Huyu mwanaume simwelewi kabisa

Huyu mwanaume simwelewi kabisa

Hivi mke wangu, hizi habari za kupimana kwenye mapenzi mnafundishaga darasa la ngapi kwani? Kwenye syllabus yangu zikupitiaga hayo makitu.

Kupimana? Eti anakupima? That is a weak ass man ambaye hawezi kukuchunguza, kuongea na wewe kupata majibu mpaka akupime...dah au ni topic mpya ya Chemistry!???

Sent using Jamii Forums mobile app
Switi hii topic itakua inafundishwa twisheni tu
 
wanaume dzaini hiyo wanakera manina zao kitonga gani hicho unashindwa ata kununua nyanya ata siku moja ila na ww nakulaumu kwa kumuendekeza pale anapokuambia naja kula ungenjibu sina chakupika ungeona angefanyaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
acha ujinga binti yani unalea lijianaume lipuuzi fala kabisa na wewe upo hakuna mpenzi hapo .. okey unalimwanaume lisilojali halafu nategemea mkatambulishane Yesu Ruwa hivi kwa nini usimkimbize huyo tegemezi.. hawezi kuja kuweza nunua hata chumvi .. khee khee halafu utakuja kusema ndoa chungu wewe unafuga mwenyewe hilo lijitu uje utegemee mabadiliko.. kwanza mwanaume wa kutumia pesa ya mwanamke si mwanaume
wanaume siku hizi hamna manka

Sent From Ikulu-Magogoni street
 
Jamani naombeni ushauri wenu ndugu zangu nilikua na rafiki wa kiume close friend yaani tulikua marafiki hasa kiasi kwamba haiwezi pita Masaa 2 hatuwasiliani usiku tunaongea mpaka SAA 5 usiku.

Kuna siku alienda kazini akachelewa kutoka akanipigia best ndio nafika alafu gesi imeisha kwakua ni rafiki sikuona ajabu nikamwambia njoo ule huku akaja kula Sijui kilitokea nini tukajikuta tupo katika mahusiano ya kimapenzi kweli mi nilikua nampenda sana before nadhani hata yeye.

Sasa kilichofanya niombe ushauri ni tabia ya jamaa kifupi tumepanga kufikia December tuwe tumesha tambulishana kwa wazazi lengo tuje tuishi pamoja ambacho simuelewi jamaa anaweza piga simu pika nakuja kula kweli najipinda napika anakula anaondoka au anaweza pata mgeni akaniambia piga ninamgeni tunakuja kula nawapikia jamaa hanunui hata mboga wala tu kujiongeza angalau alete hata nyanya tu hapana

Yeye ana kazi nzuri analipwa karibia 1million per month mimi mbangaizaji tu lakini hata huruma hana nashindwa nimuelewe juzi aliniambia njoo uninunulie lunch nikamwambia sina hela basi.

Jana kaja nimekuja kula ikabidi niandae chakula akala akaondoka jamani nashindwa kumuelewa ni mtu wa aina gani mi sio muongeaji sana nashindwa kumuambia nataka niachane nae je naanzaje? maana ukweli nampenda Jamaa ana 36 mimi nina 30.
Naombeni ushauri wenu
Hakufai piga chini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuuu hii iliwahi kunitokea, ila wanyamwezi mungu anawaonaaaa...
Nikafika mahali nikamwambia stop huwezi kugharamikia chakula basi ndiyo akabadilika akija analeta Michele,mafutA,n.k yani ukiendekelea kumkenyulia meno atakuzoea
 
Hahahaha duh unashindwa kumwambia....fanya hv kama huwezi kumuambia face2fce mtumie message
 
Mahusiano ya mwamaume na mwanamke huwa ya aina tofauti tofauti. Wengine huwa marafiki tu wa kama dada na kaka, wengine urafiki usio na masharti (wanajirusha when the need arise), na wengine hujenga uhusiano wenye malengo ya siku za usoni waishi kama mke na mme. Jua wewe unaamngukia kundi gani. Na muhimu zaidi usilazimishe kuolewa, mtu wa ndoa utamuona tu mnavyo elewana, wala huta hitaji kuuliza mtu. Jitahisi sana katika maisha ya mahusiano kuwa na maamuzi yako mwenyewe bila kushirikisha wadau, ili lolote litakalotokea uwajibike mwenyewe. Kuhusisha wadau kwa maswala ya mustakabali wa mahusioano kunaadhara mengi zaidi ya faidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamna mtu hapo, kwa umri wake si mtu wa kuanza kumuelekeza mambo madogo madogo kama hayo, litakapokuja swala la mimba si
ndio atapotea kabisa.
mwanaume akishakuzimia, hujibebesha majukumu bila hata kuambiwa.
 
Duh 30-36 ndio mnafanya mambo ya kitoto hayo au ndio mapenzi upofu.

Anyway muda unakimbia mdogo wako nakushauri mapenzi ni utu ,Pia mwambie wewe unahitaji familia.
 
Back
Top Bottom