Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,168
- Thread starter
- #241
SEHEMU YA 54...
“Nimesurika tena!” Alisema bibi Nyanjige wakati akinyanyuka kutoka ardhini ni yeye peke yake ndiye hakushambuliwa na ng’ombe siku hiyo kila ng’ombe walipomsogelea alitoa mlio ulioishia na “ssssssssss!” na ng’ombe wote walimwacha na kuwashambulia wamasai.
Baada ya kunyanyuka bibi Nyanjige alitembea kuelekea msituni huku akichechemea! Mwili wake wote ulimuuma na ulijaa majeraha sababu ya kipigo alichopata! Mbele kidogo kama kilometa moja alijikutaka akitokeza barabarani alikuwa akisikia kizunguzungu sababu ya kupoteza damu nyingi na alihisi asingeweza kuendelea zaidi na muda mfupi baadaye alianguka chini.
Ghafla alisikia muungurumo wa gari likija kwa mbali na alipojaribu kunyanyua kichwa chake kuangalia ulikokuwa ukitokea muungurumo huo alishindwa na kuendelea kulala chini! Giza lilikuwa limeyafunika macho yake
“ Ni kitu gani kile pale!” Dereva alimuuliza msaidizi wa mkuu wa majeshi baada ya kuona kitu kama mwili wa binadamu umelala chini!
“Au ni mmoja wa watu waliojeruhiwa na ng’ombe?”
“Hapana watu wa kijijini watakuwa hawajafika huku!”
“Sasa ni nani? Halafu naona yupo uchi wa mnyama! Hebu chukua bunduki yako tukamwangalie!”Mkuu wa majeshi alisema na wote wawili walichukua bunduki zao na kuanza kusogea mahali ulipolala mwili ule!
“Nimesurika tena!” Alisema bibi Nyanjige wakati akinyanyuka kutoka ardhini ni yeye peke yake ndiye hakushambuliwa na ng’ombe siku hiyo kila ng’ombe walipomsogelea alitoa mlio ulioishia na “ssssssssss!” na ng’ombe wote walimwacha na kuwashambulia wamasai.
Baada ya kunyanyuka bibi Nyanjige alitembea kuelekea msituni huku akichechemea! Mwili wake wote ulimuuma na ulijaa majeraha sababu ya kipigo alichopata! Mbele kidogo kama kilometa moja alijikutaka akitokeza barabarani alikuwa akisikia kizunguzungu sababu ya kupoteza damu nyingi na alihisi asingeweza kuendelea zaidi na muda mfupi baadaye alianguka chini.
Ghafla alisikia muungurumo wa gari likija kwa mbali na alipojaribu kunyanyua kichwa chake kuangalia ulikokuwa ukitokea muungurumo huo alishindwa na kuendelea kulala chini! Giza lilikuwa limeyafunika macho yake
“ Ni kitu gani kile pale!” Dereva alimuuliza msaidizi wa mkuu wa majeshi baada ya kuona kitu kama mwili wa binadamu umelala chini!
“Au ni mmoja wa watu waliojeruhiwa na ng’ombe?”
“Hapana watu wa kijijini watakuwa hawajafika huku!”
“Sasa ni nani? Halafu naona yupo uchi wa mnyama! Hebu chukua bunduki yako tukamwangalie!”Mkuu wa majeshi alisema na wote wawili walichukua bunduki zao na kuanza kusogea mahali ulipolala mwili ule!