pole sana kwa hali unayopitia. najua inauma sana hasa kwa mtu ambaye wewe ulimwamini kwamba awe modo kwako anapokuwa na tabia za kishenzi. si bure baba yako kaathiriwa na ""u-late blooming"" na hivyo kijikuta yuko kwenye mid life crisis.hakukua kwa kufuata njia zote za makuzi ali delay somewhere akaruka stage sasa anajirudia tena nyuma.
jambo la msingi la kufanya kwanza kabisa usiweke chuki nae, wla jeuri ila tu kaa kimya huku ukimtia mama yako moyo na kuwa na nidham njema kwa mama yako. jihimizen katika kusali na kufanya ibada ili Mungu akutane nae kwa wakati wake na hili ndilo jambo la mwisho unaloweza kufanya.
otherwise haya ni maisha yake na huwez kuingilia uhuru wake and he is your father. kama una gf wako mweke mbali asije akamuharibia siku basi.
Ushauri mzuri sana.
Mkuu pole sana, ni hali ngumu kuipitia, endelea kuomba Mungu, endelea kumsihi baba yako kwa Hekima ya hali ya juu ipo siku atabadilika kabisa. kuna watu walishapitia vitu vya ajabu sana na vya aibu sana lakini kutokana na maombi ya wengi Mungu aliingilia kati.
Pili, huyu ni mzazi wako kumbuka, na kama anakosea haikupi haki wewe ya kumkosea hata kidogo, na ukiendelea kumuwekea bifu hata akiacha laana lazima itakupata kaka, Kwenye Biblia -Mwanzo 9:20 kuna kisa cha Nuhu na wanawe , mmoja aliuona uchi wa babaye akiwa
mlevi akamcheka babaye na mwenzake akamsogelea kinyume nyume akamfunika. Baba akamlaani pamoja na ulevi wake yule aliecheka na ikawa kama alivyosema - Mungu anaangalia
haki ya mtu anapoacha baraka/laana haangalii dhambi zake. kwa hio kukosa kumheshimu akisema neno juu yako halitarudi bure believe it or not bro, watch out two wrongs never made it right)
Pia unaweza kuongea na viongozi wake wa kidini (wenye hekima) waweze kumuita, kumkanya na kumuombea Baba bila yeye kujua kuwa ni wewe uliefanya hivyo, ionekane hao viongozi ndio wameona hii kitu na kuamua kumuonya.
Upande wa pili, Mama naye
inawezekana alikua tatizo kwa upande flani, (simtuhumu) maana mambo ya wazazi ni mengi pia, wengine hufikia kuadhibiana kwa kunyimana unyumba, matokeo yake mmoja anatoka anaonja nje anapewa maufundi so inakua ngumu kurudi tena cha nyumbani. au pengine huwa anajaribu kuacha na kumrudia mkewe then anapigwa kipepsi, who knows?
Kwa hiyo silaha yako kubwa kama mtoto ni maombi, shirikisha pia waombaji wachache, Mungu akakutane na ufahamu wake aweze kumbadilisha. Mwili huwa haushauriki kaka.