Kuna siku nilikua restaurant, ni Mbezi beach vile, napata lunch, mara akatokea kijana wa kati ya 12 - had 15 yrs, akasogea nilipo, haongei ila ananitazama tyuuh, kwa muonekano wake ni km wale watoto wa mtaani, yaan yuko rafu, nlijskia aibu na huruma, nkamuagizia chakula, akakataa akasema bas nipe hela nikale nyumbani na wenzangu, nikampa 3k akashukuru na kuondoka.
Baadae eti wahudumu wananiuliza km nimempa chochote, nikajibu ndyo nimempa hela, wanashangaa na kulaumu eti yule ndo kawaida yake kufata wateja na kuomba, sasa km wanajua hawataki, kwann wanaruhusu aingie? Mie nikala nikalipa bill nikaondoka zangu. Ila niliwaza sana, mtoto km yule awe omba omba ili familia ishibe, nikajisemea kweli Dunia ni duara. 😢😢😢
Ila huyo baba sio mstaarabu na hana utu, mtoto mdogo huyo kashindwa kumkaribisha ale, mmmh