Huyu binti atanifanya niwe masikini

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,270
40,084
Nimetembelewa na mdada mrembo (pisi kali kweli), kwa sasa anakaribia wiki kukaa hapa kwangu. Anategemea by jumapili ijayo aweze kuondoka.

Tangu amefika kwangu, hela imekuwa haitulii. Kila siku hela inatoka tu, na mbaya zaidi anaujauzito wangu unaokaribia mwezi.

Leo atakuambia, naomba hela ya kusafisha kucha, mara hela ya kunyoosha wigi, mara nipe hela kidogo nitume nyumbani, mara hela ya mafuta ya kung'arisha ngozi yanagharimu elfu 60, mara nipe hela nikanunue chakula, na akishanunua hicho chakula hali; mpaka nyumba imekuwa na mabaki ya vyakula ambavyo havijatumika.

Mbaya zaidi, majuzi aliniomba twende 'club' kwa sababu ni mtu anayependa sana mziki; kwa upande wangu nikawa sijisikii vizuri, nikamwambia siwezi kwenda. Akanilazimisha, ikabidi nimruhusu yeye mwenyewe aende.

Alipoenda huko kwenye starehe akajisahau kurudi nyumbani; nikawa nampigia simu mpaka saa saba usiku hajarudi; kwa hasira, nikachukua nguo zake nikaanza kuzichana chana, kwa kuhisi labda yuko na mtu mwingine.

Asubuhi, akarudi huku anamajeraha mkononi; kwa sababu alipata ajali ya boda boda usiku wakati akirudi nyumbani. Wasamaria wema, wakambeba na kumpeleka hospitali kwa sababu alikuwa amezimia.

Baada ya kunipa hayo maelezo; ilibidi niende hospitali pamoja na kulipa bill. Lakini roho ikawa inaniuma, kwa kusababisha uharibifu kwenye nguo zake.

Ikabidi niingie gharama ya kumnunulia mavazi upya; hapa natamani hata leo aondoke, kutokana na hasara anazonipa.
 
ulifeli mwanzon inaonekana uliingia kwa gia ya kuwa una mihela

Na yeye anatembea na beat la Kwanza uliloingia nalo kuwa upo financially stable

Mueleze ukwel tu kuwa maisha yako n tia maj tia maji

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Tulikutana mazingira ya starehe, na wote tulikuwa wanywaji; kuna kipindi natumia sana na kuna kipindi situmii sana, ili nitimize malengo yangu ya kimaendeleo.
 
Namna ya kumuambia aende kwao ndio tatizo, nitaanzia wapi, nitaonekana namfukuza. Kwa sababu amesema jumapili anaondoka, ndio namsubiria tu, akiondoka tu, napoteza mawasiliano.
Mtu ana kiumbe chako unataka kumpotezea?damu yako alee nani?
Be a man, mshape unavyotaka. Akiomba hela km unaona hicho kitu sio cha maana mkatalie.
As long as ni mjamzito you have the upper hand ktk mahusiano yenu.
Na km humtaki tena mwambie kabisa kuliko kumpotezea, then yy aamue km kuikeep io mimba au kuitoa.
By theway acha hasira za kitoto, unachomaje nguzo za mwenzi wako? Did that solve any thing?
Hizo ni dalili violence in you, jitahidi kuzuia hasira zako otherwise ipo siku utakua na kesi ya kujibu.
Otherwise Good Luck.
 
URGENT SALE

Kiwanja Kina Hati Kinauzwa
Maeneo ya Kigamboni Puna Block L
Nauza bei ya Discount 6,000,000
Ukubwa wa kiwanja ni SQM 520
Huduma ya maji na umeme ipo
Tika feri ni Kilometer 30
Nipigie 0689 051480
Niamini nauza bei nzuri sana kwa maeneo hayo kiwanja kama icho ni kuanzia mil 10
Mkuu puna na YaleYale puna ni sehemu moja?
 
Mtu ana kiumbe chako unataka kumpotezea?damu yako alee nani?
Be a man, mshape unavyotaka. Akiomba hela km unaona hicho kitu sio cha maana mkatalie.
As long as ni mjamzito you have the upper hand ktk mahusiano yenu.
Na km humtaki tena mwambie kabisa kuliko kumpotezea, then yy aamue km kuikeep io mimba au kuitoa.
By theway acha hasira za kitoto, unachomaje nguzo za mwenzi wako? Did that solve any thing?
Hizo ni dalili violence in you, jitahidi kuzuia hasira zako otherwise ipo siku utakua na kesi ya kujibu.
Otherwise Good Luck.
👍👍
 
Back
Top Bottom