mamie full mlango kuachwa wazi,hataki ufungwe na rafiki zake mara waingie mara watoke
Kesha kusoma muda mrefu akakuona bongo lala akaamua kukuchezea shere! Na yupo sahihi sana na mawazo yake hivyo alishachonga na washikaji ili akutese kisaikolojia. Inteliensia inanipa mambo yafuatayo:
1. Ana relax sana unavyoteseka juu yake na huenda kila akisongwa na masomo anafikiri njia ya ku refresh mind na kupata raha ni kukuona ww unavyohangaika dhidi yake.
2. No.1 hapo juu ndiyo iliyopelekea kuwasimulia rafiki zake na wao wakataka kupata raha hiyo; hivyo wakakufanya zuzu kwa hayo waliyokutendea.
3. Kama unamtaka bado ni rahisi kumpata kwa kujifanya ----- km anavyoamini yeye na rafiki zake ila chukua tahadhari kubwa sana. Wale rafiki zake na hasa km ni wakiume watakudhuru au kukuzulia bonge la kashfa.
4. Usilipe kisasi chochote cha kuiba, kudhuru au kudharirisha maana ww utakakuwa na hatia. Tumia huo ujinga wake kwa kufuata mtiririko fulani wa hesabu za saikolojia ya mapenzi. Utampata ki ulaini sana. Fanya yafuatayo:
a. Bila kuonyesha chuki, dharau, ama ugomvi, uchune kabisa km kwamba hakuna kilichotokea na usionyeshe dalili zozote za kuonewa au kujutia. Akikusalimia au kukuuliza chochote mjibu swaafi bila shida na usimkumbushie kwa muda hadi miezi miwili. Binadamu aliyekutenda huumia mara nyingi zaidi anapokuona hujali na huchukui hatua yoyote, iwe kujuta, kukasilika, kuomba msamaha, n.k.
b. Ni PM kwa maelezo zaidi. Ukifanikiwa rudi hapa uwaeleze members!