Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,504
- 51,099
Ndani ya wiki hizi mbili kuna mambo ya kutisha yanaendelea nchini. Lakini kwa kuwa watawala wamegundua akili za Watanzania ni kufuatilia vitu vyepesi, wameamua kuinvest kwenye mpira wakati huku behind the scene wakiwa busy kuuza nchi na kupalilia ufisadi. Haya ni baadhi ya mambo ya kusikitisha yanayoendelea nchini ndani ya wiki hizi mbili
1. Waziri atoa rushwa ya mitungi 100 kwa kila mbunge
Wakati watu wakiwa busy kufuatilia kama Yanga atatwaa kombe, Waziri mwenye dhamana ya nishati amegawa mitungi 100 ya gesi kwa kila mbunge bure. Dhahiri shahiri hii ni rushwa, tena imetolewa bungeni na tena bila aibu spika ameibariki na kuitetea.
Wakati mwingine unajiuliza spika ana maslahi gani katika hili, utagundua kuwa anamaslahi mara mbili. Mosi, mume wake ni bosi pale EWURA, kwa hiyo spika ana conflict of interest kwa jambo lolote linalohusu EWURA litakaloletwa bungeni. Pili na yeye spika ni mnufaika wa mitungi mia ya bure!
Hii nchi inakwenda wapi?
2. Kuuza bandari
Hii kampuni ya Dubai iitwayo Dubai Ports(DP), imekuwa ikijaribu kutwaa Bandari mbalimbali. Mwaka 2006 ilijaribu kutwaa bandari huko Marekani lakini bunge la Marekani (Congress) lilipiga kura kukataa utwaaji huo.
Hata hivyo DP ilikuwa ikipigiwa chapuo na rais wa Marekani wa wakati huo George Bush. Kutokana na pressure kubwa ililzamika kampuni hiyo iuze share zake kwa kampuni ya Marekani ndo ifanye shughuli hizo.
Leo Samia anataka kutuletea yaleyale ya George Bush.
3. Kuna kila dalili kuna mkono wa CIA katika hili deal
Katika kujaribu kucounter nguvu ya China katika uwekezaji wa infrastructures hasa Africa, USA na washirika wake wanatumia front companies ambayo wamekita mizizi yao ili kutwaa hizi assets.
Hii move nina wasiwasi inaweza kuathiri uwekezaji wa Wachina katika bandari mpya ya bagamoyo. Na ni dhahiri Mmarekani hataki mchina ajenge hiyo bandari. Sasa swala hapa siyo kwamba kwa nini uwekezaji wa China kwenye bandari ni sawa ila wa Dubai ni no!. Jibu ni simple, Dubai wanaenda kufanya kitu rahisi ambacho sisi tukiacha uzembe na uvivu tunaweza kukifanya sisi wenyewe, wakati mchina anaenda kufanya kitu kikubwa!.
Kama tumewahi kukataa mchina asijenge bandari kwa sababu angeioperate kwa miaka takriban 40, Iweje leo tuone eti Dubai ipewe deal la miaka lukuki kwa kitu ambacho kimsingi kipo?
Mkapa aliuza NBC kwa makaburu kwa bei chee akaishia kujuta, Samia sasa anataka kuuza bandari kwa ahadi feki za modernization!.
WEKENI MKATABA WAZI TUUONE!
1. Waziri atoa rushwa ya mitungi 100 kwa kila mbunge
Wakati watu wakiwa busy kufuatilia kama Yanga atatwaa kombe, Waziri mwenye dhamana ya nishati amegawa mitungi 100 ya gesi kwa kila mbunge bure. Dhahiri shahiri hii ni rushwa, tena imetolewa bungeni na tena bila aibu spika ameibariki na kuitetea.
Wakati mwingine unajiuliza spika ana maslahi gani katika hili, utagundua kuwa anamaslahi mara mbili. Mosi, mume wake ni bosi pale EWURA, kwa hiyo spika ana conflict of interest kwa jambo lolote linalohusu EWURA litakaloletwa bungeni. Pili na yeye spika ni mnufaika wa mitungi mia ya bure!
Hii nchi inakwenda wapi?
2. Kuuza bandari
Hii kampuni ya Dubai iitwayo Dubai Ports(DP), imekuwa ikijaribu kutwaa Bandari mbalimbali. Mwaka 2006 ilijaribu kutwaa bandari huko Marekani lakini bunge la Marekani (Congress) lilipiga kura kukataa utwaaji huo.
Hata hivyo DP ilikuwa ikipigiwa chapuo na rais wa Marekani wa wakati huo George Bush. Kutokana na pressure kubwa ililzamika kampuni hiyo iuze share zake kwa kampuni ya Marekani ndo ifanye shughuli hizo.
Leo Samia anataka kutuletea yaleyale ya George Bush.
3. Kuna kila dalili kuna mkono wa CIA katika hili deal
Katika kujaribu kucounter nguvu ya China katika uwekezaji wa infrastructures hasa Africa, USA na washirika wake wanatumia front companies ambayo wamekita mizizi yao ili kutwaa hizi assets.
Hii move nina wasiwasi inaweza kuathiri uwekezaji wa Wachina katika bandari mpya ya bagamoyo. Na ni dhahiri Mmarekani hataki mchina ajenge hiyo bandari. Sasa swala hapa siyo kwamba kwa nini uwekezaji wa China kwenye bandari ni sawa ila wa Dubai ni no!. Jibu ni simple, Dubai wanaenda kufanya kitu rahisi ambacho sisi tukiacha uzembe na uvivu tunaweza kukifanya sisi wenyewe, wakati mchina anaenda kufanya kitu kikubwa!.
Kama tumewahi kukataa mchina asijenge bandari kwa sababu angeioperate kwa miaka takriban 40, Iweje leo tuone eti Dubai ipewe deal la miaka lukuki kwa kitu ambacho kimsingi kipo?
Mkapa aliuza NBC kwa makaburu kwa bei chee akaishia kujuta, Samia sasa anataka kuuza bandari kwa ahadi feki za modernization!.
WEKENI MKATABA WAZI TUUONE!