Hukumu ya Zombe: Aachiwa!

Hukumu ya Zombe: Aachiwa!

Kaka umenigusa sana zombe ni fisadi aliyeua watu very directly akina mramba , rostam ,el , jkm, karamagi na wenzao wanatuua watanzania polepole so mi nafikiri zombe ahukumiwe kunyongwa instantly na hao mafisadi wengine tuwakamate tuwaue taratibu leo unakata mguu wa kulia a month later wa kushoto unasubiri miezi miwili unakata mkono naamini kwa stahili hii tanzania itanyooka tu.

Kuhusu zombe, mramba, el, karamagi na wenzao, sina la kusema, lakini, kuhusu Rostam na JMK, nataka utueleze wamemuua nani? sio utueleze kitu ambacho unakurupuka tu, uwe na data za kutosha, kwani kumtuhumu kuua ni kosa! haya lete vitu...
 
Jamani Zombe ilikuwa ni rahisi kutoka, lakini hawa akina Bageni wanao sema waliua watu Sinza posta, ndo namshangaa Jaji na mahakama yake. kweli mnyonge hana haki, tunaweza kuzalisha suicide bombers.


???????????!!!!!!!!!!!!????????
 
Ni kweli, Zombe kaachiwa huru na mahakama kuu.

Binafsi sijawahi kuwa na imani na Jaji Masati, si kwa sababu ya hii kesi ya akina zombe, bali kesi yoyote anayopewa huyu mkulu, na ikawahusu wakubwa, lazima awashangaze wananchi.

Na huu ni usanii wa serikali kutuzuga kwamba inachukua hatua kukomesha udhalimu. kesho utawasikia wanavyopiga madomo majukwaani kwamba mahakama imeamua hivyo, kumbe walipanga kuwasafisha.

Bado najiuliza kila mara, kwanini kesi hii ilichelewa saaaana hadi "shahidi" muhimu akafariki?Na baada ya kufariki kesi ikaenda mchakamchaka?

Kwani Jaji masati alishindwa nini kwenda kumsikiliza marehemu lema muhimbili?

ngoja kwanza nikapumzike, tutaonana kesho uwanjani.
 
mmh nilimuona mamamwenye nyumba wa zombe mahali akisema waliodhani atafulia sababu mumewe kawekwa ndani walie tu,hafulii na mungu anamjalia afya na yuko na yeye siku zote nikajua huyu tayari atakua kaongea na mumewe na kampa uhakika kama kesi hamna kitu anarudi uraiani,sasa naamini hisia zangu yaani hiyo nchi ni kuzimu hakyanani duuu.
 
Hukumu nzima inapatikana wapi jamani?
 
Hukumu nzima inapatikana wapi jamani?

kawaida hukumu huwa zinachelewa sana kuchapwa, inaweza kuchukua hata miaka. Labda kwasababu hii ni kesi ya wakubwa. Kuna wananchi wengi tu, wanaotaka kukata rufaa lakini wanaambia hukumu bado haijachapwa.
 
kawaida hukumu huwa zinachelewa sana kuchapwa, inaweza kuchukua hata miaka. Labda kwasababu hii ni kesi ya wakubwa. Kuna wananchi wengi tu, wanaotaka kukata rufaa lakini wanaambia hukumu bado haijachapwa.

Waandishi wa habari si walikuwepo full time? Natumaini wataitoa muda si mrefu.
Ninataka nione Jaji alijikwamua vipi wakati alishasema inaonekana hawakuuliwa kwa kutupiana risasi kama Polisi walivyodai, wote walikua executed (Wamepigwa risasi kichogoni wote).

Kwa hiyo alishasema polisi walidanganya, sasa iweje leo wote hawana hatia? Niko confused sana.
 
zombe aachiwa.
Nsaji Mpoki
user_online.gif
Today, 07:42 PM
Duuh, Mkuu ulikuwa wapi muda wote huo? Habari imeshajadiliwa hadi topic inakaribia kuwa closed, wewe unatuletea saa hizi 07:42 PM ?!! Anyway, thanks for your post.
 
Kaachiwa sasa hivi huyo zombe

Mkuu inamaana ulikuwa na habari kabla ama maana kwa jinsi nilivyosikia ni kwamba hukumu yako jaji aliisoma kwa masaa matano na ww post yako ni ya saa tano kasoro ss inamaana hiyo mahakama ilianza saa moja asubuhi ama?
 
Naomba kuelimishwa kwa wajuao, sheria ambayo tuna imani kuwa ni msumeno ukatao pande zote mbili, inasemaje kuhusu wale waliouawa kutokana na msimamo wa kesi hii? Je, mahakama inaamuru polisi iendelee uchunguzi wa kuwatafuta waliohusika na mauaji? Au ndio yameshakwisha?

Nilisikia kuwa jaji anasema (mfano kwa upande wa Zombe), kuwa angehukumiwa kwa kutokutoa habari kuhusu mauaji hayo kwenye vyombo vya habari hadithi ingekuwa nyingine rather than kuhukumiwa kwa mauaji (siyo nukuu ya neno kwa neno).

Sasa je, wanaweza kubadilishiwa mashtaka kama rufaa itakatwa na upande wa washtaki?
 
Ni kweli, Zombe kaachiwa huru na mahakama kuu.

Binafsi sijawahi kuwa na imani na Jaji Masati, si kwa sababu ya hii kesi ya akina zombe, bali kesi yoyote anayopewa huyu mkulu, na ikawahusu wakubwa, lazima awashangaze wananchi.

Na huu ni usanii wa serikali kutuzuga kwamba inachukua hatua kukomesha udhalimu. kesho utawasikia wanavyopiga madomo majukwaani kwamba mahakama imeamua hivyo, kumbe walipanga kuwasafisha.

Bado najiuliza kila mara, kwanini kesi hii ilichelewa saaaana hadi "shahidi" muhimu akafariki?Na baada ya kufariki kesi ikaenda mchakamchaka?

Kwani Jaji masati alishindwa nini kwenda kumsikiliza marehemu lema muhimbili?

ngoja kwanza nikapumzike, tutaonana kesho uwanjani.

Unaweza kutusaidia reference ya kesi ambayo /ambazo hukupata kuwa na imani na Jaji Masati?sasa hiyo ndo sheria,serikali inashindwa kesi zake nyingi kwa kuwa waendesha mashtaka ni mambumbumbu...imagine kesi inafika mahakamani wanaitoa wanaenda kubadili mashtaka..for Zombe to be free,he deserved it bcoz wapelelezi hawakuwa makini vya kutosha. i have nothing to regret,well done Jaji Masati..Mahakama haifungi watu kwa influence ya jinsi wananchi wanavyotaka..subiri kesi za EPA na akina Maramba ndo utabaki kinywa wazi
 

kawaida hukumu huwa zinachelewa sana kuchapwa, inaweza kuchukua hata miaka. ...Kuna wananchi wengi tu, wanaotaka kukata rufaa lakini wanaambia hukumu bado haijachapwa.


Waandishi wa habari si walikuwepo full time? Natumaini wataitoa muda si mrefu.

Nemesis, Kang, etc.

Sio kwamba hukumu zinachelewa kuchapwa. Kwa Tanzania, jaji anahukumu halafu ndio anaenda kuandika!

Kuna wakati jaji wa kesi ya MV Bukoba alisema ametingwa na kazi nyingi, akapewa likizo akaandike hukumu ambazo alikuwa amekwisha zitoa. Na hakumaliza! Wahusika wakashindwa kukata rufaa, ma captain wakashindwa kujua hatima ya kazi yao, wamekaa miaka wanasubiri jaji aandike hukumu. Hiyo sio justice.

Jaji anatakiwa aje ameshika mkononi hukumu yake ambayo ndio last word from him. Sio akaandike baadae. Jaji Masati anaweza kuja hapa JF leo jioni, kwa mfano, akasoma criticisms zooote za mitaani juu ya hukumu yake, akaenda kuzi address kwenye hukumu atayokoandika. Kwa hiyo, 1) ataziba matundu ya madudu yeyote kwenye hukumu yake 2) legal analysis yake itakuwa ni ya kusikilizia public reaction. Si haki hiyo.
 
Last edited:
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imesema bado inatafakari hatua za kuchukua baada ya Mahakama Kuu kutowatia hatiani washtakiwa tisa katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara watatu wa Morogoro na dereva mmoja wa taksi.
Jaji Salum Masatu alisema katika hukumu yake kuwa waliohusika na mauaji hayo hawako mahakamani na hivyo kuifanya kesi hiyo kuwa nguvu kwake kuwatia hatiani washtakiwa hao tisa, akiwemo mkuu wa zamani wa upelelezi mkoani Dar es salaam, Abdallah Zombe ambaye alikuwa mshtakiwa namba moja.
Kwa maana hiyo, Jaji Masati aliwaachia huru washtakiwa wote tisa waliokuwa wameshtakiwa kwa kosa la kuua kwa makusudi wafanyabiashara hao watatu, Sabinus Chigumbi, Ephraim Chigumbi na Mathis Lunkombe pamoja na dereva wa taksi wa Sinza jijini Dar es salaam, Juma Ndugu.
“Siwezi kusema lolote kwa sasa kama tutakata rufaa au la," alisema mwanasheria mwandamizi wa serikali, Jackson Kashozi.
“Msimamo tutautoa mara baada ya jopo la wanasheria wa serikali kukutana ndani ya siku kumi na nne ambazo ndizo zinazoruhusiwa kisheria kukataa rufaa kama upande mmoja haujaridhika.”
Zombe na wenzake walishtakiwa kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia, kesi ambayo upande wa mashtaka unatakiwa uthibitishe bila ya kuacha shaka kuwa wahusika ndio waliotekeleza mauaji hayo.
Lakini Jaji Masati alisema hakuona sehemu ambayo washtakiwa hao walihusika katika mauaji hayo, jambo ambalo litawalazimisha wanasheria wa serikali kuandaa mashtaka mapya iwapo watataka Zombe na wenzake waadhibiwe kwa kushiriki kosa baada ya kosa kutendeka kama upande huo ulivyoomba wakati ukifanya majumuisho yake.
Wakati upande wa mashtaka ukifanya majumuisho, uliomba mahakama imuone Zombe na baadhi ya watuhumiwa kuwa ana hatia ya kuua kwa makusudi na kama haitamtia hatiani kwa kosa hilo, basi imuhukumu kwa kufanya kosa baada ya kosa, jambo ambalo Jaji Masati alilikataa kwa maelezo kuwa atawahukumu kwa kosa waliloshtakiwa.
Source: Gazeti la Mwananchi
 
kwa kweli serikali ya Tanzania inaongozwa na VILAZA, wasiokuwa na huruma kwa raia wenzao na wala hawana misingi ya taaluma zao, kama kweli raisi aliamua kuunda tume ya uchunguzi, na kweli ukweli ulijulikana sasa iweje mwanasheria wa serikali apeleke kesi mahakamani bila kuwa na ushahidi wa kutosha, ni ukweli usiofichika kwamba Zombe na wenzie wote walishiriki katika hayo mahuaji kwa asilimia mia moja, lakini ushahidi wa vithibitisho huko wapi?, ina maana serikali pamoja na vyombo vyake vyote, polisi, UWT,na wenginevyo vilishindwa kukusanya ushahidi kabla ya kwenda mahakamani
na kwa huu uzembe na uwezo duni wa wasomi wetu hata hizo kesi zote tunazoziona za ufisadi zilizopo mahakamani(Mramba, costa mahalu, Liyumba na zinginezo) zote serikali itashindwa vibaya
na sasa lazima tujue hata hii mikataba yetu mibovu tunayoingia (Madini, umeme nk), inatokana na wasomi uchwara waliopo serikalini wakiwa bize na mambo ya ufisadi pasi na kuangalia taaluma zao,
inatia uchungu sana
 
Jamani Zombe ilikuwa ni rahisi kutoka, lakini hawa akina Bageni wanao sema waliua watu Sinza posta, ndo namshangaa Jaji na mahakama yake. kweli mnyonge hana haki, tunaweza kuzalisha suicide bombers.

Mkuu tunao tayari wanajipanga tu pa kuanzia, huwezi kuwa na nchi ya miafrika ndivyo tulivyo, viongozi sampuli ya JK, mahakama mmh, bunge la ualwatan ma suicide bombers wasiwepo
 
Back
Top Bottom