Hukumu ya lema ilipikwa.

Ikumbukwe kuwa msingi mzima wa kesi ni kuwa Lema alimdhalilisha Batilda Burian katika mojawapo ya mikutano ya kampeni. Kwamba, kuna maneno aliyasema ambayo yalikuwa ni ya udhalilishaji. Sasa hilo ni jambo linalowezakujadiliwa. Wale ambao mmesikiliza hukumu maswali yafuatayo yamejibiwa vipi. Binafsi sijaweza kuchukua msimamo wa hukumu yenyewe bila kuisoma vizuri na kuelewa reasoning ya jaji:

a. Mahakama imejuaje kuwa Batilda alidhalilishwa? - Bila kumuuliza yeye wanajuaej kuwa alijisikia kudhalilika. Vipi kama aliona ni ujinga tu wala haikumdhalilisha? Hivi mtu mwingine anaweza kwenda kusema "x ameibiwa" wakati yule ambaye anadaiwa kuibiwa anaona kila kitu chake kipo salama?

b. Imethibitishwa nini kuhusu alichosema Lema ambacho ni cha udhalilishaji? Alisema maneno gani, lini na wapi na ni ushahidi gani kuwa aliyasema hayo? Kwa mfano watu watatu wakija na walikuwepo kwenye mkutano wakasema hawakusikia maneno hayo na watu wengine watatu ambao walikuwepo kwenye mkutano huo wakasema walimsikia mahakama inaamua vipi kuwa hao watu watatu wanaosema walisikia wanasema kweli?

c. Binafsi kwa kweli sijashtushwa sana na Lema kuvuliwa ubunge - kama kuna ushahidi wa kutosha sidhani kama mahakam ailikuwa na uchaguzi mwingine- kilichonishtua zaidi na kinachonisumbua ni kuwa inaonekana hukumu ilishajulikana mapema zaidi almost a week kabla. Hili ni geni sana kwenye mahakama zetu. What happened?
 
Pamoja na kupika hukumu lakini bado itakula kwao. Uwezekano wa wao kushindwa kwenye uchaguzi wa marudio ni mkubwa mno. Na kushindwa tena sasa hivi kwenye uchaguzi wa marudio ni kuendelea kujimaliza. Labda waamue kulazimisha ushindi, jambo ambalo litawagharimu sana kuua watu, jambo ambalo litakuwa ni gharika kubwa kwenye future yao kama chama. Vyovyote iwavyo, hii hukumu yao ya kupika itawatokea puani.
 
wenzetu wakenya huwa wana ka utaratibu kazuri sana wa kuwapata viongozi wa kuongoza taasisi nyeti zote.huku kwetu hawa mabwana ni ma president appointees,hv rais akisema make sure that kesi funali ushindi unapatikana atagoma jaji?

Hao unaosema wana utaratibu mzuri ndio tumeona wanauana hovyo mpaka aende Mkapa na Jakaya kuwapatanisha, au umesahau?
 
mwenyewe nilipigiwa simu na kigogo serikalini juzi akiniambia matokeo ya arusha yatabatilishwa lema sio mbunge tena.nikamwambia acha tuone kumbe kweli, jamani katiba ibadilishwe mahakama ziwe huru.
Ni aibu kubwa kwa jaji na mfumo mzima wa mahakama katika nchi hii. Historia itawatesa CCM.
 
Hao unaosema wana utaratibu mzuri ndio tumeona wanauana hovyo mpaka aende Mkapa na Jakaya kuwapatanisha, au umesahau?

Kuuana huko ndiko kuliwafanya watumie vichwa vyao na kutimiza wayatakayo wananchi. je mnataka nasi tufike huko?
You've got it coming.
 
Napendekeza Mahakama ingeondolewa kwenye kuwa moja kati ya mihimili ya nchi, iunganishwe na Serikali, (Executive) coz maamuzi yake mengi ufanyika serikalini wao ni kutekeleza kile kilichoamuliwa na serikali, hivi wanaJF mmesahau hukumu za ajabu kama ile ya kesi ya Zombe pamoja na ya mgombea binafsi?
 
je kwa mtindo huu wa mahakama, myonge atapata haki yake? ni kushusha thamani ya mahakama na uhuru wake. Majaji wae makini
 
Hii hukumu imeidhalilisha mahakama kuu na kwa kweli hatakama Chadema wanakubalika Arusha si vema kukubaliana na upindishaji wa sheria.Kwa kuwa Chadema wana wanasheria makini nina imani kuwa watatafakari na kuchukua hatua sahihi.
 
Tatizo mleta mada anayedai ni mwanasheria badala ya kuipeleka mada jukwaa la sheria kaileta jukwaa la siasa. Kwa hiyo comments huku ni za kisiasa tuu. Whether or not kesi imepikwa ni kweli kwamba hii ni kesi ya tort?

Ndugu zangu wakili wa Lema ameshapeleka Notisi Mahakama Kuu ya kuadhimia kupinga hukumu ya Mahakama Kuu. Inaonesha kwamba sehemu ambayo hawajaridhika nayo ni kuhusu Lema kuondolewa sifa ya kugombea. Ki utaratibu, kama kuna rufaa Mahakamani ni haramu kujadili usahihi au vinginevyo wa uamuzi uliyotolewa. Kma tuna hoja nzuri zaidi tuwapelekee wanasheria wa pande husika.

Naamini, kama Lema ameamua kukata rufaa Mahakama ya Rufaa bado ana imani na mfumo wetu wa sheria. Na jaji kama binaadamu pia anaweza kukosea katika maamuzi yake bila kukusudia. Kama emekosea au la refa kwa sasa ni Mahakama ya Rufaa. Ningewaomba huu mjadala tusiendelee nao bali nguvu zetu tupeleke kwa wanasheria wa pande husika. Wapo wanaoona Mahakama Kuu ilipatia na wapo wanaoona ilikosea. Nawatakia wiki endi njema
 
Tangu jana nilielezea kwamba nimepata taarifa kuvuja kwa hukumu ya mh Lema. Mods aliunganisha link yangu na nyingine zilizokuwa zinashabihana na hilo. Kitaaluma mimi ni mwanasheria na hakika kila mwenye taaluma hii na aliyekuwa akifuatilia kesi atabaki mdomo wazi juu ya hukumu iliyotolewa. Huyu jaji alichofanya ni kucheza na akili za watu, na nina uhakika alikua na hukumu mbili mkononi.

Hata mwanafunzi wa sheria mwaka wa kwanza anajua kwamba katika 'tort' ili kosa lionekane limetendwa ni lazima aliyetuhumiwa athibitishe ameathirikaje na hizo tuhuma. Inakuwaje 3rd party ndo athibitishe hilo?

Batlida hajawahi kuja mahakamani. Kesi hii inaandika historia katika mhimili wa mahakama juu ya uhuru wake. Kuna haja ya majaji katika mahakama kuu kufanyiwa enterview kama kule kenya wanavyofanya. Hii hukumu imenikumbusha mengi katika tasnia ya sheria, daima itabaki kuwa kumbukumbu mbovu kwenye mhimili wa mahakama.
hapa ndipo ninapoikubali JF....mkuu heshima sana
 
Back
Top Bottom