Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

kiongozi kuongea ongea hakuna maana kuwa ni mtendaji mzuri. Naweza kuongea mengi lakini uteelezaji 0, anaweza akawa kimya kabisa lakini uongozi wake na utendaji wake ukawa unaonekana wazi kabisa. Nani anaongea kama makamba hapa tz, utendaji wake je?
Ni lazima kuangalia jinsi wanavyodeliver bila kujali wanayoongea.
suala sio kuongea kila wakati ila mambo ya msingi ni muhimu kutoa msimamooo ueleweke..

Juzi kikao na wizara ya nishati wametoa makubaliano mojawapo ikiwa sheria ya manunuzi isiwe kikwazo cha uwekezaji katika maeneo muhimu....

Media wameripoti kwa kuunganisha na suala la dowans kawa mbogo salva kasahihisheeee.....anaogopa nini??? Tumempa heshima kubwa bado muogaaaaaaaaaaaa...

Yeye mambo yasiyo na tija anapenda kuyapigia gumzo kubwaaaaaaaaaaaaaaa....tunazidi kupata ugeni mkubwaaa eti twaheshimikaaa..hotuba ya mwezi hiyoooo...

Achambue mambo ya msingi na aongee sio press release na conference za akina salva..

We should see the president available talking on key issues like energy crisis....
 
Rais akiongea kila wakati wapo watakaosema huyu rais Kilomolomo sana.Rasi hawezi kuingilia every issue on the scene kwa sababu anaye msemaji wake.

Kama kuna mtu anayedhani kuwa Kikwete anaweza asichaguliwe na CCM kwenye mchakato wa urais mwaka 2010 ni mtu asiye na uelewa na siasa za Tanzania.

Kama kuna mtu anatamani sana Kikwete asiwe Rais wa nchi hii hapo 2010-2015 kwa sasa ameshachelewa na ataendelea kulia na kusaga meno.

Kama kuna yeyote kati yetu humu ndani anawaza Urais utatoka kambi ya upinzani kwa kipindi hicho hayuko realistic na hali halisi ya nchi hii.

Vyama vyetu havina uwezo wa kupambana na CCM hasa katika nafasi ya Urais na ingekuwa ni kwa manufaa yao kama wata concetrate katika kuwania nafasi nyingi bungeni.

Hii yote ni kwa sababu hali ya wananchi kiakili hairuhusu kuwapo na mwamko unaotakiwa ili kuleta mageuzi ya kisiasa.Tunaweza kutumia kigezo cha kuwaua maalbino kama sampuli ya ujinga wetu wa kufikiri!

Kwa hiyo kwa hali hii nani ataweza kusema kuwa Kikwete hawezi kuchaguliwa kuwa Rais?
 
Msiwe na wasi wasi vyama vitaungana na kuweka mgombea mmoja tu wa Uraisi kwa maana safari hii tunatarajia kuwa na wagombea wawili wa Uraisi Mmoja kwa tiketi ya Sultani CCM na mwengine kwa tiketi ya Vyama vya Machifu ,dalili ambazo zinaonekana hivi sasa ni baadhi ya Vyama vya machifu kuamua kuwapeleka machifu wake kugombea ubunge.

Hivyo tukae mkao wa kumwangusha Sultani CCM.
 
Nani anafaa? Hao wapinzani ndio mdebwedo kama askari wala urojo. Mara hamsini huyo Kikwete kuliko wapinzani walio lala doro.

Eti Bubu umesema wapinzani waungane! Halafu nani amwongoze mwenzie?! Nani akubali kutokuwa mwenyekiti au mgombea urais?

HAKUNA MWANANCHI(wengi) watako chagua vyama vingine.Tatizo watu tulio waamini wametutenda,hivyo ZIMWI LIKUJUALO.....
Naamini kwasasa hakuna Mtu ktk Tanzania hii anayeweza kuongoza,kama yupo hajiamini ndio maana hajajitokeza na kama hajiamini hafai maana atakua anaongoza kufuata maelekezo ya anao waamini yeye.
Wanao jitokeza sasa na kutaka uongozi wa nchi hii hawafanyi hivyo kwa utashi wa kuongoza bali wanatamani kuila keki ya Taifa wao wenyewe.
Labda wazuri hawajitokezi kutokana na taratibu za sasa ambazo zina kataa wagombea binafsi.Labda watajitokeza wazuri kama mgombea binafsi atajitokeza kwa sasa sera za vyama vyetu haviruhusu kuwepo kwa viongozi wa taifa
 
HAKUNA MWANANCHI(wengi) watako chagua vyama vingine.Tatizo watu tulio waamini wametutenda,hivyo ZIMWI LIKUJUALO.....
Naamini kwasasa hakuna Mtu ktk Tanzania hii anayeweza kuongoza,kama yupo hajiamini ndio maana hajajitokeza na kama hajiamini hafai maana atakua anaongoza kufuata maelekezo ya anao waamini yeye.
Wanao jitokeza sasa na kutaka uongozi wa nchi hii hawafanyi hivyo kwa utashi wa kuongoza bali wanatamani kuila keki ya Taifa wao wenyewe.
Labda wazuri hawajitokezi kutokana na taratibu za sasa ambazo zina kataa wagombea binafsi.Labda watajitokeza wazuri kama mgombea binafsi atajitokeza kwa sasa sera za vyama vyetu haviruhusu kuwepo kwa viongozi wa taifa

Hataa, Kikwete ni mzuri ila hayupo katika Chama ambacho kinafuata maadili ya sheria .Sultani CCM alimvuta Kikwete baada ya kugundua kuwa wananchi wengi wamemkubali na tayari baazi ya vyama vilikuwa vimeshamuarifu akipigwa na chini tu basi haraka akimbilie kwengine anakokujua.

Kosa ambalo alikuwa nalo Kikwete ni kule kuona angeweza kuwabadili mafisadi na kuwa wasamaria wema,angeweza kuwaelekeza na kufuatwa vile anavyotaka yeye ,angeweza kusikilizwa bila ya kupata pingamizi ,angeweza kuwafanya wafuasi wa Sultani CCM wawe wenye kufuata sheria na Katiba katika kuiongoza Tanzania.

Lakini pia alishindwa kufahamu au kuona ndani ya Mfalme CCM kuna minyoo ambayo hawasikii dawa ,minyoo sugu sawa na ile minyoo ya ng'ombe ambayo ni hatari kwa binadamu,inarefuka tu mpaka inakuuwa,minyoo ambayo tunaona leo ni wapi Tanzania imefikishwa ,njia panda !!Minyoo hii ambayo leo haimpi usingizi Kikwete ,kila anavyojaribu kupata usingizi minyoo inavuruga tumbo.

Kikwete anaweza kufanikisha mauaji ya minyoo hii ,ikiwa tu anaitakia mema Tanzania na WaTanzania kwa kuingilia kati suala la Katiba na kuamuru kuwa lazima lifanyiwe marekebisho ili kuinusuru Nchi.
 
Ndiyo maana nimewahi kusema hapa huyu Kikwete hafai kabisa hata kugombea tena 2010 maana kuna ushahidi wa kutosha kwamba uongozi wa nchi umemshinda. Jana Salva Rweyemamu mwandishi wa Rais, alisema kwamba Rais 'hahusiki kabisa na swala la mitambo ya Dowans' na sidhani kama anahusika na lolote ndani ya nchi yetu. Itakuwa vizuri wale ambao wanajiona wana sifa na uwezo wa kuwa Rais ndani ya nchi yetu waanza kujitokeza sasa maana kumrudisha tena Kikwete madarakani 2010 itakuwa ni kama kuitosa nchi kwenye maangamizo na huko upinzani naona bado hawataki kusikia kilio chetu Watanzania cha kuunda chaa kimoja chenye nguvu ili wachukue madaraka.

Hivi vyama vya upinzani bado vimelegalega sana kuweza kuchukua nchi lakini vikiungana basi Watanzania wengi tutakuwa tayari kuwaamini na kuwapa madaraka.

Hujachelewa mzee, anzisha chama, tukupe kula 2010
 
Wanaweza pia kutokea watakaompinga ndani ya CCM na hivyo kuhakikisha hapati tena nafasi ya kugombea 2010 kama mgombea toka CCM. Rais kama kashindwa kuongoza nchi katika awamu yake ya kwanza basi hastahili kabisa kuongezewa awamu ya pili. Kwa kipi alichokifanya katika awamu ya kwanza hadi astahili kurudishwa tena madarakani!?

Bubu hapa usibishe. Ndio maana ninasema tunapoitwa "stupid Africans who can not manage themselves" tunapoonekana watoto mbele ya wengine duniani ni kutokana na kufanya au kuendelea na yale ambayo hatustahili kuendelea nayo. 2010 sio mbali, inaweza kuwa ni muda wa u-prove kwa watu kama sisi ni kundi loa wajinga kama tunavyoitwa, au kuonesha kuwa sisi si wajinga. Sasa hivi kwa wenye akili timamu wameona sura halisi ya CCM ya sasa, ambayo ni tofauti kabisa na ile ya miaka zaidi ya kumi iliyopita, tuache kushambulia individuals kwa sababu wao wanawakilisha chama na wanabeba jina la chama, lakini 2010 ndio tuta-confirm kama sisi ni wajinga au si mabwege tna kama alivyosema Dr Mwakyembe.
 
Jana nilisikia wimbo wa taifa ukiimba, nikakurupuka kutoka nje nilipokuwa naoga.......

Kufika tu nakuta Mkubwa anaanza kutoa hotuba zake kama kawaida....

NDUGU WANANCHI HIVI PUNDE TUMETOKA KUSHUHUDIA SHEREHE ZA MUUNGANO, KWAKWELI ZILIFANA SANA NA NAMPONGEZA PINDA KWA MAANDALIZI MAZURI, TOFAUTI NA MIAKA MINGINE TULIKUWA NA MAONYESHO YA MBWA, WALIKUWEPO WATU WALIOZALIWA MIAKA 45 ILIYOPITA WAKATI WA UHURU....... MARA SWEETHEART AKAKURUPUKA HUKO ULIKOKUWA "wewe twende tukalale unasikiliza upuuzi gani? Mwanaume badala ya kuongea vitu vya maana kama dhana nzima ya Muungano anasifia sherehe.........." TV IKAZIMWA........ SIKUJUA KILICHOENDELEA MWENYE POINTI/PUMBA ZAIDI anaweza kutuambia nini kiliongelewa????
 
Duh!.

Sisi sikuhizi huku mbagala tunapenda Mpira kuliko hotuba yake hiyo.

Timing ilikuwa mbovu sijui muungwana hana washauri?, watu mjini wanapenda mpira halafu kipingi kinaendena kwa muda na mechi ya the blues na Catalans.

Unategemea nini?
 
Jana nilisikia wimbo wa taifa ukiimba, nikakurupuka kutoka nje nilipokuwa naoga.......

Kufika tu nakuta Mkubwa anaanza kutoa hotuba zake kama kawaida....

NDUGU WANANCHI HIVI PUNDE TUMETOKA KUSHUHUDIA SHEREHE ZA MUUNGANO, KWAKWELI ZILIFANA SANA NA NAMPONGEZA PINDA KWA MAANDALIZI MAZURI, TOFAUTI NA MIAKA MINGINE TULIKUWA NA MAONYESHO YA MBWA, WALIKUWEPO WATU WALIOZALIWA MIAKA 45 ILIYOPITA WAKATI WA UHURU....... MARA SWEETHEART AKAKURUPUKA HUKO ULIKOKUWA "wewe twende tukalale unasikiliza upuuzi gani? Mwanaume badala ya kuongea vitu vya maana kama dhana nzima ya Muungano anasifia sherehe.........." TV IKAZIMWA........ SIKUJUA KILICHOENDELEA MWENYE POINTI/PUMBA ZAIDI anaweza kutuambia nini kiliongelewa????
Teh teh teh teh misuse of public fund? hivi by the way kuna haja ya kutumia kodi zetu kumuhudumia kina Mzee Zombe na wenzake mpaka watakapohukumiwa? au tuzihamishie mahosipitalini tupate japo panadol? anyway muungwana ana program ya kugawa VYANDARUA kwa kila MDANGANYIKA ili tusife na malaria. Job True True!
 
Ile hotuba ilipswa kurushwa siku ileile ya Muungano, sijui kwa nini waliichelewesha!
 
Jana nilisikia wimbo wa taifa ukiimba, nikakurupuka kutoka nje nilipokuwa naoga.......

Kufika tu nakuta Mkubwa anaanza kutoa hotuba zake kama kawaida....

NDUGU WANANCHI HIVI PUNDE TUMETOKA KUSHUHUDIA SHEREHE ZA MUUNGANO, KWAKWELI ZILIFANA SANA NA NAMPONGEZA PINDA KWA MAANDALIZI MAZURI, TOFAUTI NA MIAKA MINGINE TULIKUWA NA MAONYESHO YA MBWA, WALIKUWEPO WATU WALIOZALIWA MIAKA 45 ILIYOPITA WAKATI WA UHURU....... MARA SWEETHEART AKAKURUPUKA HUKO ULIKOKUWA "wewe twende tukalale unasikiliza upuuzi gani? Mwanaume badala ya kuongea vitu vya maana kama dhana nzima ya Muungano anasifia sherehe.........." TV IKAZIMWA........ SIKUJUA KILICHOENDELEA MWENYE POINTI/PUMBA ZAIDI anaweza kutuambia nini kiliongelewa????

Kwi kwi kwi kwi kwi mkuu my wife wako atakuwa so brilliant. She knows her value of time and so would not waster her time for nonsense.

cheers
 
Jana nilisikia wimbo wa taifa ukiimba, nikakurupuka kutoka nje nilipokuwa naoga.......

Kufika tu nakuta Mkubwa anaanza kutoa hotuba zake kama kawaida....

NDUGU WANANCHI HIVI PUNDE TUMETOKA KUSHUHUDIA SHEREHE ZA MUUNGANO, KWAKWELI ZILIFANA SANA NA NAMPONGEZA PINDA KWA MAANDALIZI MAZURI, TOFAUTI NA MIAKA MINGINE TULIKUWA NA MAONYESHO YA MBWA, WALIKUWEPO WATU WALIOZALIWA MIAKA 45 ILIYOPITA WAKATI WA UHURU....... MARA SWEETHEART AKAKURUPUKA HUKO ULIKOKUWA "wewe twende tukalale unasikiliza upuuzi gani? Mwanaume badala ya kuongea vitu vya maana kama dhana nzima ya Muungano anasifia sherehe.........." TV IKAZIMWA........ SIKUJUA KILICHOENDELEA MWENYE POINTI/PUMBA ZAIDI anaweza kutuambia nini kiliongelewa????


Mkuu, hata kama ungekuwa wewe ungeianzaje hotuba? Embu tupe demo ungetuambia nini!.

kuna points za maana sana aliziongelea jana hasa lile la mafuta. Watu washaanza kugombania mafuta wakati watafiti kwa zaidi ya miaka 56 hawajaona dalili.
Wakati mwingine tupunguze chuki binafsi.
 
Mkuu, hata kama ungekuwa wewe ungeianzaje hotuba? Embu tupe demo ungetuambia nini!.

kuna points za maana sana aliziongelea jana hasa lile la mafuta. Watu washaanza kugombania mafuta wakati watafiti kwa zaidi ya miaka 56 hawajaona dalili.
Wakati mwingine tupunguze chuki binafsi.
Kwa hiyo zile fedha za walipa kodi zilizomlipa yule mshauri mwelekezi, za nini kama Kikwete anajua kuwa mafuta hakuna na na kwanini suala hilo likaingizwa kinyemela katika mambo ya muungano siku hizo wakati wakijua halipo?
Nani alimpa ujuburi Mkapa kupeleka timu ya watafiti kisiwani Pemba kabala Komandoo hajampiga stop, kilikuwa kinatafutwa nini huko, na kampuni ile ya Canada ilishatengewa hela ya walipa kodo kama haikupewa?
Kama kuna mtu aliacha kutizama mechi ya mpira (Barca na Chalse) kwa kuskiliza pumba zile huyo kapoteza muda bura kama hakuwa na jingine la kuafanya.
 
Mkuu, hata kama ungekuwa wewe ungeianzaje hotuba? Embu tupe demo ungetuambia nini!.

kuna points za maana sana aliziongelea jana hasa lile la mafuta. Watu washaanza kugombania mafuta wakati watafiti kwa zaidi ya miaka 56 hawajaona dalili.
Wakati mwingine tupunguze chuki binafsi.


Hata mimi nilipenda sana huu ufafanuzi alioutoa kuhusu mafuta.
 
Hotuba inatolewa baada ya siku mbili! by the way ile mechi ya the blues na Barca nayo ilikuwa kama hiyo hotuba tu, so i was forced to watch the "hotuba" as well!
 
Hata mimi nilipenda sana huu ufafanuzi alioutoa kuhusu mafuta.


ile hotuba alipanga kuitoa pale taifa ,mbele ya karume ..ikavuja karume akasusa kwenda kumsikiliza..jk naye akapatwa na mfadhaiko akashindwa kuisoma kwa kusononeshwa na karume..kwenye viti vya nyuma shamhuna na bosi wake nahodha wakawa wanamchora tu.....kutokana na ujumbe wa hotuba ikabidi kesho yake washauri wamwambie aisome....teh!
 
ile hotuba alipanga kuitoa pale taifa ,mbele ya karume ..ikavuja karume akasusa kwenda kumsikiliza..jk naye akapatwa na mfadhaiko akashindwa kuisoma kwa kusononeshwa na karume..kwenye viti vya nyuma shamhuna na bosi wake nahodha wakawa wanamchora tu.....kutokana na ujumbe wa hotuba ikabidi kesho yake washauri wamwambie aisome....teh!
Now You prove kuwa wazanzibar are no longer stupids.
 
Back
Top Bottom