Huyu ndiye Ruge ninayemfahamu!

Huyu ndiye Ruge ninayemfahamu!

Magwiji wa dawa za kulevya ni wale waliotajwa na Bashite halafu hadi leo wako mtaani?

Hakuna hata mmoja aliyefungwa wala kesi mahakamani. Kesi ya Wema uchunguzi haujakamilika hadi leo.

Ujinga mtupu tu.
 
Kama 'yule bwana' na Ruge ni marafiki kwa nini Ruge hakumuita chemba wakamalizana kirafiki badala ya kumuexpose kwenye jamii?usidhan tunaakili za nyumbu !tunajua kilichokuwepo nyuma ya pazia!Ruge anatumiwa!ametumika!
Uvamie kwa silaha makazi yangu ya kibiashara halafu nikuite chemba? Kuna urafiki gani wa hivyo? Silaha alikuja nayo ya nini studio na silaha ilitengenezwa mahususi kwa kumdhuru kiumbe haliye hai Je angemkuta hiyo silaha ingetumikaje kwa mfano? Mijitu mingine inafikiria kwa makwapa.
 
Vita kati ya mtoto wa town na mtoto wa kuja town
Na hatakaa amuweze,Ruge kasoma,anatoka familia iliyostaarabika nasikiaga tu kuwa baba yake alikua balozi na hata yeye mwenyewe amekaa kidogo huko oversees so ana exposure.na pia ruge ana akili ya biashara na ni mtafutaji hasa yaan mtt wa mjini.sasa sijui hao walitoka shamba but kifupi hawamwezi Ruge
 
Kwa hyo hakuvamiwa?, AMA alivamiwa kwa issue ya dawa badala ya Cd ya kuchonga?, mbona unahoji kama BASHITE Vileee...,akili ya kuvuka barabara Tu inatosha kulijua Hilo vema. Sasa wewe hata hyo hauna?.
mobile.mwananchi.co.tz/Habari/Sirro-awataka-Clouds-kutoa-ushirikiano/1597580-3936924-format-xhtml-s63y0e/index.html
 
Kinda kajichanganya yeye badala ya kuzungumzia tukio analalamika kuhusu ruge. Yeye kosa in kuvamia clouds. Bashite anatakiwa kuelewa ruge na clouds ni vitu viwili tofauti
 
Tukiachia mbali tuhuma za Bashite,
Mtu ambaye huwa simuamini kabisa ni Ruge, ni kwanini wengi wa wanaofanya nae kazi kwa karibu huishia kulalamika kudhurumiwa!?
Ila anajua kuongea vizuri aisee na anashawishi sana unapomsikiliza
 
Naona haya mambo nyuma ya pazia yako tofauti na wanavyotulisha sisi wananchi.
tena yanaweza kuwa mabaya zaidi ya tunavyolishwa sisi,ni vipi kama kuna cctv camera ilirekodi tukio zima lilivyokuwa mule ndani studio baada ya BASHITE kuvamia?
 
Ruge ni mnafiki Mkuu, alipokubali kutumikia magwiji wa Dawa za kulevya kwa kusingizia kituo chake kimevamiwa.

Kushindwa kuthibitsha tukio hilo, au kufungua jalada polisi
Ruge atoe ushirikiano kwa kamanda Sirro ili game iishe. Tumechoshwa na hz propaganda.
 
Akili za nyumbu pekee ndio zinaweza kuamini igizo hilo.
Tukio litokee ijumaa,malalamiko yatolewe j'3. Alievamiwa amtembelee mvamiaji j'mosi akae kwake hadi SAA 4 usiku wakipiga story wakati ni usiku tu uliopita alimvamia. Kisha j'tatu mvamiwa apewe muda wa kupumzika eti kachanganyikiwa.


Hapo wataamini igizo hilo manyumbu pekee. Ruge anabusara kunyamaza kwani angezidi kujiaibisha
You nailed it bro!
 
Mi nilishaachaga kumjadili bashite..naona ni afafhali house girl wangu ana akili kuliko huyo mtu..
 
Kama ulipitwa na taarifa ni kwamba Ruge alienda kutoa taarifa Oysterbay Police asubuhi baada ya siku ya tukio. Lakini kesi ya nyani hakimu Tumbiri. Najua ulipitwa tu na hii taarifa..au unafuata mkondo bila kujua ukweli. Anyway yeye yupo upande wa mpini...yanamwisho haya.
Mkuu usisahau alieshikiwa bunduki ijumaa usiku alienda asubuhi kwa mvamizi wake akashinda kutwa nzima na kupiga menu ya nguvu kwa mtesi wake hadi saa 4 usiku!! What a practical joke?
 
Nawe naomba uwe na akili kama umeonyeshwa clip mtu anavyoingia ndani na askari, why wasionyeshe clip ya kilichojili ndani, wameishia kulalama tu oooh! tumetishiwa na mitutu ya bunduki, mara Soud kapigwa, why wasionyeshe kilichoendelea ndani?
sijui kwanini lakini kumbuka aliyevamia ana nguvu ya serikali sasa kibusara huwezi kupambana na serikali na mimi naamini hata hiyo clip ya kuingia ilivuja bila kupangwa au ilipangwa ivuje kwa malengo fulani na huwezi jua labda kuna clip zaidi ya yaliotekea huko nyuma ya pazia ambazo hazijawekwa hadharani ambazo zinaweza kuwa mbaya zaidi ila wamezisitiri kwa matumizi ya baadae,maana mtu mliyekuwa mnamjua kama ndugu yenu leo kuwavamia na mitutu hii kwanza ni dharau kubwa kwamba kaonyesha anaweza kuwafanya kitu chochote na msimfanye kitu lazima mjiulize mara mbili mbili.kumbuka kuvamiwa kwa mitutu sio lazima watu wapigwe risasi ndio ujue kwamba walivamiwa.
 
Back
Top Bottom