BiMkubwa
JF-Expert Member
- Jan 9, 2007
- 529
- 98
Kwanza pole sana kwa yanayo kupitia ni maisha ila kinachotakiwa ni nyie kuwa strong kwa ajili ya mama yenu na kupata afya ya kisaikolojia. Je mama ni mfanyakazi au mama wa nyumbani? je wewe ni mwanafunzi? Naomba ufanye jambo moja tumia hasira na aibu uliyonayo juu ya matendo ya baba yako kama chachu ya kujitafutia maisha tofauti. kama ni mwanafunzi soma kwa bidii kama ni mfanyakazi jitenge na makundi bali elekeza nguvu zako kujijenga kimaisha. jiendeleze. kwa upande wa mama yako atafute likizo fupi ya kujipumzisha ili ajipange upya. akirudi aishi kama hamuoni baba yako wala asiyafikirie matendo yake. hakuna kitu kinachoweza kumsumbua akili mtu kama mwenza asiyekujali wala hana habari na wewe. atumie muda wake kuwatazama watoto wake mambo mengine yawe secondary. Primary goal yake ni kuwa na furaha na afya. Baba yako ni mtu mzima. lutumia muda mwingi mkiwazia anayofanya ni kumpa nafasi ya kuharibu maisha yenu. msisahau kumweka Mungu ktk maombi yenu ya kila siku. Kila chenye mwanzo hakikosi mwisho.