Huyu ndiye Rais anayetufaa 2015

Huyu ndiye Rais anayetufaa 2015

Wengine wote wana hadhi ya kuwa raisi isipokuwa huyo mwizi wa mke wa mtu. Anahamasisha vurugu pia ni mdini.

Ama kweli kulia alie tetere akilia bundi uchoro.. Mbona mnamuongelea sana huyo Josephine wake kama mke wa mtu, au ndio mlikua washenga wake??
 
kama wasipoiba kura rais atakuwa DK PETER WILBROD SLAA....

idadi ya wapiga kura ikiongezeka hasa maeneo ya mijini na watu wa vijijini, wakielimishwa zaidi juu ya matatizo yanayoikumba nchi kwa kuendelea kuikumbatia CCM
 
Kwa nini tusijadili wkanza sifa za mtu anayepaswa kuwa rais wetu 2015 ili tuweze kupima ni nani mwenye sifa tunazozihitaji?

mpaka sasa hivi wewe ujaweza kupima ni nani anafaa kuwa rais wetu 2015????, sifa za kila mtu hapo zinajulikana Dr SLAA ni mwanzo mwisho.
 
LIPUMBA ATAPATA KURA MBILI,YAKE NA YA MKE WAKE MTATIRO,MEMBE HAWEZI HATA KUFIKIRIWA,LOWASA ATASHINDANA SANA NA SLAA,PINDA HAWEZI HATA KIDOGO KUINGIA KWENYE HIYO LIST

MSHINDI NI DR WILBROAD PETER SLAA

mkombozi wetu

Hivi huyo mzee atamaliza hata huu mwaka kweli?
 
mfumo uliopo ni tatizo,pia hata mfumo wa chama tawala nao ni tatizo katika nchi hii,kila anayetoka anamwaandaa wakuja kuziba mapengo yake.ndo maana sisi Watanzania wenye uchungu na nchi hii tunataka mabadiliko ya ukweli.tunataka chama kipya kituongoze, kije na mfumo mpya tena wenye tija kwa wananchi.Alipokuja Kikwete wengi tulidhani tumepata mkombozi,kumbe tulikuwa tunajishindilia msumari wa moto kwenye kidonda.Aliposema waacheni wazee wapumzike wenye aili tukajua kulindana kwanza,mwananchi baadaye.Tuna taka rais ambaye yupo tayari kula mihogo ikulu kuliko kuwaona wananchi wake wanatelekezwa katika nchi yao waliyotunukiwa na mwenyezi Mungu.Tunataka kiongozi mwenye ubavu wa kumwambia mkewe kuwa ikulu si pango la wafanyabiashara na wahuni.

Tunataka kiongozi wenye kujua kuwa wana wa nchi hii ndo waajiri wake wakuu,na anachotekeleza ni matakwa ya wajiri wake.Tunataka kiongozi asiye na uroho wa madaraka akiamini kuwa cheo ni dhamana,hatotunia cheo chake kwa faida yake binafsi na familia yake.tunataka kiongozi atayethamini madini yaliyopo hapa nchini ni mali ya watanzania,na hatajinufaisha na kujimilikisha migodi na ardhi kwa mahawara zake na familia yake.kiongozi atakayerudisha imani ya wananchi na uzalendo uliopotea miongoni mwa watanzania.

tunaomba Mungu atuwezeshe tubadilishe katiba ya nchi bila mizengwe ili miongoni mwao wana wa magamba wasipate hata mmoja na rais awe Dr. Slaa
 
Sidhani hao waliotajwa ndio wanastahili, badala ya kuuliza na kati ya hawa atakuwa rais mjadala ungekuwa nini tunahitaji na kuweka malengo kisha tuangalie na anaweza kutufikisha. Sioni mantiki kujua nani atakuwa rais kabla hatujasema atatufanyia nini..
 
ukweli rais ajae ni slaa iwe kwa alali ata kwa kuiba kura ni lasima dr slaa ashinde mpo apo
 
Hamna wa maana hapo, kweli tz imefilisika kiuongozi. Tz baada ya Nyerere haijwahi kua na Rais kiongozi wa kweli mwenye dira..wote wanakuja wanafanya madudu yao maka 10 inaisha wanastaafu na kuendelea kutusumbua na ving'ora vyao mjini hapa

tumefilisika kisiasa na kiuongozi hadi tunafikiriaviongozi mafisadi,(EL), viongozi boya, (Pinda), viongozi bora liende,(BM), viongozi siasa ni mtaji (Lipumba), viongozi wa kinadharia ili nipate, (slaa ambaye alidanganya pale mzumbe kua watapunguza bei ya simenti wakati haiwezekani bila kuondoa kodi na uongo mwingine kama huu)

Tumefilisika
 
Ni swali lililoulizwa na idhaa ya kiswahili ya radio ujerumani leo,, lilihusisha viongozi 5 wa vyama vya siasa,
NI NANI ATAKUWA RAIS 2015 KATI YA HAWA:?

1. BERNAD MEMBE
2. EDWARD ROWASA
3. PM PINDA
4. DR SLAA
5. PROF. LIPUMBA
Mimi nadhani kati ya wote hao hakuna atakayekuwa rais. Kwa utafiti wangu niliofunya tukishirikiana na wanaccm wenzangu, naona Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania atakuwa ROSTAM AZIZ
 
Kwa mtazamo wangu, Dr. Shein amekuwa ni kiongozi wa CCM ambaye afungamani na vikundi ndani ya CCM, hana kashfa kama ilivyo kwa viongozi wengine wa CCM, PhD yake ni ya ukweli, Ni mchapa kazi kwani Zanzibar inaonekana sasa ilivyotulia na kuna mambo mengi ambayo yanaonekana kwamba kuna maendeleo yanafanyika. Kifupi huyu mzee ametulia ukilinganisha na wengine ndani ya CCM, hata wapinzani sijawasikia wakimuongelea ubaya au mabaya yake huyu mzee.

Je inawezekana CCM ikamsimamisha kama mgombea uraisi 2015?, Itakuwa vipi ikiwa ni Dr. Sla'a Vs Dr. Shein 2015. upinzani utakuwa mkubwa au yatakuwa ni yaleyale tu.
 
Tatizo ni Dr Shein si mwanamtandao halafu mpemba hivyo nafasi ya kushinda nafasi ya kiti cha urais ni ndogo mno. Halafu ni mtu mwadilifu sasa mafisadi hawamtaki ndio maana walimpeleka Zanzibar akamalizie pensheni yake kule apumzike. Ushauri mzuri mkuu ila kama mchangiaji hapo alivyotangulia kuukaribisha ushauri huo ni sawa sawa kuomba Dr Salim Ahmed Salim agombee tena Urais ni ngumu mno.
 
If that would be the case then Slaa will have do concede defeat even before the NEC announces elections schedule. There is no any politician, be from CCM or opposition, that can come close to Shein's wit.
 
Kama ambavyo wakristo walivoichukulia na kueneza propaganda kuwa cuf ni chama cha kidini (waislamu) ndio hivyoivyo waislamu wanavyokitambua chadema kuwa ni chama cha wakristo (wakatoliki), kama ambavyo tumegawika ivi basi ccm itaendelea kutamba na kutesa kwa kutumia theory ya divide and rule.
 
Back
Top Bottom