Camilo Cienfuegos
JF-Expert Member
- Apr 23, 2015
- 19,228
- 68,247
Huyu ni mbunge wetu anaemaliza muda wake hapa jimboni Kinondoni.
Katika muda wote aliokaa madarakani kama mbunge wetu hatuna cha kujivunia kutoka kwake, kwani Kinondoni pamoja na kuwa ni mjini lakini huduma za kiafya bado ziko chini, barabara za mitaani ndio usiseme ziko hoi, yaani tunashindwa hata na barabara za mitaa ya Temeke.
Mbaya zaidi, hali ya maji baadhi ya maeneo imebaki kuwa janga sugu ndani ya jimbo hili. Sasa imefika wakati imetosha.
Leo hii ndio unakumbuka shuka wakati kumekucha, unakuja kugawa rushwa kwa Wanaccm wenzako ili wakuchague tena kura za maoni. Watakupitisha huko CCM lakini nguvu ya umma (Ukawa) itakumaliza ifikapo Oktoba 25.
Nenda Iddi Azzan, tutakumbuka labda kwa ongezeko la mateja jimboni kwako.
Katika muda wote aliokaa madarakani kama mbunge wetu hatuna cha kujivunia kutoka kwake, kwani Kinondoni pamoja na kuwa ni mjini lakini huduma za kiafya bado ziko chini, barabara za mitaani ndio usiseme ziko hoi, yaani tunashindwa hata na barabara za mitaa ya Temeke.
Mbaya zaidi, hali ya maji baadhi ya maeneo imebaki kuwa janga sugu ndani ya jimbo hili. Sasa imefika wakati imetosha.
Leo hii ndio unakumbuka shuka wakati kumekucha, unakuja kugawa rushwa kwa Wanaccm wenzako ili wakuchague tena kura za maoni. Watakupitisha huko CCM lakini nguvu ya umma (Ukawa) itakumaliza ifikapo Oktoba 25.
Nenda Iddi Azzan, tutakumbuka labda kwa ongezeko la mateja jimboni kwako.