Zanzibar 2020 Hussein Mwinyi, ilikuwaje ukawa Mbunge wa Mkuranga, mkoa wa Pwani, na sasa unaenda kugombea urais Zanzibar?

Mwinyi ni Mzanzibar kwa asili yake. Amekuwa mkaazi wa mkuranga hivyo alikuwa na sifa za kugombea huko. Sifa kuu ya kugombea zanzibar ni uwe mzaliwa kwa asili au uwe umekaa (kuishi zanzibar miaka 5 mfululizo). Kwa sifa hizo ndio akaenda Zanzibar kugombea ubunge. Hadi anapendekezwa alikuwa mbunge kutoka Zanzibar.
 
CCM in kama kwao hii siyo ishu.

Wanajiamini sana hawa. Wanaamini chochote watakachokiamua Dodoma, kinakuwa hicho na hivyo Zanzibar.

Sina hakika kama 2020 itakuwa hivyo tena. Nadhani wanatakiwa kufundishwa somo ngumu sana ambalo hawajawahi kujifunza tangu kuzaliwa Tanzania na Zanzibar.

wanatakiwa kufundishwa kuwa, shilingi ina pande mbili. Wanatakiwa kuuona upande wa pili wa shilingi hawa mwaka huu 2020.

Uongo na ulaghai wa CCM ni LAZIMA ufikie mwisho.
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom