Humphrey Polepole ‘awashukia’ Kinana na Makamba

Humphrey Polepole ‘awashukia’ Kinana na Makamba

Kuna watu ni wendawazimu ndani ya uongozi wa chama. Kama unatii unaruhusiwa kufanya makosa yote ila ukigoma kufanya wanachotaka ndiyo makosa yako yanatangazwa.

Kama ni kweli huyo kiongozi alikuwa na hayo makonteina 700 ambayo hayakulipiwa kodi, na hakufanywa chochote kwa sababu ni kiongozi mtuifu wa chama, basi CCM ni jumba la wahalifu watiifu.

Vinginevyo, tuamini tu huyu Polepole ni mwongo na mnafiki.
 
Lolote analoongea Polepole linabaraka za Mwenyekiti.
Huyu anatumika vibaya bila yeye kujua kuwa anatumika.
1: Atueleze yale makontena yaliyodaiwa kuwa ni yamakonda yaliishia wapi na kodi ililipwa kiasi gani pamoja na kwamba boss wake alitoa tamko?

2: Nafasi aliyonayo kwa sasa, hao anaowatuhumu walisha itumikia kwa muda mrefu na kwenye nafasi kubwa zaidi. Hivyo asidhani kuwa atakaa hapo milele. Akisha tumika hatabaki salama.
 
Daah Kinana mwizi sana,kontena 700 bado meli yake ikakamatwa na meno ya tembo daah kutafuta mtu msafi CCM ni sawa na kutafuta bikra kwenye wodi ya wazazi.

dodge
Huko hakuna msafi, Ngoja siku Ngosha atoke tutakavyohesabiwa madudu yake.
 
Chadema na wakati wenu kuwachukua hao na ikibidi wapeni form wagombee.
 
Unapokuwa na Katiba kama hii ya kwetu na mifumo dhaifu ya uongozi inayotegemea aliyeko madarakani huwezi kuwa kiongozi wa ngazi yoyote ile ukakosa kashfa. Na hata kama itakuwa ndogo kwa kiasi gani, inaweza kukuzwa na kumtia mtu kwenye hatia kubwa tu. Ni hekima zilizokuwa zikifanywa na viongozi waandamizi waliotangulia tu ndizo zimeleta utulivu hadi hivi leo. Akina polepole wajifunze uhalisia huo. Wanaanzisha utamaduni mbaya sana kwenye taifa. Utamaduni wa visasi. Ni vizuri wajikite kujenga Taifa lenye mfumo imara unaoanza na Katiba imara. Nguvu hii waliyonayo inatokana na Katiba hiyo hiyo itakayotumika na "watoto" wa akina Makamba na Kinana kuibua kesi dhidi ya wababe wa leo.

Haya wanayokuja nayo CCM sasa hivi, tutarajie makubwa huko mbele. Si muda mrefu kinga kwa Marais itakuwa historia. Na hapo ndipo tutakapokuja kujua thamani ya uvumilivu, "kupotezea" na heshima kwa viongozi wastaafu.

Na miongoni mwa matokeo ya mifumo hii wanayokuja nayo akina pole pole ni kuzuka utamaduni mpya wa kung'ang'ania madarakani. Huwezi kuachia madaraka ukijua kwamba atayeingia anaweza kukubadilishia kibao. Nchi nyingi za Afrika zimeangamia kutokana na utamaduni huu wa visasi.

No way, there must be a certain level of tolerance to our elders and retired senior staff if we still need long term sustainable peace and stability.
 
Kuna watu ni wendawazimu ndani ya uongozi wa chama. Kama unatii unaruhusiwa kufanya makosa yote ila ukigoma kufanya wanachotaka ndiyo makosa yako yanatangazwa.

Kama ni kweli huyo kiongozi alikuwa na hayo makonteina 700 ambayo hayakulipiwa kodi, na hakufanywa chochote kwa sababu ni kiongozi mtuifu wa chama, basi CCM ni jumba la wahalifu watiifu.

Vinginevyo, tuamini tu huyu Polepole ni mwongo na mnafiki.
Mkuu ndio tujue kuwa watu wapo ccm si kwa sababu ya mapenzi yao bali kulinda madhambi yao.
 
CCM maji yanakorogeka

tumsubiri mwenyekiti wa UVCCM na yeye aje awatukane kina Mzee Kinana
 
Kweli aisee,we subiri uone wakina Dotto James,Popepole,Dr.Bushiru,Paramagamba,Ma co. Ya wakandarasi yenye mahusiano na wakuu wa CCM watakavyo fukuliwa makaburi yao.

dodge
Na hapa ndipo itakuwa kiini cha kutotaka kuwa nje ya madaraka. Kwa inavyoonyesha viongozi wa awamu hii watakuwa waoga sana kutoka madarakani.
 
Siku moja ikitokea (ipishie mbali) Bw. Makonda kuondolewa madarakani na pengine akaonekana na Kakesi kokote, pamoja na kumsema sema vibaya kote lakini OOOOOH watakuja mbio kumtetea na saa ingine atabatizwa kuwa kamanda. Tuhuma za Bw. Kinana juu ya makontena ni za enzi na enzi. Kwamba ni kwa nini haikusemwa mwanzo, bado haiwezi kuzuia kusemwa leo. Acha asemwe na ikiwezekana hatua stahiki dhidi yake zichukuliwe ili baadaye zitumike kama funzo kwa wanaoendelea madarakani.
Walikua wapi kumshitaki au Kumwajibisha wakati yupo madarani Mpaka wasubili atoke ndo wamseme au kumshitaki auoni kua huo ni udhaifu kwa serikali ya Ccm?
 
Na hapa ndipo itakuwa kiini cha kutotaka kuwa nje ya madaraka. Kwa inavyoonyesha viongozi wa awamu hii watakuwa waoga sana kutoka madarakani.
Kweli mkuu labda wang'ang'anie hayo madaraka milele lkn siku wakitoka tu ndio watajua watu walikua wanaogopa mamlaka walizokua nazo tu na wala hawawaogopi wao as an individual.

Wakitoka madarakani tu ataibuliwa 'PACHA WA MUSIBA' yeye huyu atakua Special kuelezea ufisadi uliofanywa Na viongozi wa awamu ya 5 wkt wakiwa madarakani,watatafutana mzee.

dodge
 
Unapokuwa na Katiba kama hii ya kwetu na mifumo dhaifu ya uongozi inayotegemea aliyeko madarakani huwezi kuwa kiongozi wa ngazi yoyote ile ukakosa kashfa. Na hata kama itakuwa ndogo kwa kiasi gani, inaweza kukuzwa na kumtia mtu kwenye hatia kubwa tu. Ni hekima zilizokuwa zikifanywa na viongozi waandamizi waliotangulia tu ndizo zimeleta utulivu hadi hivi leo. Akina polepole wajifunze uhalisia huo. Wanaanzisha utamaduni mbaya sana kwenye taifa. Utamaduni wa visasi. Ni vizuri wajikite kujenga Taifa lenye mfumo imara unaoanza na Katiba imara. Nguvu hii waliyonayo inatokana na Katiba hiyo hiyo itakayotumika na "watoto" wa akina Makamba na Kinana kuibua kesi dhidi ya wababe wa leo.

Haya wanayokuja nayo CCM sasa hivi, tutarajie makubwa huko mbele. Si muda mrefu kinga kwa Marais itakuwa historia. Na hapo ndipo tutakapokuja kujua thamani ya uvumilivu, "kupotezea" na heshima kwa viongozi wastaafu.
Uongozi wa visasi ndio maana watu wanaogopa hata kuongea ukweli kwa kuhofia kufanyiwa kitu kibaya.
 
Haka ka chakubanga bhana....

Kalikuwa kanamwita Lowassa fisadi alipokuwa upinzani, alivyorudi CCM hatukasikii tena kakibweka...

Yaani mtu anaonekana mchafu akitoka CCM...

Na inaonekana mtu akiwa CCM ni fisadi ila akija CHADEMA ni malaika msafi, jiulize kwa nni?
 
Jamaa wote wawili ni wanajeshi so shuruti zozote kwao sio kitu kigeni .Ni inaonyesha jinsi chama kilivyofilisika kimawazo sasa wanatafuta makossa yao .There is nothing to lose kwao ,wameyatafakari yote hayo na huu sio mwisho wa dunia mnawatisha na wengine wasiwe na misimamo yao iwe ya mwenyekiti which is wrong .CCM ijifunze kukubaliana kwa kutokukubaliana na sio vinginevyo
 
tapatalk_1576419509993.gif


Sent using Jamii Forums mobile app
 
So Leo ndio tunapata habari ya kontena? Kwanini hatukupashwa habari kipindi kile kile cha tukio? Au pole pole amezijua hizi habari Jana ?

Walimtunzia heshima kama washabiki mlivyotaka, lakini amezingua wanamuweka wazi aonekane,
 
Back
Top Bottom