Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

SEHEMU YA 51...

Magari matatu yakiwa na askari wapatao sitini yaliondoka makao makuu ya jeshi kwenda kijiji cha Kiambali, kwa sababu walimfahamu bibi Nyanjige na maajabu yake waliondoka na silaha za kutosha, kila mwanajeshi akiwa na bunduki yake na pia mabomu.
“Kama ni yeye basi mkamlete akiwa hai!”
“Sawa mkuu!”
*
*

Kutoka jijini Dar es Salaam hadi kijiji cha Kiambali kupitia Kibaha, Chalinze ulikuwa ni mwendo wa masaa manne waliingia kijijini hapo majira ya saa nane mchana! Wote walishangazwa na hali waliyoikuta, ng’ombe waliokuwa wakikimbia huku na kule mikia ikiwa imenyooka, walionekana kama wamepatwa na kichaa mamia ya watu walikuwa wamelala ardhini wakivuja damu na wengine walikuwa wakichomwa kwa pembe za ng’ombe ardhini, wengi walikuwa wamekufa.

Dereva aliegesha gari lake na wanajeshi walianza kushuka taratibu kutoka garini bunduki zao zikiwa tayari kufanya kazi, ghafla walishitukia kundi kubwa la ng’ombe kama mia mbili likija kwa kasi kuelekea mahali walipokuwa wamesimama,wanajeshi wote walihisi hatari.

“Jamani hawa ng’ombe hawana kichaa kweli?” Maaskari waliulizana na kuwageukia vijana wa kimasai.
“Nyie vijana vipi hawa ng’ombe wenu?”
“Hata sisi hatuelewi kabisa tuliacha hali ni shwari kabisa hapa kijijini sijui kimetokea nini!”

Wakati wakiongea hayo tayari ng’ombe walishafika na kuanza kuwashambulia wanajeshi kwa pembe zao kali, walijaribu kupiga risasi lakini haikusaidia ng’ombe walizidi kuja mbio, baadhi ya wanajeshi walirusha hata mabomu yalipolipuka yaliua ng’ombe wachache!Makundi mengine makubwa zaidi ya ng’ombe yalizidi kujitokeza na kuwashambulia wanajeshi! Kifupi hali ilitisha.

Wakati yote hayo yakitokea mkuu wa majeshi alikuwa bado hajateremka garini, hali aliyoishuhudia ilimtisha, badala ya kushuka alijikuta akifunga mlango wa gari zaidi! Hakuna kilichokuwepo zaidi ya kujiokoa na alilazimika kumwamuru dereva aliondoe gari kuokoa maisha yao.

Ni wao tu wawili waliokoka hata vijana wa kimasai pia walikufa katika mashambulizi hayo ya ng’ombe! Lilikuwa ni tukio la ajabu katika historia ya Tanzania.
 
Daaaa hii story balaaaa tushushie mzigo mwingine basi Babu Shunie
 
SEHEMU YA 52...

Dereva aliliendesha gari kwa kasi huku akipiga honi iliyowatisha ng’ombe waliokimbia kulifuata gari, njiani alizipita maiti nyingi za watu zikiwa zimelala chini na wengine wengi walikimbia huku na kule kuokota maisha yao.

Mkuu wa majeshi na dereva wake walifanikiwa kutoka kijijini ndani ya gari wakiwa salama salimini lakini wenzao wote waliokuwa nao walikufa, jambo hilo liliwasikitisha sana, mpaka wakati huo hawakufanikiwa kuelewa kama kweli bibi Nyanjige alikuwa katika kijiji hicho au la! Kilikuwa kitendawili.

“Inawezekana kweli yupo na ameitumia elimu yake ya viumbe niliyosikia kuwa anayo kuwatia ng’ombe vichaa ili wafanye mauaji bibi mimi anatisha jamani!” Alisema mkuu wa majeshi msaidizi.
“Nafikiri inawezekana sasa kitafanyika kitu gani ili bibi huyu akamatwe maana anazidi kuua watu!”

“Hata mimi nashindwa kuelewa, acha kwanza tupeleke taarifa hii kwa wakubwa, nafikiri kutakuwa na kitu cha kuamua!” Alijibu mkuu wa majeshi msaidizi huku mwili wake ukitetemeka kwa hofu mpaka wakati huo alikuwa haamini kama kweli alikuwa amenusurika katika janga hilo la kushambuliwa na ng’ombe.

“Hivi kumbe ng’ombe ni hatari eh?”
“Mimi ndio nimegundua leo kuwa ng’ombe wanaweza kuua kikatili! Tunakula nyama yao kila siku kumbe ni viumbe hatari”
*
*

Bibi Nyanjige hakuwa tayari kuingia mikononi mwa wanajeshi kwani kitendo hicho kwake kilimaanisha kifo! Alikuwa tayari kufa kwa kupigwa na wananchi wenye hasira lakini si kuingia mikononi mwa wanajeshi ambao alijua alishawatia hasira kali kupita kiasi.

Pamoja na mawazo hayo alishindwa afanye nini ili ajiokoe kwani alizungukwa na idadi kubwa ya wamasai wenye silaha za jadi kama mikuki, pinde na mishale! Alikuwa amepoteza damu nyingi sana lakini bado alihisi kuwa na nguvu mwilini mwake ambazo zingemwezesha kukumbia lakini alisita kuchukua uamuzi huo akiogopa kushambuliwa kwa mikuki na mishale.
 
SEHEMU YA 53...

Jua lilizidi kumchoma akiwa amelala ardhini, muda wote alifikiria namna ya kujinasua mikononi mwa kifo lakini alikosa njia! Mara nyingi alishawhi kunusurika vifo katika mazingira magumu lakini siku hiyo alishindwa kuelewa ni kitu gani angefanya kujiokoa!

Majira ya saa saba ikiwa ni saa moja tu kabla magari ya wanajeshi hajawasili kijijini, wazo lilimwijia bibi Nyanjige kichwani mwake, wazo la kutumia mifugo kama ng’ombe iliyokuwa mingi kijijini hapo kujiokoa! Aliielewa lugha ya ng’ombe na alijua ni maneno gani huwatia ng’ombe vichaa na hasira.

Baada ya fikra hizo alikunja mdomo wake na kutoa muungurumo kama wa ng’ombe ambao kwa mbele uliishia na maneno “uwooou” watu wote waliokuwa wamekusanyika eneo hilo kumshangaa bibi Nyanjige walicheka walipomwona akifanya kitendo hicho! Alirudia kufanya hivyo mara nyingi na kadri alivyozidi kutoa muungurumo huo ndivyo watu walivyozidi kucheka! Hawakuelewa ni nini alichokuwa akifanya.

Ghafla bila kutegemea wamasai walishtukia ng’ombe wengi wakija mbio kuelekea eneo hilo huku mikia yote ikiwa imesimama wima nyuma yao! Dalili kuwa ng’ombe walikuwa wamepatwa na kichaa.
Kijiji cha Kiambali kilikuwa cha wafugaji wa Kimasai tupu na kilikuwa na ng’ombe wasiopungua 10,000 ukiondoa ndama 5,000! Ng’ombe wote waliruka kutoka mazizini mwao na kukimbilia kuelekea mahali sauti ya bibi Nyanjige ilikokuwa ikitokea, nao walikimbia huku wakitoa mlio huohuo ambao hatimaye ulisambaa kijiji kizima!

Mlio huo ulikuwa ni matusi makubwa kwa ng’ombe wote kijijini humo, uliwatia hasira mbaya sana ng’ombe wote na kukimbia kwenda mlio ulikotokea ili kupambana! Wanakijiji hawakuelewa lolote kwa sababu wao hawakuelewa lugha ya ng’ombe pamoja na kuwa waliishi nao, ilihitaji elimu kubwa sana kuelewa kilichokuwa kikitokea.

Ng’ombe walipofika eneo la tukio bibi Nyanjige alitoa tena mlio mwingine na ng’ombe wote walianza kuwashambulia wamasai waliokuwa eneo hilo kwa kutumia pembe zao zenye ncha, wamasai wengi walikufa mbele ya macho ya bibi Nyanjige!
 
Hahahaha nawaza hapa nikiona ng'ombe nitoe huo mlio, huyu bibi kanishinda tabia, endelea mama
 
Back
Top Bottom