Huyu Mzee Matonya aliyepata msamaha wa Rais ni nani na alifanya kosa gani?

Mimi bado napinga Uamuzi wa Magufuli wa kuwasamehe kina Babu Seya hata Kama ni uamuzi halali!

Nategemea Mashirikia ya haki za Watoto wapinge nao!

Watu wameenda mpaka Court of appeal na wamefanya review ya Kesi bado wamekutwa na hatia Halafu wanaachiwa kwa kweli sijaipenda hata Kama Rais Ana haki hiyo!

Maamuzi kama haya yanafanya wanainchi waweze kutafakari umuhimu wa kuwa na sheria na katiba bora zaidi. Hili ni swala moja kati ya mengi ambayo yanahitaji mabadiliko makubwa kwenye sheria za nchi hii. Mkuu anaweza akawa hana kosa kwa sababu sheria imempa nafasi hiyo. Lakini sisi wengine tunajifunza nini?
 
Halafu katiba inasema Rais atatoa msamaha huo kwa nia ya kutenda haki!! Sasa najiuliza tu Alikua na nia ya kutenda haki ipi kwa babu seya?

Ndipo tunapotakiwa kuijadili Katiba yetu he inakidhi??

Kuna mahali Katiba yetu INA matundu mengi yanayotakiwa kuzibwa.Muhanga wa kulawitiwa haki yake iko wapi?Au kama kawaida ni kosa la kubambikia?

Najiuliza Mahakama zetu tuziamini kwa asilimia 100 au ziko compromised na watawala,wenye pesa au wanasiasa?
 
Unafiki wa Watanzania naushudia kwenye huu Uzi.
Duniani kote bila unafiki mambo hayaendi vuta picha Libya walivyomgeuka Gadafi, wazimbabwe walivyo mgeuka Mugabe na sasa Trump anautangaza mji wa Jerusalem kuwa makao makuu ya Israel watu ndo wanakumbuka hivi ni kweliee!
 
Kama amekaa mahabus miaka 7,then akahukumiwa maisha halaf akatumikia kifungo miaka 37 hawez kuwa yule omba omba,ina maana kahukumiwa wakat mm nazaliwa na hyu matonya ombaomba nilishamwona kwa macho,so nadhan ni mtu mwngine ila majina yamefanana
Matonya omba omba kumbukumbu zangu zinasema alisha fariki huko dodoma
 
Mimi bado napinga Uamuzi wa Magufuli wa kuwasamehe kina Babu Seya hata Kama ni uamuzi halali!

Nategemea Mashirikia ya haki za Watoto wapinge nao!

Watu wameenda mpaka Court of appeal na wamefanya review ya Kesi bado wamekutwa na hatia Halafu wanaachiwa kwa kweli sijaipenda hata Kama Rais Ana haki hiyo!
But Katiba imempa Raisi uwezo wa kumuachia mfungwa yeyote
 
Katiba hiyo imempa Madaraka Rais hata Mtu akikulawiti Wewe Yeye ndie Mwenye Mamlaka ya kusamehe sio Wewe muathirika.
Tatizo liko kwenye katiba yetu imempa Raisi madaraka makubwa sana ndio maana hata hukumu ya hii kesi ilileta gumzo kubwa sana mtaani.
 
Back
Top Bottom