Na sasa hivi asilimia kubwa za nyumba ndogo (80%) ninazozifahamu mie ni mabinti wa Kichaga jamani. sehemu nnapofanyia kazi kitengo cha watu kumi na nne watano tumeoa uchagani haha, harusi nyingi sana saa hivi utakuta bibi harusi ni mchaga. ktk ujana wangu mpaka naoa asilimia tisini ya ma ex wangu walikuwa wachaga sijui kwa nini, labda preference ya mwanamke anayenipagawisha inapatikana huko hahaha, anyway all in all kwangu mie kuna mambo mengi sana yanachangia watu kuwaona mabinti wa kichaga wazuri/wabaya.
Kuna jamaa yangu ni mchaga tunafanya naye kazi aliniambia kabla sijao tena akinitania SHEMEJI MIMI SIWEZI OA MWANAMKE WA KICHAGA SABABU NI WAKOROFI SANA. ALINIAMBIA KWAO UCHAGANI MABINTI WA KICHAGA HUPENDWA SANA NA BABA ZAO INGAWA KIMILA HAWANA HAKI KIIVYO, SO KUTOKANA NA HILO HUWA HAWANA UNYENYEKEVU SANA NA YEYE KAOA MSUKUMA WA SHINYANGA.
Wenzetu wachaga wamepiga sana hatua kielimu, kifedha so familia nyingi za huko hasa Marangu, machame nk utakuta mwanamke kwanza amekwenda shule vizuri, na hata kwao wanajiweza, hii inachangia sana mwanamke kuwa na msimamo nilishasikia siku moja nikiwa Marangu akina mama wakimzungumzia binti yao wanasema kuliko mwanangu ateseke atarudi nyumbani hata biashara ntamfungulia, so dhana kama hizi zinawafanya mabinti wa kichaga kutokuwa na unyenyekevu/heshima sometimes kwa waume zao hasa kama mwanaume unakotoka si familia bora km kwa mwanamke. vile vile makabila mengine wanawake hufunzwa jinsi ya kuishi na mume, kumnyenyekea na heshima tele, lkn Uchagani ni kicheni party hizi za mjini, Send off na Harusi kwisha kazi na kwa binti wa kichaga aliyetoka narudia tena kwenye familia bora wazeiya kama huna mkoko/Usafiri dah grade yako itakuwa chini sana hata kwenye vikao vyao vya family za huko ukienda hautakuwa na heshima kiivyo. Kutokana na uwezo wa hali bora basi hata watoto wanaozaliwa huko huwa BOMBA hii inafanya wanaume wengi wapende TOTOZ za kichaga ingawa kwa muonekano wa uzuri huo unaweza ukawa na matumaini mengi lkn yasiwepo na kuleta failures kwenye uhusiano/ndoa hiyo. Hasa pale ambapo malezi yanapokuwa tofauti, KM wewe ni msukuma/mngoni au kabila lolote lile kutokana na tamaduni za kwenu unajua kabisa mke lazima afuate misingi fulani labda ulishazoea kuona mama yako au pengine akina mama wa kabila lenu wanatabia ya kuamka asubuhi sana kabla hujaenda kazini anakuwekea maji, anakuamsha anakuwekea chai, nguo zinapigwa pasi mzee hata kama na yeye anafanya kazi lkn anawajibu wa kuamka kwanza kabla yako kurekebisha mambo, hii inakujenga akilini kwamba hata utakapooa mkeo atatakiwa afuate mfano kama huu, lakini pale mambo yanapokuwa tofauti basi mahusiano huanza kuwa si mazuri na kuhamishia lawama za jumla kwa kabila alilotoka mwenzi wako. Nilipokuwa ktk uchumba huyu mke wangu ambaye ni mchaga alikuwa akiniuliza vitu vingi sana kuhusu mapenzi, style za kubanjuana, na nilimkoleza kweli kweli unacheza tena na mtoto wa KINGONI hahahah sometimes alikuwa akimlaumu sana Mother wake Eti alikuwa akimfungia sana ingawa alikuwa na Boyfriend wake ambaye hunipaga sana story zao za wakati huo hahaha lkn nilimuona akiwa mgeni sana kwenye mambo mengi sana ya mapenzi na akishangaa waziwazi sometimes tunagombana nikizidisha anasema eti HUO NI UMALAYA. lkn sasa kazoea na maisha yanaendelea. Kweli Kutokana na maendeleo yalivyo kwao huko Moshi ukioa mtoto wa kichaga huna budi kutafuta maendeleo kwa udi na uvumba coz wanapokutana wao utaona kila wakati kuna mabadiliko km ni gari basi wameongeza moja km ni nyumba utasikia tumehamia au tunajenga mbezi, au fulani ka graduate chuo kikuu anakwenda masters nje, so hivi vitu vinafanya hawa mabinti sometimes wawe selective au kuwa frustrated km alipo hakuna maendeleo na sometimes kusababisha mahusiano kulegalega.
Kuna ex wangu mmoja yeye alikuwa ananiambia nianze kutafuta biashara ya kufanya coz baba yake anaendesha petrol stations hapa town na kaka yake ana import computers yeye ana kama 20 mil ktk mgao wa family so nianze kutafuta biashara ya kufanya imagine huyu alikuwa amemaliza form six tuu anasubiri kwenda chuo kitu alichoniambia ni kwamba ndugu zake wana NYODO za kupindukia so niwe tayari kuwakabili, mie nikaona hapa hapajakaa sawa sawa mtoto alipoenda soma UGANDA mie nikakata kamba kimtindo.
MWingne baada ya hapo alikuwa anasoma Muhimbili pale facult of medicine huyu alikuwa mpole sana lkn hakuweza fikia viwango nilivyojiwekea hahaha. Kuna mengi sana ambayo nime ya experience ha hii jamii ya kichaga niki yaandika hapa patajaa