Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

SEHEMU YA 54...

“Nimesurika tena!” Alisema bibi Nyanjige wakati akinyanyuka kutoka ardhini ni yeye peke yake ndiye hakushambuliwa na ng’ombe siku hiyo kila ng’ombe walipomsogelea alitoa mlio ulioishia na “ssssssssss!” na ng’ombe wote walimwacha na kuwashambulia wamasai.

Baada ya kunyanyuka bibi Nyanjige alitembea kuelekea msituni huku akichechemea! Mwili wake wote ulimuuma na ulijaa majeraha sababu ya kipigo alichopata! Mbele kidogo kama kilometa moja alijikutaka akitokeza barabarani alikuwa akisikia kizunguzungu sababu ya kupoteza damu nyingi na alihisi asingeweza kuendelea zaidi na muda mfupi baadaye alianguka chini.

Ghafla alisikia muungurumo wa gari likija kwa mbali na alipojaribu kunyanyua kichwa chake kuangalia ulikokuwa ukitokea muungurumo huo alishindwa na kuendelea kulala chini! Giza lilikuwa limeyafunika macho yake
“ Ni kitu gani kile pale!” Dereva alimuuliza msaidizi wa mkuu wa majeshi baada ya kuona kitu kama mwili wa binadamu umelala chini!

“Au ni mmoja wa watu waliojeruhiwa na ng’ombe?”
“Hapana watu wa kijijini watakuwa hawajafika huku!”

“Sasa ni nani? Halafu naona yupo uchi wa mnyama! Hebu chukua bunduki yako tukamwangalie!”Mkuu wa majeshi alisema na wote wawili walichukua bunduki zao na kuanza kusogea mahali ulipolala mwili ule!
 
SEHEMU YA 55...

Walishangaa kukuta ni mwili wa bibi kizee! Dereva aliusukuma kwa mguu wake wa kulia ukalala chali, hawakuamini macho yao walipokuta alikuwa ni bibi Nyanjige!
Bunduki zote mbili zilimlenga bibi Nyanjige ardhini na hasira ilizidi kuwapanda mkuu wa majeshi na dereva wake, mioyo yao iliwaambia wammiminie idadi kubwa ya risasi ikilinganishwa na unyama alioufanya bibi kizee huyo lakini walishindwa kufanya hivyo baada ya kufikiria agizo walilopewa na mkuu wa majeshi.

“Ikiwezekana mmlete akiwa hai ili akaushwe na kuwekwa jumba la makumbusho...!” Kauli hiyo ya mkuu wao ilikuja vichwani mwao.
“Nyie mbwa hebu nipigeni hizo risasi zenu ili mimi nife nipumzike! Au hamjui kutumia bunduki nini? Nyie wapumbavu sana yaani bibi kama mimi nimewasumbua kiasi hicho?” Bibi Nyanjige alisema maneno ya kutia hasira ili kuwalazimisha wampige risasi! Alitamani kufa kwa risasi kuliko kuingia mikononi mwa wanajeshi.

“Para tat lita-pa! Pa! Pa!”Risasi zilisikika zikilia
“Mkuu umefanya nini sasa? Umesahau maneno tuliyoelezwa kuwa tumepeleke akiwa hai?”Dereva aliuliza.
“Hasira imenipanda sana!” Alisema msaidizi wa mkuu wa majeshi baada ya kumimina risasi.

“Sijafa bado nipigeni za kichwa!” Alisema bibi Nyanjige huku akicheka kwa dharau.
Mkuu wa majeshi alijiandaa tena kumimina risasi lakini dereva wake alimuwahi na kumnyang’anya bunduki yake!

“Ha! Ha! Ha! Mmeshindwa kuniua sasa subirini mimi niwamalize!” Alisema bibi Nyanjige.

Je, nini kitaendelea
 
SEHEMU YA 55...

Walishangaa kukuta ni mwili wa bibi kizee! Dereva aliusukuma kwa mguu wake wa kulia ukalala chali, hawakuamini macho yao walipokuta alikuwa ni bibi Nyanjige!
Bunduki zote mbili zilimlenga bibi Nyanjige ardhini na hasira ilizidi kuwapanda mkuu wa majeshi na dereva wake, mioyo yao iliwaambia wammiminie idadi kubwa ya risasi ikilinganishwa na unyama alioufanya bibi kizee huyo lakini walishindwa kufanya hivyo baada ya kufikiria agizo walilopewa na mkuu wa majeshi.

“Ikiwezekana mmlete akiwa hai ili akaushwe na kuwekwa jumba la makumbusho...!” Kauli hiyo ya mkuu wao ilikuja vichwani mwao.
“Nyie mbwa hebu nipigeni hizo risasi zenu ili mimi nife nipumzike! Au hamjui kutumia bunduki nini? Nyie wapumbavu sana yaani bibi kama mimi nimewasumbua kiasi hicho?” Bibi Nyanjige alisema maneno ya kutia hasira ili kuwalazimisha wampige risasi! Alitamani kufa kwa risasi kuliko kuingia mikononi mwa wanajeshi.

“Para tat lita-pa! Pa! Pa!”Risasi zilisikika zikilia
“Mkuu umefanya nini sasa? Umesahau maneno tuliyoelezwa kuwa tumepeleke akiwa hai?”Dereva aliuliza.
“Hasira imenipanda sana!” Alisema msaidizi wa mkuu wa majeshi baada ya kumimina risasi.

“Sijafa bado nipigeni za kichwa!” Alisema bibi Nyanjige huku akicheka kwa dharau.
Mkuu wa majeshi alijiandaa tena kumimina risasi lakini dereva wake alimuwahi na kumnyang’anya bunduki yake!

“Ha! Ha! Ha! Mmeshindwa kuniua sasa subirini mimi niwamalize!” Alisema bibi Nyanjige.

Je, nini kitaendelea
Ha! ha! shunie malizia moja ya jion
 
SEHEMU YA 55...

Walishangaa kukuta ni mwili wa bibi kizee! Dereva aliusukuma kwa mguu wake wa kulia ukalala chali, hawakuamini macho yao walipokuta alikuwa ni bibi Nyanjige!
Bunduki zote mbili zilimlenga bibi Nyanjige ardhini na hasira ilizidi kuwapanda mkuu wa majeshi na dereva wake, mioyo yao iliwaambia wammiminie idadi kubwa ya risasi ikilinganishwa na unyama alioufanya bibi kizee huyo lakini walishindwa kufanya hivyo baada ya kufikiria agizo walilopewa na mkuu wa majeshi.

“Ikiwezekana mmlete akiwa hai ili akaushwe na kuwekwa jumba la makumbusho...!” Kauli hiyo ya mkuu wao ilikuja vichwani mwao.
“Nyie mbwa hebu nipigeni hizo risasi zenu ili mimi nife nipumzike! Au hamjui kutumia bunduki nini? Nyie wapumbavu sana yaani bibi kama mimi nimewasumbua kiasi hicho?” Bibi Nyanjige alisema maneno ya kutia hasira ili kuwalazimisha wampige risasi! Alitamani kufa kwa risasi kuliko kuingia mikononi mwa wanajeshi.

“Para tat lita-pa! Pa! Pa!”Risasi zilisikika zikilia
“Mkuu umefanya nini sasa? Umesahau maneno tuliyoelezwa kuwa tumepeleke akiwa hai?”Dereva aliuliza.
“Hasira imenipanda sana!” Alisema msaidizi wa mkuu wa majeshi baada ya kumimina risasi.

“Sijafa bado nipigeni za kichwa!” Alisema bibi Nyanjige huku akicheka kwa dharau.
Mkuu wa majeshi alijiandaa tena kumimina risasi lakini dereva wake alimuwahi na kumnyang’anya bunduki yake!

“Ha! Ha! Ha! Mmeshindwa kuniua sasa subirini mimi niwamalize!” Alisema bibi Nyanjige.

Je, nini kitaendelea
Santeeeeee,,,
 
SEHEMU YA 56

Tukio la bibi Nyanjige kutoroka kwa mara nyingine liliwashangaza viongozi wote wa jeshi na kuwafanya washindwe kuelewa bibi huyo alikuwa wa aina gani kwani alifanya mambo makubwa yasiyolingana na umri wake kabisa! Vichwa viliwagonga wakuu wa jeshi! Ilikuwa ni mara ya tatu bibi Nyanjige kutoroka mikononi mwao. Jambo hilo liliwakera sana.

Maiti zote zilizokufa kwa kuumwa na nyuki zilitolewa ndani ya chumba na kufanya idadi ya watu waliokufa katika harakati za kumsaka bibi Nyanjige kuwa zaidi ya elfu sita! Jambo hilo lilimtia hasira kila mtu katika jeshi, ilikuwa ni aibu kwa jeshi kubwa kama hilo kushindwa kumkamata kibibi kama bibi Nyanjige!

Kufuatia tukio hilo Mkuu wa majeshi hakuwa na jambo jingine la kufanya zaidi ya kujiuzuru wadhifa wake mara moja na aliteuliwa mwingine palepale! Hiyo ilifanya wakuu wa majeshi waliojiuzuru sababu ya bibi huyo kufikia wawili!

“Hii ni aibu tena aibu kubwa sana kwa jeshi lenye watu makini kama mimi, naahidi nitamtia mbaroni tu! Subirini!’ Alisema mkuu mpya wa majeshi baada ya kuapishwa na wanajeshi wote walimpigia makofi!

Siku iliyofuata msako mkubwa ulitangazwa nchi nzima kumsaka bibi kizee aliyeshindikana kutiwa mbaroni! Mikoa yote ilitaarifiwa na ni mchana wa siku hiyo hiyo taarifa zilifika makao makuu ya jeshi kutoka mbugani Mikumi kuwa gari alilotoroka nalo bibi Nyanjige lilikutwa limetelekezwa karibu na lango la kuingilia kwenye Mbuga ya Mikumi! Taarifa hiyo ilimaanisha wazi bibi Nyanjige alikuwa amekimbilia ndani ya Mbuga ya Mikumi.

“Askari wote waliopo katika kikosi cha jeshi la 201 KJ mkoani Morogoro waondoke haraka iwezekanavyo kwenda mbugani Mikumi na waliopo Kilosa pia wapelekwe huko huko Mikumi, jeshi jingine nitaliongoza mimi kutoka hapa Dar es Salaam nina uhakika kufikia kesho huyu bibi atakuwa amekwishatiwa mbaroni!”Alisema mkuu wa majeshi baada ya kupokea taarifa hiyo.
 
SEHEMU YA 57

Amri hiyo ya mkuu wa jeshi ilitekelezwa kwa haraka, wanajeshi wa kambi ya Morogoro na wa Kilosa waliondoka katika magari na kupelekwa hadi mbugani na mamia ya wanajeshi walisafirishwa kwa magari ya jeshi kutoka Dar es Salaam na Dodoma hadi katika mbuga hiyo hiyo kwa lengo la kumsaka bibi Nyanjige.

Kwa idadi hiyo ya askari wengi walikuwa na uhakika bibi Nyanjige angekamatwa.
Helkopta zisizo na idadi zilipita angani zikimsaka bibi huyo machachari, ulikuwa ni msako mkali kuliko msako mwingine wowote uliowahi kufanyika katika historia ya Tanzania! Hata msako wa porini Kongo haukuwa mkali kiasi hicho! Wanajeshi wote walikuwa na hasira kali ya kutaka kumtia bibi Nyanjige mikononi mwao na kumuua kikatili, waliamini alikuwa ameliaibisha jeshi.

************** Kwa siku tatu mfululizo kulikuwa na hekaheka ya aina yake mbugani, kila kichaka kilichoonekana mbele ya wanajeshi kilifyekwa na kusabararishwa ili mradi ulikuwa ni msako wa bibi Nyanjige lakini bado hakuonekana mahali popote, wanajeshi hawakukata tamaa sababu walijua kwa uhakika alikuwa ndani ya pori hilo.

“Mpaka tumpate haiwezekani hata kidogo jeshi kubwa kama hili lishindwe kumkamata bibi kizee wa aina hii tu!”
“Ingawa historia yake inashangaza ni lazima atiwe mbaroni, safari hii hatumpeleki akiwa hai tena, tutamuuua huku huku porini tu!”

“Kweli sababu tukimfisha watataka kumkausha ili wamhifadhi, ninajua atawatoroka na kutufanya sisi kuacha familia zetu kuja kumtafuta huku porini, hii haiwezekani hata kidogo ni lazima tumuue!”Wanajeshi waliendelea kuongea huku wakiendeleza msako wao porini, kwa kutwa nzima walipita kila mahali porini wakimtafuta bibi lakini hawakufanikiwa kumpata wala kuona dalili yoyote ya kuonyesha mahali alikokuwa. Ikawa usiku ikawa asubuhi siku ya kwanza ikapita!
 
SEHEMU YA 58

Siku ya pili kama ilivyokuwa imepangwa na mkuu wa majeshi aliyekuwa pamoja na wapiganaji wake msako uliendelea, wanajeshi walikuwa wamechoka lakini waliendelea na msako wao bila kukata tamaa, azimio lao likiwa ni hakuna kurudi nyumbani bila bibi Nyanjige, pamoja na kukatakata miti na hata kuchoma hifadhi kwa moto bado hawakufanikiwa kumwona bibi Nyanjige, walishindwa kuelewa mahali alipokuwa!

Wanajeshi wasiopungua elfu tatu walimtafuta bibi Nyanjige mbugani kwa siku zote tatu bila mafanikio hatimaye walianza kupoteza matumaini kabisa lakini siku ya nne asubuhi waliibukia sehemu iliyokuwa wazi na iliyolundikwa udongo mwingi kama tripu za mchanga zilizomwagwa tayari kwa ujenzi.
“Mh!”Mmoja wa maaskari aliguna
“Vipi afande?”

“Nashangaa ni nani amerundika mchanga huu hapa?”
“Labda watu wa hifadhi walitaka kujenga hoteli!”
“Hoteli?”
“Ndiyo!”
“Hoteli eneo hili alale nani?”
“Watalii!”
“Hapana, sitegemei hata siku moja kama kunaweza kuwa na mtalii wa kulala katikati ya pori kiasi hiki!”

“Aisee hebu angalieni pale!” Alisema mmoja wa wanajeshi akiwaonyesha shimo kubwa lililokuwa mbele yao.
“Shimo?”
“Ndiyo!”
“Sijui la nini?”
“Hebu twende tukalione!” Waliongozana wakitembea kuelekea mahali lilipokuwa shimo hilo, wote walibaki midomo wazi kukuta shimo refu likielekea ardhini na mwisho wake haukuonekana, lilikuwa shimo lenye uwezo wa kupitisha mtu mzima na pembeni yake kulionekana alama za miguu.

“Mh jamani hii si miguu ya mtu?”
‘Ndiyo tena kwa jinsi miguu hii ilivyo midogo lazima ni ya mwanamke!”
“Inawezekana kabisa!”
“Lakini nani alichimba shimo hili?”
“Hata mimi sijui labda ni wachimbaji wa madini walitaka kuufanya huu mgodi!”
“Hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kuja porini kwenye wanyama wakali kiasi hiki kuanzisha mgodi labda kama anataka kuliwa na simba!”
Wanajeshi karibu mia mbili walikusanyika eneo hilo na kuendelea kulishangaa shimo lililokuwa mbele yao halikuwa la kawaida hata kidogo, kifupi lilitisha na walijua ni lazima ndani yake kulikuwa na kitu, wanajeshi wengine walihisi bibi nyanjige alikuwa ndani yake.
 
SEHEMU YA 59

“Mimi nafikiri hii miguu ni ya huyu bibi Nyanjige hakuna mwingine, hebu nifungeni kamba mimi niingie hadi ndani nikachanguze ila nikitingisha kamba basi mjue nina matatizo mnivute haraka!”Alisema mwanajeshi huyo na kamba ililetwa haraka na akafungwa kiunoni na kuanza kushushwa taratibu kuingia shimoni! Kamba ilikwenda hadi ikafika mwisho bila mwanajeshi huyo kufika chini, shimo lilionekana kuwa refu na lilikuwa na kiza kinene alitumia tochi kuona ndani, ilibidi wamvute haraka na kumtoa hadi nje.

“Vipi afande?”
“Jamani huko ndani ni kiza kitupu na shimo bado linaendelea sijui ni kitu gani kimechimba shimo refu kiasi hiki!”
“Huko ndani hujaona dalili yoyote ya bibi Nyanjige?”
“Hapana ila kuna alama za mtu alikuwa akikanyaga ukutani akishuka shimoni!”
“Umeona alama za miguu?”
“Ndiyo tena na mikono!”
“Sasa?”

“Sijakata tamaa unganishe kamba nne ili iwe ndefu zaidi niingie tena, ninafikiri bibi yupo humuhumu shimoni!”Alisema askari huyo huku akitabasamu, alionekana jasiri kupita kiasi
“Au tudumbukize bomu ndani ili ateketee?” Aliuliza mkuu wa majeshi na wanajeshi waligawanyika makundi mawili juu ya suala hilo wengine wakisema ni sawa lakini wengine walikataa na kufanya afande aliyejitolewa atumbukizwe tena.

Palepaple kamba iliunganishwa na kuwa ndefu, afande huyo aliyeitwa Alphonce kwa mara nyingine alitumbukizwa shimoni, safari hi alifika hadi chini akimulika kwa tochi yake lakini alipotua tu chini alishangaa kusikia akikabwa na kitu kama mzizi mkubwa shingoni.

Pumzi ilianza kupungua baadaye na baadaye alishindwa kabisa kuhema, macho yakamtoka, kabla hajakata roho alisikia sauti ya mwanamke akicheka kwa sauti ya juu.
 
SEHEMU YA 60

Baada ya kuliacha gari kwenye lango la kuingilia mbugani bibi Nyanjige alikimbia huku akichechemea hadi katikati ya mbuga ambako alikuta kundi kubwa la pundamilia, alipiga mluzi mrefu na wa ajabu Pundamilia wote walisogea karibu yake na kumzunguka!Lengo lake lilikuwa ni kufika katikati ya pori kwenye wanyama wengi ili ajichimbie huko na kuunda jeshi jingine kali la wanyama na kupambana na jeshi la serikali kama wangejaribu kumsaka tena. Alimshukuru Mungu kwa elimu ya viumbe aliyokuwa nayo bila elimu hiyo alijua asingekuwa hai.

“Jeshi nitakalounda safari hii litaushangaza ulimwengu huu! Nataka niache historia nyuma yangu nataka dunia inielewe na nikifa watu wote waseme bibi nyanjige aliishi na kuusumbua ulimwengu nataka nirudishe heshima ya mwanamke iliyopotea siku nyingi!”Aliwaza bibi Nyanjige akiwa katikati ya kundi kubwa la pundamilia walioketi chini na kuwazunguka, heshima kutoka kwa wanyama ilikuwa ni ileile aliyopata msituni Kongo.

Mahali alipokuwa palimhakikishia usalama lakini bado alikuwa na wasiwasi wa kusakwa! Gari aliloliacha kwenye lango la kuingilia mbugani lilitosha kabisa kuonyesha mahali alikokuwa na hivyo kuendelea kusakwa.
“Kama ni hivyo inabidi nisogee mbele zaidi na haraka iwezekanavyo hawa washenzi lazima watakuja, hilo nalijua wazi!”

Alinyanyuka haraka na kumchagua pundamilia mmoja mwenye nguvu kati ya Pundamilia waliomzunguka na kupanda juu yake kama vile watu wapandavyo farasi, huo ndio ulikuwa usafiri wake hata wakati akiwa katika msitu huko kongo!

Alimshika mkia na Pundamilia na kuanza kuukunja! Kitendo hicho kilimfanya Pundamilia aondoke kwa mwendo wa kasi ya ajabu,bibi alizidi kuukunja mkia wakipita katikati ya mbuga na kupishana na wanyama wengi wakali lakini hapakuwa na wasiwasi wowote sababu wanyama wote walimtii, mbele zaidi alitokeza katika sehemu ya wazi na aliuachia mkia wa Pundamilia akasimama.
 
Back
Top Bottom