Humphrey Polepole huijui CCM wewe

N
Hivi karibuni nilimtahadharisha Humphrey Polepole kutokana na mwenendo wake usiofaa wa kumpinga Rais Samia pamoja na Serikali yake kutokana na kinyongo chake cha "kupigwa chini " kwenye nafasi ya Ukatibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Taifa.

Kwanza niseme mapema kabisa kwamba Humphrey Polepole hakuwa mtu sahihi wa kuvaa " viatu" vya Nape Nnauye kwenye nafasi ya Ukatibu wa Siasa na Uenezi Taifa.

Kwakuwa siasa ndo uwanja pekee ambapo kila kitu kinawezekana basi Hayati Magufuli katika Ujenzi wake wa "CCM MPYA" akamfanya Mwanaharati Humphrey Polepole kuwa Katibu wa Siasa na Uenezi Taifa, nafasi kubwa ambayo ilikuwa ni aibu kushikwa na mtu ambaye hakuwahi hata kuwa Mwenezi wa tawi wa CCM.

Kilichonisukuma kuandika uzi huu ni haya mabadiliko madogo aliyofanya Mheshimiwa Spika Job Ndugai katika Kamati za Bunge kwa mujibu wa matakwa ya kanuni ya 135(3) -(5) ya kanuni za kudumu za Bunge, Toleo la Juni 2020.

Humphrey Polepole amehamishwa kutoka kwenye kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za mitaa ambapo alikuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo na kupelekwa Kamati ya Sheria Ndogo ambapo nadhani atakuwa Mjumbe wa kawaida tu.

Ujumbe wa Polepole kwenye kamati Ndogo ya Sheria utakuwa wa kawaida sana kwa sababu kuu mbili; mosi, Polepole atakuwa Mjumbe wa kawaida kwa maana hatakuwa Mwenyekiti wa kamati hiyo.

Pili hiyo kamati ndogo ya sheria ni " technical committee" ina wajibu katika masuala ya sheria ambapo Polepole si Mwanasheria bali ni mtu wa "DS" ( Development Studies), Polepole ni layman hivyo hataweza "kujiachia " kama afanyavyo kwenye Shule yake ya Uongozi huko YouTube.

Nachukua nafasi hii kufanya mambo makubwa mawili kama ifuatavyo:
Kwanza, kumpongeza Mheshimiwa Spika Job Ndugai pamoja na Bunge lake tukufu kwa mabadiliko hayo yenye busara kubwa sana ndani yake.

Pili, kumjulisha Polepole kuwa haijui CCM! CCM is just like a green Snake in the green Grass! It is an invisible creature in some areas but it can bite you anytime.
yi wachawi wa ccm mnajuana.
 
Pamoja na yote kaka yetu Komredi Polepole hakustahili kuwa KATIBU MWENEZI WA CCM....

Funzo limepatikana.....

Huko mbele makosa hayatojirudia.....
Nani alistaili? Tuiangalie CCM katibu mwenezi akiwa Polepole na tuiqngalie CCM Nape akiwa katibu mwenezi! Hipi CCM iliyoimara?
 
CCM is just like a green Snake in the green Grass! It is an invisible creature in some areas but it can bite you anytime.
Umeipamba sana, acha hiyo, CCM ni mashetani kama shetani wengine, inawekwa madarakani na polisi, haina lolote katu! Ni nyepesi kama ubua, haina lolote!
 
Nani alistaili? Tuiangalie CCM katibu mwenezi akiwa Polepole na tuiqngalie CCM Nape akiwa katibu mwenezi! Hipi CCM iliyoimara?
Uimara kwenye nini?!!!

CCM ilikuwa "one man show"....

Mzee baba ni hayati JPM pekee aliyekuwa nyota wa mchezo...unabisha?!!😁
 
Uimara kwenye nini?!!!

CCM ilikuwa "one man show"....

Mzee baba ni hayati JPM pekee aliyekuwa nyota wa mchezo...unabisha?!!

CCM ya Nyerere nyota wa mchezo alikuwa nani?
CCM ya Mwinyi nyota wa mchezo alikuwa nani?
CCM ya Mkapa nyota wa mchezo alikuwa nani?
CCM ya Kikwete nyota wa mchezo alikuwa nani?
CCM ya Samia nyota wa mchezo mpaka sasa nani?

Juzi gazeti la mwananchi limeriport "Shughuli za Chadema zakwama bila Mbiwe" Nyota wa mchezo pale Chadema ni nani?

Kwanini hamtaki Mbowe aachie uenyekiti? Nyota wa mchezo Chadema ni nani?
 
Hivi karibuni nilimtahadharisha Humphrey Polepole kutokana na mwenendo wake usiofaa wa kumpinga Rais Samia pamoja na Serikali yake kutokana na kinyongo chake cha "kupigwa chini " kwenye nafasi ya Ukatibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Taifa.

Kwanza niseme mapema kabisa kwamba Humphrey Polepole hakuwa mtu sahihi wa kuvaa " viatu" vya Nape Nnauye kwenye nafasi ya Ukatibu wa Siasa na Uenezi Taifa.

Kwakuwa siasa ndo uwanja pekee ambapo kila kitu kinawezekana basi Hayati Magufuli katika Ujenzi wake wa "CCM MPYA" akamfanya Mwanaharati Humphrey Polepole kuwa Katibu wa Siasa na Uenezi Taifa, nafasi kubwa ambayo ilikuwa ni aibu kushikwa na mtu ambaye hakuwahi hata kuwa Mwenezi wa tawi wa CCM.

Kilichonisukuma kuandika uzi huu ni haya mabadiliko madogo aliyofanya Mheshimiwa Spika Job Ndugai katika Kamati za Bunge kwa mujibu wa matakwa ya kanuni ya 135(3) -(5) ya kanuni za kudumu za Bunge, Toleo la Juni 2020.

Humphrey Polepole amehamishwa kutoka kwenye kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za mitaa ambapo alikuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo na kupelekwa Kamati ya Sheria Ndogo ambapo nadhani atakuwa Mjumbe wa kawaida tu.

Ujumbe wa Polepole kwenye kamati Ndogo ya Sheria utakuwa wa kawaida sana kwa sababu kuu mbili; mosi, Polepole atakuwa Mjumbe wa kawaida kwa maana hatakuwa Mwenyekiti wa kamati hiyo.

Pili hiyo kamati ndogo ya sheria ni " technical committee" ina wajibu katika masuala ya sheria ambapo Polepole si Mwanasheria bali ni mtu wa "DS" ( Development Studies), Polepole ni layman hivyo hataweza "kujiachia " kama afanyavyo kwenye Shule yake ya Uongozi huko YouTube.

Nachukua nafasi hii kufanya mambo makubwa mawili kama ifuatavyo:
Kwanza, kumpongeza Mheshimiwa Spika Job Ndugai pamoja na Bunge lake tukufu kwa mabadiliko hayo yenye busara kubwa sana ndani yake.

Pili, kumjulisha Polepole kuwa haijui CCM! CCM is just like a green Snake in the green Grass! It is an invisible creature in some areas but it can bite you anytime.
Mugambo wanaruka na kukanyagana
 
Mkuu, mbona sifa hizo ulizotaja kuhusu ccm ni sifa za lucifer, aliyemdanganya Adam na Hawa pale bustanini? unataka kutuelimisha nini kuhusu ccm?
 
Pili, kumjulisha Polepole kuwa haijui CCM! CCM is just like a green Snake in the green Grass!
anaijua fika na ndiyo maana alikuwa bado ataendelea kukisema anachokiamini kwamba ni sahihi kwa CCM, kwa ufupi tu ni kwamba hayupo peke yake - huyu si kama yule aliyesema anajiandaa kwa kazi ya ukampeni manager.
 
Katika kipindi chake cha kuwa katibu mwenezi CCM alifanikisha ushindi mkubwa kwa wagombea wa nafasi mbali mbali kuanzia Serikali za Mitaa, Udiwani, Ubunge na nafasi ya Urais...ndugu Humphrey Polepole amefanikisha ushindi huo wa kihistoria kwa CCM, Halafu leo hii unasema hafai ?
Ushindi au uporaji?? Ngoja aisome namba sasa na mwenzake Bashiru. Uzuri wa haya mambo unalipwa hapa hapa duniani
 
Acha upotoshaji. Dhamira yoyote ya chama cha siasa ni kuchukua dola. Polepole amefanikisha ushindi wa wabunge wengi wa CCM ambao hawana maslahi na wananchi.

Sio mtu wa kubezwa. 2025 wengi wa wabunge wa CCM mizigo kule mjengoni watamkumbuka.
Na dhamira ya mwanasiasa mwerevu ni ipi? Yeye alibugi sana na kushindwa ku balance politics zake kwa siku zijazo wakati yeye bado kijana. Yaani kwa akili yake alidhani mwendazake is there to stay.
 
Kwanza punguza haraka, fanya nenda taratibu,
Hicho unachokitaka, mwishowe utaharibu,
Kisha ichunge mipaka, isije yakakusibu,
Ili uwe na baraka, liendee polepole.


Ajabu umechomoka, mithili ule mshale,
Kwa siri ukatoroka, ukasahau ya kale,
Na huko kufokafoka, huwezi kufika pale,
Kama wataka baraka, liendee polepole.


Muda wa kupambazuka, na watu wangali macho,
Ndio wakumbuka shuka, ujifunikie kwacho,
Heri kunyoa kusuka, kipaji hauko nacho,
Ili uwe na baraka, liendee polepole.



Wakatabahu
DustBin
 
Hujafafanua, polepole iwe na spidi ya miles/hour ngapi vile!???

NB: Kwa wengine 120km/h bado ni polepole :)
 
Back
Top Bottom