Hukumu ya Mgombea Binafsi Juni 17, 2010

hakuna hukumu yoyote ambayo mtu anaweza kutudokeza inayohusisha serikali kwenye mahakama ya rufani au kuu ambayo tunaweza kusema kuwa mahakama ili bow to the pressure of the gvt.. kuanzia kesi za wahujumu uchumi, valambhia, uhaini n.k mahakama zetu za juu zimekuwa huru mara zote. Tatizo liko kwa serikali kutekeleza hukumu hizo.

Kuna kesi moja ya uchaguzi........nakumbuka kuna mgombea either alipinga uchanguzi usifanyike au alikata rufaa kuhusu matokeo.......na maamuzi yakawa eti kw akuwa serikali ime-spend pesa nyingi hivyo haitakuwa busara............well i'm still looking for the record......nikiipata nitaiweka hapa...........yaani mahakama iliboa kichizi
 
Zak Malang, hii picha uliyoiona hata nami binafsi naiona picha kama hii, kuwa uamuzi ule wa Mahakama Kuu ulikuwa sahihi, ila kwa vile maandalizi ya Uchaguzi Mkuu yameisha kamilika, suala la mgombea binafsi liandaliwe lakini kwa ajili ya 2015!.

Nadhani jamaa walishaamua maamuzi mazito, hii chelewa chelewa toka siku zile mpaka leo, ni kuyapitisha maamuzi hayo huku na kule, hatimaye CJ ametiwa siagi na kulainika, ndio maana amechelewa kutoa uamuzi kwa kujivuta vuta, ili angalau wapigania demokrasia ya kweli, wamwelewa kuwa muda uliobakia ni mdogo.

Hii ndio nafasi pekee, the great opportunity kwa Jaji Ramadhani kusimama ahesabiwe na kuacha his mark kwenye justice pillars za nchi yetu. Nyalali (RIP), ameacha mark kwenye Tume ya Nyalali, hii sasa ndio nafasi ya CJ Agustino Ramadhani kuacha dole gumba lake, vingenevyo siku zijazo atajaishia kukumbukwa zaidi kama mpiga kinanda bora zaidi alikipiga kwa miaka mingi zaidi pale kanisani St. Alban.

Na tusubiri mlio wa zumari, ataleta wimbo mpya au wa yule aliyemlipa?. Jibu ni Alhamisi!.


Hahaha....kwa kweli amepiga kinanda miaka mingi sana pale St. Alban....yaani niliingia kanisani pale nikiwa shule ya msingi miaka hiyo jamaa anagonga kinanda pale!
 
Ni kesi ya mgombea huru, sio mgombea binafsi. Choice of words matters. Mgombea ambaye hajafungwa na itikadi ya chama chochote ni mgombea huru. Ubinafsi wake uko wapi?

Kuna watu ambao heri wafe kuliko kutenda maovu. Watu wenye mioyo ya kishahidi. Naamini Augustino Ramadhani anaweza kuwa mmoja wapo. Hata akiitwa na kutishwa atasimama kwenye sheria. Lakini si maoni yake tu ndiyo yatakayochukuliwa. Si kuna jopo la majaji?
 
Ni kesi ya mgombea huru, sio mgombea binafsi. Choice of words matters. Mgombea ambaye hajafungwa na itikadi ya chama chochote ni mgombea huru. Ubinafsi wake uko wapi?

Kuna watu ambao heri wafe kuliko kutenda maovu. Watu wenye mioyo ya kishahidi. Naamini Augustino Ramadhani anaweza kuwa mmoja wapo. Hata akiitwa na kutishwa atasimama kwenye sheria. Lakini si maoni yake tu ndiyo yatakayochukuliwa. Si kuna jopo la majaji?

Mwalimu nadhani maneno yote yanatumika kwa usahihi; Mgombea binafsi si sawa na "mgombea mbinafsi" - hii inamtafsiri "private candidate" kwa maana ya kwamba mgombea ambaye amesimama kugombea nafasi ya uongozi bila kutokuwa na chama. Mgombea huru inatafsiri "independent candidate" kwa maana ya kwamba ni mgombea ambaye hakusimamishwa rasmi na chama chake au hakutaka kusimamishwa na chama chake japo anapoingia Bungeni au anaposhika nafasi bado akawa anakutana na wenzake wa chama chake.

Chifu Sarwatt aliyeshinda kiti cha Mbulu alikuwa ni mwanachama wa TANU lakini Tanu haikumsimamisha lakini akagombea na kushinda. Na aliposhinda bado alikuwa ni mwanatanu na hata kupewa nyadhifa nyingine.

Kesi hii inahusu wagombea wa aina zote mbili.
 
Rev. Mtikila will go down in history as a true pioneer of democracy in our country. He has fought several times to ensure that basic Tanzanian's rights are not infringed by the government. Unlike many Tanzanians, who prefer to whine like chickens without heads, Mtikila has devoted his life in challenging the establishment.

I firmly believe that the government is going to loose on this case because those seven judges have pride and they are not going to allow the government to bully them or marginalize the high court.
 
hakuna hukumu yoyote ambayo mtu anaweza kutudokeza inayohusisha serikali kwenye mahakama ya rufani au kuu ambayo tunaweza kusema kuwa mahakama ili bow to the pressure of the gvt.. kuanzia kesi za wahujumu uchumi, valambhia, uhaini n.k mahakama zetu za juu zimekuwa huru mara zote. Tatizo liko kwa serikali kutekeleza hukumu hizo.
Japo sikumbuki vizuri ni kesi gani, ila nakumbuka uchaguzi wa mwaka 2005 kuna mtu alifile kesi kusimamisha uchaguzi mkuu, Mahakama Kuu ilitupilia mbali maombi hayo na ketoa sababu ikiwemo gharama kubwa zilizoshatumika kwa maandalizi.

Hakuna shaka kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Rufani kusupport uamuzi wa Mahakama Kuu, ili itatoa time extension kwa serikali kuwa mgombea binafsi ni uchaguzi wa 2015.

Mahakama wakati ikitoa uamuzi, sio kila wakati inazingatia haki pekee, bali pia inazingatia na mazingira husika na hasara itakayotokana na uamuzi huu wa mahakama.

Hata mimi nina imani sana na CJ Ramadhani, lakini bado nina maswali yasiyo na majibu kuwa hii issue kwa upeo wangu finyu, naiona kama iko straight forward, sasa muda wote huu kuja kutoa uamuzi baada ya Juni 15, walikuwa wanafanya nini siku zote?!, nikajijibu walikuwa wanaijadili hukumu na wenye nchi yao ndipo waitoe.
 
I predict mahakama ya Rufaa will blast your government in words that will remain in infamy!
Kesho nitafanya reference ya sentensi yako hii, ila pia ushauri wa bure kwako na wengine wote wenye matumaini kuwa "keep hoping for the best, but prepare for the worst"- Mgombea binafsi ni 2015!.
 
Wakuu,

Kinachotia wasi wasi kwenye hili ni kwa nini verdict haikutolewa April as scheduled, ije itolewe leo mid June 2010.
Yatakuja maneno mengi sana, ila msumari lazima uwe serikali ijiandae kwa mgombea huru 2015!!

Hill nchi imejaa drama ati...
 
Tuepuke wishful thinking na kuiangalia Judiciary ya Tanzania beyond personalities.Ina maana zile ripoti mbalimbali zinazoituhumu Idara ya Mahakama kuwa ni miongoni wa vinara wa rushwa zilikuwa uzushi?Na hata tukiweka kando hoja hiyo,huu mlolongo wa majaji wanaoteuliwa na mtu mwenye rekodi ya ufisadi haimaanishi walakini hata kwa hao wateuliwa?Baadhi ya majaji walihusika katika kutia saini mikataba ya kifisadi (walipokuwa wanasheria wanaojitegemea),sasa watabadilika ghafla kwa vile tu wamepewa ujaji?
Binafsi natarajia maumivu tu come hiyo hukumu.
 
Tuepuke wishful thinking na kuiangalia Judiciary ya Tanzania beyond personalities.Ina maana zile ripoti mbalimbali zinazoituhumu Idara ya Mahakama kuwa ni miongoni wa vinara wa rushwa zilikuwa uzushi?Na hata tukiweka kando hoja hiyo,huu mlolongo wa majaji wanaoteuliwa na mtu mwenye rekodi ya ufisadi haimaanishi walakini hata kwa hao wateuliwa?Baadhi ya majaji walihusika katika kutia saini mikataba ya kifisadi (walipokuwa wanasheria wanaojitegemea),sasa watabadilika ghafla kwa vile tu wamepewa ujaji?
Binafsi natarajia maumivu tu come hiyo hukumu.

Mlalahoi uko katika point haswa ndio maana nasemaga humu jamvini Tanzania ni society of lawlessness hamna kitu!!! But let us be optimistic pengine shinikizo kutoka kwa wafadhili wanaweza kubadilika but I am very skeptical.
 
Kiravu%285%29.jpg

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Rajabu Kiravu.




[FONT=Arial, sans-serif]Mahakama ya Rufani Tanzania kesho itatoa hukumu kuhusu mgombea binafsi katika uchaguzi wa kisiasa dhidi ya rufaa iliyofunguliwa na Mwenyekiti wa Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Hukumu hiyo itatolewa baada ya mahakama hiyo kusikiliza marafiki wa mahakama ambao Aprili 8, mwaka huu walitofautiana kwa baadhi yao kuunga mkono upande wa Jamhuri na mwingine kuupinga.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Marafiki hao walioalikwa na Jaji Mkuu, Augostino Ramadhani, ni pamoja na Profesa Palamagamba Kabudi na Profesa Jwani Mwaikusa, ambao kitaaluma ni wanasheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Zanzibar, Othman Masoud. Mwingine ni Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Rajabu [/FONT][FONT=Arial, sans-serif]Kiravu.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Profesa Kabudi alikubaliana na Serikali kuwa mahakama haina mamlaka ya kurekebisha kifungu chochote cha katiba kauli ambayo iliungwa mkono na Masoud.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Hata hivyo, Profesa Mwaikusa alisema mahakama kwa mujibu wa mgawanyo wa madaraka miongoni mwa mihimili mitatu, ina mamlaka ya kutamka kifungu chochote kinachokwenda kinyume cha katiba.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Kwa upande wake, Kiravu, alisema umebakia muda mfupi kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu hivyo kama wagombea binafsi wataruhusiwa, hatua hiyo itaathiri maandalizi ya uchaguzi huo.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Walitoa maoni yao walipokuwa wakichangia hoja za mwisho kwa mahakama hiyo iliyokuwa imeketi chini ya jopo la majaji saba, wakiongozwa na Jaji Ramadhani, kusikiliza rufaa iliyowasilishwa na serikali kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuruhusu mgombea binafsi.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Akizungumza na Nipashe, Wakili wa Mchungaji Mtikila, Riachard Rweyongeza, alisema kuwa amepokea hati ya kuitwa mahakamani kesho kwa ajili ya kuendelea na kesi hiyo.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Kwa mujibu wa rufaa hiyo namba 45 ya mwaka jana, serikali iliwasilisha mahakamani hapo ikipinga hukumu ya iliyotolewa na waliokuwa majaji wa Mahakama Kuu, ambao ni Jaji Mstaafu Amir Manento, Salum Massati, Jaji wa Mahakama ya Rufani kwa sasa na Thomas Mihayo (Mstaafu), ambao walikubaliana na ombi na Mtikila na kuruhusu kuwepo kwa mgombea binafsi nchini.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Katika rufaa hiyo, serikali imetoa sababu sita za kukata rufaa hiyo zikiwemo; Mahakama Kuu ilikosea kujipa mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo; ilikosea kutengua vifungu vya Katiba ya nchi; na kukosea kisheria kwa kupunguza matakwa ya lazima ya Ibara 30(5) na 13(2) ya Katiba ya nchi.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Sababu nyingine ni kujipachika mamlaka ya kibunge ya kutunga sheria, kukosea kisheria kwa kuiweka Katiba ya nchi katika vyombo vya kimataifa na pia ilikosea kuitolea maamuzi kesi hiyo bila kuweka suala hilo bayana.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Mara ya kwanza, serikali ilikata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu, katika Mahakama hiyo ya Rufaa mwaka 2007, ambayo ilidai mahakama hiyo ya chini ilikosea kisheria kutafsiri Ibara ya 21(1) (c), 39 (1) (c) (b) na 69 (1) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.[/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Hata hivyo, rufaa hiyo ilitupiliwa mbali na Mahakama ya Rufaa baada ya kukubaliana na ombi la wakili wa Mtikila, Richard Rweyongeza kwamba, rufaa hiyo haina msingi na kwamba imejaa dosari za kisheria.[/FONT]
[FONT=Arial, sans-serif]Awali katika hukumu ya Mahakama Kuu ilivyotolewa Mei, mwaka 2006, ililiruhusu kuwepo kwa mgombea binafsi katika uchaguzi, kwa sababu Katiba ya nchi inatoa haki hiyo. [/FONT]
[FONT=Arial, sans-serif]Mahakama Kuu ilibainisha kuwa katiba inatamka wazi kuwa, kila mwananchi ana haki ya kuchagua au kuchaguliwa kuwa kiongozi na haiweki masharti kuwa hilo lifanyike kwa mtu kujiunga na chama fulani. [/FONT]
[FONT=Arial, sans-serif]Mapema Mwaka 1993, Mtikila alishinda kesi kama hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, lakini licha ya uamuzi huo wa mahakama, Bunge lilishindwa kutunga sheria ya kuruhusu mgombea binafsi hivyo alifungua kesi hiyo ya kikatiba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ambapo alishinda tena. [/FONT]



CHANZO: NIPASHE

Tungoje Majibu ya [FONT=Arial, sans-serif] rufaa iliyofunguliwa na Mwenyekiti wa Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila. itakuwaje ?
[/FONT]
 
Ni matumaini yangu want JF wa anga mahakama watatuweka ahead as usual na ma breaking news.
 
Wakuu,

Kinachotia wasi wasi kwenye hili ni kwa nini verdict haikutolewa April as scheduled, ije itolewe leo mid June 2010.
Yatakuja maneno mengi sana, ila msumari lazima uwe serikali ijiandae kwa mgombea huru 2015!!

Hill nchi imejaa drama ati...

kwa sababu kwenye Bunge hili hili itapitishwa sheria ya kufanyia mabadiliko sheria ya Vyama vya siasa ya 1992 pamoja na Katiba..
 
Rev. Mtikila ameiambia BBC kwamba usiku kucha leo hakulala kwa kutofahamu ni hatua gani atachukua endapo hukumu ya Mahakama ya rufaa itamwangusha. Mimi namshauri tu kwamba wakati wa kuwa na mgombea binafsi hasa kwenye ngazi ya URAIS bado. Aachane kwa sasa na mradi huu ambao nia yake ni nzuri tu kwa hapo baadae. Kwa sasa hatuna chaguzi huru, hatuna tume huru ya uchaguzi, miundombinu ya uchaguzi bado ni duni sana, elimu ya uraia ni ya kiwango cha chini sana kwa wapiga kura wetu, umasikini wa watu wetu unatisha, vyombo vya dola bado ni vya chama kilekile,.....
Tuna mengi ya kushughulikia kwa sasa kabla ya hili la mgombea huru.
 
kwa sababu kwenye Bunge hili hili itapitishwa sheria ya kufanyia mabadiliko sheria ya Vyama vya siasa ya 1992 pamoja na Katiba..
.
Hii ni habari njema na ya matumaini, japo kwenye nafsi yangu bado nina mashaka kusubiri hukumu, kufuatia kuchukua muda mrefu, kauli kama hizi, nazihesabu kama authority ya aina fulani, tuisubiri tuu hiyo hukumu kama uthibitisho, tuelekee kwenye Tanzania njema zaidi kisiasa ambayo itaandamana na chaos za kisiasa maana hata kina sisi tuliojikalia pembeni, tutaingia ulingoni.
 
wakati wa kuwa na mgombea binafsi hasa kwenye ngazi ya URAIS bado. Aachane kwa sasa na mradi huu ambao nia yake ni nzuri tu kwa hapo baadae. Kwa sasa hatuna chaguzi huru, hatuna tume huru ya uchaguzi, miundombinu ya uchaguzi bado ni duni sana, elimu ya uraia ni ya kiwango cha chini sana kwa wapiga kura wetu, umasikini wa watu wetu unatisha, vyombo vya dola bado ni vya chama kilekile,.....
Tuna mengi ya kushughulikia kwa sasa kabla ya hili la mgombea huru.
Mahakama ikikazia ile hukumu ya uhuru wa kugombea, then, hata wa urais watajitokeza, presidential materials 10 times better than JK, wapo ila pia ni kweli nakubaliana na wewe, bado hatuna chaguzi huru, hatuna tume huru ya uchaguzi, miundombinu ya uchaguzi bado ni duni sana, elimu ya uraia ni ya kiwango cha chini sana kwa wapiga kura wetu, umasikini wa watu wetu unatisha.
 
Back
Top Bottom