Safari_ni_Safari
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 23,273
- 17,096
Martin Luther King Jr aliyasema haya...bahati mbaya hakuwahi kuiona ndoto yake akiwa hai...naamini aliiona huko aliko.
Nami nathubutu kusema ninayo njozi...
Tafadhali jumuika nami katika njozi hii.....lete ya kwako
Nami nathubutu kusema ninayo njozi...
- Ya kuiona Tanzania mpya amabayo WAtanzania wote wanafaidika na mkate wa nchi
- Ya kuona viongozi au watawala wetu hawawi na nguvu nyingi za kimaamuzi mpaka wanajisahau
- Ya kuona mtanzania wa kawaida hanunuliki kabisa kwa gharama yoyote ile ili agawe haki yake ya kikatiba
- Ya kuiona Tanzania inabaki Jamhuri na sio usultani wa watu kurithishana madaraka
- Ya kuona kila mhalifu anashitakiwa na kuhukumiwa kwa uhaklifu wake bila kuogopa utajiri wake,umaarufu wake,ukaribu wake na watawala
- Ya kuona kiongozi wangu anatenda yale anayo yaahidi na kukubali pale anaposhindwa kwa kuwajibika kuachia madaraka bila kulazimishwa
Tafadhali jumuika nami katika njozi hii.....lete ya kwako