Huu ndio ugaidi sasa sio zile muvi za mapangoni!

Huu ndio ugaidi sasa sio zile muvi za mapangoni!

NAKEMBETWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2012
Posts
3,517
Reaction score
3,139
Kwanza nawapa pole ndugu zetu Wakenya kwa janga lililotokea leo!

Nadhani wote tumeona yanayotokea kwa majirani zetu!
Tunaomba vyombo vyetu vya ulinzi vijipange kikamilifu kwa majanga kama haya, na ikibidi sasa kianzishwe kikosi maalumu cha kupambana ishu kama hizi zinapotokea maana hatuwezi kusema tutakuwa salama muda wote.

Nchi zingine wana vikosi maalumu kabisa kwa ajili ya kucounter attack pindi magaidi wanapofanya uvamizi kama huu, naona hapa Tanzania kuna FFU tu ambao wamespecialize tu kwenye Kutuliza Ghasia na Fujo za raia!
 
nakE hujamalizia uzuri ionye serikali na vyombo vyake vya dola hasa kova wasilitaje kwa mizahamizaha yao hili neno Ugaidi!!!

Wachungulie kwa jirani zetu kisha watie adabu.
 
Last edited by a moderator:
nakE hujamalizia uzuri ionye serikali na vyombo vyake vya dola hasa kova wasilitaje kwa mizahamizaha yao hili neno Ugaidi!!!

Wachungulie kwa jirani zetu kisha watie adabu.
kweli mkuu inafikia kipindi hawa wanausalama wetu na viongozi ni kama wanakuwa wanajipendekeza kwa magaidi na kuupa promo ugaidi kwa mambo ambayo ni uhalifu tu wa kawaida!
 
tusiombe hawa magaidi wakaingia tz maana itakuwa ishu
hakuna anayeombea ila lolote linaweza kutokea hivyo tahadhari na kujiandaa ni muhimu!

ni sawa na kuwa na kikosi cha zimamoto haina maana unaombea nyumba ziwake moto!
 
endeleeeni kuuchochoa moto, mkodhani mnawakomoa waislamu, watoto yatima wanalelewa tayari waitwa magaidi sijui watu wanajifunza zao karatee magaidi lwakatare sijui kafanyaje gaidi. huu wote ni ulimbukeni ujuha na ugwangwahero. watakapokuja hao mnaowaombea waje ndio mtaelewa kuwa wale si waislamu kama hawa wanaowachinjia vitoeo vyenu, wanashiriki vipaimara na mazishi yenu kisha baadae unabana nyuma ya monitor unawatukana. siku zote kidole gumba hakina thamani mpaka kikatike ndio utajua. Msichezeeee amani kwa viroba vyenu.
 
Kwanza nawapa pole ndugu zetu Wakenya kwa janga lililotokea leo!

Nadhani wote tumeona yanayotokea kwa majirani zetu!
Tunaomba vyombo vyetu vya ulinzi vijipange kikamilifu kwa majanga kama haya, na ikibidi sasa kianzishwe kikosi maalumu cha kupambana ishu kama hizi zinapotokea maana hatuwezi kusema tutakuwa salama muda wote.

Nchi zingine wana vikosi maalumu kabisa kwa ajili ya kucounter attack pindi magaidi wanapofanya uvamizi kama huu, naona hapa Tanzania kuna FFU tu ambao wamespecialize tu kwenye Kutuliza Ghasia na Fujo za raia!

Kuna ffu kaz yake kupiga CUF na Chadema wakiandamana na siyo kutuliza ghasia za raia
 
endeleeeni kuuchochoa moto, mkodhani mnawakomoa waislamu, watoto yatima wanalelewa tayari waitwa magaidi sijui watu wanajifunza zao karatee magaidi lwakatare sijui kafanyaje gaidi. huu wote ni ulimbukeni ujuha na ugwangwahero. watakapokuja hao mnaowaombea waje ndio mtaelewa kuwa wale si waislamu kama hawa wanaowachinjia vitoeo vyenu, wanashiriki vipaimara na mazishi yenu kisha baadae unabana nyuma ya monitor unawatukana. siku zote kidole gumba hakina thamani mpaka kikatike ndio utajua. Msichezeeee amani kwa viroba vyenu.

Mkuu Id yako imenikumbusha MANSAKANINI MUSA WA TUNKA MANINI
 
endeleeeni kuuchochoa moto, mkodhani mnawakomoa waislamu, watoto yatima wanalelewa tayari waitwa magaidi sijui watu wanajifunza zao karatee magaidi lwakatare sijui kafanyaje gaidi. huu wote ni ulimbukeni ujuha na ugwangwahero. watakapokuja hao mnaowaombea waje ndio mtaelewa kuwa wale si waislamu kama hawa wanaowachinjia vitoeo vyenu, wanashiriki vipaimara na mazishi yenu kisha baadae unabana nyuma ya monitor unawatukana. siku zote kidole gumba hakina thamani mpaka kikatike ndio utajua. Msichezeeee amani kwa viroba vyenu.

Nashukuru sana msemaji, maana nilikua na wazo kama hili nilitaka kusema ila umepita mulemule.
 
Kama boko haram walivyomuondoa goodluck jonathan na hawa boko haram kenyatta asipokaa vizuri watamuondoa!

Hapo kwenye red, una maana Al Shabab? Jaribu kutofautisha Boko Haram na Al Shabab, soma hapa:

Boko Haram: It means Western education is forbidden, and officially called Jama'atu Ahlis Sunna Lidda'Awati Wal-Jihad, Arabic meaning "Group of the People of Sunnah for Preaching and Jihad". Boko Haram is the Hasua name for The Congregation of the People of Tradition for Proselytism and Jihad. It is a group and militant organization based in the northeast of Nigeria, north Cameroon and Niger. Founded by Mohammed Yusuf in 2002, the organization seeks to establish a "pure" Islamic state ruled by sharia, putting a stop to what it deems Westernization. The group is known for attacking Christians, Muslims and government targets, bombing churches, mosques, schools and police stations, and kidnapping western tourists, but has also assassinated members of the Islamic establishment who have condemned their operations over the years

Al-Shabab: It means The Youth in Arabic is a Somali group that wants to turn Somalia into a fundamentalist Islamic state. It emerged as the radical youth wing of Somalia's now-defunct Union of Islamic Courts, which controlled Mogadishu in 2006, before being forced out by Ethiopian forces. Al-Shabab Al-Shabaab's predecessor was al-Ittihad al-Islami (AIAI) - a terrorist group, strengthened after the fall in 1991 of Siad Barre's military regime and during the years of lawlessness that ensued. It was partially funded by former al Qaeda leader Osama bin Laden. There are numerous reports of foreign jihadists going to Somalia to help al-Shabab, from neighbouring countries, as well as the US and Europe. It is believed to have between 7,000 and 9,000 fighters.
 
mkuu kama hujui si uulize tu uambiwe. badala ya kulalamika kama kondoo anayechinjwa. vikosi vya kupambana na magaidi vipo.
 
Ugaidi ni kitu kikubwa na hatari Sana. Tatizo polisi wetu wanatumia Kama kigezo cha kisiasa. Wakati mwingine ujambazi, vibaka au hata uarifu wa kawaida tu utasikia ugaidi. Madhara yake wananchi wanaandaliwa kisaikorojia kwa aina ya ugaidi ambao sio halisi/fake. Siku ugaidi ukitokea Kama huku tunaouona knya wengi watakufa kwa stress na heart attacks. Na hofu itakuwa sio ya kawaida.

Hali alisi ni hofu juu ya mbwa mwitu ambao hawakuwa hata na panga lkn jiji zima lilisimama kwa siku mzima.

Tunatakiwa kuwa serias. Police lzm waachane na siasa wafanye kazi zao.

Najua TZ sisi ni bora Sana kwa ulinzi lkn siasa zisituaribu.
 
Tena wakome kuwatajataja ovyo.Hasa huyu kanda maalumu.
 
wanachofanya wanausalama wetu, ni kuchukua tahadhali kabla ya hatari! sasa wewe unataka hadi magaidi watulipue kama kenya ndo waanze kuchukua tahadhali?

vyombo vya usalama lazima viwe mbele kutukinga kabla Madhara hayajatokea.

so tusibeze hata kidogo na kuanza kutetea wajinga Hawa.
 
Kuna ffu kaz yake kupiga CUF na Chadema wakiandamana na siyo kutuliza ghasia za raia
Malizia kwa kusema intelejensia yao inaishia kwenye mikutano na maandamano ya CDM na CUF pekee.

Huko ndiko utaalam wao wa intelejensia yao 'walicospecialize' ambako huwa 'wananusa' haraka sana na kugundua kuwa kutatokea vitendo vya kigaidi.
 
KWetu tuna FFU kazi yao ni kuwangoja tu wapinzani waingie barabarani.......... baaaaas
 
...kwetu ugaidi ni mikutano ya chadema na cuf, akitokea mtu kashika panga tu kama amboni basi polisi hawawezi mpaka jeshi lije....
 
mkuu kama hujui si uulize tu uambiwe. badala ya kulalamika kama kondoo anayechinjwa. vikosi vya kupambana na magaidi vipo.

Ugaidi upi unaouongelea? Ule wa Polisi kurusha bomu kwenye mkutano wa Chadema Arusha?
 
Last edited by a moderator:
Hili la ugaidi tujipange muda wote. Sociologia ya ugaidi bado ni mpya na watalaam wanaendelea kuifanyia kazi kila kuchao.

Hili ni jambo la kumuomba Mungu atusaidie sana hasa wakati watu wengi wamekata tamaa. Maisha magumu na mambo hayaendi, kwa hali kama hii inakuwa rahisi sana kuwarubunu vijana kujiunga na makundi hatari kama haya.

Tumesoma kupitia vyanzo mbalimbali hata baadhi ya vijana wa ulaya na America wakihusishwa na makundi haya haramu. Popote pale tunapotoa huduma za kijamii Tanzania tujitahidi tujaribu kuwafikia wote bila upendeleo hasa kundi la vijana.
 
Back
Top Bottom