kwa sababu zinawasaidia kuendelea kuchaguliwa.kihalisia wanaowapa (kama wapo)ni wale wapambe wao,ili waendelee kuwadanganya wengine kuwa mbunge huyu anafaa sana.Kwa vile mtaji wa viongozi wetu ni ujinga wetu na unafiki wa wajanja wachache wanaotulaghai ili wao wapate visehemu ya viposho hivyo.
Nachelea kusema kwamba kuwapa wabunge nyongeza yeyote ya fedha katika kipindi cha ukata huu, ni kudunisha demokrasia na ni unyonyaji.
Kwa kauli zao wanatudhihirishia kuwa wanahitaji fedha ya kuwahonga wananchi ili waendelee kuchaguliwa hata kama hawafai.
 
Mhhh Huyo ndo mzee wa uzawa policies..........ameshakwiba UDA ili azibe mapengo ya vipato...bado anawibia kina mama kupitia PRIDE...Ama kweli mwenye shibe hamjali mmwenye njaa..........
 
Hivi kwa wastani Jimbo moja lina wapiga kura wangapi na wabunge wangapi? Iddi Yanga unaweza kutupa takwimu ulisaidia wangapi na leo hii wako wapi (yaani wamekombokaje kimaisha kwa misaada hiyo)? ni lini kazi ya Mbunge imekuwa kutoa misaada na si kuisimamia mapato na matumizi ya serikali ili wananchi wawe na maisha mazuri? Hivi katika hiyo 200, 000 inayotolewamsaada ni ngapi kama siyo bukubuku zaidi buku teni? mbona unapingana na spika aliyesema nyongeza ya posho ni kwa ajili ya kupanda kwa bei za hoteli za Dodoma na nyama choma pale chako ni chako? SI NI KWELI KWAMBA NA WEWE 2015 UNANUIA KINONDONI BAADA YA IDDI AZAN KUTANGAZA KUTOGOMBEA NA HIVI KUANZA KUJIWEKEA MAZINGIRA WEZESHI?
 
Yaani, hawa watu hawajui wanachosema au ni sababu wanatuona sisi wananchi wapiga kura wao ni majuha?

tatizo wanashindwa kushirikiana na wananchi kuhamasisha kazi za kimaendeleo na kujigeuza wao ni wahisani wa kutoa misaada.
 
Mimi mbunge wangu sijamuona huu mwezi wa tano sasa. Hizo posho atakuja kutugawia lini?
 
Fisadi Iddi Simba anaongea Nini!

Huyu mzee ni fisadi wa kukubuhu na ndio maana alifukuzwa uwaziri wa viwanda kwa sababu ya kula magendo ya vibari vya sukali. Ufisadi uko ndani ya damu yake na ndio maana akiwa Mwenyekiti wa UDA akishirikiana na meya wa jiji mwizi wakaihujumu kampuni ya uma na fedha zikawekwa kwenye account ya Simba kama vile ilikuwa mali yake!! Sio hivyo tu huyu mzee anahusika pia na kubaka ardhi ya watu huko Katavi [ akishirikiana na Pinda] na kuiuzia kampuni ya kutoka IOWA marekani maelfu ya ekari za ardhi. Sio muadilifu hata chembe na hafai kusikilizwa na wazalendo wa nchi hii.
 
Back
Top Bottom