Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Nitarudi.... kitambo sana niliisoma kwenye magazeti ya Shigongo.
 
SEHEMU YA 48...

Jeshi lilishituliwa sana na vifo vya wanajeshi wake msituni viongozi hawakuelewa ni nani aliyezitungua ndege zao kiasi hicho ingawa waliamini mtambo uliotumika kuzitungua ulikuwa wao.
Walioshindwa kuelewa bibi Nyanjige aliwezaje kuwashawishi wapiganaji wao mpaka wakafikia uamuzi wa kulisaliti jeshi lao! Siku zote waliamini wapiganaji wao walikuwa waaminifu kupita kiasi.

Hakuna mtu hata mmoja aliyehisi bibi Nyanjige ndiye alifanya ukatili huo baada ya kuingia katika jeshi lao bila kugundulika.
Msako mwingine mkali zaidi uliitishwa wanajeshi zaidi ya elfu sita walitumwa kwenda kuuvamia tena msitu kumsaka bibi Nyanjige, bado waliamini alikuwemo msituni! Ni maaskari katika msako wa mara ya pili walioigundua maiti ya askari waliyehisi alizitungua ndege zao ukiwa ndani ya kichaka!

Kilichopelekea maiti hiyo igundulike ni harufu kali iliyosikika wakati wakipita pembeni mwa kichaka, walipoingia ndani walikuta maiti ya mpiganaji mwenzao ikiwa imelala bila magwanda zaidi ya chupi! Gauni chafu lilikuwa pembeni.

Walipoliangalia gauni hilo waliligundua kwa haraka kuwa lilikuwa la bibi Nyanjige! Wote walielewa kilichotokea waligundua ni bibi Nyanjige aliyezitungua ndege zao na ni yeye aliyetega mabomu na kuwaangamiza maaskari wenzao! Hasira zilizidi kuwapanda wanajeshi na kila mtu alipania kumpata bibi huyo.
“Lazima apatikane!”

Gauni la bibi Nyanjige lilipopelekwa makao makuu ya jeshi, wakubwa walishindwa kuelewa ni uwezo gani aliokuwa nao bibi huyo kizee hadi asumbue jeshi kiasi hicho!
“Alikuwa na nguvu gani mpaka kumuua askari wetu kisha kumvua nguo, nafikiri magwanda yake ya askari aliyavaa mwenyewe ndio akaanza kutungua ndege zetu?” Aliuliza mkuu wa majeshi!

“Nafikiri ni hivyo sijui hivi sasa atakuwa wapi?” Msaidizi wake Brigedia Mwita alijibu
 
SEHEMU YA 49...

“Hakuna sehemu yoyote anayoweza kuwa amekimbilia zaidi ya humohumo porini! Hivyo hakikisheni pori lote linazingirwa ili asipate mahali pa kutokea! Na mkimpata naomba maiti yake iletwe hapa makao makuu, tunahitaji kuikausha ili iwekwe makumbusho kwa ajili ya historia ya nchi yetu kwani mpaka sasa siamini kama kuna bibi kizee anayeweza kufanya maajabu kiasi hiki……!” Mkuu wa majeshi alimwambia msaidizi wake na kabla hajamaliza simu yake ililia.

“Hallow, nani anaongea?” Aliuliza.
“Ni mimi Brigedia Bukuku!” Alijibu Brigedia aliyekuwa akiongoza msako msituni.
“Ndiyo Brigedia mnaendeleaje?”
“Tunaendelea vizuri nilitaka tu kukutaarifu kuwa tayari ule mtambo wa kutungulia ndege tumeupata ulikuwa umefichwa kichakani kabisa!”
“Vizuri, endeleeni na kazi mpaka mmkamate huyo bibi kizee, yupo hapohapo porini!”
“Sawa afande!”
*
*

Habari za msako wa bibi Nyanjige zilishaenea kila mahali mjini na vijijini, hapakuwa na mtu asiyefahamu juu ya bibi huyo! Hata katika kijiji cha wamasai cha Kiambali ambako bibi Nyanjige aliendelea kusambuliwa kwa mawe akidhaniwa mchawi, kijana mmoja aliikumbuka sura yake na kupiga kelele akiwaomba wenzake wasitishe zoezi la kumpiga.

“Nimemkumbuka huyu bibi!” Alisema kijana huyo kwa kimasai.
“Ni nani?”
“Ni bibi Nyanjige!”
“Mama yangu nimekwisha!”Bibi Nyanjige alijisemea moyoni akiwa amelala chini damu nyingi zikimtoka katika majeraha aliyoyapata sababu ya kipigo kibaya alichopewa na wananchi wenye hasira, alijua kutambuliwa kulimaanisha kifo!

Alijua tayari alishaingia mkononi mwa wanajeshi na kwa zawadi iliyokuwa imetolewa na serikali hapakuwa na njia ya kuwshawishi wamasai wamwachie.
“Bibi Nyanjige ndiye nani?”
“Si anayetafutwa kwa mauaji!”
“Una hakika ndiye huyu?”
“Ni yeye!” Kijana huyo aliendelea kusisitiza.

“Sasa tufanye kitu gani?”
“Mimi naomba tuchague morani watatu ili twende kupeleka taarifa hizi makao makuu ya jeshi waje wamchukue!” Alisema kijana huyo na maneno hayo yalimfikia bibi Nyanjige moja kwa moja, aliomba wazee wa Kimasai wamkatalie kijana huyo lakini haikuwa hivyo, wazee wote walikubaliana na jambo hilo.
 
SEHEMU YA 50...

Usiku huohuo kwa kutumia baiskeli morani watatu waliondoka kuendesha baiskeli zao hadi mjini Korogwe ambako waliziacha kwa marafiki na kupanda mabasi kuelekea Dar es Salaam.
Waliingia jijini saa moja asubuhi na kufika makao makuu ya jeshi saa mbili na nusu ambako baada ya kujieleza kuwa walikuwa na taarifa za mahali bibi Nyanjige alikokuwa walipokelewa vizuri na kuonana na mkuu wa jeshi kama walivyoomba.

“Yule bibi tunaye!” Ndivyo walivyosema baada ya salamu zao kwa mkuu wa majeshi msaidizi aliyewapokea kabla hawajaenda kuonana na mkuu wa majeshi mwenyewe!
“Bibi gani?” Aliuliza mkuu wa majeshi msaidizi.
“Bibi Nyanjige!”
“Nyanjige?” Aliendelea kuuliza kwa mshangao.

“Ndiyo!”
“Mnae nyinyi? Mmempataje wakati kahangaisha jeshi kiasi kikubwa?”
“Kweli tunaye kama huamini tupatie vijana wako twende nao hadi kijijini kwetu lakini zawadi itakuwa yetu sisi!” Alisema mmoja wa Morani.

“Hilo si tatizo ili mradi tu awepo kwa sababu mkitusumbua hatutafurahi!”
“Wewe tupe tu vijana na gari twende nao!”
“Si vijana bali mimi mwenyewe nitaondoka nanyi!”
“Tena wewe ndiyo vizuri zaidi!”
“Haya hebu nisubirini kwanza nije!” Alisema mkuu huyo wa majeshi na kutoka nje ya ofisi na kwenda moja kwa moja kwa mkuu wa majeshi na kumweleza habari za vijana wa kimasai walioingia ofisini kwake.

Mkuu wa majeshi hakuiamini habari hiyo aliuona kama uongo fulani na kuomba awaone vijana wa kimasai walioleta taarifa, mkuu wa majeshi msaidizi alitoka kwenda kuwachukua na kuwapeleka ofisi ya bosi wake.

Mkuu wa majeshi alipowauliza vijana hao maswali majibu yao yaliendeela kuwa yaleyale na walijibu kwa uhakika zaidi, jambo lililowafanya wakuu wa majeshi waamini kila kitu!Hapakuwa na ubishi wala kusita tena bali mkuu wa majeshi alimwamuru msaidizi wake pamoja na wanajeshi wengine waongozane na vijana wa kimasai kwenda kijijini kuona kama kweli bibi waliyedai kuwa nae alikuwa bibi Nyanjige!
 
Duh tamuuuuuu mfano hakunaaa[emoji39][emoji39][emoji39][emoji39]
 
Back
Top Bottom