Huu sio UTU-kipindi cha TAKE ONE cha CLOUDS TV

Tunasafari ndefu hili la clouds nalo no bomu linalosubiri kulipuka ... maadili ya kazi ni lazima ujue kiswanglish na blah blah nyingi ama?
 
Jana ilitokea nikawa naangalia kipindi cha 'take one' cha Zamaradi. Kuna binti ambay kwa umri anaonekana yuko chini ya miaka kumi na minane. Binti huyo anasema alikuja Dar Es Salaam kwa ajili ya kufuata ndoto yake ya kuwa mcheza sinema uki akimwacha mama yake anayeugua maradhi yanayoyokana na kukosa kinga za mwili. Aliendelea kufunguka kuwa mtu wa mfano kwake ni Lulu. Binti huyu aliingia Dar Es Salaam kwa maneno yako akiwa hajawahi kumjua mwanamume yoyote.
Habari ya dada huyu inasikitisha kwani anasema alikuja Dar Es Salaam akiwa na shilingi elfu thelathini tu mkononi. Akiwa Dodoma aliambiwa kwamba wasanii wengi wanapatikana maeneo ya Ilala. Alifika ubungo na kuelekea Ilala ambako hakukutana na msanii yoyote wa sinema. Matokeo yake akajikuta akiishi na mlinzi wa magari hapo Ilala. Mlinzi alianza kumtaka kimapenzi na ikabidi Dada akimbilie Sinza ambapo alikutana na Hemed. Hemed alimgandisha dada huyu mpaka kiza kikamkuta akiwa nje yanyumba hapo Sinza. Dada huyo katika kusubiri akakutana na wadada (sema: madada powa) ambao walichukua na kuanza kuishi naye hapo Sinza. Wadada hao walikuwa wakimfanyisha kazi za nyumbani na kumfungia ndani kama mtumwa na mwisho wakatumia ushamba wake kuanza kumletea wanaume. Binti huyu anasema kwamba mwanamume wa kwanza alikuwa anatokea Ilala na alikuwa na dalili zote za maradhi ya ukimwi. Jamaa huyu wa Ilala akutumia kinga katika kumwingilia kimwili huyu binti. Binti huyu aliendelea kusema kwamba kwa wastani alikuwa akilala na wanaume watatu kwa siku na alihishi katika nyumba hiyo kwa miezi mitatu mpaka alipofanikiwa kutoroka.
Binti huyu amepoteza matumani lakini anasema sasa hivi anataka kupima na kujua hali yake ya kiafya. Pili anaogopa hizi habari kumfikia mama yake kwani hajui kama ndoto yake ya kuwa muigizaji itatimia.
Kipindi kitaendelea wiki ijayo.

My Take:
Kwa nini Zamaradi na Wahariri wa TV Clouds hawakuilinda 'privacy' ya huyu binti ambaye ni mdogo kiumri na hajui madhara ya habari yake na picha kurushwa hewani? Maelezo yake yalikuwa 'graphical' na sijui lengo la Zamaradi lilikuwa ni nini? Kuuza kipindi ?

Story ya yule binti inasikitisha sana,Clouds walikosea sana kuionesha kwa TV,ni heri ingekua kipindi cha redioni.Nilikaa nikaimagine ni mdogo wangu amepitia huo mkasa mwili ukasisimka.Its so sad kwakweli.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Me mwenyewe nilishangaa wameshindwa kuziba hata uso wa yule dada? Kwa kweli clouds media wajipange sana, sidhani kama Zamaradi anajua ethics za kazi yake!
 
Jamani tusikurupuke na kusema hawa watu walikuwa unprofesional, kwa kwawaida huwezi kuonyesha sura ya mtu kama hajatoa ridhaa yake kwani hapo anaweza aku sue for breach of duty which is a tort. Lakini kama mtu ameridhia basi kutakuwa hakuna 'breach of Duty'.
Nakumbuka kwenye kipindi cha last week cha wanawake live walikuwa wanawahoji watoto wadogo na waliwaficha sura zao. sasa kwa huyo zamradi sijui makubaliano yake na huyo binti.
But either way i feel its best not to diclose their identity becase you never know nani anaangalia hicho kipindi.
Ni hayo tu.
 
Zamaradi kama unaskia ama wapambe wako wanapita humu..NAOMBA part II msiiendeleze..Haikuwa sahihi kumuuliza maswali ya kafanywa mara ngapi na upuuzi wa namna hiyo..nilitegemea ungejikita zaidi jinsi ya kuweza kumsaidia au kuomba wasamaria wema wamsaidie..It totally Unethical and Unprofessionally.

Maswali yalikuwa yakitoto mno...
 
Zamaradi hana ethics za uandishi wa habari, na huyo editor hakumhoji huyo binti kabla ya kurusha hewani? japo ilikuwa ni live. Eti ulilala na wanaume wangapi kwa siku? Soo what? Kwa nn ww Zama usianze na ww kazi hiyo? Quite unethical questions. Stop next session please. TCRA mpo wapiii? :crying: :crying:
 
Haya ndio makosa ya watangazaji wenyewe ambayo yana viponza vyombo vya habari!
 
Back
Top Bottom