Kahama- shy
JF-Expert Member
- Oct 18, 2024
- 1,951
- 2,694
Habari za Leo jumapili ndugu zangu Natumaini nyote na mnaendelea na majukumu, Leo nikasema nifue nguo zangu hapa Nyumbani, Leo jumapili ila sabuni dukani huko Nina deni nifanyeje, hiyo Asubuhi Kuna watoto Huwa wanachunga mbuzi nikamuita mmoja nikamuangiza mara Moja chap sh 2000 alete sabuni ya unga na kipande,
Eeh si mara kaenda mazima subiri subiri na wewe wenzake Nyumba ni wapi nikaenda, namkuta na mother ake wamekaa ameniona ndukii kumbe alikuwa anagalia kila njia ntatokea wapi! namwambia yule mama ata hanielewi ananijibu "Baba nyie wenyewe mlielewana huko Mimi sikuwepo akija ntamuuliza"
Dah! imeniuma Nimejiinamia nawaza nimshikilie mbuzi mmoja ndo wanilipe, huyu mtoto nikimshika naweza kupata kesi niachane nae, na mother ake anielewi, roho inaniuma wakuu najuta natamani muda urudi nyuma nikanunue mwenyewe tu nimerudisha ndani!
Nilikuwa nimeandika mpaka kikaratasi ili ata akipita mtoto mdogo nimuagize tu😢
Eeh si mara kaenda mazima subiri subiri na wewe wenzake Nyumba ni wapi nikaenda, namkuta na mother ake wamekaa ameniona ndukii kumbe alikuwa anagalia kila njia ntatokea wapi! namwambia yule mama ata hanielewi ananijibu "Baba nyie wenyewe mlielewana huko Mimi sikuwepo akija ntamuuliza"
Dah! imeniuma Nimejiinamia nawaza nimshikilie mbuzi mmoja ndo wanilipe, huyu mtoto nikimshika naweza kupata kesi niachane nae, na mother ake anielewi, roho inaniuma wakuu najuta natamani muda urudi nyuma nikanunue mwenyewe tu nimerudisha ndani!
Nilikuwa nimeandika mpaka kikaratasi ili ata akipita mtoto mdogo nimuagize tu😢